John Haramba
JF-Expert Member
- Feb 4, 2022
- 365
- 1,373
Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Tulia Ackson, jana Machi 14, 2022 aliwatembelea na kuwajulia hali Joseph Haule maarufu kama Profesa Jay pamoja na Mama mzazi wa Mbunge wa Viti Maalum CHADEMA, Halima Mdee, Bi. Theresia Mdee ambao wamelazwa na kupatiwa matibabu katika Hospitali ya Taifa Muhimbili iliyopo Jijini Dar es Salaam.
Dkt Tulia ameelezwa kuwa hali za wagonjwa hao zinaendelea kuimarika kila siku tofauti na awali ambapo, pia ametumia nafasi hiyo kuwapongeza na kuwashukuru wahudumu wa hospitali hiyo wakiwemo madaktari ambao wamekuwa wakijitolea kwa nguvu zote katika kuokoa maisha ya watu.
Source: Dodoma Zone
Dkt Tulia ameelezwa kuwa hali za wagonjwa hao zinaendelea kuimarika kila siku tofauti na awali ambapo, pia ametumia nafasi hiyo kuwapongeza na kuwashukuru wahudumu wa hospitali hiyo wakiwemo madaktari ambao wamekuwa wakijitolea kwa nguvu zote katika kuokoa maisha ya watu.
Source: Dodoma Zone