Stephen Owawa ajipanga kugombea ubunge Rorya 2015

Taifaletu

Member
Feb 21, 2011
34
17
Wana JF juzi nilikuwa kwenye utafiti mkoani Mara nilikuwa nimepangiwa wilaya ya Rorya,Wakati tukiwa kazini nilisikia wananchi wakisema kuwa Mbunge wao yuko likizo ndio maana hasikiki Bungeni,Mbunge wa Rorya kwa sasa ni Lameck Airo,katika pita pita zetu niliwauliza wanajiandaaje kwa uchaguzi wa 2015? sehemu nyingi walisema kuwa kuna kijana mwaka 2010 alikuwa compaign manaja wa Mgombea Ubunge Jimbo la Rorya Kupita CHADEMA aliwaambia kuwa atarudi kugombea Ubunge au Udiwani 2015 anaitwa Stephen Owawa.


Naombeni CV ya huyu jamaa.
 
Wana JF juzi nilikuwa kwenye utafiti mkoani Mara nilikuwa nimepangiwa wilaya ya Rorya,Wakati tukiwa kazini nilisikia wananchi wakisema kuwa Mbunge wao yuko likizo ndio maana hasikiki Bungeni,Mbunge wa Rorya kwa sasa ni Lameck Airo,katika pita pita zetu niliwauliza wanajiandaaje kwa uchaguzi wa 2015? sehemu nyingi walisema kuwa kuna kijana mwaka 2010 alikuwa compaign manaja wa Mgombea Ubunge Jimbo la Rorya Kupita CHADEMA aliwaambia kuwa atarudi kugombea Ubunge au Udiwani 2015 anaitwa Stephen Owawa.


Naombeni CV ya huyu jamaa.

Hajamaliza chuo UDSM alifukuzwa kutokana na migomo mwaka 2009.
 
Aliingia UDSM 2005 akafukuzwa,akarudi 2006 akisimamishwa 2007 baadae akarudi,2008 akasimamishwa mwezi moja,2009 akasimamishwa mwaka mzima wakarudi baada ya kumaliza kesi na kushinda serikali dhidi ya viongozi wa DARUSO,na amemaliza rasmi 2010 yeye na silinde,Machibya nakumbuka hayo machache amekuwa akifukuzwa kutokana na msiamo mkali wa kuongoza mgomo kupinga sera ya Uchangiaji elimu ya juu Tanzania,ni hayo machache ninayofahamu wadau
 
Aliingia UDSM 2005 akafukuzwa,akarudi 2006 akisimamishwa 2007 baadae akarudi,2008 akasimamishwa mwezi moja,2009 akasimamishwa mwaka mzima wakarudi baada ya kumaliza kesi na kushinda serikali dhidi ya viongozi wa DARUSO,na amemaliza rasmi 2010 yeye na silinde,Machibya nakumbuka hayo machache amekuwa akifukuzwa kutokana na msiamo mkali wa kuongoza mgomo kupinga sera ya Uchangiaji elimu ya juu Tanzania,ni hayo machache ninayofahamu wadau
Yupo pia humu JF, nikipata tym nitamsanua aje kufunguka
 
hajamaliza chuo udsm alifukuzwa kutokana na migomo mwaka 2009.

alimaliza b.com in accounting mwaka 2010 na kupata upper second class. Kwahiyo usipotoshe umma. Lkn kwa nafasi yake kwasasa hawezi kuwa mbunge wa rorya. Bado anahitaji muda wa kuwa mentored.
 
Wana JF juzi nilikuwa kwenye utafiti mkoani Mara nilikuwa nimepangiwa wilaya ya Rorya,Wakati tukiwa kazini nilisikia wananchi wakisema kuwa Mbunge wao yuko likizo ndio maana hasikiki Bungeni,Mbunge wa Rorya kwa sasa ni Lameck Airo,katika pita pita zetu niliwauliza wanajiandaaje kwa uchaguzi wa 2015? sehemu nyingi walisema kuwa kuna kijana mwaka 2010 alikuwa compaign manaja wa Mgombea Ubunge Jimbo la Rorya Kupita CHADEMA aliwaambia kuwa atarudi kugombea Ubunge au Udiwani 2015 anaitwa Stephen Owawa.


Naombeni CV ya huyu jamaa.

Tehe tehe...nikimkumbuka huyu jamaa huwa nacheka sana.alijaribu kugombea uenyekiti wa faculty of commerce and management UDSM mwaka 2007 akashindwa..nilikuwa darasa moja mbele yake..kinachonifanya nimkumbuke ni jinsi alivyokuwa akitetemeka kwa woga wakati akizungumza mbele ya darasa letu..muonekano wake ni wa kijana anayependa siasa kabisa.I just doubt his courage.
 
Wabongo kwa upotoshaji, Stephen Owawa yuko National Audit Office,zile ajira mpya 100,sina hakika yupo mkoa gani ila nilikuwa nae training pale Landmark Oct 2011. Mtafute fb yupo hai, pia kwny jukwaa la CHADEMA VS CCM
wala usipate tabu mkuu, yupo bukoba kagera kwa post hiyo uloitaja.
 
