Stara Thomas!

starat.jpg


Aliyekua muimbaji wa nyimbo za bongo fleva Stara Thomas sasa amempa Bwana Yesu maisha yake!
Hapo awali alisikika kwa nyimbo maarufu kama Sikia, Sitorudi nyuma, my body na Chldren rights ambapo hivi karibuni amevuma na wimbo wa nipigie alioshirikishwa na AT.
“Nilipata wito kutoka kwa Yesu kwa kuwa aliwaita watu wote wasumbukao na kulemewa na mizigo waende kwake atawapumzisha” alisikika akisema Stara
Awali alikua akiabudu dhehebu la Jamatrine kwa sasa anaabudu kanisa la Shalom lililoko Mbezi Salasala! Karibu kwa Bwana Yesu Stara!


Source: Stara Thomas ameokoka! « Strictly Gospel
Gospel inalipa wewe. Stara kashindwa kujua kama yuko kwenye bongo fleva au dansi/zouk. Kaona pia huko hakulipi sana. Kadhalika ni kwa muda sasa kapotea hawani. Kaona Gospel ni all weather. We subiri tu na utamsikia kwa kishindo kama cha Rose Mhando. Subirini tu. Ila all the Best, Stara
 
Mshike yesu kweli. Ila angalia isije ikawa umeenda huko kuvuna hela kwenye gospel music industry baada ya kuona huko ulikokuwa ufurukuti.
 
amechukue na mumewe maana bado ni hasara akimuacha tcc club chang'ombe akila maisha na viche**** vijana kwa wazee ni hasara mbinguni na ktk mfuko wa stara pia. Bwana ampe nguvu amvute na mumewe!!!
 
starat.jpg


Aliyekua muimbaji wa nyimbo za bongo fleva Stara Thomas sasa amempa Bwana Yesu maisha yake!
Hapo awali alisikika kwa nyimbo maarufu kama Sikia, Sitorudi nyuma, my body na Chldren rights ambapo hivi karibuni amevuma na wimbo wa nipigie alioshirikishwa na AT.
“Nilipata wito kutoka kwa Yesu kwa kuwa aliwaita watu wote wasumbukao na kulemewa na mizigo waende kwake atawapumzisha” alisikika akisema Stara
Awali alikua akiabudu dhehebu la Jamatrine kwa sasa anaabudu kanisa la Shalom lililoko Mbezi Salasala! Karibu kwa Bwana Yesu Stara!


Source: Stara Thomas ameokoka! « Strictly Gospel

Umemkaribisha kwa bwana Yesu kwa kuwa kaingia kanisa la SHALOM. Je, kule JAMATRINE si kwa Yesu? Ni kwa nani?
 
hakuna jipya wapo wenzake wengi wamenena hilo na wanaendelea... Uchafu wao ngoja tuone.
 
Haya makanisa ya kisasa yaani tabu kweli kweli, siku hizi yamechuja ni kama kichaka cha kujifichia wezi, miaka ya themanini na tisini yalikuwa moto kweli kweli, yaani mtu akiwa huko watu walimuona kama malaika vile.

Sasa huyu nae kahama kanisa moja kwenda lingine eti ndio kuokoka!, matusi hayo.
 
Yohana 10:27 "Kondoo wangu husikia sauti yangu nami nawajua, nao hunifuata" big up Stara!!
 
Haya makanisa ya kisasa yaani tabu kweli kweli, siku hizi yamechuja ni kama kichaka cha kujifichia wezi, miaka ya themanini na tisini yalikuwa moto kweli kweli, yaani mtu akiwa huko watu walimuona kama malaika vile.

Sasa huyu nae kahama kanisa moja kwenda lingine eti ndio kuokoka!, matusi hayo.
mjukuu acha kejeli,
Mtu ni maamuzi yake
hivi unajua Yesu alikuja kwa ajiri ya akina nani? kama wewe ni mwema au mtakatifu basi Yesu hakuja kwa ajiri yako.
Alikuja kwa ajiri ya wezi,wanyanganyi,wachawi,walevi,wazinzi,waasherati ,wafisadi na wenye tabia kama za hivyo
sasa wewe kama unaanza kumnyooshea mwenzako basi kwanza jiangalie wewe mwenyewe .
Kama unamlaumu huyu dada basi unamlaumu Yesu na Aliyemleta Mungu.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom