Statement: Positive results from Buzwagi processing trial

Statement: Positive results from Buzwagi processing trial

Mwanzoni walitulipa copper silver na Gold nado nauli ya kusafirisha mzigo pango la bandari kavu na ushuru wa bandari,

sasa tutaambulia ka royalty ka Gold peke yake! Na mzigo mwingine unatupwa jalalani, kumbuka copper ni kama chuma hupata kutu na kupotea. Kimsingi tumeliwa.
Poa tu !
 
Mwanzoni walitulipa copper silver na Gold nado nauli ya kusafirisha mzigo pango la bandari kavu na ushuru wa bandari,

sasa tutaambulia ka royalty ka Gold peke yake! Na mzigo mwingine unatupwa jalalani, kumbuka copper ni kama chuma hupata kutu na kupotea. Kimsingi tumeliwa.
Poa tu !
 
Hiyo kopa ikinyeshewa mvua inatengeneza kopa oxide ambayo ni kutu, na ichanganyikana na salfa unapata kopa oksaidi ambayo ni hewa ya sumu na hutawanya mawimbi ya mvua kuanzia sasa tusitegemee kuvuna chochote kanda ya ziwa labda tuanze kulima tende.
Wazo zuri, tende tunaagiza nje hivyo tutaokoa fedha za kigeni
 
Hasara nyingine kwa serikali. Ama kweli usicheze na mwenye akili.

Kilichofanyika hapa ni sawa na mtu mwenye shamba la mahindi (dhahabu) lililokuwa na mashina machache yaliyopo hapa na pale ya mbaazi (copper) na alizeti (silver). Alikuwa anavuna kwa kutumia combine harvester iliyokuwa inachambua mahindi punje kubwa na kuacha mahindi yenye punje ndogo, yakiwa yamechanganyika na mbaazi na alizeti.

Mchanganyiko wa mahindi punje ndogo, mbaazi na alizeti ulikuwa unapelekwa kwenye kiwanda chenye uwezo wa kutenganisha. Lakini katika mchanganyiko huo, katika thamani, 80% yalikuwa ni mahindi yenye punje ndogo.

Baada ya kuzuiwa kupelekwa mchanganyiko wa mahindi yenye punje ndogo, mbaazi na alizeti kwenye kiwanda, mvunaji ameamua kutafuta harvester mpya ambayo sasa itakuwa na uwezo wa kutambua mahindi yote hata kama yana punje ndogo kwa ufanisi wa 80%. Anaamua kuvuna mahindi tu, na kuacha mahindi ya punje ndogo 20% pamoja na mbaazi na alizeti, vyote viozee shambani.

Kwa sababu mchanganyiko wa mahindi yenye punje ndogo, alizeti na mbaazi, katika thamani, 80% yalikuwa mahindi ya pune ndogo, sasa alizeti na mbaazi haviwezi kuvunwa na kupelekwa kiwandani kwa faida.

Ikumbukwe kuwa silver na copper katika ile Au-Cu-Ag ore, concentration yake haifiki hata 0.1%. Ilikuwa inaongezeka baada ya kufanya concentration. Sasa haitakuwepo concentration. Hivyo Cu na Ag havitaweza kuwa extracted kwa faida.

Nini maana yake?
1) Ag itabakia kwenye tailings za mgodi, na haitachenjuliwa tena na kuuzwa
2) Cu itabakia kwenye tailings, haitachenjuliwa wala kuuzwa tena
3) Fine Au 20% itabakia kwenye tailings, na haitaweza kuchenjuliwa tena. Ifahamike kuwa mgodi wa Buzwagi average grade per tone ni 4g. Ina maana 20% ya average grade ni 0.8g/t.
4) Contractor wa usafirishaji makinikia na wafanyakazi wake, mambo yameishia hapo
5) Vituo vya mafuta mapato yake yatapungua
6) Mapato ya bandari yaliyohusiana na usafirishaji wa concentrates yameishia hapo
7) Kodi iliyokuwa ikitokana na mauzo ya concentrate ya Au-Cu-Ag, yameishia hapo.
8) Hakutajengwa kiwanda cha kuchenjua concentrates

Tulichoongeza ni royalty ya gold bar, na furaha ya moyo kuwa hatuibiwi kwa sababu sasa dhahabu inayozalishwa tutaiona kwa macho yetu, haipo katika mwonekano wa mchanga.

Nimeamini mwenye akili hakosi jibu. Wakati wote huwa na jibu la kukabiliana na mazingira yanayomzunguka. Mjinga unaweza kudhani umepata kumbe umepatikana
Poa tu, wacha tuongeze tozo ya hicho wanacho chenjua.
 
Those are corporate action, recapturing the lost faith of its shareholders whilst preventing slump fall of its share price in financial markets
 
Hebu jielekeze kwenye taarifa ya uzalishaji acha kulalamika tu.
Huo ni uthibitisho kuwa mchanga una dhahabu nyingi sana kama professor Mruma alivyobainisha
.....hao ni mpaka Lissu aseme !
 
Hawa ACACCIA si ni wezi?, tunaendelea vipi kuwaruhusu wachakate dhahabu kwa njia nyingine?. Mimi nilidhani mwizi anapaswa kupigwa full-stop kukaribia mali ilipo!
 
Udhibiti uimarishwe kwenye usafirishaji wa gold bars, zote zihakikiwe DSM kabla ya export.
Binadamu hubadili mbinu kila siku kutimiza lengo lake (Jema au baya).
 
Nyumbu sikulaumu, ndio uwezo wa kufikiri ulipofikia.
Tutakutana 2020
Ni upumbavu kutetea kitendo cha Rais kufunfisha watu kukwepa kodi! Ni upumbavu zaidi kutumia kigezo cha unyonge wa mkulima! Mkulima anayezalisha zaidi ya tani 1 ana unyonge gani? Yaani hata mkulima anayezalisha tani 100 naye ni mnyonge? Kwa kifupi mkulima hata akizalisha tani 1000, kwa maelekezo na mafundisho ya Magufuli ataweza kukwepa kodi kwa kusafirisha mzigo kidogo kidogo. Halafu wewe unaona sawa? Neno pumbavu ni stahili yako kabisa.

Pili, kulipa kodi (haswa income tax) uifanya serikali kuwa responsible kwa wananchi wake. Na mwananchi kuwa na haki ya kuisema serikali. Sasa mtu asipolipa hawezi kuwa na uchungu na nchi yake hata kidogo! Kwa mtu mpumbavu atafurahia hili, pasipokufahamu kwamba mwanasiasa Magufuli anataka wakulima wasiwe responsible citizens ambao serikali inapaswa kuwajibika kwao.

Hivi huoni huo mkanganyiko?
Btw, mwambie Magufuli naye aanze kulipa kodi. Siyo ana free ride tu na sisi walipa kodi kumgharamia kila kitu, halafu bado anafanya ufisadi Ikulu! Ptuuuu!
 
Back
Top Bottom