Stella Manyanya amkaba koo Dr Slaa

Mkuu hapa issue sio kwamba alichofanya ni kibaya issue ni kwamba ni sawa na kumtupia jiwe nyani akalidaka akakuponda nalo hapa wewe ndio utakayeumia zaidi
 
Kama wanajuana its okay lakini sometimes kwenye hili Game la Siasa sio vema kuwapa wenzako makombora ambayo wanaweza kuyabadilisha au kuyatumia kwenye Propaganda


ukweli unauma ndio maana manyanya kapayuka...kwa kifupi ni kuwa wabunge wengi wa ccm hawasomi tafiti na kujua ukweli wa mambo..wengi wao mle ndani hawajui kitu kazi kushambulia watu.....alichoambiwa ni kweli....na angekuwa mkweli huyo manyanya angesema humo bungeni kile kilichotumwa kwake.....maana kaambiwa ukweli....
 
Hivi kumbe neno unafiki ni baya eeh!! nilikuwa sijui. Mwishowe tutaanza kuikana lugha yetu!!

Sasa kama mtu nim mnafiki tumuiteje mwalimu? labda utusaidie nenoi mbadala.

Ulisikia neno mnafiki zuri?

Kuna adabu ya kuzungumza na watu, na kuwaita wanafiki, waongo, wazandiki, sio moja ya adabu hizo.
 
Nope, i am just wishing slaa to be a man enough to ask his wife and clarify the matter... if he leaves this to josephine yanaweza kuishia kwenye mipasho ya wanawake

that is the stand i would take being a leader and the head of family...

Mzee Makini; nashauri tu kuwa issue kama za Manyanya take them with a pitch of salt. Kwa jinsi Manyanya alivyomsema Dr. Slaa bila title yake, amemuaddress binafsi kama alitamka hayo, alitamka kama institution hivyo Manyanya knows what she is saying ie personal. Ndiyo maana hata SMS ni personal.

Kwa maoni yangu naungana na baadhi ya wachangiaji humu kutambua issue ya uelewa wa wananchi dhidi ya wabunge wao wanapopewa dose na akina Dr. Slaa kwenye harakati za kuwaelimisha wananchi.

Msameheni injinia Manyanya msg yake kwetu ni kuwa harakati za CDM zinamuathiri which is expected and intended
 
Mbona hajatuambia hiyo sms imeandikwa nini jamani? Haileti sense, kama ametukanwa kwani bungeni ndani kuna kutuo cha polisi na mahakama? Duh! Hili taifa 99.9999999% watu wake ni vilaza. Nashukuru mi nipo kwenye percent iliyobaki.
 
Ulisikia neno mnafiki zuri?

Kuna adabu ya kuzungumza na watu, na kuwaita wanafiki, waongo, wazandiki, sio moja ya adabu hizo.

Naomba unisaidie kujua adabu ya kuzungumza na mtanzania aina ya eng.,manyanya kwakuwa kure kwetu adabu niliyofundishwa ni kusema ukweli, nyeupe ni nyeupe tu!!

Na inapotokea mtu ni muongo, mzandiki, ama mnafiki natakiwa kumuitaje? natumia adabu gani kumueleza sifa yake?? ni hayo tu mwalimu.
 
This tarnishes her good image completely!hapo mwanzo sikujua kama huyu mama ni non sense kiasi hichi!shame upon you!!
 
aaaa mtani unaniangush an. you cant swallow everything here.
 
Kwenye sms hapo mbona hapajatulia. Bifu gani na mchumba wa Rais wa Ukweli!! Stella aseme ukweli!!
 

Ukitaka kuelewa somo la adabu tuanze na kufikiri unazungumza na wazazi wako. Kama mama yako muongo, utamwita muongo au utamtafutia neno au maneno mengine ya kufikisha ujumbe wako? Kama baba yako mnafiki jee? Hiyo nyeupe ni nyeupe uliofundishwa kwenu unaitumiaje hapo kwa wazazi wako?

