Abdallahking
JF-Expert Member
- Mar 19, 2018
- 3,983
- 10,804
- Thread starter
- #41
SEHEMU YA 27
Ilipoishia jana usiku...... ...Mara nikawaona askari wanne tena ni wale wale wa treni wakiwa wanakuja kwa mbali eneo tulipokuwa na yule mdada.. Endelea..... ".....Uhh...! uhh....! uhh....! uhh....! uhh...!" Tayari kijasho chembaa kikawa kinanitoka pamoja na kuwa na kaubaridi pale chini ya mti nilipokuwa nimepitiwa na usingizi mzito baada ya wale wadada walipodondosha mitungi yao ya maji na kunikimbia, "Mungu wangu.....! Kwanini tena jamani naendelea kuziota hizi ndoto za mauaji mimi.....?" Nilijikuta nikiilaumu nafsi yangu kwani ni kweli nilikuwa nikiota ndoto za ajabu ajabu,Eti nimeliona treni limeharibika mpaka nikamuua mzee wa watu na kumvua nguo na kuzivaa mbaya zaidi eti nikaota nimekamatwa na yule mtoto wa huyo Mzee Mhhh...!,
"....Eeeh mwenyezi Mungu niondolee ndoto chafu hizi zisiniandame tena....?" Nikasali kimoyomoyo kisha nikainuka pale chini ya ule mti niliokuwa nimepitiwa na usingizi kisha nikaenda hadi pale wadada walipondondosha ile mitungi yao ya maji na kuanza kukombeleza japo niweze kupata vijimaji kidogo. Jua la Asubuhi likiwa tayari limeshachomoza kabisa na mpaka kufikia leo nilikuwa natimiza siku ya pili bila kupata chochote tumboni zaidi ya hivi vijimaji. Nilikuwa sina jinsi yoyote zaidi ya kuendelea na safari huku nikiwa sijitambui ninapoelekea,nilitembea tena umbali wa kama kilometa sita hivi ndipo nilipokutana na vinyumba vidogo vidogo. Furaha ikanijaa zaidi moyoni mwangu pale nilipowaona watu. "...Wale wadada walionikimbia kulee,mmoja wapo yulee ngoja nimuwahi nimuulize kitu...!" Nikatembea fasta mpaka alipo na nikajua tu hajui kiswahili wala kiingereza kwa hiyo hapa nikutumia njia ya vitendo atanielewa, Safari hii yule dada hakuonesha woga wowote akanipeleka mpaka nyumbani kwao nikakutana na wazazi wao wakanipokea vizuri tu huku wakiongea wenyewe kwa lugha yao. "....Lengula... Pela ine.....!" "...Isa kuno....!" Yule mzee akatoka nje na kurudi na wazee wenzake wakiwa na shauku ya kutaka kunijua kiundani zaidi. "Lengula Mweni.....!" "Pela ine Cilyo.....!" Mara nikashangaa wameleta chakula pamoja na kombe kubwa la maji hivyo nikaanza kuambulia maneno nikajua "kumbe 'Cilyo' inamaana ya chakula...!" Sikukiweza kula kile chakula kwani ilikuwa kama maugali ugali ambayo hayajaiva vizuri yaliyochanganywa na mimboga ya majani iliyoungwa ovyo ovyo tu,Sema kutokana na njaa ya siku mbili niliyokuwa nayo,nilijikuta nafakamia hivyo hivyo na kushushia na yale maji.. "Naomba niongezeni tena maji ya kunywa...." Huku nikioneshea kwa vitendo kuwa nahitaji niongezewe maji, "Pela ine I majie....!" Yule Mzee akamuamlisha mtoto wake aniletee,aliponiletea nikayanywa kisha nikamsikia akimtuma tena kwa mara ya pili yule mtoto. "Ya Na Ubwite Bane Nsansa.....
" Akatoka halafu baada ya muda akarudi na dada mmoja mweupe aliyeonekana kama mtu tofauti na wao kuanzia mavazi hadi nywele zake alivyozitengeneza, "How are you....?" "am fin., wh ar u....?" Nikajua nimeshapata mtetezi wangu kuwa yule dada alikuwa akijua kiingereza lakini nilijiuliza sana ametokea wapi na amejuaje kiingereza maeneo haya,nilijiuliza mara mbili mbili bila ya kupata jibu, "whr ar u cme frm?" "Am frm South Africa to Tanzania..!" Nikamdanganya huku nikiangalia kwa pembeni kwani woga na aibu vilikuwa vimeshakuwa vimenitanda mule ndani huku wale wazee wakitusikiliza kwa ukaribu japokuwa hawakujua chochote pale. "Ar u Tanzanian....?" "Yes of course..." "Waaaooh...! Do u knw how to spk swahil language.....?" "Ndio....." Nikamjibu kwa kiswahili mpaka akashangaa na hakuweza kuamini ndipo nilipoanza kujitambua kuanzia sehemu niliyopo. "Hapa tupo kusini Magharibi mwa Zambia na siyo mbali sana na mpakani mwa Tanzania" "Ulisema unaitwa nani...?" " Brendah BreBre...." Nikamdanganya nikijua kuwa siku akijua kuwa naitwa Levina inaweza ikaleta matatizo yoyote. "Unaskia Brendah...", "Abee...!" "....Hiki kijiji kinaitwa 'Nakonde' ni maarufu sana hapa Zambia na hizi lugha wanazoongea huku ni ki 'Bemba' na ki, 'Njanja' ndicho wanachozungumza sana lakini ki 'Bemba' ndicho tunachozungumza sana,na nadhani umeshakisikia kabla sijaingia hapa..." "Happy..., Nafurahi sana kukufahamu....!" "Hata mimi nafurahi sana Brendah...!" Baada ya pale tukakumbatiana na kutoka na huyo dada anayeitwa 'Happy' na kuongozana naye mpaka kwenye kijumba chao, Jioni ilikuwa imeshatimia huku nakajua nako kakitaka kuzama,nikiwa tayari na ninayemwamini ni mtetezi wangu,nilipewa maji ya kuoga nikajisafisha damu zote zilizogandia mwilini na baada ya hapo alinipa nguo zake nivae kisha akanipa chakula cha usiku, "Kwahiyo Happy...?unasoma au....?"
"Hapana Brendah, Mimi nafanya kazi kulee 'Custom' (Mpakani)tena ni mbali kidogo na hapa huwa nakuja kuchukuliwa na Gari asubuhi sana...!" huku tukiendelea kupiga naye stori nyingi za maisha huku zangu nikizificha ficha asizijue hata kidogo,ilipotimia tena mda wa kulala alinipa shuka na kulala naye katika kitanda chake. Kwa mara nyingine nikafurahia maisha kwani ilipofika asubuhi niliamka kwa furaha zote huku mwili wangu ukisisimka mara kwa mara nadhani ni kutojiamini na mazingira niliyokuwa nayo, Nilivyoamka sikumkuta Happy bali niliambulia kikaratasi kilichoandikwa ujumbe pembeni yangu, Nikakichukuwa na kukisoma. "NAELEKEA OFISINI SAMAHANI SANA BRENDAH KWA KUTOKUAGA.,NISINGEWEZA KUKUAMSHA LAKINI USIHOFU MCHANA NITARUDI TUTAKUWA PAMOJA..UTAJIPIKIA CHAKULA NA MTAKULA HAPO NYUMBANI. Wako Mpendwa HAPPY. Nilipomaliza nilisisimka tena nikatoka nje na kukata mjiti kisha nikachukuwa kikombe cha maji nakuanza kupiga mswaki... *********** * * * Levina kaanza maisha mapya, atadumu hapo? * * * Vipi upande wa Gervas imeishia vipi...?
Ilipoishia jana usiku...... ...Mara nikawaona askari wanne tena ni wale wale wa treni wakiwa wanakuja kwa mbali eneo tulipokuwa na yule mdada.. Endelea..... ".....Uhh...! uhh....! uhh....! uhh....! uhh...!" Tayari kijasho chembaa kikawa kinanitoka pamoja na kuwa na kaubaridi pale chini ya mti nilipokuwa nimepitiwa na usingizi mzito baada ya wale wadada walipodondosha mitungi yao ya maji na kunikimbia, "Mungu wangu.....! Kwanini tena jamani naendelea kuziota hizi ndoto za mauaji mimi.....?" Nilijikuta nikiilaumu nafsi yangu kwani ni kweli nilikuwa nikiota ndoto za ajabu ajabu,Eti nimeliona treni limeharibika mpaka nikamuua mzee wa watu na kumvua nguo na kuzivaa mbaya zaidi eti nikaota nimekamatwa na yule mtoto wa huyo Mzee Mhhh...!,
"....Eeeh mwenyezi Mungu niondolee ndoto chafu hizi zisiniandame tena....?" Nikasali kimoyomoyo kisha nikainuka pale chini ya ule mti niliokuwa nimepitiwa na usingizi kisha nikaenda hadi pale wadada walipondondosha ile mitungi yao ya maji na kuanza kukombeleza japo niweze kupata vijimaji kidogo. Jua la Asubuhi likiwa tayari limeshachomoza kabisa na mpaka kufikia leo nilikuwa natimiza siku ya pili bila kupata chochote tumboni zaidi ya hivi vijimaji. Nilikuwa sina jinsi yoyote zaidi ya kuendelea na safari huku nikiwa sijitambui ninapoelekea,nilitembea tena umbali wa kama kilometa sita hivi ndipo nilipokutana na vinyumba vidogo vidogo. Furaha ikanijaa zaidi moyoni mwangu pale nilipowaona watu. "...Wale wadada walionikimbia kulee,mmoja wapo yulee ngoja nimuwahi nimuulize kitu...!" Nikatembea fasta mpaka alipo na nikajua tu hajui kiswahili wala kiingereza kwa hiyo hapa nikutumia njia ya vitendo atanielewa, Safari hii yule dada hakuonesha woga wowote akanipeleka mpaka nyumbani kwao nikakutana na wazazi wao wakanipokea vizuri tu huku wakiongea wenyewe kwa lugha yao. "....Lengula... Pela ine.....!" "...Isa kuno....!" Yule mzee akatoka nje na kurudi na wazee wenzake wakiwa na shauku ya kutaka kunijua kiundani zaidi. "Lengula Mweni.....!" "Pela ine Cilyo.....!" Mara nikashangaa wameleta chakula pamoja na kombe kubwa la maji hivyo nikaanza kuambulia maneno nikajua "kumbe 'Cilyo' inamaana ya chakula...!" Sikukiweza kula kile chakula kwani ilikuwa kama maugali ugali ambayo hayajaiva vizuri yaliyochanganywa na mimboga ya majani iliyoungwa ovyo ovyo tu,Sema kutokana na njaa ya siku mbili niliyokuwa nayo,nilijikuta nafakamia hivyo hivyo na kushushia na yale maji.. "Naomba niongezeni tena maji ya kunywa...." Huku nikioneshea kwa vitendo kuwa nahitaji niongezewe maji, "Pela ine I majie....!" Yule Mzee akamuamlisha mtoto wake aniletee,aliponiletea nikayanywa kisha nikamsikia akimtuma tena kwa mara ya pili yule mtoto. "Ya Na Ubwite Bane Nsansa.....
