Story: The Hidden Truth (Ukweli Uliofichika)

Story: The Hidden Truth (Ukweli Uliofichika)

The Hidden Truth ( Ukweli uliofichika)

Nani Anahusika?

Mtunzi: Akida Siri Rambao
Contact: 0658328596
Email akidasiri@gmail.com

MSIMU WA PILI

SEHEMU 5 E : PENZI

Tuendeleeee...

...nimefurahi kukufahamu Shalon” kwa furaha aliongea Karimu “Mi pia nimefurahi kukutana nanyi nyote mkiwa wazima, mnisamee tu kwa kuwapotezea muda wenu” aliongea kwa ibu Shalon akiwa na maandalizi ya kuondoka “Wala usiwaze kuhusu hilo hakuna lililo haribika mbona” Karimu aliongea tena huku akitabasamu, “Haya naomba ruhusa niwaache tutatafuta siku nyingine tutaongea mengi zaidi” Shalon alikusanya vilivyo vyake na kusimama “In Shaa Allah” Karimu alijibu kisha yeye pamoja na Salimu walifata kunyanyuka kwa ajiri ya kutoka eneo hilo.

Kigogo Road, Kinondoni-Dar es Salam
Ndani ya daladala itokayo Kariakoo hadi Ubungo, Karimu kama kawaida akaaanza kuzitoa sifa kwa namna alivyomuona Shalon, katika mazungumzo ya hapa na pale Salimu akagutuka kuwa kuna ujumbe uliingia katika simu yake na wala hakutazama ni wa nani. Aka simamisha mwendo na kuweka mizigo ardhini akatoa simu na kuuufnugua ujumbe huo.

Baada ya ya kuusoma alitoa mguno huo mpaka Karimu akageuka kumtazama. “Vipi kulikoni ndugu?” safari hii akasimama akimtazama Salimu. “Shalon muda ule tunaongea pale, si alinitumia meseji bwana ndo nimekumbuka muda huu saa zile nilisikia lakini nikapotezea” Salimu alibaki anajikuna kichwa akaamua kuirudisha mfuko wa nyuma na mwendo ukaanza tena. “Anasemaje kaka hujaniambia bado” Karimu alivunja ukimya “ Acha tu sijui siku hizi wanawake wanatoa wapi ujasiri wa kutongoza wanaume” aliongea Salimu akionesha kutokupendezwa “Ehhh sijasikia vizuri au inamaana Shalon amekutongoza… au sijaelewa?” aliongea Karimu kwa sauti ya kunong’ona. “Shalon ananitaka ananipenda sana tu ndivyo alivyo niambia tena amesema anaomba asikatishwe kunipenda” aliongea Salimu kwa sauti ya Kunog’ona “Duhh kaka dodo hilo katika msufi mzee usilikalie kimya sasa”. Karimu aliongea akisisitiza kwa kumpiga piga pajani.

Ukonga Road, Ilala-Dar es Salam
‘Yani likizo yangu imezaa matunda nina bahati sana sikutegemea kama nitakuja kukutana na kijana yule katika maisha yangu huu ni mwanzo mzuri kwangu’, Shalon alijiwazia huku uso ukiwa kwenye kioo akitazama nje. ‘I need a man like him’ alijisemea nafsini.

Mara akiwa katikati ya mawazo ya furaha sura ikaingiwa na mashaka alionekana kukumbuka kitu ambacho kwa kasi ya ajabu kilianza kuififisha furaha yake mfano wa matone ya damu yanapo ingia katika glass ya maji. “Ohh comon what this? Ohh shit” alijikuta akijisemea peke yake kwa sauti ndogo ya kunong’oneza na kisha akajishika kichwa akijutia jambo. ‘Inamaana nitakuwa nimeharibu…ohh nimejiharibu’ Shalon alijikuta akijishika kichwa kwa mikono yote miwili huku akiwa katika siti ya nyuma katika Taxi aliyokuwemo.

Mara alishtushwa na sauti ya dereva huyo “Binti tayari tumefika” aliongea tax drever “Ohh asante alifungua pochi yake na kutoa noti za elfu kumi kumi takribani tatu chap chap na kumpatia dereva ambaye alizipokea akiwa katika siti yake na kuonekana kama mtu aliyepatwa na mshangao sana baada ya kuzipokea akizitazama mdomo kauachama kisha Shalon huyo akafungua mlango na kutoka. “Binti samahani” Haraka Dereva akatoka garini huku akiwa ameshikilia note za elfu kumi kumi mbili, wakati huo Shalon alikuwa akitembea taratibu akielekea katika lango la Restaurant hiyo huku akiwa bize na simu akiandika andika mara akashtuka alipo shikwa bega. “Samahani umenizidishia pesa binti…makubaliano yetu yalikuwa ni elfu kumi na sio elfu thelathini, shikaa” Dereva akaunyoosha mkono wake wa kuume ukiwa na pesa akizielekeza kuzirudisha kwa Shalon. “Oghh…” Shalon aligutuka na kujishika kichwa kwa mkono wake mmoja mmoja ukiwa umeshikilia simu hand bag ikining’inia kwapani kuonesha alikuwa amevurugwa na mambo Fulani, kisha akatabasamu huku akimtazama “…asante usijali, chukua tu tumia, ni zako”, Shalon aliongea na kulitoa tabasamu. “Kweli! asante sana Binti” Dereva akiwa na macho yenye furaha alitoa shukran zake akizishikilia pesa kwa mikono miwili. “Unaweza nipatia namba zako na jina lako nitakuwa nakutumia mara kwa mara umekuwa muaminifu sana” Shalon aliongea huku akiendeleza tabasamu lake “Ohh asante sana binti niite Mzee Kidevu au kidevu inatosha… namba zangu ni 065832…” alimalizia Dereva huyo na Shalon naye akimalizia kusave namba hizo katika simu yake ya mkononi kisha wakaagana na Dereva akaondoka zake akiwa ni mwenye furaha sana na kumuacha Shalon na hamsini zake.

Zaina Resataurant, Ukonga – Dar es Salam
Shalon akasogea zaidi na kuingia katika Restaurant. “Shalon mbona umechelewa sana jamani unajua Mzee amekutafuta hujapokea kanipigia simu hapa nikamwambia umeenda Toilet aisee siku moja nitashtukiwa uongo huuu itanikosti sana” bwana mmoja alimvamia Shalon kwa lawama pindi tu alipoingia. Shalon alionekana kumtazama tu bwana huyo akioneakana kuchoka malalamiko hayo. “James sikia sipendi kubanwa banwa we si nakulipa na baba anakulipa mshahara basi endelea kutulia mi nitampigia baba nikitaka sawa”. Shalon aliongea na kusogea pahala inapo tolewa huduma ya chakula aliongea vitu Fulani na muhudumu wa hapo kisha akapatiwa mfuko Fulani huyo akarudi sehemu alipo kuwa amesimama bwana James akamtizama kwa muda kisha akaongea “Twende zetu home” Shalon aliongea na kuongoza nje na kumuacha James akitingisha kichwa kwa masikitiko kisha huyo akatoka kumfata.

Bunju, Kinondini -Dar es Salam
Nyakati za usiku, Shalon akiwa yumo chumbani mwake kajikalia kitandani mkononi ameshikilia simu yake akiperuzi katika baadhi ya mitandao ya kijamiii kichovu chovu alingia Facebook akatoka akaingia twiter mwisho akamalizia Instragram lakini hakufurahia kama siku zingine inavyokuwa. Shalon aliitambua hali yake haikuwa sawa na alitambua kinachomfanya awe hivyo suluhisho alilo liona ni kumpigia simu Salimu na kuongea naye. Maamuzi hayo yalionekana kupigwa vita na akili yake. Sasa ikawa vuta nikuvute akitaka kutuma meseji anaona sivyo akiona kupiga simu ndiko sahihi pia nafsi inakataa. Alipo kuja tahamaki tayari ilikuwa ni saa tatu na robo usiku hiyo saa aliisoma kupitia simu yake ambayo alikuwa ameishikilia mikononi wakati huo wote huku amevalia kigauni cheupe chepesi chenye kuonesha maumbile yake ya ajabu aliyoumbwa nayo, hakika alikuwa ni mrembo. Shalon akakitazama chumba chake chenye hadhi kubwa kutokana na kupambwa vitu vya thamani kubwa sana, alijiona ana kila kitu katika maisha lakini alipungukiwa mtu anaye mpenda sana ndiye aliye kosekana pahala hapo. Shalon aktoka kitandani na kusimama akaiweka simu yake katika kitanda kisha kavua kigauni chake cheupe alichokuwa amekivaa kwa mataharisho ya kulala. Shalon akaanza kupiga hatua fupi fupi akisogelea kabati kubwa lililo jengewa kwa ustadi katka ukuta lililo na kioo kikubwa kinacho weza muonesha mtu kuanzia chini mpaka juu. Shalon akasimama na kuanza kukitazama kifua chake kilicho jaa vizuri na kuziacha chuchu zake zilizo simama kupendeza akaipandisha mikono yake kukagua kifua chake hicho kisha akatabasamu ‘Shalon your so beutyfull’ alijiongelea nafsini aliyatoa macho yake katika kifua na kuja katika maeneo ya kiunoni ambapo kulikuwa na kitovu kilicho tumbukia na cheni ya rangi ya dhahabu ikiwa imepita kiunoni. Shalon alikitazama kiuno chake chembamba akakishika kwa mikono yake na kujigeuza geuza akijaribu kutazama vizuri hips na miguu yake iliyo nona vizuri pamoja na shemu zake za nyuma. ‘Sizani kama na weza kuonekana si vutii mbele ya Salimu nampenda sana’ aliongea tena nafsini kisha akageuka kurudi pahala peney kitanda akapanda kitandani kisha akajilaza huku akiwa ni mwenye ujasiri wa kutosha na sio uwoga tena kama awali.

ITAENDELEA....
 
The Hidden Truth ( Ukweli Uliofichika)

Nani Anahusika???!!

Mtunzi : Akida Siri Rambao
Contact : 0658328596
Email : akidasiri@gmail.com

MSIMU WA PILI

SEHEMU YA 5 F: PENZI

Tuendelee...

Shalon ni msichana anayechukua elimu yake katika shule ya Horizon International High scholl katika mchipuo ECA huko South Afrika alikuwa akisumbuliwa sana na vijana wengi hata watu wazima wenye familia zao wengi wakija na dau kubwa kumlaghai kimapenzi lakini hakuwahi tetereka juu ya vijana wale wakizuru, wanijeria na wengineo walio kuwa wakitoka mataifa mbali mbali kwa ajili ya masomo shuleni hapo. Alichokiweka mbele ni ufaulu na malengo kwanza.

*****

“My Hero” aligota katika jina hilo kwenye kioo cha simu yake kisha akaanza kuandika jumbe fupi na kuanza kuusoma kwa sauti. “Habari za usiku huu, vipi mliweza kufika salama?” ‘Ni sawa’ alijiwazia kukubaliana na alichokiandika kisha akatuma.

Wakati huo Shalon akiwa kasha tuma ujumbe wake wa maneno kwa Salimu, Salimu yeye alikuwa yumo kitandani kajilaza akisoma kitabu cha Riwaya kilichoitwa “she is with me” kilichoandikwa na Jessica Cunsolo ambacho alikuwa akikisoma mara nyingi anapokuwa ametulia kukitumia kama sehemu ya burudani kwake. Salimu aligeuza shingo baada ya kushtushwa na kamlio ka ujumbe wa sauti na kuichukua simu yake iliyokuwa juu ya meza ya mbao na kufungua nakuusoma ujumbe aliotumiwa. Salimu alitabasamu kivivu kisha akaandika na yeye alafu akautuma kwa Shalon baada ya hapo akajilaza na kuendelea na shughuli yake ya awali. Shalon alipokea ujumbe wa maneno akaufungua haraka haraka “Habari ni njema Shalon, tulifika salama na hapa tupo zetu school” aliusoma ujumbe huo Shalon akatabasamu kisha akatazama dari kama ni mtu anashukuru. “Ohh mnasoma level ipi ya elimu kwani” akautuma ujumbe huo. “Tupo hapa Kibaha High school kidato cha tano” ‘waoo nimefurahi sana kulijua hili’

Basi mambo yakawa ni kuchat walichat na kuendelea kuchat sana mpaka saa tano amapo Salimu muda wa maongezi ukamuisha. Shalon akaamua kutumia fulsa hiyo kumpigia na mazungumzo yakaendelea. “…ndio nimejisikia vibaya sana Salimu nimejikuta nikieleza hisia zangu kwa ghafla sana kitu ambacho mi mwenyewe sikukitegemea nikajiulaumu na kujilaumu hadi sasa” Shalon aliongea wakati huu akiwa amekumbatia doli kubwa la rangi ya pink “Ni sawa pole ndivyo inavyokuwa kuna wakati mambo huzidi na kujikuta mtu ukikosa uvumilivu inatokea…” ikasikia sauti ya Salumu baada ya kuweka laud spika “…Basi mi naomba nikutakie usiku mwema Salimu na am so sorry for waste your time, naomba tuendelee kuwasiliana na penda kuwa karibu nawe toka leo napenda kukitumia kipindi hiki cha likizo walau niwe karibu nawe”, aliongea Shalon kwa mapozi na sauti legevu ya kudeka “Usiwe na wasiwasi Shalon nawe ulale unono”. ‘Nimeona tu aibu tungeongea mpaka kukuche’ Shalon alijisemea nafsini nakujilaza chali bado akiwa utupu wa mnyama.

Kibaha High School, Kibaha - Mkoa wa Pwani

Siku iliyofuata asubuhi, Salimu na Karimu wakiwa wanaendelea na maandalizi ya safari ya Bagamoyo Salimu alitumia fulsa hiyo kumuhadithia Karimu kila kitu kuhusu usiku wa jana yake ulivyokuwa wakati mwenzake huyo alipo kuwa hoi kwa usingizi huku ya Bagamoyo. “Ebwana wee, duuh! mi najua tu wewe bado muoga ila utakuwa unampenda hilo ndilo ninalo amini”. Salimu alimtazama Karimu kisha akasikitika. “Kaka sijui lakini mi siwezi kukubishia maana we mwenzangu mzoefu lakini mi hata sielewi kweli ni binti mrembo na mzuri hata nikimkumbuka najikuta namtamani lakini sikufichi simuoni moyoni mwangu labda kwa sababu ya lile tukio au…lakini hapana tangu hata sijamuongelesha nilihisi kusisimka mwili mfano wa mtu anapo kutana na simba mwituni nilihisi uoga” Salimu aliongea na kuacha kukunja nguo. “Hhahhahaaha….kaka inamaana unamaanisha nini mbona sikuelewi mzee?” Karimu akiwa na macho ya mshangao nayeye aliacha kupiga kiwi viatu na kumtazama Salimu. Salimu akaongea “…yani kaka mfano mtu aliyesikia habari za kushtua au …enhee ni kama mtu anapo patwa hisia za tatizo anavyo hisi basi ndivyo nilivyokuwa siku ile sema nilishindwa namna ya kuielezea kwako siku ile ya masimulizi” Salimu alimaliza huku akimtazama Karimu kwa jicho la kuthibitisha akisemacho. “Duuuh, mzee au ni mchawiii ahh haiwezekani we bwana utakuwa hujazielewa hisia zako tulia uzisome vizuri achana na kuendekeza mawazo ambayo sio we cha msingi kuwa flexible soft your heart and usikilize utaniambia siku moja, ila nakushauri endelea naye tu usimvunje moyo” Karimu aliongea kwa utulivu tena bila kituo.

Itaendeleaaa...
 
Sante sana mkuu yaani nipo road nikipaki kazi ni moja
 
The Hidden Truth ( Ukweli Uliofichika)

Nani Anahusika???!!

MSIMU WA PILI

SEHEMU 5 G : PENZI

....“Duuuh, mzee au ni mchawiii ahh haiwezekani we bwana utakuwa hujazielewa hisia zako tulia uzisome vizuri achana na kuendekeza mawazo ambayo sio we cha msingi kuwa flexible soft your heart and usikilize utaniambia siku moja, ila nakushauri endelea naye tu usimvunje moyo” Karimu aliongea kwa utulivu tena bila kituo.


Tuendelee...

.... Salimu alisikiliza kwa makini na kuyapa uzito maneno ya Karimu na kuahidi kuyafanyia kazi.

*****

Safari ilipowadia Salimu na Karimu wakaswagana hao wakaelekea zao Bagamoyo wakachukua magazeti karibia yote na kurudi nayo Kibaha. Waliamua kuimalizia likizo yao Kibaha kwa sababu maalumu wao hawakukabidhi chumba katika utawala waliomba kubaki kwa kudai wanafanya Tution kwa ajili ya maandalizi ya muhula mpya, walitaka kutumia likizo hiyo kusoma taarifa zote zinazo muhusu marehemu Bwana Richard kwa ufasaha na kuwatambua watu wake wakaribu na namna walivyokuwa wanaishi.

Hakuna ugumu walioupata kwa kweli kwa sababu hawakuwa na mtu ambae wangemgharimia kuhusiana na upelelezi wao huo zaidi ya magazeti ambayo asilimia kubwa yalimuelezea bwana Richard kwa ufasaha “Natamani sana kuonana na shangazi zangu lakini sitaweza, najiskia vibaya sana Karimu” mara kazaa aliongea hivyo na kumfanya Karimu asawajike “Hakuna marefu yanayokosa ncha” Karimu alimliwaza. Wiki za mwanzo mwazo tayali walikuwa na habari nyingi za marafiki na jamaa wakubwa wa marehemu Richard na habari zao kuhusu familia zao zilivyo na namna wanavyoishi.

Waliona mambo mengi ikiwemo kifo cha mke wa Samuel aliyefariki kwa kusemekana alianguka bafuni, wakaliona jina la Shalon akiwa ndiye mtoto pekee wa Samuel katika kipindi chake chote cha maisha. Kuna mambo mengi waliyagundua kupitia magazeti yale ya muda mrefu. Moja ya mambo hayo ni kufifia kwa mahusiano kati yao ya Samuel na Pater dhidi ya Richard. Walidadavua wakanyambua vichwani mwao mashaka juu ya watu wawili ambao ni Samuel na Pater yakawaingia akilini, waliwashuku marafiki hao kuwa huenda wakawa wanahusika na kifo cha bwana Richard. Waliamini kuwa wivu tu na roho mbaya katika maisha ndio vinavyopelekea usaliti mafarakano na mauaji baina ya watu wakaribu kama ndugu na marafiki na isitoshe kikulacho kinguoni mwako, huo ndio mwanzo walio upata.

Mioyo na tamaa ya kuwa mapolisi ilionekana wazi ikiwa imetawala katika vifua vyao walishiba imani ya uchungu kesi iliyotupwa mbali mika mingi iliyopita, hawakuwa na sifa za kitaaluma zinazowafanya wawe wapelelezi tayali lakini taratibu zao pamoja na mbinu zao ziliwapa moyo wa mafanikio siku moja.

Itaendelea...
 
The Hidden Truth ( Ukweli Uliofichika)

Nani Anahusika???!!

MSIMU WA PILI

SEHEMU 5 G : PENZI

....“Duuuh, mzee au ni mchawiii ahh haiwezekani we bwana utakuwa hujazielewa hisia zako tulia uzisome vizuri achana na kuendekeza mawazo ambayo sio we cha msingi kuwa flexible soft your heart and usikilize utaniambia siku moja, ila nakushauri endelea naye tu usimvunje moyo” Karimu aliongea kwa utulivu tena bila kituo.


Tuendelee...

.... Salimu alisikiliza kwa makini na kuyapa uzito maneno ya Karimu na kuahidi kuyafanyia kazi.

*****

Safari ilipowadia Salimu na Karimu wakaswagana hao wakaelekea zao Bagamoyo wakachukua magazeti karibia yote na kurudi nayo Kibaha. Waliamua kuimalizia likizo yao Kibaha kwa sababu maalumu wao hawakukabidhi chumba katika utawala waliomba kubaki kwa kudai wanafanya Tution kwa ajili ya maandalizi ya muhula mpya, walitaka kutumia likizo hiyo kusoma taarifa zote zinazo muhusu marehemu Bwana Richard kwa ufasaha na kuwatambua watu wake wakaribu na namna walivyokuwa wanaishi.

Hakuna ugumu walioupata kwa kweli kwa sababu hawakuwa na mtu ambae wangemgharimia kuhusiana na upelelezi wao huo zaidi ya magazeti ambayo asilimia kubwa yalimuelezea bwana Richard kwa ufasaha “Natamani sana kuonana na shangazi zangu lakini sitaweza, najiskia vibaya sana Karimu” mara kazaa aliongea hivyo na kumfanya Karimu asawajike “Hakuna marefu yanayokosa ncha” Karimu alimliwaza. Wiki za mwanzo mwazo tayali walikuwa na habari nyingi za marafiki na jamaa wakubwa wa marehemu Richard na habari zao kuhusu familia zao zilivyo na namna wanavyoishi.

Waliona mambo mengi ikiwemo kifo cha mke wa Samuel aliyefariki kwa kusemekana alianguka bafuni, wakaliona jina la Shalon akiwa ndiye mtoto pekee wa Samuel katika kipindi chake chote cha maisha. Kuna mambo mengi waliyagundua kupitia magazeti yale ya muda mrefu. Moja ya mambo hayo ni kufifia kwa mahusiano kati yao ya Samuel na Pater dhidi ya Richard. Walidadavua wakanyambua vichwani mwao mashaka juu ya watu wawili ambao ni Samuel na Pater yakawaingia akilini, waliwashuku marafiki hao kuwa huenda wakawa wanahusika na kifo cha bwana Richard. Waliamini kuwa wivu tu na roho mbaya katika maisha ndio vinavyopelekea usaliti mafarakano na mauaji baina ya watu wakaribu kama ndugu na marafiki na isitoshe kikulacho kinguoni mwako, huo ndio mwanzo walio upata.

Mioyo na tamaa ya kuwa mapolisi ilionekana wazi ikiwa imetawala katika vifua vyao walishiba imani ya uchungu kesi iliyotupwa mbali mika mingi iliyopita, hawakuwa na sifa za kitaaluma zinazowafanya wawe wapelelezi tayali lakini taratibu zao pamoja na mbinu zao ziliwapa moyo wa mafanikio siku moja.

Itaendelea...
Sasa mawazo ya Salimu na Karimu Ni sahihi au laa

Nani anajua Kama malengo yao yatatimia???

Ili kujuaa tuendelee kufatiliaa kwa kina
 
The Hidden Truth ( Ukweli Uliofichika)

Nani Anahusika???


SEHEMU YA 6 A: UPELELEZI

“Wakati hatua za kipelelezi zikiendelea kuchana mbuga kila uchwao, mtu asiyejulikana anaonekana akiwa nyuma akifata hatua zao, Salimu na Karimu wanafanikiwa kugundua nyendo za watu waliohusika na mauji ya familia yake. Wakiwa mgahawani wakifatilia hatua za maadui zao timu ya Meroda inaonekana kuwepo eneo hilo hilo. Je! kuna usalama?”

Katikati ya Jiji -Dar es Salam

Siku ya matembezi ilifika vijana waliambatana wakaingia katikati ya jiji moja kwa moja katika maeneo ya mgahawa ule ambao uliwatoa mbio miezi kazaa nyuma. Walienda wakaenda wakaenda tena na tena kila siku wiki ikakata hawakupata hata vumbi la upelelezi wao.

Kalimu imani ikaanza kumtoka alianza kuhisi kupoteza muda kitu ambacho kwa Salimu kilikuwa hakipo bado matumaini mengi alikuwa nayo moyoni na hakuvunjika moyo “Kaka sikiliza siku ile ilikuwa kama ajari tu kaka kuwakuta pale naonelea tutafute njia nyingine mbadala nahii”. Kalimu sikilza kaka unajua natambua jinsi gani kazi hii ilivyokuwa ngumu, lakini tuvute subra tuzile mbivu” Salimu alitoka katika kitanda na kusimama na kuanza kupiga hatua fupi fupi akimfata Karimu alimshika bega “Kaka nahitaji sana msaada wako nakutegemea sana” Karimu alimtazama Salimu kwa hisia za huzuni kisha akampa mkono kuonesha kukubaliana nae kisha hao wakashika njia wakitembea.

*****

Siku zote hizo za tafiti za kina Salimu na nduguye zikifanyika bwana mmoja mtumzima tena shupavu aliyeonekana Kibaha High School miezi kazaa iliyopita akitoka na bahasha kwenye ofisi ya mkuu wa shule alikuwa nyuma yao tangu siku ile. Mara kazaa alionekana akiongea na mlinzi wa shule hiyo wakati mwingine akimpatia makaratasi Fulani. Nyakati zote hizo bwana huyo alionekana ni mtu anaependa sana kwenda na muda na akiwa makini sana na jambo analolifanya. Wakati mwingi alionekana akipokea simu na kuzijibu na kupokea nyingine kokote pale atakapo kuwa.

Itaendeleaaa

mambo yameanza kunoga
 
The Hidden Truth ( Ukweli Uliofichika)

Nani Anahusika???!!

MSIMU WA PILI

SEHEMU 6 B : UPELELEZI


Ilipoishia...
....mwingi alionekana akipokea simu na kuzijibu na kupokea nyingine kokote pale atakapo kuwa.

Tuendelee...

Kariakoo-Dar es Salam

Bwana asiyejulikana ni nani ambaye haaishi kufatilia nyendo za kina Salimu siku hiyo akiwa na muonekano wa vijana wa mjini akawa chekibobu haswa. Mara mwendo wake ukawa ni wakuvizia akionekana akichungulia pembeni ya gari moja iliyo egeshwa mita chache karibu na jengo la mgahawa akiwatazama kina Salimu wakitokomea ndani ya mgahawa huo. Bwana yule naye akatazama kulia kwake kidogo akapiga hatua kazaa na kumalizia kushoto kwake ambako ndiko kulikuwa target yake huyo akatoka kwa mwendo wa kawaida akielekea katika mgahawa huku akiiweka miwani yake ya rangi vizuri.

“Karibuni sana tuwahudumie nini” mwanamke wa makamo alisimama pembeni yao akiwa amevalia sale spesheli kabisa akiwatazama Salimu na Karimu kwa nyuso ya furaha vijana walitazamana. “Ohh sawa, kuna vitafunwa gani” “Hahaaaa…” muhudumu alicheka kidogo na kujiziba mdomo kwa mkono wake wa kuume. “Vipi anti mbona unatucheka?”, kwa aibu akijizuia kuendelea kucheka huku tabasamu lake likiendelea nyusoni. Wakati huo huo bwana yule teyari alikwisha ingia akatafuta kipembe na kuweka kambi.

Yule mhudumu baada ya kujizuia zuia cheko yake aliendelea “Hapana mmenikumbusha mbali tu jamani namna mlivyotamka vitafunwa wala hakuna la ziada…Menu hii yapa mnaweza chagua mkitakacho Karibuni sana” Muhudumu aliwaonesha kijarida kidogo cha orodha za vyakula kilichokuwa kipo mezani hapo na kuendelea kusimama akisubiri. Salimu alikuwa wakwanza kupitisha macho akachagua na Karimu akafuata muhudumu akatoweka pahala hapo na kuwaacha wakisubiri.

Kipindi hicho bwana yule kwa jicho makini aliendelea kuwatazama. Haikuchukua muda Muhudumu aliwasulisha mahitaji katika meza ya kina Salimu na kuondoka. Walikunywa chai kwa pozi taratibu maana walijua lililowapeleka hivyo hawakuwa na haraka mwisho wakamaliza wakalipa gharama zao kisha wakatulia macho sasa yakawa katika Flat screen iliyo mbali kidogo na walipo wakitazama taarifa ya habari toka katika kituo cha CNN. “Kaka unajua leo tumejitoa kimasommaso haswa baada ya karibia mwezi mzima tukivizia tu pale kwa mshona viatu tukiondoka kapa?” “Ni kweli ndugu ila kwa muda mfupi tumejikuta tukiyajua mambo mengi kupitia ubishi wa pale kwa mzee chongo muhuza magazeti tukibishana mambo ya mpira na siasa lakini tunapata taarifa nyingine mpya za huu mji” Salimu aliongea “Ni kweli Kaka nafkiri ndio maana leo tumeamua kujitoa kimaso maso huenda tukapata kitu”. Waliongea mawili matatu huku muda ukiyoyoma waliagiza maji wakabadili mikao huku macho yakiwa wazi kuwafatilia wanao ingia na kutoka katika mgahawa huo.

Mezani kulikuwa na gazeti la The Gardians na Mwananchi walipokezana kulisoma wakasoma hadi matangazo ya viwanja na nyumba huku wakiendelea kuchunguza hali ya hewa ya mgahawa huo. “Kaka saizi unajua saa sita na dakika tano bado tupo tu hapa” Karimu alikunja sura akionekana kuchoka aliliweka gazeti mezani huku akimtazama Salimu, “Najua lakini tusubiri tu kaka nahisi kuna jambo linakuja tusubiri” Karimu akatazama pembeni hasira zikiwa zimeanza kumpanda “Sawa” Karimu aliuma meno kwa nguvu.

Baada ya vijidakika vichache kupita ikaonekana gari nyeusi ikiingia na kupaki katika sehemu ya maegesho. Salimu alimkanyaga...

Itaendeleaaa...
 
The Hidden Truth ( Ukweli Uliofichika)

Nani Anahusika??

MSIMU WA PILI

SEHEMU YA 6 C : UPELELEZI

Ilipo ishia...
Baada ya vijidakika vichache kupita ikaonekana gari nyeusi ikiingia na kupaki katika sehemu ya maegesho.

Tuendeleee...

Salimu alimkanyaga Karimu mkanyago wa tahadhari na kumfanya aache kuikodolea simu yake na kumtazama Salimu kwa mshangao Salimu alimpa ishara atizame nje ya vioo vya madirisha, Karimu aligeuka kiaina na kutazama kwa kuiba iba nae alishuhudia likiwa ndo linamalizikia kusimama macho yalimtoka akamgeukia Salimu akisubiri maelekezo. Salimu alimpa ishara nyingine kwa mkono kuwa atulie kama maji mtungini nae akatulia tuli. “Sinilikwambia” Salimu alinong’ona. Wanaume wanne waliovalia suti nyeusi tii machoni miwani meusi vichwani wakiwa wamenyoa vipara kasoro mmoja wao tu amabe alionekana kuwa na nywele nyingi wakishuka garini na sasa wakielekea katika mlango mkubwa wa mgahawa huo.

Wanaume hao wa kazi walipo ingia walisogea hadi katika sehemu ambayo palionekana kuandaliwa kwa ajili yao wakakaa, sehemu waliyokaa haikuwa mbali na walipo kina Salimu na kuwafanya kuwaona vizuri. Nje ya Mgahawa gari nyingine aina ya………….ilionekana ikingia Salimu aliiona pia akamshtua Karimu ajionee walishuka wasichana watatu ambao waliingia na kukaa upande mwengine ulio wafanya kutengeneza makundi matatu na alama ya pembe tatu. Salimu aliwaangalia kwa makini huku akiwaza, kabla Salimu hajapata jibu la aliwazalo alionekana mzee mmoja mrefu mwembamba akitokea katika upande wa jikoni huku akiangaza angaza akatazama upande ambao waliketi kina Meroda akatoa ishara ya kutingisha kichwa na Meroda naye alifanya hivyo wakati huo kwa jicho pancha Salimu aliuona mchezo huo na akatulia tuli kama maji mtungini.

Mzee huyo akaendelea kutupia macho huku na kule kama mtu anaejilinda asionekanne na mtu huku akipiga hatua za kawaida kuelekea katika meza ambayo wanaume wa kazi walikuwa wamefikia na kujikalisha wakiendelea kunywa vinywaji vyao walivyoagiza punde tu walipo fika. Salimu aliendelea kuwaza kwa dakika kama tatu hivi bila kumshilikisha Karimu hiyo yote ni kwa sababu ya uwoga wa kushtukiwa nyendo zake, aliwaza akaona isiwe shida akakivunja kimya “Kaka ngoja nikaagize Soda usifanye kitu tofauti” Salimu akanyanyuka na kuelekea sehemu ambayo palikuwa na huduma ya vinywaji akienda kwa kupita upande ule wa wale jamaa anaowapeleleza.

Karimu kwa upande wake alishindwa hata kuitikia maana ilikuwa kama tukio la kushtukiza aliamua kumsindikiza tu kwa macho mdomo ukiwa wazi kama vile mtu ambaye hakusikia au amesikia lakini hajaelewa. Salimu alipo kuwa anakaribia kuipita meza ya wahusika wake alisikia mmoja wao akisema “…Sweet Super Market…”


Itaendeleaaa...

Kuna usalama? Kina Salimu watafanikiwa kupata wanachokitaka na kutoka salama????
 
The Hidden Truth ( Ukweli Uliofichika)

Nani Anahusika???

MSIMU WA PILI

SEHEMU 6 D : UPELELEZI

Ilipoishia...

...Salimu alipo kuwa anakaribia kuipita meza ya wahusika wake alisikia mmoja wao akisema “…Sweet Super Market…”

Tuendelee...

Salimu alihefadhi jina hilo akaenda kwa mwendo ule ule mpaka alipo pakusudia na kuchukua soda mbili na kurejea nazo safari hii masikio akiwa kayatega vizuri kunasa habari nyingine “…eee lazima iwe saa mbili usiku na sio vinginevyo…” alipo karibia kukatiza tu sauti nyingine ikasema “…ndio ni kesho…” Salimu bila kuonesha badiriko lolote la kimwili kwa mwendo wake ule ule akafika pahala pake huku akizuga kwa stori ambazo hazikuwepo pahala hapo kitu ambacho Karimu kwa haraka alikielewa naye ikampasa ashirikiane nae katika maongezi yaliyokosa mwanzo wake. “Tulia hivyo hivyo tuwe wapole” Salimu aliingiza katikati ya maongezi yao yasiyokuwa na mwanzo.

Wanaume wa kazi baada ya kumaliza maongezi yao walinyanyuka wakampatia mkono wa kwaheri mwenyeji wao kisha wakaondoka zao kabisa katika eneo hilo.

Baada ya dakika tano kupita “Kaka twende zetu au vipi” “Tusubiri kama lisaa hivi ndio kisha tuondoke” Karimu uchovu ulimjaa alibaki kusikitika tu akaitika kishingo upande. Salimu alimuonesha Karimu wasichana warembo kwenye moja ya kona Karimu aligeuka kutazama akacheka kidogo “Umenichangamsha kaka, Unajua siku hizi sikuelewi usiniambie ushampenda mtu” Salimu alicheka kidogo “Hakuna natamani tu kuungana nao meza moja” “Basi Twende zetu tusilaze damu ikaganda hahahaha” Karimu tayari alishasimama yu tayari kwa kwenda tabasamu likiwa usoni maana alipenda sana kukaa karibu na wasichana na kubadirishana mawazo wakizubaa zubaa anapita.