Aliingia UDSM 2005 akafukuzwa,akarudi 2006 akisimamishwa 2007 baadae akarudi,2008 akasimamishwa mwezi moja,2009 akasimamishwa mwaka mzima wakarudi baada ya kumaliza kesi na kushinda serikali dhidi ya viongozi wa DARUSO,na amemaliza rasmi 2010 yeye na silinde,Machibya nakumbuka hayo machache amekuwa akifukuzwa kutokana na msiamo mkali wa kuongoza mgomo kupinga sera ya Uchangiaji elimu ya juu Tanzania,ni hayo machache ninayofahamu wadau
Huyu ni aina ya makamanda tunaowahitaji.
 
kwa mara ya kwanza naingia Udsm, mwanaharakati wa kwanza kumfahamu alikuwa Owawa.
Jamaa ni jasiri sana tena ninachompendea hana jazba.
Huyu ndiye aliyeongoza mgomo wa 2008 october au november, na tukaenda nyumban kwa takriban miez miwili.
 
wala usipate tabu mkuu, yupo bukoba kagera kwa post hiyo uloitaja.

Yaaas, yupo Bukoba anaumbua wezi wa mali za Uma, ni mpiganaji hasa,jamaa kazaliwa kuwa kiongozi popote atapopita, Landmark kwenye training pia alikuwa representative wetu
 
Tehe tehe...nikimkumbuka huyu jamaa huwa nacheka sana.alijaribu kugombea uenyekiti wa faculty of commerce and management UDSM mwaka 2007 akashindwa..nilikuwa darasa moja mbele yake..kinachonifanya nimkumbuke ni jinsi alivyokuwa akitetemeka kwa woga wakati akizungumza mbele ya darasa letu..muonekano wake ni wa kijana anayependa siasa kabisa.I just doubt his courage.


Ila jamaa ni jasiri na anajiamini sna,Nakumbuka 2007 alikuwa mwaka wa kwanza anagombea mweyekiti wa kitivo,pia nakumbuka amewahi kuwa mwenyekiti wa Mtandao wa wanafunzi Tanzania TSNP,Mbunge wa katika serikali ya DARUSO,Rais wa Wanafunzi SHYCOM shinyanga,Kingine ninachokumbuka ni kutokuwa na jazba katika kujenga hoja na kufikisha ujumbe kwa wanafunzi UDSM na mahojiano yake kwenye TV.

Nakumbuka makala zake mwanahalisi
 
Hajamaliza chuo UDSM alifukuzwa kutokana na migomo mwaka 2009.


Acha unafiki wewe mimi nimegraduate naye 2010 UDSM sijui huu uongo utawapeleka wapi. Alisimamishwa masomo 2009 pamoja na akina DAvid Silinde, Anthony Machibya na baadaye walirudishwa chuo ndo tukamaliza wote 2010
 
Owawa lazima achukuwe Jimbo ,ni mpiganji atakayeongeza chachu ya mabadiliko bungeni.Ana uwezo mkubwa sana wa kujenga hoja na ushawishi,pia ameonekana kwenye harakati nyingi sana kuanzia Shycom mpaka UDSM.Alisimamishwa chuo mwaka mmoja ila aliendelea mwaka unaofuata na kuhitimu B-Com 2010 .Nilifanikiwa kukutana naye Dec mwaka jana Mjini Bukoba anapofanya kazi ofisi ya CAG tulizungumza mengi sana.

Wadau tunaomfahamu tunampa baraka zote, tutasimamia zoezi zima la yeye kuwakilisha wanyonge kwa minajili ya kutetea haki zao.
 
Naona wachangiaji wengi humu hamuifahamu na wala hamuijui jimbo la RORYA. Sikumbuki kuwa OWAWA alienda Rorya kwa mara ya mwisho lini na kwenye kampeni ya uchaguzi mkuu 2010 OWAWA hakukanyaga Rorya. Owawa anajulikana sana Dar na kwenye vyombo vya habari lkn siyo ndani ya Rorya. Mimi namfahamu sana Kamanda Owawa na namkubali sana ktk medani za siasa na kwenye harakati zake. Ningependa kumshauri kama ana nia ya kugombea Ubunge akagombee jimbo lingine na siyo Rorya. Siasa za Rorya siyo siasa za kwenye vyombo vya habari na mitandao ya jamii. Owawa najua ni mwanarorya, ila namkaribisha Rorya!
 
Rorya 2015 Ni yule kijana wa Issa Michuzi anayeishi Marekani, sijui Yohana Meshack vile. anaandika sana makala ya Kiuchumi...CCM hatumtaki,
 
Tehe tehe...nikimkumbuka huyu jamaa huwa nacheka sana.alijaribu kugombea uenyekiti wa faculty of commerce and management UDSM mwaka 2007 akashindwa..nilikuwa darasa moja mbele yake..kinachonifanya nimkumbuke ni jinsi alivyokuwa akitetemeka kwa woga wakati akizungumza mbele ya darasa letu..muonekano wake ni wa kijana anayependa siasa kabisa.I just doubt his courage.

Owawa huyu huyu ninayemjua mimi?

Owawa huyu huyu aliyekuwa akiwafanya akina Mtatiro na Deo waione Revolution Square chungu?

Owawa huyu huyu aliyekuwa akiamua kukuunga mkono ujue lazima wewe ni raisi wa chuo tayari?

Owawa huyu huyu aliyekuwa akimfanya Mkandara apatwe tumbo la kuhara kila akimuona?

Owawa huyu huyu aliyeweza kushawishi hadi wasichana wakawa wanashiriki migomo?

Owawa huyu huyu aliyekuwa ana 100% ya mkopo lakini anatetea wengine?


Au una Owawa mwingine?.
 
kwa mara ya kwanza naingia Udsm, mwanaharakati wa kwanza kumfahamu alikuwa Owawa.
Jamaa ni jasiri sana tena ninachompendea hana jazba.
Huyu ndiye aliyeongoza mgomo wa 2008 october au november, na tukaenda nyumban kwa takriban miez miwili.

Upo sahihi.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom