Story behind your date of birth

Story behind your date of birth

i wonder how these things work out mana most of the people kuna kuendana flani,,even me,,bt where this knowledge come from??!
 
Mkuu mimi nimezaliwa 7 mwezi wa tisa...
Mkuu RadioActive ikiwa wewe umzaliwa Tarehe 7/09 Namba yako ya bahati ni namba 7 (If U were born on the 7th, 16th, 25th of any month then U r number 7.) Kila kitu fanya wewe kuanzia tarehe 7 ya mwezi wowoe ule utafanikiwa. Wewe Nyota yako ni (Virgo)Mashuke Utakuwa na Maelewano na Mtu Mwanamke au Mwaname Mwenye Nyota ya Samaki (PISCES).

MziziMkavu haya mavitu huwa siyaamini.
But nimesoma hapa yangu, inaonyesha kuna Ukweli kwa Mimi. Big up xana.
Mkuu 2013 uamini au usiamini hizi namba zipo na zinafanya kazi yake kama kawaida kazi kwako.
 
MziziMkavu mi nimezaliwa tar 29 mwez wa tatu, naomba kuijua nyota yangu na mambo yote yahusihayo nyota yangu

NYOTA YA PUNDA AU KONDOO (ARIES)

  • Hii ni nyota ya kwanza katika mlolongo wa nyota 12.
  • Wenye nyota hii ni wale waliozaliwa kati ya tarehe 21st March na tarehe 19 April ya mwaka wowote.
  • Sayari yao ni Mars (Mariikh)
  • Siku yao ya bahati ni Jumanne
  • Namba yao ya bahati ni 9
  • Rangi yao ya Bahati ni Nyekundu.
  • Asili yao ni Moto.

NYOTA YA PUNDA AU KONDOO KATIKA MAPENZI NA MAHABA

Kwa vile wao ni wenye nyota ya kwanza mara nyingi wenye nyota hii wanapenda kuwa mbele. Wanakuwa wakarimu na wenye pendo kwa wapenzi wao.
Ni watu wenye kupenda kushirikiana na watu wengine, wanapenda mikusanyiko ya jamii na wacheshi. Ni watu wazuri kuwa nao karibu na mara nyingi wao wanakuwa ndio maisha na roho ya kundi wanalojihusisha nalo. Hivyo inatokana na tabia zao za asili za uchangamfu. Hata hivyo wakiudhiwa huwa ni viumbe wenye hasira kali.
Wenye nyota hii ni wepesi sana kuvunjika moyo na hii inatokea wakati wapenzi wao wanapowaangusha au kuwadharau katika mapenzi ambayo wao wanayachukulia kwa uzito mkubwa.
Pamoja na uchangamfu walio nao wenye nyota ya Punda wana moyo dhaifu usiovumilia matatizo na wanaweza kudhuriwa kirahisi katika mapenzi.
Wanaingia katika mapenzi na kupenda kirahisi. Mara nyingi wanawafanya wapenzi wao ndio nguzo au kiegemezo na hapo ndipo matatizo yanapoanza.
Wasipopata njia ya kutatua matatizo ya kimapenzi huwa wanachanganyikiwa na wanafadhaika sana hasa wanapogundua kwamba wapenzi wao ni binadamu kinyume na walivyofikira wao.
Kwao wazo la kuwa waaminifu kwa mpenzi mmoja milele linapewa kipaumbele katika mambo ya mahaba, lakini wakiona mambo yanaenda kombo basi ni mwepesi sana kuondoka kwenda kutatufa mpenzi mpya sehemu nyingineyo.
Kwa ujumla wenye nyota ya Punda ni watu wenye mapenzi motomoto, tatizo lao kuwa hawapendi kusikiliza ushauri wa kimapenzi, na hawakubaliani na mambo nusu nusu. Ni watu wenye kutegemea mazuri wakati wote na hawakubali kushindwa. Hupenda kukimbilia katika mapenzi bila kufikiri wanapohisi wamepata mpenzi wa kweli. Ni wepesi kuvutwa katika mapenzi na ni wenye miamko ya ghafla au misukumo ya kiwazimu ambayo wakati mwingine inawafanya waonekane wapumbavu.

NYOTA YA PUNDA KATIKA FEDHA

Wenye nyota hii wanapenda sana kutumia nguvu au kulazimisha na siyo waoga. Mipango yao ya kifedha wanayoipanga inakuwa na ubora wa hali ya juu inayopendeza na inayowavutia watu wengine. Hii inatokana na uwezo wao, shauku na vipaji vya kiakili kuhusiana na masuala ya fedha.
Hakuna sehemu yeyote ambayo mwenye nyota ya Punda atafanya shughuli yeyote bila watu kupendezwa na mipango yao. muda wote wako tayari kuchukua majukumu bila kujali chochote na mwisho wake mafaniko yanakuwa makubwa. Suala la kujiliza ni kuwa je wanaweza kufanya hivyo kwa muda mrefu?
Jibu ni hapana watu wa Punda wanatambulika kwa tabia yao ya ufuatiliaji wa mambo, bila kuchoka lakini tabia yao ya kiburi katika mambo madogo madogo ya kibiashara na kikazi wakati mwingine huhatarisha mradi au kazi zao zote.
Wanapenda kutumia fedha kiholela bila kupata uhakika kwamba zitarudi au zipo. Hulka yao ya kuwa mbele na kupenda kuishi kiuaminifu huwafanya wakose kinga kwa wajanja wanao penda kuwatapeli.
Kitu kimoja ni kwamba Mungu amewapa uwezo wa kufanya kazi vizuri wanapokuwa wao viongozi au wasimamizi. Wanakuwa na nia na moyo wa kufanya mambo mapya, lakini ajabu ni kwamba hawana subira wala mbinu za utawala hasa katika masuala ya fedha.
Papara zao za kujua mambo zaidi mara nyingi husababisha utatanishi kwa watu wote wanaowazunguka na wanao wakilisha.
Kimaisha wenye nyota ya Punda wanapenda sifa na kuonyesha matunda ya kazi zao au uwezo wao kifedha kwa kununua magari mazuri, nguo zenye thamani kubwa na vito vya thamani ili waonekane pamoja na ukarimu wao wakati mwingine hubadilika na kuwa wabinafsi na wachoyo.
Kwa ujumla wenye nyota hii ni watu wenye ari na uwezo wa kuanzisha mambo na wanapenda kupata maendeleo ya kimaisha na kuwa na miradi mipya. “NATAKA” ndio neno lao kubwa. Wanahitaji sana fedha, uwezo na uvutio ni wakati mchache sana huangalia maslahi ya watu wengine. Huwa wanakabiliwa na tatizo la kuchagua fedha au mamlaka, hata hivyo mapenzi yao ya kuwa na uwezo huwa yanashinda.
{mospagebreak}

NYOTA YA PUNDA (AFYA ZAO)

Wenye nyota hii ni watu wenye nguvu na afya nzuri. Wakati wote wao wanakuwa hawana subira ya kungoja kufanya shughuli zinazowahusu. Ni watu ambao hawapendi kabisa kuugua au kupata maradhi. Mara nyingi wanakuwa na uwezo wa ajabu wa kupona maradhi yanyaosumbua.
Kwa vile nyota hii ya Punda inatwala kichwa maradhi yao mengi yanahusiana na kuumwa kichwa na homa za mara kwa mara ambazo hupotea kama zilivyokuja.
Tatizo lao kubwa la kiafya ni la “Adrenalini” (Hii ni Homoni inayotoka ndani ya mwili wakati mtu anaposhtushwa au kukasirika, ambayo inafanya moyo upige haraka na kuutayarisha mwili kupambana na khatari). Watu hawa wanafanya kazi bila kuchoka na inatakiwa nguvu zao zielekezwe sehemu inayohusika, ikitokea vinginevyo huwa wanakosa raha na kuwa na wasiwasi.
Wasiwasi huo unasababisha “Adrenalini” kumwagika kwa wingi wanakuwa wepesi kuudhika na kukasirishwa na kuwa na Hamaki au ghadhabu za haraka ambazo huwaletea matatizo ya mzunguko wa damu katika Ubongo na macho.
Watu wa Punda wanahitaji kufahamu kwamba wao hawana kinga hivyo mapumziko ni muhimu kwao. Wanatakiwa wapendelee kutembea kwa miguu au wajihusishe na michezo ili kuondoa mzigo wa uchokozi, hakami na hasira walionao.
Utaratibu maalum wa kula chakula vile vile ni muhimu, na wenye nyota hii wanashauriwa kukiepusha na kahawa na sukari nyeupe ambao inaongeza mfadhaiko katka mfumo wa neva na tezi za “Adrenalini”. Ni wachache sana wenye nyota hii ambao wana matatizo ya uzito kwa sababu wanajishughuoisha sana na shughuli mbalimabli.
Kwa ujumla wenye nyota hii wanapokata tamaa huwa wanaathirika, na tbaia yao ya haraka haraka inawafanya wawe katika vita na miili yao wenyewe. Matokeo yake ni kuathirika kiafya. Wanatakiwa wajifunze tabia ya nyota ya Mizani ya ushirikiano. Tabia hii pamoja na kwamba itawapunguza kasi zoa katika utendaji lakini itawasaidia kudhibiti matatizo yao ya kiafya.

NYOTA YA PUNDA (MAISHA YAO)

Punda wanapenda sana kujihusisha na masuala ya kuwafanya waishi vizuri kama binaadamu wengine. Wanapenda sana vitu vyenye msisimko vya pekee na utaona hivyo katika nyumba zao.
Kuweka makazi ya kudumu kwa mtu wa Punda ni moja ya mitihani mikubwa ambayo ana lazima atekeleze lakini kwa watu wengine jambo hili wanalichukulia kama mojawapo ya mambo mengi ya kimaisha ambayo wakipata fedha anataka watekeleze.
Moja ya hulka za Punda ni kuthibiti namna nyumba zao zinavyoendeshwa. Hivyo inamaanisha kwamba wanahitaji kupata mwenzi mwaminifu ambaye atatekeleza yote atakayoagizwa kuyafanya hapo nyumbani. Vinginevyo tabia zao za kutokupumzika na tamaa ya kufanya mambo mapya itawafanya wapoteze hamu ya maisha yao ya nyumbani.
Wanapokuwa tayari wameweka mizizi yao wanakuwa waaminifu kwa familia zao. Hata hivyo kuna hatari kwamba wasipoweza kupata wanachokitaka hapo nyumbani wanaweza kusimama na kuondoka.
Hawawezi kuficha hisia zao kwa yeyote wanayemualika katika nyumba zao ukikosa atakuambia na hawategemei hata walioalikwa nao kuficha hisia zao vile vile.
Kutokana na shauku na hamu kubwa ya kuthitisha maisha yao, ni vizuri Punda wakawa waangalifu, wasiwe wajeuri au wakandamizaji katika nyumba zao.
Ni watu wanaozipenda familia zao na mara nyingi wanatumia nyumba zao kama sehemu ya kufanyia kazi badala ya mapumziko.

{mospagebreak}

NYOTA YA PUNDA (LIKIZO NA SAFARI)

Nyota ya Punda ni nyota yenye asili ya moto, maana yake ni watu wenye ari na nguvu zisizo na mipaka, na mara nyingi wanatatufa vitu vinavyowafurahisha. Wanapenda sana kusafiri aidha katika biashara au kwa kujifurahisha.
Wenye nyota hii wana tabia ya kujenga uhusiano mkubwa katika tabia fulani. Hii inapotokea wanapenda kutumia muda wao mwingi katika mazingira hayo ili wayaelewe vizuri. Wanajua kabisa sehemu au mji ambao watajisikia wako nyumbani.
Muda mwingi huwa wanapenda mazingira mapya na hii inawafanya kupata uzoefu mkubwa mara nyingi wanakuwa ni waalimu wazuri sana. Ukweli wa mambo ni kwamba walimu wengi wa shule wanaowaongoza wanafunzi katika safari za nje ni wenye nyota ya Punda.
Punda ni wasafiri majasiri na wanapenda vyombo vinavyokwenda kasi. Kwao ni bora kusafiri kwa ndege kuliko kupanda basi linaloenda polepole. Huwa wanapenda kusafiri daraja la kwanza kama wakikosa kabisa basi watasafiri daraja la pili.
Ukiwa katika likizo pamoja na mwenye nyota hii unaweza ukaudhika kwa sababu wao mara nyingi wanatafuta mambo mapya na wanakuwa hawatulii sehemu moja kwa kutegemea ujasiri wao.
Kwa ujumla kwa vile wenye nyota ya Punda ni watu wasiokuwa na subira kwa rafiki zao wa duniani hawapendi kungoja watu wakubaliane na mipango yao ya safari ambayo wanaweza kubadilisha bila taarifa. Kwa sababu hiyo mara nyingi wanasafiri peke yao, au wanaweza kujitenga mbali na walio karibu nao. Hivyo watu wa Punda wanashauriwa kuwa na subira ya kuwangoja wenzi wao katika likizo au safari zao.

NYOTA YA PUNDA (TABIA ZAO)

Tabia ya wenye nyota ya Punda ni wakali na wachangamfu, wenye hisi na wanaoweza kujieleza wakiwa na ari ya kufanya chochote. “SASA HIVI” hivyo ndio mambo wanayotaka kusikia.
Ni watu wasiokuwa na surbira, kila kitu kinafanyika kwa msukumo na haraka haraka. Wenye nyota hii ni viongozi majasiri ambao hawaoni karaha kuchukua majukumu. Wao wakati wote wanajiona kwamba “Wanajua sana”.
Pamoja na kwamba wanakuwa wa kwanza kukamata mambo ya msingi ya jambo lolote wao wanakuwa wa mwisho kuliacha na ni wafuatiliaji wazuri.
Kwa upande mwingine watu hawa wewe wape njia ya kutatua tatizo au ya kufanya jambo jipya, utashangaa jinsi watakavyolichambua na kulitekeleza jambo lenyewe.
Jambo la kushangaza kwa wenye nyota hii ni kwamba tatizo lao kubwa linakuwa kusitasita au kuchelewesha jambo. Pamoja na kwamba wao wanapenda mambo ya haraka lakini yakiwa hayawavutii basi huwa hawana haraka nayo.
Vile vile wanaweza kuwa butu. Mara nyingine hufanya makosa makusudi au kuwachokoza wafanyakazi wenzao kuonyesha ubinafsi wao ili wafanikiwe.
Kwa ujumla wenye nyota hii ni watu ambao wanajipendelea. Ni watu ambao “MIMI KWANZA” ndio tabia yao wanapenda waonekane kwamba wao ndio wanajua zaidi na tabia hiyo inawasaidia, ukweli wa mambo ni kwamba wenye nyota ya punda kila walitakalo wanalipata.
{mospagebreak}

TABIA YA PUNDA (KATIKA NGONO)

Wanapokuwa chumbani, tatizo kubwa la wenye nyota hii ni ubinafsi. Watu wa Punda huwa wanapenda kujishughulisha sana na mambo ya ngono na wanategemea kwamba wapenzi wao nao wajihusishe kikamilifu katika tendo hilo. Wakiona kwamba wapenzi wao hawako makini wakati wa ngono basi hujihisi kwamba hawapendwi na hawatakiwi.
Wenye nyota hii ni watu wenye bashashi na wacheshi na hiyo inawafanya wawe ni watu wenye hisia kali na haraka, hivyo inakuwa vigumu kwao kufanya mambo kwa mpangilioi na pole pole. Hivyo inawafanya wasiweze kuwachezea wapenzi wao kabla ya ngono.
Hisia zao kubwa ni kufanya tendo la ndoa na ni wakati huo huo bila kungoja.
Kutokana na ubinafsi huwa wanasahau kabisa hisia za wapenzi wao. Kwa kweli ni watu ambao wanajipendelea sana katika tendo la ndoa na hiyo huwa inawaletea matatizo katika uhusiano wao wa kimapenzi.
Wakati wanapochagua mpenzi Punda wanashauriwa wahakikishe kabisa wanapata wapenzi ambao wana ashiki au nyege za haraka haraka kama wao.
Katika kipindi cha kubembeleza pendo (kutongoza) watu wa Punda wanatakiwa waonyehse tabia ya asili ya ukarimu na mahaba ili wapendeke na vile vile wajaribu kuachana na tabia yao ya asili ya hisia kali na ukali.
Wanaume wa nyota hii wanapenda sana kujiona kwamba wao ni mabingwa na mashujaa katika ngono.
Kwa ujumla watu wa nyota hii ni wenye kuhitaji sana ngono. Ni watu ambao hawataki kukataliwa. Wanaume wa nyota hii wana ashiki na hamasa za kufanya ngono kuliko kupenda na wanaliangalia hilo wanapotafufa wapenzi kwa wanawake nao wana hamu kubwa ya kufanya tendo la ndoa.
Hakika wenye nyota hii wanaweza kuwa wapenzi wazuri.

NYOTA YA PUNDA (KAZI ZAO)

Wote wake kwa waume waliozaliwa katika nyota hii wana kipaji cha asili cha uongozi na wasiwasi wa kushindwa katika utekelezaji.
Kwao kitu cha pili au wao wenyewe kuwa namba mbili. Wanawake katika hali ya ushindani ambapo wanaweza kutekeleza kazi zao katika spidi au haraka wanayoitaka ambayo mara nyingi inakuwa mara mbili ya spidi ya kawaida, kila kitu kitakuwa sawa.
Wenye nyota hii huwa wanafanya vizuri shughuli zao za kazi au taaluma, mradi shughuli hizo ziwe zinazoleta athari. Hawapendi kuburuzwa wala kuishi bila kupata ushindani ni kawaida mara nyingi katika kazi zao hutokea migongano kati yao na wale wenye mamlaka juu yao. Wanapenda sana kupambana na hali ya ushindani wa kikazi na mara nyingi huwa wakiasisi shughuli mpya au kutoa mawazo mapya. Vile vile wanapenda sana ushindani wa kutafuata kitu kilichopotea.
Watu wa Punda ni watu ambao wanaweza kuhisi jambo lolote, ni watu wanaopenda kutumia nguvu katika kazi na wakifanya kazi yoyote wanaifanya kwa moyo mmoja. Wakiwa katika kazi, hupenda kufanya kazi peke yao au katika kazi hiyo wawe ni wasimamizi.
Kwa ujumla kwa vile watu wa Punda wanafanikiwa katika ushindani wanafurahi sana wanapofanya kazi ambazo zenye vipingamizi na ambazo utekelezaji wake unahitaji akili nyingi na nguvu.
Watu wa aina hii wakishindwa kutekeleza majukumu yao huwa wanavunjika moyo vibaya sana. Wanapenda sana kufanya kazi katika mazingira ambayo yanahitaji muda maalum kutekeleza mambo fulani.
{mospagebreak}

NYOTA YA PUNDA (FAMILIA ZAO)

Wazazi wenye nyota ya Punda wanakuwa wakarimu sana kwa watotowacheshi watafanya kila njia kuwahimiza wawe huru na watawaruhusu wafanye majaribio mbali mbali ya kimaisha na kuwahimiza kuchukua majukumu makubwa kwa gharama yeyote. vile vile watawahimiza watoto wao wawe na tabia ya ushindani badala ya kuwafundisha michezo.
Wazazi wenye nyota hii watawapa watoto wao nafasi kujisimamia wenyewe katika mambo yao. tatizo lao moja ni kuwa hawapendi watoto ambao ni ving’ang’anizi na wanaohofia usalama wao.
Watoto ambao ni waangalifu waoge na wanaofanya mambo kwa kufikiria wanakuwa hawaendani sana na wazazi wenye nyota ya Punda kwa sababu Punda hawapendi watoto wenye haya, waoga na wepesi kutishwa.
Wazazi wa nyota hii wanaweza kuwa wakali, wasiokuwa na mbinu na wenye kauli za ukali ambazo zinaweza kuudhi mtoto yeyote mwenye moyo mdogo. Tabia hii mara nyingi inasababisha migongano kati ya mzazi na mtoto na kutokuelewena kunakuwa kukubwa.
Wazazi wa Punda wanashauriwa kujilinda katika kuwashinikiza watoto wao kwa nguvu na haraka na kuwaruhusu watoto hao wakue na wafanye vitu katika njia za kawaida.
Kwa ujumla wazazi wa Punda ni wenye msukumo lakini wanajivunia sana watoto wao ni wazazi wenye makaka na wanapenda sana utani kwa vile hata wao mioyo yao ni ya kitoto. Mzazi wa kike anapenda ushindani hasa katika mausuala ya maisha na kuishi lakini hata yeye anapenda utani hasa anapokuwa nyumbani.

NYOTA YA PUNDA (MAUMBO YAO)

Wenye nyota ya Punda ni wenye uso mrefu mpana paji lao la uso hutanuka likiambatana na fuvu lililokaa vizuri. Macho yao ni makali na yenye kuonyesha uzima na uhai na yaliyotumbukia kwa ndani.
Nyusi zao ni nyeusi zenye kuonekana wazi au zilizo dhahiri kama zimepakwa wanja. Pua zao ni za bapa na midomo yao ni mipana.
Unapozungumza na wenye nyota hii naye atakusimamia wima mbele yako na kukuangalia moja kwa moja kwenye macho yako.
Tabia yao hiyo inawafanya waonekane wao ni wenye tabia za kigomvi au ushauri lakini ukiangalia kwa undani utagundua kwamba ni wakweli na wanaoweza kuaminiwa.
Hata hivyo kipindi cha kukusimamia wima inakuwa kifupi hasa anapokuona mpuuzi.
Kimaumbile ni watu wepesi na mwendo wao ni wa madaha. Miili yao kidogo imeinamia mbele ya misuli yao inaonekana imekakamaa, hiyo ni kwa sababu ya kujishughulisha sana bila kupumzika.
Sifa za wanaume wa Punda ni kwamba wako makini na wenye msimamo. Ni wembamba na miili yao ni yenye misuli iliyojikunja kunja.
Wanawake nao ni wembamba na maumbile yao siyo ya kupendeza sana, mikono yao na miguu yao ni yenye nguvu. Matamanio yao na uwezo wao huwa inawafanya wawe wanawake wenye tabia za kiume.
Kwa ujumla alama ya Kondoo ni pembe zake na mambo yote yanayohusiana na pembe hizo. Wenye nyota hii wanapenda kupambana na maisha. Kimaumbile athari zao huonekana mara moja. Kama vile kujiamini, namna wanavyosalimia watu na vicheko vyao. Vitendo vyao hivyo vinakujulisha kwamba huyu ni Punda.
{mospagebreak}

NYOTA YA PUNDA (VYAKULA VYAO)

Kama ilivyo katika tabia zao wenye nyota ya Punda vile vile wanapenda vyakula vya haraka haraka.
Ukweli ni kwamba mawazo yao mara nyingi yanakuwa katika maisha kuliko chakula pamoja na kwamba wanakuwa na hamu na uwezo mkubwa wa kula. Wanapenda chakula kizuri lakini kiwe cha haraka na rahisi kutayarisha.
Wanapenda sana kufanya karamu tafrija ambazo wana kipaji kikubwa cha kuzitayarisha na wanazifurahia. Katika karamu hizo vyakula vyao vinakuwa vya haraka ambavyo vinagawiwa wima wima bila kucheleweshwa.
Wakati wanapokuwa hawafanyi karamu au tafrija wanapenda chakula chochote kinachotayarishwa upensi na ambacho kinaweza kulika huko wanatembea, kama vile asusa na vyakula vyepesi kama biskuti, chipsi n.k.
Wanapenda ladha iwe nyepesi na viwe na pili pili na viungo vingi. wanapenda sana vyakula vinavyopooza au kutuliza njaa kama viazi, tambi na maziwa.
Huwa wanapenda sana ladha za uchachu kama limao limao au ndimu ndimu au mbilimbili vile vile wanapenda sana mkate na Jibini au vyakula vilivyo kaangwa kama nyama.
Wanatakiwa wawe waangalifu katika kula mafuta hasa vyakula vya kipuuzi puuzi ambavyo vinaweza kuwaletea madhara.
Kwa ujumla wenye nyota hii wanapenda sana tafrija, na vyakula wanapenda viwe vile vinavyotayarishwa mbele ya wageni na viwe vilivyokaangwa na vyenye ladha nzuri. Vyakula hivyo viwe ni vyepesi kutayarisha visivyopoteza muda.

NYOTA YA PUNDA (VIPAJI VYAO)

Wenye nyota hii wanapenda sana kupambana na maisha na wanakuwa na mambo mengi sana vichwani mwao kiasi kwamba wakati mwingine wanasahau vipaji vyao vya asili.
Tabia hiyo waliyo nayo haiwapi muda wa kufanya mambo mengine kama ya ubunifu. Kwa asili, wao ni watu wabunifu na wakati mwingine wanapata wasiwasi katika ubunifu wao.
Kuna wakati wenye nyota hii wanashindwa kutofautisha kati ya vipaji vyao na matakwa yao. ambayo yanakuwa makubwa na yenye shinikizo. Watapata msaada katika hili iwapo watafanya jitihada za maksudi za kuwasiliana na busara zao za asili kuwa kupata mapumziko na kufanya taamuli (Meditation).
Kipaji cha wenye nyota hii kinahusiana na kichwa ambacho ndio nyota yao inapotawala hivyo “Frenologia” (Ujuzi wa tabia ya mtu kwa umbo la kichwa chake iko chini ya nyota hii.
Kwa kuongezea wenye nyota hii wana kipaji cha kutafsiri ndoto na kipaji cha kusikia sauti ndani ya kichwa.
Kwa ujumla watu wa Punda wanapenda njia ya utabiri ambazo zinatoa matokeo ya haraka kama vile kutumia karata , dhumna, au dadu (dice).
Taamuli (meditation) ni jina au mbinu nzuri kwa wenye nyota hii kuongeza kipaji chao. Ikiwa watafanya taamuli kwa dakika ishirini wakati wa usiku au kitu cha kwanza wanapoamka asubuhi, akili na miili yao itatuliza. Hivyo itawafanya wawe na uwezo wa kutumia nguvu zao za kimwili na kiakili pamoja na kuendeleza au kukuza vipaji vyao.
{mospagebreak}

NYOTA YA PUNDA (BAHATI ZAO)

Watu wa nyota hii wana tabia ya kitoto ya kuamini kwamba mazuri yatatokea kwa amri ya Mungu. Kwa hiyo inawawia vigumu kufikiria uwezekano wa kushindwa katika jambo lolote.
Wakiwa ni waliozaliwa katika nyota yenye kuasisi mambo, wengi wao hudharau kutopata matumaini katika jambo moja na kurukia jambo lingine.
Kwa sababu shauku yao ni ya kuambukiza mara nyingi hufanikiwa kuwashawishi wengine wakubali kuongozwa nao hata kama kuna khatari.
Mara nyingi hawana muda wa kutoa mashitaka wala kuwaza makosa yaliyofanyika mwanzoni, wao wanaamini kwamba wakati wote mafankii yapo na kwa vile wamezaliw ana roho ya ujasiri wa kupenda vituko wako tayari wakati wowote kuyaweka maisha yao katika hatari ili wafanikiwe.
Tabia yao ya kutojali na misukumo au mihemko ya ghafla inawafanya wawe na sifa zilizokithiri za kubahatisha mambo.
Hakimu kwa bahati, hii kwao inakuw asiyo tatizo kwa sababu hawafanya kitu kimoja kwa muda mrefu, ghafla huwa wanarukia katika jambo lingine.
Watu wa Punda wana moyo wa ujasiri wa ushindani na wanafanya vizuri iwapo katika hali hiyo kutakuwa na uadui hasa mtu na mtu.
Katika michezo ya karata ua kupimana nguvu au kuwekeana dau watu wa Punda wana pata bahati sana.
Kwa ujumla watu wa nyota hii wanapenda kubahatika na wanachukia sana kukosa pamoja na kwamba faida zoa wanazopata zinalingana na hasara zinazowafika.

NYOTA YA PUNDA (URAFIKI)

Wenye nyota ya Punda ni wachangamfu, wanaosema kweli na wenye uwazi katika urafiki wao. Kama walivyo katika kila kitu kwenye maisha yao.
Ni wazuri katika kuanzisha urafiki, wakati mwingine wanakuwa wawazi sana katika mazungumzo yao na vitendo vyao kiasi kwamba huwaogopesha baadhi ya marafiki.
Kwa upande mwingine wao wanapendwa kwa sababu ya uaminifu wao na kusema kweli.
Watu wa Punda wanathamini sana uhuru wao na wanapenda kufanya vitu katika njia zao wanachukia sana kufugika au kuogopa watu kwa hiyo urafiki sio kitu muhimu kwa wenye nyota hii . wakati mwingine huwa wanajisikia furaha wanapokuwa katika kundi la watu wanaopenda vituko na mambo ya ajabu.
Watu wa Punda wako katika kundi moja na wale wenye nyota zenye asili ya moto na tabia zao zinafanana. Mfano wale wenye nyota ya Mshale wanakuwa marafiki wao wazuri ambao wanachangia tabia ya kupenda vituko.
Hata hivyo huwa hawapendi au hawaoni umuhimu wa kuwa na rafiki mwenye nyota ya Mapacha. Kwa wenye nyota ya Ndoo kwa vile wanathamini uhuru wao basi wao wanaweza kuelewana nao.
Watu wenye nyota zenye asili ya udongo Mbuzi, Ng’ombe na Mashuke wanakuwa marafiki wazuri wa Punda kwa Sababu wanamsaidia kutekeleza mipango yake kivitendo, pamoja na kwamba madhari na akili za hao Ngo’ombe, Mbuzi na Mashuke kupunguza nguvu ya urafiki wa kudumu.
{mospagebreak}
Kwa ujumla wote wenye nyota zenye asili ya moto mara kwa mara wanakuwa na tofauti na wenye nyota ya Punda hasa katika masuala ya ushindani mfano ni nyota ya simba na Punda wote huwa wananeemeka kutokana na uadui usioepukika katika urafiki wao, kama ikiwa katika kazi au nyumbani au kwenye starehe au wanapokuwa pamoja katika michezo.