" Akatoka halafu baada ya muda akarudi na dada mmoja mweupe aliyeonekana kama mtu tofauti na wao kuanzia mavazi hadi nywele zake alivyozitengeneza, "How are you....?" "am fin., wh ar u....?" Nikajua nimeshapata mtetezi wangu kuwa yule dada alikuwa akijua kiingereza lakini nilijiuliza sana ametokea wapi na amejuaje kiingereza maeneo haya,nilijiuliza mara mbili mbili bila ya kupata jibu, "whr ar u cme frm?" "Am frm South Africa to Tanzania..!" Nikamdanganya huku nikiangalia kwa pembeni kwani woga na aibu vilikuwa vimeshakuwa vimenitanda mule ndani huku wale wazee wakitusikiliza kwa ukaribu japokuwa hawakujua chochote pale. "Ar u Tanzanian....?" "Yes of course..." "Waaaooh...! Do u knw how to spk swahil language.....?" "Ndio....." Nikamjibu kwa kiswahili mpaka akashangaa na hakuweza kuamini ndipo nilipoanza kujitambua kuanzia sehemu niliyopo. "Hapa tupo kusini Magharibi mwa Zambia na siyo mbali sana na mpakani mwa Tanzania" "Ulisema unaitwa nani...?" " Brendah BreBre...." Nikamdanganya nikijua kuwa siku akijua kuwa naitwa Levina inaweza ikaleta matatizo yoyote. "Unaskia Brendah...", "Abee...!" "....Hiki kijiji kinaitwa 'Nakonde' ni maarufu sana hapa Zambia na hizi lugha wanazoongea huku ni ki 'Bemba' na ki, 'Njanja' ndicho wanachozungumza sana lakini ki 'Bemba' ndicho tunachozungumza sana,na nadhani umeshakisikia kabla sijaingia hapa..." "Happy..., Nafurahi sana kukufahamu....!" "Hata mimi nafurahi sana Brendah...!" Baada ya pale tukakumbatiana na kutoka na huyo dada anayeitwa 'Happy' na kuongozana naye mpaka kwenye kijumba chao, Jioni ilikuwa imeshatimia huku nakajua nako kakitaka kuzama,nikiwa tayari na ninayemwamini ni mtetezi wangu,nilipewa maji ya kuoga nikajisafisha damu zote zilizogandia mwilini na baada ya hapo alinipa nguo zake nivae kisha akanipa chakula cha usiku, "Kwahiyo Happy...?unasoma au....?"
"Hapana Brendah, Mimi nafanya kazi kulee 'Custom' (Mpakani)tena ni mbali kidogo na hapa huwa nakuja kuchukuliwa na Gari asubuhi sana...!" huku tukiendelea kupiga naye stori nyingi za maisha huku zangu nikizificha ficha asizijue hata kidogo,ilipotimia tena mda wa kulala alinipa shuka na kulala naye katika kitanda chake. Kwa mara nyingine nikafurahia maisha kwani ilipofika asubuhi niliamka kwa furaha zote huku mwili wangu ukisisimka mara kwa mara nadhani ni kutojiamini na mazingira niliyokuwa nayo, Nilivyoamka sikumkuta Happy bali niliambulia kikaratasi kilichoandikwa ujumbe pembeni yangu, Nikakichukuwa na kukisoma. "NAELEKEA OFISINI SAMAHANI SANA BRENDAH KWA KUTOKUAGA.,NISINGEWEZA KUKUAMSHA LAKINI USIHOFU MCHANA NITARUDI TUTAKUWA PAMOJA..UTAJIPIKIA CHAKULA NA MTAKULA HAPO NYUMBANI. Wako Mpendwa HAPPY. Nilipomaliza nilisisimka tena nikatoka nje na kukata mjiti kisha nikachukuwa kikombe cha maji nakuanza kupiga mswaki... *********** * * * Levina kaanza maisha mapya, atadumu hapo? * * * Vipi upande wa Gervas imeishia vipi...?