Abdallahking
JF-Expert Member
- Mar 19, 2018
- 3,983
- 10,804
- Thread starter
- #21
SEHEMU YA 15
Ilipoishia... Mara nikaona karatasi pale Mezani imefunikwa kwa hofu niliyokuwa nayo nikaiwahi haraka haraka kwenda kuichukua lakini kabla sijafika pale ndo nakaribia tu mara.. Endelea..... Nikasikia kama sauti ya mtu anabisha hodi,haraka haraka nikaikodolea saa yetu ya ukutani ikanionesha ni saa Tisa na robo usiku, nikawa najiuliza., "....Huyu ni nani anayebisha hodi sa hivi..!" Sikuitikia ile hodi nilichokifanya nikaichukuwa ile karatasi na kuanza kuisoma., "...MWANANGU WA PEKEE LEVINA, KWANINI UNATAKA KUNIUA BILA YA KOSA LOLOTE?.., NIMEHANGAIKIA MAISHA YAKO KWA MDA MREFU MPAKA SASA.,NIMESIKITIKA SANA KUKUTA TIKETI YA NDEGE CHUMBANI KWAKO NA SAFARI NI KESHO,BILA HATA KUNIAMBIA CHOCHOTE MWANANGU..?MPAKA NIKAAMUA KUCHUKUWA UAMUZI HUU WA KUJIUA NITANGULIE MBELE YA HAKI, NAKUTAKIA MAISHA MEMA, Mimi MAMA YAKO, Mama Levina." "..No..! No..! No..! Mama..! Kwanini umewahi kufanya hiivyooo...!
" Nikajikuta nauvua moyo wa kikatili na kuanza kumuonea huruma tena Mama huku nikielekea mlangoni kwa yule mtu aliyekuwa anabisha hodi, "...Hapa mezani nimekuta kikopo cha sumu ya panya na hii karatasi, yeye Mama atakuwa wapi sasa..?" Kabla sijaufungua mlango nikalipenyeza jicho langu kwenye tobo la kuwekea ufunguo., "...Mungu mkubwa.,huyu ni Mama yangu kabisa, ona na kanga nilizomnunulia kipindi kileee ni hizi hizi...!" Sikutaka hata kuuliza ni nani kwani sauti nilikuwa siiskii lakini kwanilivyokuwa nimemchungulia dhahiri atakuwa ni Mama yangu, "..Itakuwa alienda chooni kipindi kile nilivyoenda chumbani..? Lakini ile sumu na barua kwanini aliamua kuandika vile..? Inamaana anajua picha lote litakavyokuwa....?" Ni kati ya maswali niliokuwa nikijiuliza bila kupata majibu kwani ni kweli choo chetu kimejengwa nje ya nyumba na yule niliyemchungulia ni Mama yangu kabisa., Nikachukuwa vile vitu nilivyokuwa nimeshika ambavyo ni kamba kubwa nene pamoja na Panga kisha nikavitupia uvunguni mwa kochi ili Mama asijue lolote kisha nikarudi pale kwa ajili ya kumfungulia.,kadri nilivyokuwa nashika kitasa ndivyo nilikuwa naona mlango unazidi kuwa mgumu nikausukuma kwanguvu kuelekea ndani nilipo, mara nikasikia kishindo cha mtu amedondoka mbele yangu, "...Mamaa...! Mamaa...! Ni wewe Mama.....!" Niliugeuza ule mwili nakuanza kuutingisha maskini ni kweli alikuwa Mama japo Mwili ulikuwa umeshabadilika na kuwa mweusi kama mkaa,huku damu yake ikibadilika na kuwa maji kama kamasi ikiteleza kutokea masikioni,puani na Mdomoni, Ngozi yake ilijikunja sana lakini halmashauri yangu ya kichwa ikafanya kazi fasta na kujua kuwa huenda alikunywa ile sumu kidogo halafu akaenda chooni wakati anarudi ikamzidia., Bila kupoteza mda nikauvuta ule mwili nakufunga mlango kwa ufunguo halafu nikamburuza mpaka sebuleni kisha nikaingia chumbani na kutoa Biblia., "Eeeh Mungu Baba muweza wa yote...!
Natubu mbele za haki najua kama mimi ni Mwana mkosefu kwa kitendo nilichofanya na nitakachoendelea kukifanya ila naomba kusamehewa...Amina.." Nilipomaliza nikaingia chumbani kwangu na kuchukua Gunia kubwa na koleo kisha nikalipitia lile panga pale uvunguni sebuleni na kuuburuta ule mwili kuelekea nje ya nyumba yetu,nawaombeni sana wasomaji mnisamehe kwa nilichokifanya mbeleni, Nikauburuta ule mwili mpaka karibu na eneo lilipokuwa na kaburi la Baba,nikaulaza na kuchukuwa panga langu kisha nikaanza kutenganisha upande mmoja mmoja nikianzia na mikono,Shingo na miguu yote miwili hakika sikuwa levina yule mlokole bali nilikuwa Levina Mkatili tena mnyama kama simba Dume tena yule anayoogopewa na kila mtu duniani.,Nilichana kitambaa cha nguo yangu na kujifunika usoni kisha nikaanza kumkatakata Mama eneo la usoni ili nipoteze ushahidi kama ikija kujulikana,nahisi damu ilikuwa imeganda kwani sikushuhudia hata chembe ya damu ikimtoka. Nilipomaliza nikachukuwa viwiliwili nikaanza kudumbukiza kwenye ule mfuko kisha Nikachukuwa koleo nakuanza kuchimba kashimo kadogo kwa ajili ya kumfukia ili niendelee kupoteze ushahidi kabisa, nikiwa ndo namalizia kuchimba mara simu yangu ikaita, "...haloo..! Aaah Gervas" "...enh Mmefikia wapi..?" "...Mama tayari nimemwacha na mtu na keshokutwa safari itakuwepo usijali mpenzi wangu..!" "...Okey, msalimie sana Mama yako mwambie bado namkumbuka na kuna zawadi yake tayari nimemwandalia..," "...Usijali Gerva,amekusikia..!" Nikakata simu nakumalizia kuchimba pale fasta fasta nilipomaliza nikashindilia na kokoto zilizokuwa karibu.,kisha nikaingia ndani kwa mbwembwe. "...Zoezi la kwanza limeisha na bado Mama yake Gervas, atanitambua huko tunapoenda..!" Nilijisemea kimoyo moyo huku nikijiamini kwa kile nilichokifanya mda si mrefu,nilipofika sebuleni nikapiga magoti na kuomba tena., "...Najua jamii yote itachukizwa nami, lakini mtetezi wangu ni wewe Baba uliye juu mbinguni.., Eeeh mwenyezi Mungu mlaze Mama yangu Mahala pema peponi,Amina.." Nilipomaliza kusali tu ghafla nikaanza kujihisi mabadiliko makubwa kwenye mwili wangu sana sana eneo la tumbo, niliumia sana,nilijikaza bado ikawa haisaidii uchungu ulinizidia mpaka nikajihisi mimba inataka kuchomoka,nilishindwa kuvumilia nikaanza kugala gala pale chini lakini nikawa kama ndo nalichochea tumbo liendelee kuuma,miguu ikavimba kwa haraka nikawa najiburuza sasa kuelekea chumbani..,kwa maumivu yaliokuwa yamenizidia mpaka nikajikuta nimeingia chumba cha Mama ambaye tayari nimeshamuua,kwa kujikokota taaratibu mpaka eneo la 'dressing tebo' huku nikitafuta dawa yeyote ya kutuliza maumivu,nikajishikiza kwa mkono mmoja huku mkono mwingine ukiwa unafungua droo za lile 'dressing tebo'.. "....Mamaaaaaaa..! Mamaaaaaa...! Mamaaaaa...!
Mi sijakuua Mama ulikunywa sumu mwenyewe Mama...!" Sura yangu ilikuwa imekutana na kioo cha ile 'dressing tebo' ghafla ikatokea sura ya Mama katika kile kioo, Nilichanganyikiwa na kujiona zaidi ya kichaa kwani usiku ule ule nilitokomea kusikojulikana huku nikiwa mtupu nimevalia 'nait dres' na nywele zikinivuruga, Kulipokucha asubuhi kila mtu alikuwa akinishangaa kwani nilikuwa tayari majalalani nikiokoteza vyakula vichafu, ukinisogelea utakuwa unatafuta balaa na Mimi kwani nikaa si Levina tena., "Ng'aaam...! Ng'aaam..! Piiiiiipi..! Pipiiii...! Oya pisha njia gari inakasi hiyo we fala nini..? Embu pisha nitakuitia Mama yangu aje akugonge..?" Nilikuwa tayari chizi kwani Mikononi nilikuwa nimeshika mifuniko ya ndoo huku nikiendesha kama gari nazunguka zunguka wapita njia wakinishangaa.. "...Gervas panda twende wewe...konda wadai nauli haoo..!" Uchizi wangu uliendelea na ilipofika mda wa usiku sana,Vijana kama sita hivi nafikiri walikuwa ni majambazi kwani walikuwa na makoti makubwa huku wamekunja sura zao walipita eneo nililokuwa nimejibanza na kujikunyata pale jalalani. "....Oyaa masela eenh..!" "...washkaji huyu chizi vipi..,embu mchekini..!" "...Oyaa hapa si Marekani.?" "...Fala nini..?" "...Masela mi nina nyege sana kama vipi njooni basi..!" Niliwaita wakanifanya kitendo kibaya wote wale huku nikifurahia kwa kile kitendo. "...kama vipi na kesho mje basi..! Au siyo masela..?" Nikatoka eneo lile nikiwa na mimba yangu huku nikijitembelea kusiko julikana usiku ule, hata nilipowaona polisi sikuogopa kabisa, "...We binti chizi nini? Unafata nini hapa Polisi..? Nilijikuta nimeingia kituo cha polisi huku nikiwa sina hata chembe ya woga..! "
...Kwani masela nyie vipi? Mi muuaji Mmesikia..? Mimi ndo niliomuua Baba Ali, Pendo na hata Mama yangu nimemuua mimi..!" "....Afande John, unarisikia hiri ritoto rinavyoropoka..? Binti unaitwaga rinani?" "...Mi naitwa Levina.,oyaa kwanza nipe bangi nitoe stimu..!" "...Haroo hiri siro ri revina tunaroritafutaga..?" "...Hamuwezi kunitafuta nyie mabwege labda mumtafute Afande Deus..!" "Nani...? embu riingize rokapu ritatusaidia kumpata huyo revina..,nakujua juu ya rimkuu rifande Deus..!" * * * Levina tayari chizi na kaingia Polisi bila kujijua,itakuwaje? * * * Vipi Gervas akija kujua atamsaidia? * * * Itakuwaje mwili wa mama yake Levina ukijulikana?
Ilipoishia... Mara nikaona karatasi pale Mezani imefunikwa kwa hofu niliyokuwa nayo nikaiwahi haraka haraka kwenda kuichukua lakini kabla sijafika pale ndo nakaribia tu mara.. Endelea..... Nikasikia kama sauti ya mtu anabisha hodi,haraka haraka nikaikodolea saa yetu ya ukutani ikanionesha ni saa Tisa na robo usiku, nikawa najiuliza., "....Huyu ni nani anayebisha hodi sa hivi..!" Sikuitikia ile hodi nilichokifanya nikaichukuwa ile karatasi na kuanza kuisoma., "...MWANANGU WA PEKEE LEVINA, KWANINI UNATAKA KUNIUA BILA YA KOSA LOLOTE?.., NIMEHANGAIKIA MAISHA YAKO KWA MDA MREFU MPAKA SASA.,NIMESIKITIKA SANA KUKUTA TIKETI YA NDEGE CHUMBANI KWAKO NA SAFARI NI KESHO,BILA HATA KUNIAMBIA CHOCHOTE MWANANGU..?MPAKA NIKAAMUA KUCHUKUWA UAMUZI HUU WA KUJIUA NITANGULIE MBELE YA HAKI, NAKUTAKIA MAISHA MEMA, Mimi MAMA YAKO, Mama Levina." "..No..! No..! No..! Mama..! Kwanini umewahi kufanya hiivyooo...!
" Nikajikuta nauvua moyo wa kikatili na kuanza kumuonea huruma tena Mama huku nikielekea mlangoni kwa yule mtu aliyekuwa anabisha hodi, "...Hapa mezani nimekuta kikopo cha sumu ya panya na hii karatasi, yeye Mama atakuwa wapi sasa..?" Kabla sijaufungua mlango nikalipenyeza jicho langu kwenye tobo la kuwekea ufunguo., "...Mungu mkubwa.,huyu ni Mama yangu kabisa, ona na kanga nilizomnunulia kipindi kileee ni hizi hizi...!" Sikutaka hata kuuliza ni nani kwani sauti nilikuwa siiskii lakini kwanilivyokuwa nimemchungulia dhahiri atakuwa ni Mama yangu, "..Itakuwa alienda chooni kipindi kile nilivyoenda chumbani..? Lakini ile sumu na barua kwanini aliamua kuandika vile..? Inamaana anajua picha lote litakavyokuwa....?" Ni kati ya maswali niliokuwa nikijiuliza bila kupata majibu kwani ni kweli choo chetu kimejengwa nje ya nyumba na yule niliyemchungulia ni Mama yangu kabisa., Nikachukuwa vile vitu nilivyokuwa nimeshika ambavyo ni kamba kubwa nene pamoja na Panga kisha nikavitupia uvunguni mwa kochi ili Mama asijue lolote kisha nikarudi pale kwa ajili ya kumfungulia.,kadri nilivyokuwa nashika kitasa ndivyo nilikuwa naona mlango unazidi kuwa mgumu nikausukuma kwanguvu kuelekea ndani nilipo, mara nikasikia kishindo cha mtu amedondoka mbele yangu, "...Mamaa...! Mamaa...! Ni wewe Mama.....!" Niliugeuza ule mwili nakuanza kuutingisha maskini ni kweli alikuwa Mama japo Mwili ulikuwa umeshabadilika na kuwa mweusi kama mkaa,huku damu yake ikibadilika na kuwa maji kama kamasi ikiteleza kutokea masikioni,puani na Mdomoni, Ngozi yake ilijikunja sana lakini halmashauri yangu ya kichwa ikafanya kazi fasta na kujua kuwa huenda alikunywa ile sumu kidogo halafu akaenda chooni wakati anarudi ikamzidia., Bila kupoteza mda nikauvuta ule mwili nakufunga mlango kwa ufunguo halafu nikamburuza mpaka sebuleni kisha nikaingia chumbani na kutoa Biblia., "Eeeh Mungu Baba muweza wa yote...!
Natubu mbele za haki najua kama mimi ni Mwana mkosefu kwa kitendo nilichofanya na nitakachoendelea kukifanya ila naomba kusamehewa...Amina.." Nilipomaliza nikaingia chumbani kwangu na kuchukua Gunia kubwa na koleo kisha nikalipitia lile panga pale uvunguni sebuleni na kuuburuta ule mwili kuelekea nje ya nyumba yetu,nawaombeni sana wasomaji mnisamehe kwa nilichokifanya mbeleni, Nikauburuta ule mwili mpaka karibu na eneo lilipokuwa na kaburi la Baba,nikaulaza na kuchukuwa panga langu kisha nikaanza kutenganisha upande mmoja mmoja nikianzia na mikono,Shingo na miguu yote miwili hakika sikuwa levina yule mlokole bali nilikuwa Levina Mkatili tena mnyama kama simba Dume tena yule anayoogopewa na kila mtu duniani.,Nilichana kitambaa cha nguo yangu na kujifunika usoni kisha nikaanza kumkatakata Mama eneo la usoni ili nipoteze ushahidi kama ikija kujulikana,nahisi damu ilikuwa imeganda kwani sikushuhudia hata chembe ya damu ikimtoka. Nilipomaliza nikachukuwa viwiliwili nikaanza kudumbukiza kwenye ule mfuko kisha Nikachukuwa koleo nakuanza kuchimba kashimo kadogo kwa ajili ya kumfukia ili niendelee kupoteze ushahidi kabisa, nikiwa ndo namalizia kuchimba mara simu yangu ikaita, "...haloo..! Aaah Gervas" "...enh Mmefikia wapi..?" "...Mama tayari nimemwacha na mtu na keshokutwa safari itakuwepo usijali mpenzi wangu..!" "...Okey, msalimie sana Mama yako mwambie bado namkumbuka na kuna zawadi yake tayari nimemwandalia..," "...Usijali Gerva,amekusikia..!" Nikakata simu nakumalizia kuchimba pale fasta fasta nilipomaliza nikashindilia na kokoto zilizokuwa karibu.,kisha nikaingia ndani kwa mbwembwe. "...Zoezi la kwanza limeisha na bado Mama yake Gervas, atanitambua huko tunapoenda..!" Nilijisemea kimoyo moyo huku nikijiamini kwa kile nilichokifanya mda si mrefu,nilipofika sebuleni nikapiga magoti na kuomba tena., "...Najua jamii yote itachukizwa nami, lakini mtetezi wangu ni wewe Baba uliye juu mbinguni.., Eeeh mwenyezi Mungu mlaze Mama yangu Mahala pema peponi,Amina.." Nilipomaliza kusali tu ghafla nikaanza kujihisi mabadiliko makubwa kwenye mwili wangu sana sana eneo la tumbo, niliumia sana,nilijikaza bado ikawa haisaidii uchungu ulinizidia mpaka nikajihisi mimba inataka kuchomoka,nilishindwa kuvumilia nikaanza kugala gala pale chini lakini nikawa kama ndo nalichochea tumbo liendelee kuuma,miguu ikavimba kwa haraka nikawa najiburuza sasa kuelekea chumbani..,kwa maumivu yaliokuwa yamenizidia mpaka nikajikuta nimeingia chumba cha Mama ambaye tayari nimeshamuua,kwa kujikokota taaratibu mpaka eneo la 'dressing tebo' huku nikitafuta dawa yeyote ya kutuliza maumivu,nikajishikiza kwa mkono mmoja huku mkono mwingine ukiwa unafungua droo za lile 'dressing tebo'.. "....Mamaaaaaaa..! Mamaaaaaa...! Mamaaaaa...!
