Spika Ndugai ana personality disorder?

Spika Ndugai ana personality disorder?

Naona wazi kuwa Mh. Mnyika alikosea. Lkn naona pi wazi kuwa mh .spika alikosea hata zaidi. Adhabu na kosa havilingani kabisa.
Ingetosha tu kumtoa Kikao kimoja.
 
Ongea yote hadi ya chumbani kwako. Uzuri sisi tunajiamini na hatuna mihemko ya kisiasa
Hatimaye umekuja kwenye angle,ningejua toka mwanzo kuwa wewe mwana lumumba nisingepoteza muda kufanya mjadala!
 
Hatimaye umekuja kwenye angle,ningejua toka mwanzo kuwa wewe mwana lumumba nisingepoteza muda kufanya mjadala!
Wewe huelewi maana ya SISI. tena ni aibu kutofanya mjadala na mtu kisa ni wa itikadi flani, ni udhaifu wa hali ya juu unaopelekea taifa letu pendwa kuonekana taifa la mbumbumbu
 
Hapa kuna kudharaulika kiti cha spika. Spika ni mtu mkubwa saba katika hii nchi, anashikilia moja ya mihimili mitatu ya dola. Hata kama wewe ni mpinzani na kuna kitu kimekukera heshimu tu kiti cha spika. Kiti cha spika kikiheshimika hata anayekalia kiti hicho atajiheshimu. Linganisha na enzi za Pius Msekwa na Samuel Sitta, kiti cha spika kiliheshimika na spika hakuwa na tatizo na wabunge. leo hii mtu anatukana mubashara bungeni eti spika ni fala au sijui nini... Mara mwingine anakataa kutii amri ya spika mwenye mamlaka yake unategemea nini? Spika nae ni mtu na ana mihemuko yake, lazima afure pale kiti chake kinapodharauliwa. Kwa Suala la Mnyika juzi hekima tu ingetumika. Mnyika angekaa tu kimya kama alivyoamriwa wala asingetakiwa kutoka nje. Tena pale amri ya kutoka nje angejongea mwenyewe nje nani angemgusa? Angeonesha ana hekima na kila mtu angekuwa upande wake. Lakini kwa sasa mtu yeyote anayemtetea mnyika ni kwa sababu tu ya mihemukio ya kisiasa, kiukweli mnyika alidharau kiti cha spika.
Yawezekana akili unazo ila unajitoa fahamu au huna fahamu lakini unajitia una akili.

Pius Msekwa na Samwel Sitta waliheshimika na sio kwamba kiti kiliheshimika. SPIKA NDIO KITI. Heshima hujengwa na spika kwa matendo yake na namna anavyodeal na matatizo yaliyo mbele yake.

Haki ndio huleta heshima na usawa. Ni spika ndio alikuwa wakwanza kuintertain malumbano kwa kusema maneno ya kumsifia mtukanaji mmoja. Amsha akili yako. Hata wewe ukikosa haki, watoto wako mwenyewe uliowazaa watakufanyia ukaidi.
 
Wewe ni askari gani wewe!!! Siyo kauli ya kiungwana hiyo!!
 
Wewe huelewi maana ya SISI. tena ni aibu kutofanya mjadala na mtu kisa ni wa itikadi flani, ni udhaifu wa hali ya juu unaopelekea taifa letu pendwa kuonekana taifa la mbumbumbu

Utafanyaje mjadala na mtu ambaye ameamua kuweka akili zake mfukoni?
 
Wewe ukiwa mkuu wa kaya/familia halafu atokee mtoto aseme baba fala na mtoto mwingine amwite mtoto mwenzake mwizi, je utalinganisha kauli hizo? suala la spika kuitwa fala ni jingine, na la mnyika kuitwa mwizi ni jingine. Tena spika ana hekima sana, Kuitwa fala? Wapinzani hamna shukrani kabisa, ingekuwa ni mimi ndie spika aliyeniita fala asingekuwa mbunge maisha yake yote

Kwahiyo hoja yako kosa ni akifanyiwa spika ila akifanyiwa mbunge mwingine sio kosa. Hoja yako hapo juu ndio maana halisi ya unafiki. Kama unafanya hilo kwa watoto wako watakuwa wanakuzarau ila hujui tuu.
 
