Gunst
JF-Expert Member
- Jan 2, 2015
- 2,925
- 5,405
Ni kawaida yangu kurudi nyumbani kuanzia saa 3:30 usiku, ila leo nimelazimika kuwahi kurudi nyumbani (saa 1:00 jioni) kutokana na sababu zangu binafasi.
Kwakweli ni siku nyingi sijaangalia taarifa ya habari, hivyo ilipofika saa 2 usiku kwakuwa nimewahi kurudi nyumbani na sijagusa ulabu nilichukua rimoti ya TV nikaweka ITV ili niangalie taarifa ya habari, ghafla mke wangu alinirukia kama nyani na kuninyang'anya rimoti huku anahema.
Wakati namshangaa akanambia kwa ukali:
"usiniharibie starehe zangu, huu ni muda wa tamthilia, kama unapenda sana taarifa ya habari nunua TV ya chumbani".
Kwa upole ilinibidi nielekee chumbani kujilaza, na sitompa unyumba wiki nzima kwa kunikwaza.
USHAURI: Enyi Startimes heshimuni muda wa taarifa za habari, hizi tamthilia za wanawake wekeni mchana na jioni tu ili kuepusha migogoro ya familia.
Kwakweli ni siku nyingi sijaangalia taarifa ya habari, hivyo ilipofika saa 2 usiku kwakuwa nimewahi kurudi nyumbani na sijagusa ulabu nilichukua rimoti ya TV nikaweka ITV ili niangalie taarifa ya habari, ghafla mke wangu alinirukia kama nyani na kuninyang'anya rimoti huku anahema.
Wakati namshangaa akanambia kwa ukali:
"usiniharibie starehe zangu, huu ni muda wa tamthilia, kama unapenda sana taarifa ya habari nunua TV ya chumbani".
Kwa upole ilinibidi nielekee chumbani kujilaza, na sitompa unyumba wiki nzima kwa kunikwaza.
USHAURI: Enyi Startimes heshimuni muda wa taarifa za habari, hizi tamthilia za wanawake wekeni mchana na jioni tu ili kuepusha migogoro ya familia.