Mi sijakuua Mama ulikunywa sumu mwenyewe Mama...!" Sura yangu ilikuwa imekutana na kioo cha ile 'dressing tebo' ghafla ikatokea sura ya Mama katika kile kioo, Nilichanganyikiwa na kujiona zaidi ya kichaa kwani usiku ule ule nilitokomea kusikojulikana huku nikiwa mtupu nimevalia 'nait dres' na nywele zikinivuruga, Kulipokucha asubuhi kila mtu alikuwa akinishangaa kwani nilikuwa tayari majalalani nikiokoteza vyakula vichafu, ukinisogelea utakuwa unatafuta balaa na Mimi kwani nikaa si Levina tena., "Ng'aaam...! Ng'aaam..! Piiiiiipi..! Pipiiii...! Oya pisha njia gari inakasi hiyo we fala nini..? Embu pisha nitakuitia Mama yangu aje akugonge..?" Nilikuwa tayari chizi kwani Mikononi nilikuwa nimeshika mifuniko ya ndoo huku nikiendesha kama gari nazunguka zunguka wapita njia wakinishangaa.. "...Gervas panda twende wewe...konda wadai nauli haoo..!" Uchizi wangu uliendelea na ilipofika mda wa usiku sana,Vijana kama sita hivi nafikiri walikuwa ni majambazi kwani walikuwa na makoti makubwa huku wamekunja sura zao walipita eneo nililokuwa nimejibanza na kujikunyata pale jalalani. "....Oyaa masela eenh..!" "...washkaji huyu chizi vipi..,embu mchekini..!" "...Oyaa hapa si Marekani.?" "...Fala nini..?" "...Masela mi nina nyege sana kama vipi njooni basi..!" Niliwaita wakanifanya kitendo kibaya wote wale huku nikifurahia kwa kile kitendo. "...kama vipi na kesho mje basi..! Au siyo masela..?" Nikatoka eneo lile nikiwa na mimba yangu huku nikijitembelea kusiko julikana usiku ule, hata nilipowaona polisi sikuogopa kabisa, "...We binti chizi nini? Unafata nini hapa Polisi..? Nilijikuta nimeingia kituo cha polisi huku nikiwa sina hata chembe ya woga..! "
...Kwani masela nyie vipi? Mi muuaji Mmesikia..? Mimi ndo niliomuua Baba Ali, Pendo na hata Mama yangu nimemuua mimi..!" "....Afande John, unarisikia hiri ritoto rinavyoropoka..? Binti unaitwaga rinani?" "...Mi naitwa Levina.,oyaa kwanza nipe bangi nitoe stimu..!" "...Haroo hiri siro ri revina tunaroritafutaga..?" "...Hamuwezi kunitafuta nyie mabwege labda mumtafute Afande Deus..!" "Nani...? embu riingize rokapu ritatusaidia kumpata huyo revina..,nakujua juu ya rimkuu rifande Deus..!" * * * Levina tayari chizi na kaingia Polisi bila kujijua,itakuwaje? * * * Vipi Gervas akija kujua atamsaidia? * * * Itakuwaje mwili wa mama yake Levina ukijulikana?