Yawezekana akili unazo ila unajitoa fahamu au huna fahamu lakini unajitia una akili.

Pius Msekwa na Samwel Sitta waliheshimika na sio kwamba kiti kiliheshimika. SPIKA NDIO KITI. Heshima hujengwa na spika kwa matendo yake na namna anavyodeal na matatizo yaliyo mbele yake.

Haki ndio huleta heshima na usawa. Ni spika ndio alikuwa wakwanza kuintertain malumbano kwa kusema maneno ya kumsifia mtukanaji mmoja. Amsha akili yako. Hata wewe ukikosa haki, watoto wako mwenyewe uliowazaa watakufanyia ukaidi.
Twende vizuri tu, acha lugha zisizofaa. Spika alikuwa wa kwanza kuintertain malumbano kwa kusema maneno ya kumsifia mtukanaji mmoja.
Hii ni sentensi yako. Sijui kama usikivu wako uko sawasawa. tafadhali kapitie mwenendo wote wa bunge wa hiyo siku, ikiwezekana kacheki hansad halaf uje upya. pia sijakuelewa unaposema Pius Msekwa na Samwel Sitta waliheshimika na sio kwamba kiti kiliheshimika. Kwa hiyo unaniambia kiti cha spika hakikuwa na heshima?
 
Habari ya mjini ni MBOWE na WEMA KATIKA MAPENZI MAZITO.
 
"One can compromise on program but not on principles"
 
Utafanyaje mjadala na mtu ambaye ameamua kuweka akili zake mfukoni?
Tatizo lenu mmezoea kupelekeshana tu kama Nyumbu. si kila unachokiamini wewe na mwingine amini, tena bila hoja yoyote ya msingi
 
Kwahiyo hoja yako kosa ni akifanyiwa spika ila akifanyiwa mbunge mwingine sio kosa. Hoja yako hapo juu ndio maana halisi ya unafiki. Kama unafanya hilo kwa watoto wako watakuwa wanakuzarau ila hujui tuu.
Nimeomba kufahamishwa kosa alilofanya spika hamtaki kulionesha
 
Kama Ndugai ana pita huku au wasaidizi wake anatakiwa arudi bungeni na kukiri udhaifu wake na kuomba radhi. Hii itamjengea heshima.
Hapa ni pale Mh. Mbowe alipo wahi kusema anamuomba Mungu viongozi wa bunge wawe wana hudhuria kwenye misiba ili wajue maisha ya binadamu yana mwisho
 
Pole sana,kama bado hujawa zwazwa moja kwa moja,take a moment,think clearly na utaona toka mwanzo umeendeshwa na mihemko!Nimechelewa kuligundua hilo
Sina mihemko. siku zote nasimama kwenye ukweli. Siko kwenye itikadi ya chama chochote hapa tz lakini sisiti kupinga chama chochote kinachoenda kinyume na misingi ya kitaifa
 
Wewe huelewi maana ya SISI. tena ni aibu kutofanya mjadala na mtu kisa ni wa itikadi flani, ni udhaifu wa hali ya juu unaopelekea taifa letu pendwa kuonekana taifa la mbumbumbu
Kufanya mjadala na mtu anayejitoa ufahamu inakera nani upetezaji wa muda usiovumilika.
Wewe huelewi maana ya SISI. tena ni aibu kutofanya mjadala na mtu kisa ni wa itikadi flani, ni udhaifu wa hali ya juu unaopelekea taifa letu pendwa kuonekana taifa la mbumbumbu
 
Sina mihemko. siku zote nasimama kwenye ukweli. Siko kwenye itikadi ya chama chochote hapa tz lakini sisiti kupinga chama chochote kinachoenda kinyume na misingi ya kitaifa
Nisaidie wapi umewahi kumkosoa JPM,niwekee link tu nitaamini maneno yako!
 
Back
Top Bottom