Stephen Owawa ajipanga kugombea ubunge Rorya 2015

Naona wachangiaji wengi humu hamuifahamu na wala hamuijui jimbo la RORYA. Sikumbuki kuwa OWAWA alienda Rorya kwa mara ya mwisho lini na kwenye kampeni ya uchaguzi mkuu 2010 OWAWA hakukanyaga Rorya. Owawa anajulikana sana Dar na kwenye vyombo vya habari lkn siyo ndani ya Rorya. Mimi namfahamu sana Kamanda Owawa na namkubali sana ktk medani za siasa na kwenye harakati zake. Ningependa kumshauri kama ana nia ya kugombea Ubunge akagombee jimbo lingine na siyo Rorya. Siasa za Rorya siyo siasa za kwenye vyombo vya habari na mitandao ya jamii. Owawa najua ni mwanarorya, ila namkaribisha Rorya!

Kama mtu anaweza tumpe moyo na kusema ukweli,mimi nakumbuka kuwa amekuwa akienda Rorya kila mara ila alichosema kuwa bado ni mapema kwa mtu anataka kuingia kwenye siasa za Rorya lazima ajipange kwanza,ni kweli alikuwa Anasaidia kampeni mgombea Ubunge wa CHADEMA martin Ochola Ndira,nakumbuka 2010 nilikutana nao Shirati,Osiri,Busanga,Nyambori,Kirongwe,Bugire,utegi na Kinesi,kwa hiyo kusema kuwa hafiki Rorya nadhani uongo,mwaka huu mwezi wa tano alikuwa Randa,Kagwaa,Bugire na Masonga.Nadhani njia anayotumia kujipanga kwa jimbo la Rorya ni tofauti sana na njia tuliyozoea.Mwaka jana mwezi wa kumi na mbili alikuwa Rorya uku akiwasiliana na wazee wakimila ili aweze kuandika kitabu kinachohusu Rorya na Changamoto zake.


Ila inabidi ajipange sana kwa sababu tatizo la kwao Rorya ni watu kurubuniwa na pesa na kuacha wenye uwezo,labda kuamka kwa wananchi inaweza kumsaidia.Binafsi nampa big up sana kwa uwezo binafsi na ujasiri alionao,jamaa kwenye ukweli utamchoka atakwaambia bila kupindisha,atafute ngawira ili ajaribu kama ataweza.
 
Hakuna lolote,owawa endelea kufanya kazi national audit siasa tangu chuo hauwezi!
 
CDM kumsimamisha Owawa ni kutafuta kupoteza jimbo mahakamani, Owawa sio raia hii inathibitishwa na viambatanishi vyake wakati wa udahili pale UD. Mwenyewe alitaka kupoteza faili lile lakini bila kujua faili likaishia kwa rafiki yake kijana wa Zoka.
 
Kamanda Owawa salamu kwako mahali ulipo. Kwanza nakushukuru kwakua ulisimama kidete kututetea sisi ambao hatukupata mkopo 2008 na hadi tukapata. Nilikua rafiki yako mkubwa sana miongon mwa madogo wa mwaka huo. Msimamo wako ni mkali na wala sijutii kukaa nyumbani kwa muda baada ya ule mgomo wa 2009 mwachibya akiwa rais wa daruso. Namkumbuka pia yule mganda Ojang kama sijakosea jina lake. Alikua anamfanya Musseven asilale pale campala kwa hoja nzito. Dah sijui yuko wapi mganda yule...
 
Isije kuwa anamkimbia Prof.Asad!teh,teh,tehila nenda mwana ofisi yenyewe hii imekuwa tia maji tia maji
 
Huyu bwanamdogo namkumbuka pale udsm nilimuacha anaharakati za siasa za daruso.all the best
 
Namkumbuka Steven Owawa na kundi lake wakina Silinde, Nassari, Odong na Adam ingawa Adam kasaliti harakati anambwelambwela na udiwani wa mahakama. Nina imani kubwa na huyu mtu hachoki kupambana tuliomkuta udsm tunamjua vyema wanarorya mpeni nafasi.
 
Lakini tusimsahau aliyebeba bango kuelekea ikulu peke yake kudai posho ya elfu kumi kwa wanafunzi...huyu ni Richard Mwita....kwa sasa ni mwalimu alikuwa Bukoba na juzi kahamia jijini Mwanza.
Harakati zake kama kawaida....
 
huyu jamaa ataisaidia sana kambi ya upinzani kwenye masuala ya fedha na uchumi,anafaa kuwa waziri kivuli kwny hiyo angle,yupo vizuri sana kichwani,pamoja na misukosuko yote aliyoipata chuoni bado aliweza kupata upper second na kufaulu interview iliyokua na ushindani mkubwa nchi nzima ya national audit.
 
huyu jamaa ataisaidia sana kambi ya upinzani kwenye masuala ya fedha na uchumi,anafaa kuwa waziri kivuli kwny hiyo angle,yupo vizuri sana kichwani,pamoja na misukosuko yote aliyoipata chuoni bado aliweza kupata upper second na kufaulu interview iliyokua na ushindani mkubwa nchi nzima ya national audit.
Mkuu huyu hata kwenye LAAC atasaidia sana,atakuwa ni muheshiwa mwenye knowledge,skills na experience ya Auditing!ktk hiyo interview ya NAO kulikuwa na applications 18,000 mchujo wa written tukabaki vichwa elf 2 ivi,sasa ngoma kwenye oral,watu 100 wanatakiwa ila candidates ni ka 300 ivi.Owawa was the One,pia ma-underground king tukawemo kwenye msafara.Owawa ni kichwa ila ukimya wake sometimes unanitisha
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom