Mr Acky
JF-Expert Member
- Nov 24, 2019
- 234
- 313
- Thread starter
- #161
Mtunzi Akida Siri Rambao
Email akidasiri@gmail.com
MSIMU 3
Ilipoishia...
Sauti hizo zilipelekea kuupamba usiku huo uliokosa mbalamwezi na kuwa na giza totoro kuwatoa upweke na wasiwasi na kuwa fanya wasichana hao kuendelea kupamba moto na tumaini la kutoka salama.
Tuendelee...
Makomandoo hao wakike kwa haraka bila maongezi wakatokomoea na kutokomoea zaidi mbali kabisa wakiacha eneo la makao makuu likiwa nyuma mbali huku mioyo yao ikiwa na furaha ya kuondokana na utumwa wa maasi.
Mabegi yakijeshi yakiwa mgongoni, viatu miguuni vyenye soli ngumu visivyoingiza aina yoyote ya ncha kali pamoja na suruali zao ngumu nyeusi vifuani wakiwana mashati magumu ya mikono mirefu kuzuia mikwaruzo ya hapa na pale ndivyo viwalo vilivyo hefadhi miili yao usiku huo. Safari iliwachukua muda mrefu baada ya heka khamsini kwisha walikutana na chaka kubwa lisilojulikana ukubwa wake hivyo matembezi ya mchaka mchaka chinja yaliwachukua karibu saa moja na nusu baada ya yale mawili waliyoyapoteza wakivuka mashamba ya bhangi wakiwabado ndani ya milki ya kambi. Hatimaye wakakutana na ukuta mrefu sana, wote wakatabasamu na kuona mwanga wa tumaini la kutokomea kabisa pasina kujulikana kabisa.
Haraka haraka bila kulemba kila mmoja akatoa kamba ngumu ya manira spesho kabisa ianayotumiwa na wanajeshi maalumu katika kupandia na kuvuka sehemu za hatari. Kila mmoja alichukua nanga ndogo ya kupandia milima na sehemu zingine za juu na kuifunga vizuri tayari kwa matumizi. Kila mmoja akarudi hatua kazaa nyuma na kuirusha kwa ustadi kamba yenye kichwa cha nanga upande wa pili wa ukuta kisha wakazivuta kuweka kikwazo na kuona zimeshakamana sawa sawa haraka wakaaanza kukwea kwenda juu pasina kuongea kitu na walipo fika juu ya ukuta wenye upana wa futi mbili sasa wakaanza kuandaaa namna ya kushuka ambapo zoezi halikuwa refu wakafanikiwa.
Wakaanza kukusanaya vitu na kutia katika mabegi na mchaka mchaka wa kukimbia hatua fupi fupi ukaanza. Safari iliwachukua tena masaa mawili mengine na nusu hivi bado wakiwa katikapoli wakipanda na kushuka milima kwa tabu lakini hawakujari. Bado dalili ya kukutana na nyumba za watu hazikuonekana lakini hawakujari hilo wawo mbele kwa mbele. Ilikuwa teyari ishafika saa tisa za usiku wasichana sasa wakiwa vichakani bila mazungumzo.
Hatimaye baada ya mwendo mwengine wa lisaa limoja wakakutana na barabara ya rami ambayo walionekana kuitambua maana hakuna aliyeonesha uso wa mshangao zaidi ya kurudi tena vichakani wakielekea upande wa magharibi.
Baada ya dakika ishirini tu za matembezi ya kawaida kwa mbali ulionekana mji mdogo, walichokifanya kwanza ni kubadirisha nguo na kuvaa mavazi ya kawaida kisha wakachukua vitu vya msingi ikiwemo fedha za kutosha na kisha mabegi wakayatelekeza yakiwa na zana zile kichakani hao wakajitokeza katika changanyikeni bila kujulikana na mtu yeyote yule. “Habari kaka tunahitaji usafiri wa kutufikisha Mombo”, Monica aliongea huku akiliegemea gari hilo la rangi ya kijivu mojawapo ya magari yaliyokuwa yameegeshwa pembeni ya mgahawa mkubwa wa mmachame mmoja aliyefahamika kwa jina la Mushi “ohh mtaiweza bei mabinti?...”
bwana huyo aliyekuwa amesimama akiligonga gonga gari lake kwa vidole aliwajibu hukua akiwatazama kwa macho ya matamanio, kabla hajajibiwa akaedelea “usiku huu mtanipa elfu khamsini kila mmoja la sivo msubiri magari asubuhi” alimaliza kuongea safari hii jicho la tama ya ngono lili ganda katika kifua cha Monica kilichokuwa kikionesha matiti yake yaliyo jaa. Monica wala hakujali akavuta mkoba wake uliokuwa kwapani na kuufungua. Kwa macho ya wizi dereva wa taxi aliona maburungutu ya pesa yaliyomfanya ashtuke, monica akatoa kiasi na kumpatia. Dereva akazipokea na kuzihesabu laki moja na nusu keshi na kutabasamu hukua kiwaonesha kwa ishara kupanda garini.
Itaendeleaa...
Email akidasiri@gmail.com
MSIMU 3
Ilipoishia...
Sauti hizo zilipelekea kuupamba usiku huo uliokosa mbalamwezi na kuwa na giza totoro kuwatoa upweke na wasiwasi na kuwa fanya wasichana hao kuendelea kupamba moto na tumaini la kutoka salama.
Tuendelee...
Makomandoo hao wakike kwa haraka bila maongezi wakatokomoea na kutokomoea zaidi mbali kabisa wakiacha eneo la makao makuu likiwa nyuma mbali huku mioyo yao ikiwa na furaha ya kuondokana na utumwa wa maasi.
Mabegi yakijeshi yakiwa mgongoni, viatu miguuni vyenye soli ngumu visivyoingiza aina yoyote ya ncha kali pamoja na suruali zao ngumu nyeusi vifuani wakiwana mashati magumu ya mikono mirefu kuzuia mikwaruzo ya hapa na pale ndivyo viwalo vilivyo hefadhi miili yao usiku huo. Safari iliwachukua muda mrefu baada ya heka khamsini kwisha walikutana na chaka kubwa lisilojulikana ukubwa wake hivyo matembezi ya mchaka mchaka chinja yaliwachukua karibu saa moja na nusu baada ya yale mawili waliyoyapoteza wakivuka mashamba ya bhangi wakiwabado ndani ya milki ya kambi. Hatimaye wakakutana na ukuta mrefu sana, wote wakatabasamu na kuona mwanga wa tumaini la kutokomea kabisa pasina kujulikana kabisa.
Haraka haraka bila kulemba kila mmoja akatoa kamba ngumu ya manira spesho kabisa ianayotumiwa na wanajeshi maalumu katika kupandia na kuvuka sehemu za hatari. Kila mmoja alichukua nanga ndogo ya kupandia milima na sehemu zingine za juu na kuifunga vizuri tayari kwa matumizi. Kila mmoja akarudi hatua kazaa nyuma na kuirusha kwa ustadi kamba yenye kichwa cha nanga upande wa pili wa ukuta kisha wakazivuta kuweka kikwazo na kuona zimeshakamana sawa sawa haraka wakaaanza kukwea kwenda juu pasina kuongea kitu na walipo fika juu ya ukuta wenye upana wa futi mbili sasa wakaanza kuandaaa namna ya kushuka ambapo zoezi halikuwa refu wakafanikiwa.
Wakaanza kukusanaya vitu na kutia katika mabegi na mchaka mchaka wa kukimbia hatua fupi fupi ukaanza. Safari iliwachukua tena masaa mawili mengine na nusu hivi bado wakiwa katikapoli wakipanda na kushuka milima kwa tabu lakini hawakujari. Bado dalili ya kukutana na nyumba za watu hazikuonekana lakini hawakujari hilo wawo mbele kwa mbele. Ilikuwa teyari ishafika saa tisa za usiku wasichana sasa wakiwa vichakani bila mazungumzo.
Hatimaye baada ya mwendo mwengine wa lisaa limoja wakakutana na barabara ya rami ambayo walionekana kuitambua maana hakuna aliyeonesha uso wa mshangao zaidi ya kurudi tena vichakani wakielekea upande wa magharibi.
Baada ya dakika ishirini tu za matembezi ya kawaida kwa mbali ulionekana mji mdogo, walichokifanya kwanza ni kubadirisha nguo na kuvaa mavazi ya kawaida kisha wakachukua vitu vya msingi ikiwemo fedha za kutosha na kisha mabegi wakayatelekeza yakiwa na zana zile kichakani hao wakajitokeza katika changanyikeni bila kujulikana na mtu yeyote yule. “Habari kaka tunahitaji usafiri wa kutufikisha Mombo”, Monica aliongea huku akiliegemea gari hilo la rangi ya kijivu mojawapo ya magari yaliyokuwa yameegeshwa pembeni ya mgahawa mkubwa wa mmachame mmoja aliyefahamika kwa jina la Mushi “ohh mtaiweza bei mabinti?...”
bwana huyo aliyekuwa amesimama akiligonga gonga gari lake kwa vidole aliwajibu hukua akiwatazama kwa macho ya matamanio, kabla hajajibiwa akaedelea “usiku huu mtanipa elfu khamsini kila mmoja la sivo msubiri magari asubuhi” alimaliza kuongea safari hii jicho la tama ya ngono lili ganda katika kifua cha Monica kilichokuwa kikionesha matiti yake yaliyo jaa. Monica wala hakujali akavuta mkoba wake uliokuwa kwapani na kuufungua. Kwa macho ya wizi dereva wa taxi aliona maburungutu ya pesa yaliyomfanya ashtuke, monica akatoa kiasi na kumpatia. Dereva akazipokea na kuzihesabu laki moja na nusu keshi na kutabasamu hukua kiwaonesha kwa ishara kupanda garini.
Itaendeleaa...
