Nimekuwa nikiifuatilia Star TV kwa muda mrefu hata kabla mchakato wa uchaguzi haujaanza. Niliifurahia kwa sababu walikuwa wakiita wachambuzi ambao wanachambua kwa kutumia independent mind.
Toka mchakato wa uchaguzi uanze hii TV imeanza kupoteza credibility, wanaita wachambuzi huku wanawapangia nini cha kuongea, unawaona watu wazima wanaongea mambo ambayo hayapo kwenye nafsi zao. Nimejaribu kufanya utafiti kupata habari za ndani kulikoni, mtu mmoja aliyepata za ndani ni kwamba Star TV imelipwa na CCM kufanya upendeleo wa makusudi katika habari na uchambuzi wake. Mtu huyu ameenda mbali zaidi akasema wamehakikishiwa na CCM kwamba hata wakipigwa faini na TCRA kama walivyofanyiwa Magic FM na TBC CCM wako tayari kulipa faini!
Ni jambo lililo wazi kwamba Star TV inamilikiwa na kada wa CCM Diallo, hilo halina ubaya na ana uhuru wa kikatiba kufanya hivyo. Kinachosikitisha ni kujifanya wako balanced wakati sisi watazamaji tunag'amua. Katika nchi zilizoendelea baadhi ya vyombo vya habari huwa vina declare interest katika uchaguzi kwamba wanaunga mkono chama au mgombea fulani. Kwa hiyo nawashauri star TV watutangazie wazi kwamba katika mchakato huu wa uchaguzi wanaunga mkono CCM bila kificho, tutawaheshimu kwa hilo na hiyo ni sehemu ya demokrasia ya kweli.
Nawasilisha