NYOTA YA PUNDA (MITINDO)

Mitindo ya Punda ni yenye kuchangamka na nguo zisizo na madoido. Wanapenda wawe wanavaa kulingana na wakati. Mavazi yao huwa yanaambatana na mabegi, saa nzuri au mikufu na vito vyenye kupendeza.
Hata hivyo watu wa Punda hawapendi kupanga kununua au kushona nguo. Wanapendeza sana wakiwa katika mavazi ambayo ni mepesi kuliko nguo zile zilizosanifiwa na zenye madaha.
Suti zilizotafauti yaani suruali na koti tofauti, zikiambatana na buti pamoja na skafu na glavu ndio mavazi hasa na nyota ya Punda. Mavazi hayo yanaendana hasa na tabia yao ya ujasiri na mambo ya ajabu.
Wengi wenye nyota hii huwa wanapenda kuvaa suti za michezo ambazo pia zinaendana na namna yao ya maisha.
Wanapoamua kuvaa nguo, waume kwa wake wanakuwa wavaaji wazuri. Wanapenda nguo zilizoshonwa vizuri na zinazoeleweka.
Rangi zao zinakuwa Nyekundu na Njano na mara nyingi hupendelea nguo zisizo na nakshi.
Wanapenda mitindo thabiti na vitambaa ambavyo ni vyepesi kuvitunza. Wanawake wanapenda sana mikufu ya dhahabu na hereni za kuning’inia.
Kwa ujumla watu wa punda wanapenda kuvaa kulingana na mitindo na wanapenda nguo ambazo zinawafanya watu wakiwaona washituke wakiamua kuvaa nguo maalum basi mavazi hayo yataambatana na vitu vya ziada kama mikufu. Pete, saa visivyo ghali. Hiyo huwainawafanya waonekane na wakati katika mavazi ya aina yeyote.

NYOTA YA PUNDA (TASWIRA YA UMBO)

Inapofikia hali ya kuweka miili katika hali bora wenye nyota hii wana bahati kubwa kutokana na hali halisi ya maisha yao ya kujishughulisha. Kwa kuongezea labda wawe wanapenda kula lakini kama ilivyoanishwa na nyota yao ni watu ambao hawapendi sana vyakula vinavyoweza kuwaletea unene.
Hata hivyo wanafurahia chakula na wanapenda vyakula vyepesi. Kama ikiwa Kalori zinazoingia mwilini zinazidi zinazotoka basi uzito wao huongezeka.
Inapofikia hali ya kupunguza uzito wenye nyota hii wanakuwa hawana subira, wanapenda mlo ambao utapunguza uzito wao upesi na katika muda mfupi inavyowezekana ikiwa ni pamoja na kujiadhibu wenyewe kwa kujimyima chakula kwa muda mfupi wakiwa na imani yakupata matokeo.
Kwa wenye nyota hii muda wa siku chache au hata wiki moja ni muda tosha wa kujinyima chakula ili kupunguza unene.
Baada ya hapo ni juu yao kuwa na ratiba maalum ya ulaji wao ikiambatana na mazoezi ya kila siku, kama kuongelea, kukimbia, au kutembea kwa nguvu kwa muda mrefu wenye nyota hii wanahitaji mazoezi ya kila siku ili waweze kupunguza uzito. Vinginevyo itawawia vigumu baadaye.
{mospagebreak}
Kwa ujumla wenye nyota hii huwa wanapata uzito mkubwa kwa sababu huwa wanajishughulisha sana kula milo ya kawaida ikiambatana na vitu vitamu vilivyojaa Kalori wanapokuwa wamechoka.
Wanashauriwa kutumia muda wao kula tu milo ya kawaida hiyo itawasaidia kuondoa au kupunguza unene na kuboresha afya zao.

NYOTA YA PUNDA (USHINDANI NA UADUI)

Wenye nyota hii wanapenda sana ushindani na kuonyesha madaraka na uwezo wao, kwa sababu hii wanachukiwa na watu wengi. Wanapenda sana wawe wa kwanza na watatumia mbinu zozote ili wafanikiwe.
Punda wako wazi na waaminifu katika malengo yao ni watu wenye kusema ukweli na haamini visingizio, ulaghai wala kuficha siri.
Wanapenda kufanya mipango yao moja kwa moja na mtu yeyote akiingilia huwa unazuka ugomvi. Ikitokea hivi watu wa Punda huwaeleza wagomvi wao bila kuficha kinachoendelea.
Kutokana na ukweli na uwazi wao wenye nyota hii huwaudhi sana watu wengine kwa maneno yao na vitendo vyao.
Ni tabia yao kutojali hisia za watu na wala hawana muda wa kufikiri, maneno wanayosema au vitendo vyao vitawaathiri vipi wenzao.
Mara nyingi watu wa Punda, hushinda vita vyao kutokana na uwezo wao na nguvu zao za ukatili lakini ikitokea pakatakiwa kujieleza au kutoa hoja au diplomasia huwa wanashindwa kujieleza.
Wakiwa katika siasa hali ya uadui huibuka kutoka kila upande, wao huneemeka sana Kisiasa kutokana na upinzani na uadui mkali uliopo duniani ambao wao hufurahia.
Kwa ujumla watu wa Punda ni washindani katika sehehmu zote, ni madereva wanaopenda kwenda kasi hivyo wanapenda mashindnao ya magari. Mara nyingi watu wa nyota hii wanapenda michezo yenye ushindani au kutumia nguvu ikiwa kama jambo la kupitisha muda au kazi yake, na hii inawapa changamoto katika kuendeleza ushindani wao wa Asili.

NYOTA YA PUNDA (MANUNUZI)

Kama tulivyoona tangu mwanzo wenye nyota hii wanapenda ushindani, kushughulika na vitendo na hawapendi kabisa kufuata utaratibu kwa hivyo kununua vitu ni mojawapo wa mambo wanayoyapenda sana.
Vile vile wanapenda kupungua na kupanda kwa manunuzi au msisimko wa kwenda dukani katika mitaa inayopendeza au katika nchi za nje.
Wenye nyota hii wanapokwenda kufanya ununuzi hufanya juhudi ya kuamka mapema ili wawakwepe watu, na manunuzi yao wanayafanya haraka haraka.
Huwa wanakwenda kutoka duka moja hadi jingine wakizunguka kiuerevu kufanya manunuzi.
Wanapenda kununua vitu vya wiki nzima na orodha yao lazima vitakuwepo vyakula vya kupikwa kwa haraka au vya kuliwa papo kwa papo kama nyama za kopo au Samaki wa Kopo. Mara nyingi hawana muda wa kupika na hawapendi kutumia muda wao mwingi jikoni.
Kwa hiyo kitu ambacho hawa watu wa Punda wanapenda kununua. Jibu ni kwamba wanunue chochote ambacho kitaharakisha mwendo wa maisha yao.
Mfano wanapenda magari yanayo kwenda kasi au vitu ambavyo wanaviota, kama ramani, glavu za kuendesha gari na viatu.
Kwa ujumla watu wa Punda huwa hawapendi kwenda dukani kila siku lakini wanaona raha ikiwa kwa kufanya hivyo watapata ushindani.
Wanapenda kushindana na rafiki zao ili kuonyesha nani atanunua mwanzo na kitu kizuri au kubishana katika bei ya kitu fulani, hiyo inawafanya wajisikie raha sana

Mwanamme Au Mwanamke Mwenye Nyota ya (Aries) Punda Atakuwa na Mapenzi ya Ukweli Pamoja na Maelewano na.Mtu Mwenye Nyota ya(Libra) Mizani.

Ukiwa na shida ya kimaisha mambo yako hayaendi huna bahati kazini au unataka upate cheo kazini au unataka yako Pete ya Bahati au una Maradhi yasiyopona Ma-Hospitalini au unataka kuowa mke au Mwanamke kuolewa na mchumba wako.Au unataka ufumbuzi wa mambo yako yaliyo kwama kimaisha unaweza kunitafuta kwa kubonyeza hapa.Mawasiliano
 
Mkuu RadioActive ikiwa wewe umzaliwa Tarehe 7/09 Namba yako ya bahati ni namba 7 (If U were born on the 7th, 16th, 25th of any month then U r number 7.) Kila kitu fanya wewe kuanzia tarehe 7 ya mwezi wowoe ule utafanikiwa. Wewe Nyota yako ni (Virgo)Mashuke Utakuwa na Maelewano na Mtu Mwanamke au Mwaname Mwenye Nyota ya Samaki (PISCES).

Mkuu 2013 uamini au usiamini hizi namba zipo na zinafanya kazi yake kama kawaida kazi kwako.

Naomba uNitajie tarehe 13 mwezi wa 9. Namba ya bahati?
 
Kwenye maelezo yako kuhusu nyota hapo juu umenichanganya sana. Umeandika kuwa mwenye nyota ya pisces yani samaki na virgo au mashuke ndo wanatakiwa kuoana kwa mujibu wa nyota zao.

Swali linakuja kwenye namba mfano namba 5 best match wake ni namba 1,2,6,8 na 9 kama sijakosea, ukifuatilia unakuta mwenye nyota ya hivyo ana namba tofauti na hizo hapo inakuwaje?
Mambo ya nyota na namba ni vitu Tofauti unaweza ukawa na nyota nzuri ila namba ukawa na tofauti vile usivyotarajia. Utabiri wa Namba na Utabiri wa Nyota ni vitu tofauti kabisa.
 
Yangu ni tarehe 26 oktoba,inakuaje hapo?
Mkuu Namba yako ya bahati ni hiz hapa namba1,4, 8. Na namba 5 (If U were born on the 8th,17th,26th of any month then U r number 8..)

NUMBER 8

You are a very strong personality, there's no one out there will understand you. You are very good at pointing your finger at some thing and say "this is

what".
You are more likely to suffer from the early ages. I mean poverty. If your times are not good you might lose either of your parent and end up looking

after your entire family. You often suffer all the way in life.

The problems will not allow you to study further, but you will learn the life in a very practical way. You are the one who will fight for justice and may

die in the war too. You are normally very reserved with handful of friends and most of the time live life lonely and always prepared to help others.

Well. once you get married (which is often late) then your bad lucks will go away a bit and you! u become safe. You will face un-expected problems

such as : the error, government, poisonous animals, accidents.

You are some one with great discipline, persistence, courage, strength which will take you to success. You are a great part of a family team. You are a

fighter!

Your Best match 1 ,4, 8. Good match 5 !!!
 
Naomba uNitajie tarehe 13 mwezi wa 9. Namba ya bahati?
If U were born on the 4th, 13th, 22nd, 31st of any month then U r number ( 4..) Namba yako ya Bahati ni Namba (4)

Your best Match 1, 8. Good match 5 ,6 , 7 !!! Ukiwa nampenzi mwenye kuzaliwa Tareh 1 au Tarehe 8 basi huyo mpenzi atakuwa ana maelewano na wewe mazuri. Marafiki watafute wenye kuzaliwa Tarehe 5 ,6 , 7 mwezi wowote ule ndio Marafi utakao elewana nao fuatilia utaona matokeo yake. Kisha uje unipe Feedback


NUMBER 4

You are very stubborn too, very hard working but unlucky in important matters in life, very cool, helpful, you have rough word power.. Might put lots

of people away from you, you may cause nuisance to others if you are a man, and you often understands others and their problems well. If you are a

girl you are very good with studies and arts. If you are a guy you spend most of the time after girl friends (almost) at times, you will have sort of too

much fun life with mates & girls. Your friends will spend your time & money and get away with their life and you will become empty handed and don't

know what to do... So be careful!! You love to spend anyway!!!

Your good will is you are always there to help family and friends. Tell you what you people are little gem! s, specially the girls.. You always fall in love

in younger age as well. You often live with disappointments, for an example you have got a degree in some thing... but you will be unemployed.. or will

do very ordinary jobs.

But you will take care of your family very well...All you need to be careful of people who will take advantage of your kind heart. And beware of your

relations too..

You are radical, patient, persistent,a bit old-fashioned, you live with foundation & order...

Your best Match 1, 8. Good match 5 ,6 , 7 !!!
 
Mimi naendana na nan trh yangu ni22/3
Wewe Ukiwa ni Mwanamme Au Mwanamke Nyota yako ni (Aries)Punda Utakuwa na Maelewano na Mtu Mwenye Nyota ya(Libra) Mizani aliyezaliwa Toka Kati ya Tarehe 23 September na 22 Oktoba ya mwaka wowote
 
shukrani saaana mkuu....kwa maana hiyo kama 1,2,9 na 6,8 so kama ikiwa mwezi wa 3 yaani tarehe 1 mwezi 3 hakuna kitu maana haija match...inakuwaje hapo..? na katika ku match inaamaana kitu chochote utakachofanya iwe kuhama eneo moja kwenda jingine..kutafuta mchumba...kuomba kazi..naomba unieleweshe mkuu...usichoke
ınategemea Tarehe gani umezaliwa? Kila Tarehe inakubaliana na tarehe yake muhimu. Na kuhus ku (Match) Kuelewana na hiyo Tarehe kwa mfano Mtu aliye zaliwa Tarehe 6 au Tarehe 15 au Tarehe 28 mwezi wowote ule, (If U were born on the 6th, 15th, 24th of any month then U r number 6..) namba yake ya Tarehe ya Bahari itakuwa ni Tarehe 6 mwezi wowoe ule. Kwa Mfano ukicheza bahati nasibu kwa tare hiyo (6) ujuwe unaweza kushinda hiyo Bahati nasibu au ukitaka kusafiri au kuowa mke au kuanza biashara mpya hiyo ndio Tarehe yako ya kufanikiwa kwa kila kitu katika maisha yako. Namba zako muhimu katika Maisha yako ni Tarehe 1,6,9. (Your best match 1, 6, 9. Good match 4, 5 !!!) Na watu ukitaka kuelewana nao wawe wamezaliwa tarehe 4 au tarehe 5 mwezi wowote ule ndivyo ilivyo Mkuu.
 
Mi nimezaliwa 13/4 na mpenzi wangu 2/7 ,mbona mambo yanakwenda vizuri tu.
Wewe umezaliwa Taarehe 13/4 una nyota ya Ng'ombe tabia yake ni udongo baridi, wakati mpenzi wako amezaliwa Tarehe 2/7 ana nyota ya Kaa tabia yake ni maji baridi munaelewana hakuna tabu hapo.
 
MziziMkavu, Mimi nimezaliwa July 27th naomba nipe maelekezo yangu.
Wewe Kwakuwa umezaliwa Tarehe July 27 Namba yako ya Bahati ni namba (9) If U were born on the 9th,18th,27th of any month then U r number 9... Your Best match 3, 5, 6, 9. Good match 2 . Namba zingine nzuri kwako ni namba ya Tarehe 3,5,6, na 9 yenyewe. mtu wa kuwa na karibuna wewe awe ana namba ya tarehe 2 atakuwa mtu mtakae elewana sana na wewe.

NUMBER 9

Hey...you guys are the incompatibles people in the world. You are so strong, physically and mentally... You are often have big-aims. You will work hard

and hard to get there. Normally you suffer in the early age from family problems and generally you will have fighting life.. But when you achieve what

you have done, it's always a big task you have done! You are so much respected in the community, you are a person who can make a challenge and

successfully finish the matter off.

You are very naughty in your younger age, often beaten up by your parents and involve in fights and you seemed to have lots of injuries in your life

time. But when u grow you become calm and macho type.

Love is not an easy matter for you. You are good in engineering or banking jobs coz people always trust you.

Your family life is very good, but will have worries over your children.

Your such qualities are humanitarian, patient, very wise & compassionate.

You are born to achieve targets and serve every one all equally without any prejudice.

You are totally a role model to anybody in the world for a great inspiration.

Your Best match 3, 5, 6, 9. Good match 2

 
Nakupa yangu....20/02.
Mkuu Kwa kuwa wewe umezaliwa Tarehe 20/02 Namba yako ya Bahati ni namba 2 If U were born on the 2nd, 11th, 20th, 29th of any month then U r number 2... Namba nzuri Kwako ni namba 5 na namba 9.

NUMBER 2

No matter what, you will be loved by every one coz your ruler is the moon and every one loves the Moon. Well.. You are a person who day dream a lot,

you have very low-self confidence, you need back up for every move in your life, you are very much unpredictable. Means you do change according to

time and circumstances, kind a selfish, have a very strong sense of musical, artistic talent, verbal communication.

Your attitudes are like the Moon, comes to gloom and fade away so everybody can expect changes in you. You can be a next Mahatma Gandhi who does

peace love or you can be a Hitler who wants to destroy the man kind and peace (I mean in the community and your own home).

If you really have a deep thought about your own believe in God you can feel the difference which will make you stronger! Most of the time your words

are a kind of would be happening true! So without any knowledge you can predict the situation. You will become poets, writers, any Artistic business

people!

You are not strong in love, so you will be there and here till you get marry.. If U r a girl you will be a responsible woman in the whole family. If U r

a man you will involve in fights & arguments in the family or Vice-versa. Means you will sacrifice your life for the goodness sake of

Your family...You are gentle , intuitive with a broad vision, a power behind the scenes, well balanced People!!!

Your best match is 2 ,5 ,9 no other people can put up with you !!!

 
Mh mh mzizi Mimi no 8 mjew Wangu no 2 jamani that's explains kwanini sjuhzi sikosi kwnye lile jukwaa la wapweke la mshana jr duh..mamaaa weee
 
Mimi nimezaliwa tarehe 23 March. Hii imekaaje mkuu MziziMkavu?
Kwa kuwa wewe umezaliwa Tarehe 23/03 Namba yako ya Bahati ni namba 5. If U were born on the 5th, 14th, 23rd of any month then U r number 5... Namba nzuri kwako kuweza kushirikiana na watu wenye namba hizi 1,2, na 9. na namba 6 na namba 8 Your best match 1 ,2 ,9. Good match 6 ,8 !!!

NUMBER 5

You are very popular within the community, you can get things done by just chatting..to even enemies! You have a pretty good business mind, you are

often have no-idea what is today is like, or tomorrow is like, you are a person who does anything when your head thinks "lets do this". You will be

famous if you open up a business, get involve in share dealings, music etc.. Very popular with sense of humor ,you are the one your friends and families

will always ask for help, and you are the one actually get money on credit and help your friends. You will have more than 1 relationship, but when u

get settle down you will be a bit selfish anyway. Coz your other half will have a pretty good amount of control in you, be careful! You tend to go for

other relationships! Contacts even you are married at times 'coz your popularity..

You are someone who get along with anyone coz the number 5 is the middle number.. Changes & freedom lovers you are! You are an explorer with magic

on your face. You learn your life through experience and it's your best teacher!!!

Your best match 1 ,2 ,9. Good match 6 ,8 !!!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom