Bishop Hiluka
JF-Expert Member
- Aug 12, 2011
- 7,147
- 14,711
- Thread starter
- #181
Taxi - (57)
Huyu Joyce alikuwa na nini hasa kilichomfanya Madame Norah afanye yale asiyokusudia kuyafanya? Hata hivyo, kitu kimoja alichokuwa na uhakika nacho ni kwamba alijisikia furaha sana moyoni kila alipoamua kumsaidia Joyce, basi!
Baada ya kitambo kirefu cha majadiliano kati yao, Madame Norah aliaga na kuondoka akiwaacha Joyce na Nyaso wanakamilisha maandalizi ya mradi ule.
* * * * *
Baada ya kutoka eneo la Karakata, Sammy alimchukua mtu mmoja aliyemkuta Jet Club na kumpeleka katika ofisi za Kampuni ya Magazeti ya Serikali (TSN) zilizopo barabara ya Mandela, katika eneo la Tazara.
Alimwacha yule abiria pale TSN kisha akageuza gari lake na kutaka kuingia katika barabara ya Mandela akitaka kwenda Ilala Sharif Shamba, mara akamuona mwanamume mmoja raia wa kigeni aliyekuwa anatokea ndani ya majengo ya kituo cha Mamlaka ya Reli ya Tanzania na Zambia (Tazara) aliyemjia mbio huku akimpungia mkono.
Alikuwa mwanamume wa makamo, mrefu na kipande cha mtu aliyejazia vyema. Mwili wake ulichorwa michoro mbalimbali na alikuwa amevaa fulana nyeusi ya mikono mifupi, kaptura ya rangi ya khaki yenye mifuko mikubwa pembeni na miguuni alivaa raba. Mgongoni alikuwa amebeba begi kubwa la safari.
Sammy aliamua kumsubiri. Hata hivyo, alikuwa amesimama katikati ya barabara ya mchepuko iliyotokea katika jengo la TSN na hivyo kuzuia magari mengine. Gari moja aina ya Toyota RAV4 jeusi lililokuwa nyuma yake likitaka kuingia katika barabara ya Mandela lilianza kupiga honi, dereva wa gari lile alionekana kutokuwa na uvumilivu.
Sammy aliendelea kusubiri pasipo kumjali yule dereva wa RAV4 aliyeendelea kupiga honi kwa fujo. Hakutaka kumkosa yule abiria Mzungu aliyekuwa akivuka barabara ya Mandela akionekana kuwa na safari muhimu.
Baada ya dakika takriban mbili yule mwanamume alifanikiwa kuvuka ile barabara na kufungua mlango wa nyuma wa gari la Sammy kisha aliliweka begi lake na kuingia, akakaa katika siti ya nyuma.
“Airport please… and thanks for waiting,” (Kiwanja cha Ndege tafadhali… na ahsante kwa kusubiri) alisema yule mwanamume wa kizungu huku akijiegemeza kwenye siti.
Sammy aliliondoa gari lake na kungia katika barabara ya Mandela bila kumjibu chochote yule mwanamume wa kizungu kisha akakata kushoto akiifuata barabara ya Nyerere iliyoelekea Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere.
Muda ule wa mchana barabara ya Nyerere haikuwa na msongamano mkubwa wa magari, hivyo Sammy alikuwa akiendesha kwa mwendo wa kasi. Walikuwa kimya kabisa.
Kufumba na kufumbua gari lilikuwa likiivuka yadi ya kuhifadhi makontena ya African Inland Container Depot (AFICD) katika eneo maarufu la Mchicha na sasa walikuwa wakilisogelea eneo la Karakana ya Tazara, hapo yule mzungu akakohoa kidogo kusafisha koo lake kisha akaanzisha mazungumzo.
“Do you know English?” (Unajua Kiingereza?) yule mzungu alimuuliza Sammy huku akiachia tabasamu pana la kirafiki.
“Yes,” Sammy alijibu kwa ufupi bila kumtazama yule mwanamume.
“How did you get this car? I real like it, it’s a unique type of taxi that everyone should want to use it,” (Umeipataje hii gari? Nimeipenda sana, ni aina ya teksi yenye upekee ambayo kila mtu angependa kupanda) yule mzungu alimuuliza Sammy huku akimtazama kwa makini.
Sammy aliachia tabasamu huku akimtupia jicho yule abiria wake kupitia kioo cha katikati cha gari kinachotumika kuangalia nyuma.
“You know…” (Unajua…) Sammy alianza kujieleza lakini akasita baada ya kumuona Winifrida akiwa hajavaa sare za shule na badala yake alivaa suruali ya kubana ya jeans rangi ya samawati yenye matobo mapajani na kitopu cheupe na mgongoni alikuwa amebeba begi lake la madaftari.
Winifrida alikuwa ameongozana na kijana mmoja wa kiume aliyekadiriwa kuwa na miaka ishirini na ishirini na mbili, akiwa amevaa suruali nyeupe ya jeans na fulana nyeusi, kichwani alivaa kofia nyeusi ya kapelo. Alikuwa mrefu maji ya kunde na mtanashati sana.
Walikuwa wanatembea taratibu huku wameshikana mikono wakiifuata barabara ya vumbi iliyokatisha katikati ya majengo ya kampuni za Spedag Interfreight na Bureau Veritas Tanzania kuelekea eneo la Kiwalani.
“Shit!” Sammy aling’aka kwa hasira huku akipiga ngumi juu ya usukani na kukanyaga breki ya ghafla, gari lake likaserereka huku likiyumba barabarani na kusimama kando ya barabara ya Nyerere, usawa wa jengo la kampuni ya Bureau Veritas Tanzania.
Alishuka haraka akimwacha abiria wake na kukimbilia kule walikokuwa Winifrida na yule kijana huku akiwa amekasirika sana. Yule kijana alishtuka na kutazama nyuma, alipomuona akija mbio alikimbia akimwacha Winifrida ambaye hakuwa na ujanja. Sammy alimfikia Winifrida na kumkamata mkono kwa nguvu huku akifoka.
Winifrida aliishiwa nguvu, Sammy alimkokota kumpeleka kwenye gari lake lililokuwa limesimama kando ya ile barabara ya Nyerere. Muda wote yule abiria mzungu aliyekuwa ndani ya lile gari la Sammy alikuwa amepigwa na butwaa.
Kama mtu aliyeshtuka aliiangalia saa yake ya mkononi na kusonya huku akionekana kukata tamaa. Kwa vidole vyake viwili vya shahada na dole gumba vya mkono wa kulia aliminya pua yake kama anayevuta kamasi huku akiwatazama kwa makini Sammy na Winifrida wakivutana. Akaangalia tena saa yake ya mkononi.
“What’s wrong with you?” (Una shida gani?) yule mzungu alimuuliza Sammy kwa mshangao huku akishuka kutoka ndani ya lile gari la Sammy, mara akaiona teksi ikija upande ule, akaipungia mkono, “Taxi! Taxi!”
Ile teksi ilipunguza mwendo na kusimama mbele ya gari la Sammy, yule mzungu alifungua mlango wa nyuma wa gari la Sammy na kuchukua begi lake, akamtazama Sammy kwa mara ya mwisho huku akitoa kadi yake.
“You’ve been a prank but I want to give you a second chance, not for you but for the car. I may need it for one of my representative’s meetings,” (Umenifanyia mzaha lakini nataka nikupe nafasi nyingine, siyo yako bali kwa sababu ya gari lako. Huenda nikalihitaji kwenye moja ya mikutano yangu) yule mzungu alisema huku akimpa Sammy ile kadi yake.
Inaendelea...
Huyu Joyce alikuwa na nini hasa kilichomfanya Madame Norah afanye yale asiyokusudia kuyafanya? Hata hivyo, kitu kimoja alichokuwa na uhakika nacho ni kwamba alijisikia furaha sana moyoni kila alipoamua kumsaidia Joyce, basi!
Baada ya kitambo kirefu cha majadiliano kati yao, Madame Norah aliaga na kuondoka akiwaacha Joyce na Nyaso wanakamilisha maandalizi ya mradi ule.
* * * * *
Baada ya kutoka eneo la Karakata, Sammy alimchukua mtu mmoja aliyemkuta Jet Club na kumpeleka katika ofisi za Kampuni ya Magazeti ya Serikali (TSN) zilizopo barabara ya Mandela, katika eneo la Tazara.
Alimwacha yule abiria pale TSN kisha akageuza gari lake na kutaka kuingia katika barabara ya Mandela akitaka kwenda Ilala Sharif Shamba, mara akamuona mwanamume mmoja raia wa kigeni aliyekuwa anatokea ndani ya majengo ya kituo cha Mamlaka ya Reli ya Tanzania na Zambia (Tazara) aliyemjia mbio huku akimpungia mkono.
Alikuwa mwanamume wa makamo, mrefu na kipande cha mtu aliyejazia vyema. Mwili wake ulichorwa michoro mbalimbali na alikuwa amevaa fulana nyeusi ya mikono mifupi, kaptura ya rangi ya khaki yenye mifuko mikubwa pembeni na miguuni alivaa raba. Mgongoni alikuwa amebeba begi kubwa la safari.
Sammy aliamua kumsubiri. Hata hivyo, alikuwa amesimama katikati ya barabara ya mchepuko iliyotokea katika jengo la TSN na hivyo kuzuia magari mengine. Gari moja aina ya Toyota RAV4 jeusi lililokuwa nyuma yake likitaka kuingia katika barabara ya Mandela lilianza kupiga honi, dereva wa gari lile alionekana kutokuwa na uvumilivu.
Sammy aliendelea kusubiri pasipo kumjali yule dereva wa RAV4 aliyeendelea kupiga honi kwa fujo. Hakutaka kumkosa yule abiria Mzungu aliyekuwa akivuka barabara ya Mandela akionekana kuwa na safari muhimu.
Baada ya dakika takriban mbili yule mwanamume alifanikiwa kuvuka ile barabara na kufungua mlango wa nyuma wa gari la Sammy kisha aliliweka begi lake na kuingia, akakaa katika siti ya nyuma.
“Airport please… and thanks for waiting,” (Kiwanja cha Ndege tafadhali… na ahsante kwa kusubiri) alisema yule mwanamume wa kizungu huku akijiegemeza kwenye siti.
Sammy aliliondoa gari lake na kungia katika barabara ya Mandela bila kumjibu chochote yule mwanamume wa kizungu kisha akakata kushoto akiifuata barabara ya Nyerere iliyoelekea Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere.
Muda ule wa mchana barabara ya Nyerere haikuwa na msongamano mkubwa wa magari, hivyo Sammy alikuwa akiendesha kwa mwendo wa kasi. Walikuwa kimya kabisa.
Kufumba na kufumbua gari lilikuwa likiivuka yadi ya kuhifadhi makontena ya African Inland Container Depot (AFICD) katika eneo maarufu la Mchicha na sasa walikuwa wakilisogelea eneo la Karakana ya Tazara, hapo yule mzungu akakohoa kidogo kusafisha koo lake kisha akaanzisha mazungumzo.
“Do you know English?” (Unajua Kiingereza?) yule mzungu alimuuliza Sammy huku akiachia tabasamu pana la kirafiki.
“Yes,” Sammy alijibu kwa ufupi bila kumtazama yule mwanamume.
“How did you get this car? I real like it, it’s a unique type of taxi that everyone should want to use it,” (Umeipataje hii gari? Nimeipenda sana, ni aina ya teksi yenye upekee ambayo kila mtu angependa kupanda) yule mzungu alimuuliza Sammy huku akimtazama kwa makini.
Sammy aliachia tabasamu huku akimtupia jicho yule abiria wake kupitia kioo cha katikati cha gari kinachotumika kuangalia nyuma.
“You know…” (Unajua…) Sammy alianza kujieleza lakini akasita baada ya kumuona Winifrida akiwa hajavaa sare za shule na badala yake alivaa suruali ya kubana ya jeans rangi ya samawati yenye matobo mapajani na kitopu cheupe na mgongoni alikuwa amebeba begi lake la madaftari.
Winifrida alikuwa ameongozana na kijana mmoja wa kiume aliyekadiriwa kuwa na miaka ishirini na ishirini na mbili, akiwa amevaa suruali nyeupe ya jeans na fulana nyeusi, kichwani alivaa kofia nyeusi ya kapelo. Alikuwa mrefu maji ya kunde na mtanashati sana.
Walikuwa wanatembea taratibu huku wameshikana mikono wakiifuata barabara ya vumbi iliyokatisha katikati ya majengo ya kampuni za Spedag Interfreight na Bureau Veritas Tanzania kuelekea eneo la Kiwalani.
“Shit!” Sammy aling’aka kwa hasira huku akipiga ngumi juu ya usukani na kukanyaga breki ya ghafla, gari lake likaserereka huku likiyumba barabarani na kusimama kando ya barabara ya Nyerere, usawa wa jengo la kampuni ya Bureau Veritas Tanzania.
Alishuka haraka akimwacha abiria wake na kukimbilia kule walikokuwa Winifrida na yule kijana huku akiwa amekasirika sana. Yule kijana alishtuka na kutazama nyuma, alipomuona akija mbio alikimbia akimwacha Winifrida ambaye hakuwa na ujanja. Sammy alimfikia Winifrida na kumkamata mkono kwa nguvu huku akifoka.
Winifrida aliishiwa nguvu, Sammy alimkokota kumpeleka kwenye gari lake lililokuwa limesimama kando ya ile barabara ya Nyerere. Muda wote yule abiria mzungu aliyekuwa ndani ya lile gari la Sammy alikuwa amepigwa na butwaa.
Kama mtu aliyeshtuka aliiangalia saa yake ya mkononi na kusonya huku akionekana kukata tamaa. Kwa vidole vyake viwili vya shahada na dole gumba vya mkono wa kulia aliminya pua yake kama anayevuta kamasi huku akiwatazama kwa makini Sammy na Winifrida wakivutana. Akaangalia tena saa yake ya mkononi.
“What’s wrong with you?” (Una shida gani?) yule mzungu alimuuliza Sammy kwa mshangao huku akishuka kutoka ndani ya lile gari la Sammy, mara akaiona teksi ikija upande ule, akaipungia mkono, “Taxi! Taxi!”
Ile teksi ilipunguza mwendo na kusimama mbele ya gari la Sammy, yule mzungu alifungua mlango wa nyuma wa gari la Sammy na kuchukua begi lake, akamtazama Sammy kwa mara ya mwisho huku akitoa kadi yake.
“You’ve been a prank but I want to give you a second chance, not for you but for the car. I may need it for one of my representative’s meetings,” (Umenifanyia mzaha lakini nataka nikupe nafasi nyingine, siyo yako bali kwa sababu ya gari lako. Huenda nikalihitaji kwenye moja ya mikutano yangu) yule mzungu alisema huku akimpa Sammy ile kadi yake.
Inaendelea...