Ukishajua hapo tutasogea stage ya pili ya somo la adabu za mazungumzo
 
Mbona hajatuambia hiyo sms imeandikwa nini jamani? Haileti sense, kama ametukanwa kwani bungeni ndani kuna kutuo cha polisi na mahakama? Duh! Hili taifa 99.9999999% watu wake ni vilaza. Nashukuru mi nipo kwenye percent iliyobaki.
hiii ni nini? unakera banaaaaa.soma post zote kwa makini before

 


nadhani ni ustaarabu kaufanya mama josephine....ila juha zaidi ni huyo aliyetangaza bungeni....maana kama alitka kuijua kweli angepiga simu mara baada ya kuona hiyo sms nakumuuliza ni kwa nini josephine anasema hivyo na maeneo gani manyanya hafanyi vizuri...nina uhakika josephine angemwambia kuwa huko unakotoka hali ni mbaya wapiganie watu wako.....lakini yeye alipoona sms basi nadhani alitumia njia ya makato ya kujifanya kama anatuma m-pesa, au tigo-pesa ili ajue ni nani aliyetuma sms maana zinarudisha jina...au alienda kwenye mtandano husika wa mtumiaji .......yote kwa yote manyanya kaambiwa ukweli na ni wabunge wengi wanaonge autumbo humo wakati majimbo yao yako hovyo....refer mbunge anayetoka jimbo la kilindi na kile alichokisema jana mjengoni ndo utajua ccm wengi mle wanashambulia watu
 
Huyu si injinia? sasa udigirii umekufa au vipi?
Mkuu ukiingia ccm hata kama ni profesa lazima kuna amount flani ya loss kichwani ikupate. Ni sawa na betrii 1 mpya ukaichanganye kwenye circuit (sakiti) ya betri chakavu, ile mpya hunyonywa nguvu na kushushwa kiwango sawa na hizo chakavu. Jaribu kwenye tochi inayotumia hizi betrii za kawaida uone.
 

Tuwe wakweli, huwezi mtu akakuita mnafiki kisha ati umpigie simu wewe kwa upole umumuulize kwa nini akakwita mnafiki. Kwa hili Josephine hateteeki, alikosa ustaarabu. Na Manyanya nae ndo kabisa, hata definition ya neno ustaarabu halijui
 
nimekusoma mkuu pamoja na wadau walionishauri na nikashaurika na kubadili usemi wangu

with JF, there is a lways something new to learn and i gained one today kwenye hii thread

we fuatilia utaona kuna post nilishasema nimewithdraw proposal yangu

as said by G, the best way to treat manyanya ni ku-ignore

But between the lines nilikua nina ujumbe pia kwa josephine, aache au apunguze ule undava wa kiswahili, she is with one of the greatest men of the moment
 


wewe ungepata ule uenyekiti wa bavicha sipati picha....anyway turudi kweye mada
 
...........wanaongelea haya..... halafu wanapata posho ya kukaa......inatia uchungu sana......jamani waheshimiwa tumueni vizuri muda wetu bungeni:A S cry:
 
Tuwe wakweli, huwezi mtu akakuita mnafiki kisha ati umpigie simu wewe kwa upole umumuulize kwa nini akakwita mnafiki. Kwa hili Josephine hateteeki, alikosa ustaarabu. Na Manyanya nae ndo kabisa, hata definition ya neno ustaarabu halijui

now we are speaking the same language mwalimu.....langekuwa si mtu wa shari angepiga simu kuuliza.....mtarabu yeyote angefanya vile...na kama angetukanwa pale baada ya kupiga simu hapo tungesema josephine hakuwa mstaarabu lakini mpaka sasa ni msaarabu sana....nasubiri majibu ya jk juu ya sms yangu hap ndo ntajua kama ni mstaarabu au ntaitwa mhaini nataka kumung'oa madarakani
 

Mwalimu nimekupata lakini nachoshindwa kukushangaa ni kwamba unazunguka saaana.

Mimi nimeomba unisaidie mbadala wa maneno kama mnafiki, muongo na mzandiki.

Usisahau kwamba hapa tunatumia mfano hai wa josephine na manyanya ambao hawana uhusiano wa baba mama na mtoto. Unapozungumzia baba au mama na mwana ni kitu kingine tofauti na unapozungumzia mwanasiasa wa kitanzania tena asiyejali maslahi ya watanzania wenzake anaotakiwa kuwawakilisha na kuwasemea.

Hizi lugha laini ndizo zimetufikisha hapa tulipo, kwamba mtu anasema uongo badala ya kumwambia ukweli kwamba kasema uongo sisi tunatafuta msamiati wa kulainisha uongo na kusema ulimi umeteleza kidogo, au amepitiwa au wasaidizi wake wamemuangusha!!! hii misamiati ya kupoteza ladha ya ukweli imefika wakati tuachane nayo, watu waambizane ukweli ili kuleta uwajibikaji.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…