Hivyo jambo hilo lilimfurahisha sana na kusahau yale yaliyo muudhi dakika kazaa zilizo pita. Salimu naye akanyanyuka kitini wakabeba glass na soda zao wakaanza safari kuwafata warembo konani. “Habari zenu wadada” Karimu alichombeza kwa uchangamfu “Salama tu” Meroda ndiye aliyekuwa wa kwanza kuitikia na wenzake wakafata maana nyakati wanashauriana nampaka wanapiga hatua za kuja Meroda yeye alisha tambua sikunyingi ugeni huo.

Basi mazungumzo yao yakaendelea kana kwamba hakuna kitu chochote kilicho ingia kati yao. “Samahani, tuna weza kujumuika nanyi meza moja?” Salimu ndiye aliyezungumza safari hii mkononi kashikilia glass na mkono mwingine chupa ya soda ya PEPSI kwa sauti yake ya asili yenye bezi, Samira na Monica waligeuza shingo kumtazama Meroda kiongozi wa timu kusikiza atasema nini kabla ya wao kuamua kitu. Meroda akaacha kuchati akanyanyua sura kuwatazama hao vijana waliosimama pembeni yao kwa mara nyingine tena...


Itaendeleaaa...

Itakuwaje tunajua wasichana walio wasogeleaaa sio wasichana wa kawaida Itakuwajeee
 
The Hidden Truth ( Ukweli Uliofichika)

Nani Anahusika???

MSIMU WA PILI

SEHEMU 6 E: UPELELEZI

Ilipoishiaa...
Meroda akaacha kuchati akanyanyua sura kuwatazama hao vijana waliosimama pembeni yao kwa mara nyingine tena


Tuendelee...

.... huenda sauti hiyo ya pili ya kiume haswa ilimvutia, alitoa miwani machoni mwake na hamadi bin vuu macho yake yakakutana na ya Salimu ilistaajabisha Meroda ilimbidi atulie sekunde kazaa bila kujielewa akitazama tu akili ikahama kwa muda maana alichokutana nacho sijui kilikuwa na uchawi gani maana kilimshangaza. Akili ilipo rudi akaachia tabasamu na akawatazama wenzake kwa aibu ambayo aliishia kuificha ficha nayo ikakataa kufichwa ikadhihirishwa macho yake makubwa.

Samira na Monica wala hawakuhitaji kuelezewa waliona kitu katika macho ya kiongozi wao chenye hisia za penzi changa “Ohh mnakaribishwa karibuni mkae” wenzake walimtazama kwa mshangao mwengine. “Naitwa Karimu na huyu rafiki yangu ndugu yangu pia anaitwa Salimu ni wanafunzi wa kidato cha sita tunatarajia kufika elimu ya ngazi za juu siku za usoni” Karimu aliongea huku akizungusha glass yake kwa madaha, macho yakipita zamu kwa zamu kwa wasichan wote “Ohh vizuri…” Meroda aliiacha kabisa kuchati akaiweka simu mezani. “Naitwa Meroda, huyo ni Samira na huyo hapo ni Monica ni marafiki kama ndugu pia” “Hahaaaha kwa hiyo tunafanana kiasi” Karimu alijichekesha kidogo akimpiga piga bega Salimu la kumaanisha ‘umeona vitu hivyo mzee’.

Upande Samira na Monica bado walipatwa na sintofahamu inakuwaje Meroda akijitambulisha kirahisi kwa watu hao pasina kuwajua vizuri na sio kawaida yake!!

Stori zikaaanza wakazipiga pale wakiongea na kucheka Samira na Monica nao wakajisahurisha na kuamua kuungana na Meroda katika mazungumzo na vijana hao. Stori zikanoga sana kiasi cha kuyafanya makundi yote mawili kufahamiana na kuzoeana kwa muda mfupi.

Chakula cha mchana kiliwakutia hapo hapo wakala pamoja na warembo hao huku Meroda macho yake yakiwa haya chezi mbali na sura ya Salimu akimtazama kwa aibu aibu kitu ambacho Salimu Alisha kitambua na kumfanya awe kama hajaona.

Nyakati za kuagana zilipo timu huku upande wa Meroda ukiwa wa kwanza kuhitaji ruhusa ya kuvunja mkutanao huo Meroda akajikuta akizitoa namba kwa salimu na kufanya badilishano naye wazi wazi huku akiwa amejawa na furaha isiyopimika kwa mzani

Itaendelea...

Mambo ni

Sijui unawaza nini ndugu msomaji

Kama ni mfatiliaji najua utakuwa una picha umetazamia kutokea
 
The Hidden Truth ( Ukweli Uliofichika)

Nani Anahusika???

Mtunzi Akida Siri Rambao

MSIMU WA PILI

SEHEMU 6 F : UPELELEZI

Ilipoishia...

Meroda akajikuta akizitoa namba kwa salimu na kufanya badilishano naye

Tuendelee...

....wazi wazi huku akiwa amejawa na furaha isiyopimika kwa mzani wa kawaida kwa uzito wake. “Mzee wa kazi leo tumefanikiwa mission yetu asilimia 90 nitakwambia jioni tukitulia kwa namna gani mekuwa hivyo” Salimu aliongea huku akiwa anatabasamu mkono mmoja ukiwa mfukoni mwa suruali yake ya kitambaa akitembea kwa majivuno “Sawa ndugu yaani hapa nikifika nilale tu kwanza maaana si kwa uchovu huu, iladaah nimekuoneawivu na yule dada anaitwa nani vile hahaha?” Karimu aliongea huku akijinyoosha mikono kwa mbele. “Hahahhaa acha ujinga wewe” Salimu aliongea huku akitangulia mbele kwa hatua Karimu akiwa nyuma, hao wakatokomea katika kona moja.

Bwana yule anayefata hatua za kina Salimu alishuhudia kila kitu akajikuta akicheka “Bingoooo” alijisemea na kunyanyuka kitini akijifanya anaulevi uliokuwa umeanza kuisha.

Kinondoni Road-Dar es Salam
Nyakati hizo hizo Monica na Samira walikuwa wakimtazama tu Meroda aliyekuwa kajiegemeza katika kioo cha gari akiwaza na kutabasamu peke yake katika siti ya mbele, wakati huo Samira akiendelea kuendesha gari akajikokholesha kikokhozi kilichomshtua Meroda akatoka mawazoni. “Dada naona leo umezidiwa na furaha ambayo hukuwa nayo miaka mingi” “Acha tu lakini wala siamini kama nikweli nina furaha au ni kivuli chake” aliongea kwa taratibu huku tabasamu likiwa bado usoni mwake akisugua sugua kichwa chake kwa kucha zake ndefu za mkono wa kushoto. “Itakuwa kweli hiyo na naamini upo penzini dada” Monica akiwa upande wa nyuma aliongeza la kwake “Haya ngoja tuone maana haijawahi nitokea tangu ilipo potea” Meroda aliongea na kubadili mazungumzo.

Kibaha High School, Kibaha - Mkoa wa Pwani

“Kaka hebu nijuze basi kama ulivyo niahidi uligundua nini pale mgahawani maana uliniambia tumefaulu kuna vitu sikukuulewa na sikukuuliza mpaka usiku huu” Karimu akanyanyuka na kuegemea ukuta macho yakiwa kwa Salimu akitazama “Hahaha sawa sawa ndugu yangu aisee upo makini sana wewe” Salimu akanyanyuka toka katika mlalo wa chali na kukaa kitako “…muda ule nakwambia kaka usiondoke tusubiri subiri kwanza nyakati zile wakati wameshaingia wale mabwana siunakumbuka? wale wa dada nao wakaingia na kwambia hisia zangu zikawa na mashaka na ujio wao nikatulia kuwafatilia kwa kijicho pancha…” Salimu kwa kitendo aliigiza kwa kuyabana macho yake huku Karimu akiendelea kumtazama “…unamkumbuka yule mzee aliyetoka na kuungana na wale majamaa?” “Ahhh ngoja…” Karimu akanyanyua kichwa juu akijaribu kuvuta taswira ya yule mzee mara akatabasamu “ yeaah naikumbuka sura yake vizuri sana” “Vizuri, basi kabla hajaungana na wale jamaa alipeana ishara na yule msichana Meroda” “Eeeeh…” Karimu alijikuta akishangaa kwa sauti macho yakimtoka kama kawaida yake na akabadiri mkao “Ahhh hapana Salimu hilo limenipitaje mzee?” Karimu aliongea tena lakini kwa sauti ya wasiwasi iliyochanganyika na mshangazo kisha akauziba mdomo kwa viganja vyake vya mkono.

“Nakwambia kweli nimeona kwa macho yangu mawili tena kwa utulivu wa akili yangu si kwa kupepesa” Salimu akaendelea na masimulizi. Kipindi hiki Karimu alizidiwa na uwoga



Itaendelea...

Inaonekana yule bwana anayewafatilia kina Salimu Kufurahia namna vijana walivyocheza mchezo bila kushtukiwa

Na kina Salimu wamegundua kuwa kina Meroda sio wasichana wa kawaidaaa

AKIDA%20S.%20RAMBAO%20%3D%20THE%20HIDDEN%20TRUTH%20(UKWELI%20ULIOFICHIKA)%20(2).jpg
 
The Hidden Truth ( Ukweli Uliofichika)

Nani Anahusika???

MSIMU WA PILI

SEHEMU 6 G : UPELELEZI


“Vizuri, basi kabla hajaungana na wale jamaa alipeana ishara na yule msichana Meroda” “Eeeeh…” Karimu alijikuta akishangaa kwa sauti macho yakimtoka kama kawaida yake na akabadiri mkao “Ahhh hapana Salimu hilo limenipitaje mzee?” Karimu aliongea tena lakini kwa sauti ya wasiwasi iliyochanganyika na mshangazo kisha akauziba mdomo kwa viganja vyake vya mkono. “Nakwambia kweli nimeona kwa macho yangu mawili tena kwa utulivu wa akili yangu si kwa kupepesa” Salimu akaendelea na masimulizi. Kipindi hiki Karimu alizidiwa na uwoga macho yakizidi kutumbuliwa huku Salimu akiendelea na masimulizi yaliyoendelea kumshangaza Karimu. “Wee Salimu! kwa hiyo huo utakuwa ni uvamizi huo mhh!...” Karimu mdomo akauwacha wazi mwaa! “…Kaka kwa kweli siku wezi ndugu yangu na unisamee kwa kila kitu sasa nimeanza kukuelewa, yani naamini kwa kipaji chako hiki siku moja ndoto zetu zitatimia tu, na unanifunza mengi sana.” “Sasa tujiandae kushuhudia uvamizi wa Super market hapo kesho hii ndio kazi yetu ya pili” Salimu kwa kujiamini aliongea kwa sauti ya kishujaa. “Lakini kabla ya yote naomba kesho uichore sura ya yule bwana aliyekuwa ameungana na wale jamaa kadri utakavyoikumbuka itatusaidia mbele ya safari” Sasa vijana hao wakaanza kupeana mikakati na namna watakavyo kaa karibu na tukio hilo, majadiriano hayo yaliwapeleka hadi saa saa nane za usiku kisha wakalala.

*****

Sweet Super Market haikuwa super market ya mchezo mchezo katika jiji la Dar laa ilikuwa Super Market ya kimataifa kwa maana wale tu wenye uwezo wa njuruku na sio pesa za madafu ndio walikuwa na fulsa ya kuingia katika super Market hiyo kupata huduma, pesa za kimataifa zilitumika sehemu hiyo bila shida.

Ilichukua eneo kubwa sana kiasi cha mita Khamsini kwa kwa khamsini tena ikiwa na wafanyakazi wengi ambao wanafanya huduma kuwa nyepesi, hakuna kilichokosekana ni agharabu sana kuona vitu vimeisha katika Surper Market hiyo sio jambo jepesi. Waarabu, whindi, wachina, wazungu na waswahili hasa viongozi wa serikali na wafanya biashara wakubwa wakubwa ndio waliothubutu kuingia katika eneo hilo kukidhi haja zao nakuondoka. Mmiliki alikuwa ni Mwarabu mmoja toka Yemen alianza kuchipukia katika biashara na kuanza kuja kwa kasi kutokana na kuwekeza sana katika jiji hilo la Dar es salam.

*****

Sweet Supermarket, Kariakoo- Dar es Salam

Saa moja usiku, teyali vijana walikuwa wameshawasili karibu kabisa na maeneo ya Supermarket, huku na kule wakiendelea kutazama mazingira vizuri wakachoropoka na kukaa katika eneo la ujenzi wa ghorofa na kujibanza katika moja ya mabao macho yakiwa kwenye supermarket.

Kwa nyatu nyatu za hali ya juu Bwana yule anaye wavizia kina Salimu bila kuoneakana uso wake alijibanza katika mti mmoja uliokuwa kama mita thelethini hivi akifatilia nyendo za kina Salimu. Dakika moja ilipopita akasogea zaidi pahala walipo ili aweze kuyajua zaidi yale yaliyo waleta eneo hilo. Salimu na Karimu Walipo kuwa wamekaa macho kodo wakitazama huku na kule kuhakikisha hawapitwi na habari,bwana yule tayari alikuwa kisha wakaraibia zaidi kiasi hata cha kuweza kuwavamia na kuwa kabili akiwa na bastola ndogo mkononi akiificha isionekane kupitia koti lake.

Itaendeleaa...

 
The Hidden Truth ( Ukweli Uliofichika)

Nani Anahusika???

MSIMU WA PILI

SEHEMU 6 H : UPELELEZI

Ilipoishia....

...bwana yule tayari alikuwa kisha wakaraibia zaidi kiasi hata cha kuweza kuwavamia na kuwa kabili akiwa na bastola ndogo mkononi akiificha isionekane kupitia koti lake.

Tuendelee...

Lakini wenyewe hawakuwa na habari ya kwamba nyuma yao walitembelewa na mgeni aliyekuwa akiwavizia.

Upande wa Surper Market wasichana wawili walionekana wakielekea katika lango bila kufahamika walitokea wapi maana machoni mwa Salimu ilikuwa kama mizuka. Komandoo na yeye alishuhudia hilo tukio tena yeye aliona kwa ufasaha kwa masaada wa darubini yake ndogo ya kisasa hii ni baada ya kuzitambua hisia za vijana hao zipo katika Supermarket ambayo ilikuwa kama mita sitini na tano au sabini toka pahala walipo. Salimu alikodoa macho vizuri tena akiyumbisha kichwa akitazama kwa msaada wa taa za mbele zilizokuwa zikimulika baraza kubwa zikisaidiwa na majengo jirani hisia za kuwatambua mabinti wale zilimjia mara akagutuka. “Haaa Karimu watazame wale wasichana sio Samira na Monica wale”. Salimu alinong’ona huku akimshika bega Karimu akimuonesha kwa kidole.

Karimu nae alikodoa macho kuwachunguza kwa makini, nae alipatwa na uduwanzi baada ya kuwa hakikisha kuwa ndio wale mabinti aligeuza shingo na kumtazama Salimu kwa wasiwasi. “Nini tena hiki jamani, mbona sielewi” Karimu aliongea kwa kutetemeka. Baada ya dakika kama tano hivi Samira na Monica walionekana kutoka wakiwa na mifuko iliyoonekana ina vitu ndani yake. “Afadhali naona watakuwa watu salama” Karimu alishusha pumzi na kushukuru “Subiri tuone”. Salimu alitia neno na kuendelea kutazama wakiwa kando mbali kidogo na Super Market Samira na Monica walisimamisha Tax wakapanda hao wakaondoka Karimu akaachia tabasamu kidogo “Umeona kaka?”

Vijana wakiwa bado wapo nje wakisubiria kuona lolote macho yakiwa katika Super Market, mara zilisikika sauti za kelele zikitokea upande wa Super Market, Salimu na Karimu walituliza masikio kwa makini maana hapakuwa na utulivu wakusikia vizuri kutokana na kelele za magari kutoka mitaa tofauti na kufanya kukosekana kwa usikivu mzuri.

Bahati ikawa upande wao wakagundua sauti za kelele zinatokea ndani ya Super Market haraka walinzi wawili waliingia ndani na kuwaacha wawili nje. Muda si mwingi walinzi walionekana wakitoka na mzee mmoja aliyeonekana kuwa na maradhi ya kuchanganyikiwa kutokana na maongezi yake na kutukana hovyo walimkabiri vema japo alionekana kuwazidi kuvu kutokana na kuyumbishwa muda wote wakijitahidi kumsukuma aondoke eneo hilo. Mzee yule alionekana kuendelea kugomaa akitaka kuingia tena ndani mara ghafla walinzi wawili walio kuwa wamesimama wakiwatazama wenzao wakimkabili yule mzee aliye changanyikiwa walionekana wakianguka mmoja mmoja na wale wawili walio salia nao wakaanguka. Kufumba na kufumbua kulia na kushoto walitokea vijana wawili na yule mzee aliyechanganyikiwa akarudi ndani. Machoni mwa Salimu na Karimu ilikuwa kama wanatazama movie za kizungu katika luninga walibaki midomo wazi.

Itaendeleaa...


 
The Hidden Truth ( Ukweli Uliofichika)

Nani Anahusika

Mtunzi Akida Siri Rambao
Contact : 0658328596
Email: akidasiri@gmail.com

MSIMU 2

Sehemu 6 I : Upelelezi

Ilipoishia...

...sukuma aondoke eneo hilo. Mzee yule alionekana kuendelea kugomaa akitaka kuingia tena ndani mara ghafla walinzi wawili walio kuwa wamesimama wakiwatazama wenzao wakimkabili yule mzee aliye changanyikiwa walionekana wakianguka mmoja mmoja na wale wawili walio salia nao wakaanguka.


Tuendeleee..

Kufumba na kufumbua kulia na kushoto walitokea vijana wawili na yule mzee aliyechanganyikiwa akarudi ndani. Machoni mwa Salimu
na Karimu ilikuwa kama wanatazama movie za kizungu katika luninga walibaki midomo wazi.

Dakika tano hazikupita tayali yule mzee alitoka huku akiwa kaambatana na mtu mwengine ambaye hakutambulika lika lake wakiwa na mfuko mweusi mkubwa pamoja na bastola ndogo mikononi. Walikimbia chap chap wakaingia kwenye gari ambayo ilikaa kwenye maegesho ya Super Market huku wenzao wawili wakiwafata.

Gari hiyo ilikuwa maeneo hayo muda mrefu tangu kina Salimu wafike, waliikuta lakini hawakuwa na A wala B kuhusu gari hiyo. Basi gari iliwashwa tayali kwa kuondoka baada watu wote kuingia ndani yake chapu chapu kona kali ilikatwa mafuta yalivutwa na kusababisha mlio mkali unaoumiza masikio gari hiyo ikaingia barabarani kwa spiidi kuu na kupotelea wanapopajua wenyewe huku watu ambao walikuwa wakipita na gari zao kukaa chonjo wakitukana na kujawa na mishangao maaana si kwa spidi hiyo. Wala haikuchukua muda mwingi watu hao hao na wengineo walio sehemu jirani na hapo wakashtushwa na kelele za watu zenye kuchanganyika na vilio, macho wakaya geuzi huko wakitaharuki kutazama kulikoni.

Salimu na Karimu walitulia tuli pale walijibanza kimya wakiendelea kushuhudia, si muda watu wapigao kelele walitoka mbio mbio waki andamana wamewehuka wakiliaa. “…Majambazi haoo…wezi hao…twafaaaa” kwa maumivu mikono ikiwa vichwani, lakini haikusaidia kitu zaidi watu walikusanyika vikundi vidogo vidogo vikatokea vikijadiri tukio hilo. Salimu na Karimu walibaki kusikitika tu wakajitoa mafichoni kwa tahadhari wasibainike waliporidhika hao wakashika njia na kuondoka zao. Bwana yule anayea wafatlia kina Salimu hakumaliza kazi yake akaaendelea na miondoko ya kuwafatilia nyuma nyuma.

Kibaha High School, Kibaha - Mkoa wa Pwani

Salimu akiwa yupo bize ubaoni akielekeza kundi la wanafunzi somo la Fizikia wakati huo huo Karimu hakuwa mbali akiwa anaongezea mambo mawili matatu, Salimu Salimu ikaanza kuita, akafanya utaratibu wa kuitoa katika moja ya mfuko wa suruali chapu chapu kabla haija kata na kukuta namba mpya akamtazama Karimu kwa mshtuko kidogo ambaye alikuwa pembeni hatua chache ameekaa katika kiti naye akimtazama. ““Samahani kidogo Karimu unaweza ukaaendelea nao” Salimu akiwa na macho yawaswasi aliomgea na kutoka darasani hapo nyakati hizo za jioni kuelekea nje huku akijiwaziia ni nani huyo anaye mtafuta, alipo ona amefika pahala aliporidhia kuongea akabonyeza kitufe cha kukubali simu hiyo nakuweka sikioni akisikilizia upande wa pili mara akasikia “Hallow…” sauti ya kike nyororo yenye utulivu ilipokelewa na masikio ya Salimu na ikamfanya sekunde chache kumshughulisha kufikiri kama alishawahi isikia pahala na kutaka kuifananisha lakini hola hakupata mtu ikabidi naye aitike , “Hallow” “Habari yako” “Nzuri tu…” “Samahani kwa usumbufu naitwa Meroda siku za nyuma tulikutana katika Mgahawa ule wa kiarabu tulikuwa wasichana watatu unakumbuka?” Salimu alionekana kupata mshituko mkubwa alimeza mate kwanza kutafuta ya kuongea lakini kabla hajatia neno lolote la kukubali au kukataa maongezi toka upande huo wa pili wa simu yakaendelea “…Usiku wa leo nitakupigia naomba usizime simu”


Itaendeleaa...
 
The Hidden Truth (Ukweli Uliofichika)

Mtunzi : Akida Siri Rambao
Contact : 0658328596
Email : akidasiri@gmail.com

MSIMU 2

Sehemu 6 J : Upelelezi

Tuendeleee...

...sauti ya kike ilisikika ikiongea Salimu akabaki kuitika akaitoa simu sikioni akiwa amechoka mikono ikiwa mikononi akijiwazia. Jasho jembamba lenye ubaridi lilionekana likimtoka nyuma ya sikio.

Alichokifanya nikujifuta kwa kitamba chake cha leso alichopenda kukiweka katika mifuko ya nyuma ya suruali na karudi haraka darasani kwa ajili ya kuendelea na majukumu aliyokuwa ameyakabidhi kwa Karimu.


USIKU
Salimu akiwa kajikalia kila muda akiitupia macho simu yake kama mtu anaye subiri kitu mara simu ikaita haraka akaipokea na kusikiliza upande wa pili akigeuka huku na kule akisimama na kukaa tena mwishowe yakaisha. “Mhhh…kazi ipo kaka” akajikalia zake kitandani “Ndugu yangu nishaapendwa na jambazi kama ulivyosikia!” Salimu wa watu alijikunyata na kukishika kichwa chake asijue la kufanya huku Karimu akiendelea kugonga taratibu ubao wa kitanda cha ghorofa yeye akiwa juu akitafakari kwa kina, mara Karimu alionekana kupata wazo, “Ndugu yangu nimeshapata wazo lakini ni la hatari kwetu sote”. Salimu taratibu alianza kukunjua mikono yake kichwani pia kuzikunjua ndita alizozikunja katika paji lake la uso na kukaa vizuri kwa nia ya kumsikiliza Karimu, “Mi naonelea mkubalie tu ili kazi yetu iwe rahisi”, Salimu akaachama mdomo huku akisikitika kwa kukitingisha kichwa kukataa “Ndugu yangu naona unataka tufe mapema haiwezekani, wale wanawake si wanawake wakuchezea unajua? hilo hapana tafuta wazo lengine…” Salimu aliongea na akakaa vizuri akaendelea “…Karimu sikia ingelikuwa wapo katika ngazi ndogo ningekubali lakini wale wanaonekana ni watu wanao heshimika sana na kauaminika pia” Salimu hali ya wasiwasi ilimzidi.

Haikupita muda taswira ya Meroda ilimjia kumkumbusha namna alivyokuwa akizungumza na kucheka na ule muonekano wake wa ajabu pumzi nzito zikamtoka, “Uhhh! kwanini yote yamekuja kwa mara moja?” Salimu alijisemea mwenyewe huku akitingisha kichwa juu ya kitanda, “Kaka mimi mwenyewe hapa nilikuwa najiuliza swali hilo hilo ndugu yangu”, Karimu aliongea akajivuta na kuegemea ukuta huku akimtazama Salimu. Wakiwa kimya kila mmoja akiwaza lake kamlio ka simu kuonesha ujumbe mfupi katika simu ya Salimu ulilia nae akajizoa hadi katika meza na kuichukua ilikuwa ujumbe wa Shalon, alisikitika kwa kichwa akajisogeza kitandani na kumrushia simu Karimu nae ajionee.

“Hi Dear, I miss you so much Nice dream to you”

Karimu alisoma kwa sauti na kumtazama Salimu “Duh! Kaka mwaka huu wako ndugu yangu mhh!”, aliongea Karimu na Salimu akabaki kujishika tama. “Kaka mjibu basi mtoto huyu mwambie wewe pia usimuache kimya kimya tu kumbuka huyu naye unamkosesha usingizisi kila siku lazima akutafute na akusabahi lakini wewe mara moja moja ndio unamuunga mkono tena kwa visingizio vingi” Karimu aliuvunja ukimwa ulio tanda “Karimu eeh naomba utulie bwana unanichanganya, tena katika watu ambao hata siwaelewi ni huyu binti Shalon kwanza kwa tabia yake ya jeuri ile siku pale sina mpango naye kabisa”. Salimu shingo akaiegeuzia upande mwingine na kusonya “…yani namna ninavyojiskia juu ya Shalon bora kwa Meroda kidogo na hisi kusisimka nikimkumbuka japo wote ni wanawake warembo sana…ahh niache kwanza tafadhari, leo pia sitomjibu alale tu”. Aliongea Salimu kwa kujiamini na kumwacha Karimu akiwa kaachama mdomo akishangaa akaongea “Kaka usiniambie kwamba umeamua kumpenda Meroda wa juzi mara moja hii” “Karimu eeh mbona ndugu yangu unakuwa kinyonga mara cheusi mara chekundu unanivuruga kaka” aliongea Salimu.

Mzozo ukaanza, mwisho kila mmoja akatulia, kimya kikaaingia kimya hakuna aliyemuongelesha mwenzie kila mtu akiwaza lake, Mara mlio wa ujumbe mfupi katika simu ya Salimu ulilia na ukasababisha kukatika kwa mawazo yao wote akili ikahamia katika ujumbe mfupi ni nani na unasemaje. Salimu akaichukua simu yake na kuanza kuusoma


Itaendelee..
 
The Hidden Truth (Ukweli Uliofichika)

Mtunzi : Akida Siri Rambao
Contact : 0658328596
Email : akidasiri@gmail.com

MSIMU 2

Sehemu 6 J : Upelelezi

Tuendeleee...

...sauti ya kike ilisikika ikiongea Salimu akabaki kuitika akaitoa simu sikioni akiwa amechoka mikono ikiwa mikononi akijiwazia. Jasho jembamba lenye ubaridi lilionekana likimtoka nyuma ya sikio.

Alichokifanya nikujifuta kwa kitamba chake cha leso alichopenda kukiweka katika mifuko ya nyuma ya suruali na karudi haraka darasani kwa ajili ya kuendelea na majukumu aliyokuwa ameyakabidhi kwa Karimu.


USIKU
Salimu akiwa kajikalia kila muda akiitupia macho simu yake kama mtu anaye subiri kitu mara simu ikaita haraka akaipokea na kusikiliza upande wa pili akigeuka huku na kule akisimama na kukaa tena mwishowe yakaisha. “Mhhh…kazi ipo kaka” akajikalia zake kitandani “Ndugu yangu nishaapendwa na jambazi kama ulivyosikia!” Salimu wa watu alijikunyata na kukishika kichwa chake asijue la kufanya huku Karimu akiendelea kugonga taratibu ubao wa kitanda cha ghorofa yeye akiwa juu akitafakari kwa kina, mara Karimu alionekana kupata wazo, “Ndugu yangu nimeshapata wazo lakini ni la hatari kwetu sote”. Salimu taratibu alianza kukunjua mikono yake kichwani pia kuzikunjua ndita alizozikunja katika paji lake la uso na kukaa vizuri kwa nia ya kumsikiliza Karimu, “Mi naonelea mkubalie tu ili kazi yetu iwe rahisi”, Salimu akaachama mdomo huku akisikitika kwa kukitingisha kichwa kukataa “Ndugu yangu naona unataka tufe mapema haiwezekani, wale wanawake si wanawake wakuchezea unajua? hilo hapana tafuta wazo lengine…” Salimu aliongea na akakaa vizuri akaendelea “…Karimu sikia ingelikuwa wapo katika ngazi ndogo ningekubali lakini wale wanaonekana ni watu wanao heshimika sana na kauaminika pia” Salimu hali ya wasiwasi ilimzidi.

Haikupita muda taswira ya Meroda ilimjia kumkumbusha namna alivyokuwa akizungumza na kucheka na ule muonekano wake wa ajabu pumzi nzito zikamtoka, “Uhhh! kwanini yote yamekuja kwa mara moja?” Salimu alijisemea mwenyewe huku akitingisha kichwa juu ya kitanda, “Kaka mimi mwenyewe hapa nilikuwa najiuliza swali hilo hilo ndugu yangu”, Karimu aliongea akajivuta na kuegemea ukuta huku akimtazama Salimu. Wakiwa kimya kila mmoja akiwaza lake kamlio ka simu kuonesha ujumbe mfupi katika simu ya Salimu ulilia nae akajizoa hadi katika meza na kuichukua ilikuwa ujumbe wa Shalon, alisikitika kwa kichwa akajisogeza kitandani na kumrushia simu Karimu nae ajionee.

“Hi Dear, I miss you so much Nice dream to you”

Karimu alisoma kwa sauti na kumtazama Salimu “Duh! Kaka mwaka huu wako ndugu yangu mhh!”, aliongea Karimu na Salimu akabaki kujishika tama. “Kaka mjibu basi mtoto huyu mwambie wewe pia usimuache kimya kimya tu kumbuka huyu naye unamkosesha usingizisi kila siku lazima akutafute na akusabahi lakini wewe mara moja moja ndio unamuunga mkono tena kwa visingizio vingi” Karimu aliuvunja ukimwa ulio tanda “Karimu eeh naomba utulie bwana unanichanganya, tena katika watu ambao hata siwaelewi ni huyu binti Shalon kwanza kwa tabia yake ya jeuri ile siku pale sina mpango naye kabisa”. Salimu shingo akaiegeuzia upande mwingine na kusonya “…yani namna ninavyojiskia juu ya Shalon bora kwa Meroda kidogo na hisi kusisimka nikimkumbuka japo wote ni wanawake warembo sana…ahh niache kwanza tafadhari, leo pia sitomjibu alale tu”. Aliongea Salimu kwa kujiamini na kumwacha Karimu akiwa kaachama mdomo akishangaa akaongea “Kaka usiniambie kwamba umeamua kumpenda Meroda wa juzi mara moja hii” “Karimu eeh mbona ndugu yangu unakuwa kinyonga mara cheusi mara chekundu unanivuruga kaka” aliongea Salimu.

Mzozo ukaanza, mwisho kila mmoja akatulia, kimya kikaaingia kimya hakuna aliyemuongelesha mwenzie kila mtu akiwaza lake, Mara mlio wa ujumbe mfupi katika simu ya Salimu ulilia na ukasababisha kukatika kwa mawazo yao wote akili ikahamia katika ujumbe mfupi ni nani na unasemaje. Salimu akaichukua simu yake na kuanza kuusoma


Itaendelee..
 
The Hidden Truth ( Ukweli Uliofichika)

Mtunzi Akida Siri Rambao
Contact : 0658328596
Email : akidasiri@gmail.com

MSIMU 2

Sehemu 6 K : Upelelezi

Tuendeleee...

Salimu akaichukua simu yake na kuanza kuusoma

“Kila ninapo vuta taswira ya muonekano wako natamani kukutanisha lips zangu kwako, umeniingia sana akilini we kijana nashindwa hata kujizuia”

“Vipi! Shalon huyo?” Salimu alishtushwa na swali la Karimu maana alihama kimawazo kwa kutafakari ujumbe huo, “Ndio ni yeye” “Shabash mjibu kaka hata vya uongo basi” aliongea tena Karimu “Simjibu leo nakwambia niache”. Salimu alipaza sauti yake kwa hasira na kumfanya Karimu kutulia, basi Karimu alivuta shuka na kujilaza zake.

Kwa Salimu yeye alikuwa ka kaa tu kashikilia simu yake akitafakari, mara ukaingia ujumbe mwengine alitazama kichovu chovu, mara akatabasamu Karimu akiwa kajifunika mwili mzima na kubakisha vimacho alimtazama Salimu kimachale na kumuona anavyotabasamu akatulia kumfatilia akiwa juu katika kitanda hicho cha ghorofa, Salimu alifungua ujumbe na kuusoma

“Mambo vipi laazizi wangu, barafu wa moyo umelala?.”

Salimu hakupoteza muda alichangamka kuijibu, huku Karimu akimfatilia tu kwa makini, “Hapana nipo macho na yawaza maisha yalivyokuwa magumu” Salimu alimtumia Meroda.

“Usihofu mbele yangu huto pata shida ya maisha na utalala daima kwenye moyo wangu na nitakutunza sasa lala uwamke mapema usiku mwema”

Salimu alifurahia sana kusoma jumbe za Meroda, alirudia mara mbili mara tatu kusoma huku akitabasamu mwishowe aliiweka simu katika meza iliyokuwa karibu akavuta shuka yake na kujilaza wakati wote huo Karimu alikuwa anamfatilia tu.

Usiku wamanane

Ilikuwa ni mihemko isiyoyakawaida ikiambatana na kuweweseka huku jasho likimtoka kijana Salimu kwa namna ya mtu anayefanya kazi ngumu kwa muda mrefu akihema hovyo kwa kuchoka, teyali maaneo aliyoulaza mwili wake yalianza kuloa jasho lililotoka mwilini mwake. “Hapana …hapana Hapanaaaaaaaaa” Salimu akakurupuka toka usingizini macho yakiwa mbele kama tochi kiasi cha kumshitua Karimu. “Mzeee kuna nini aisee upo sawa ndugu” Karimu alihoji baada ya ya kuwasha taa. “Ndoto kaka ndoto mbayaa” ni maneno pekee aliyoyasema .ndani ya ndoto mbaya iliyomfanya jasho kumtoka huku akiweweseka akihema hovyo hovyo.

“Nimemuona Meroda akiwa ametukamata anatupeleka katika msitu mkubwa na wenzake” aliongea Salimu, “Ohh pole ni mawazo tu omba dua mola akuepushie” Baada ya dakika kazaa mwili ukaanza kuwa sawa na akaamini ilikiuwa ni ndoto tu na sio kweli, licha ya kujiridhisha lakini bado alikuwa na wasiwasi kuhusiana na Meroda. Moja kwa moja alinyanyuka na kwenda kujimwagia maji, alipo maliza alijikalisha kitandani na kuwaza sana hatma ya maisha yake ya siku za usoni aliamua kuwa hatoweza kupenda kwa kipindi chote mpaka aweke mambo yake sawa., hilo ndilo likawa ni ahuheni kwake kisha ndipo akalala.

Itaendeleaaa...
IMG-20211211-WA0046.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom