Spika Makinda: Mjadala hauzuiliki

Spika Makinda: Mjadala hauzuiliki

View attachment 205400
jamaa: Kwanini kila siku unaiba

mbwa: sio mimi unanisingizia

jamaa: Hizi video nilizokuonyesha za nani ??

mbwa: Sio zangu wameedit

jamaa: wiki iliyopita nzima umeiba kuku wa mama mwanakombo Juzi umeiba mboga ya mama mwajuma jana umekula chakula cha chausiku zote nimekutetea na wakanielewa.
Sasa leo umeiba fungu langu la dagaa nilionunua mia tano kwa ajili ya ugali na kachumbali ugali wenyewe kilo bora ungekuwa nusu ningekunywa na maji ningelala

Mbwa: Nisamehe sirudii tena

jamaa: Sasa hili ni "Onyo la mwisho unanisikia"

Mbwa:Ndio

jamaa: Sasa ukirudia tena nakurudisha kwenu Iringa
 
Bi Kiroboto ana machale, maana wabunge ilikuwa wamuondoe yeye kwanza kwa kutokuwa na imani nae halafu mambo mengine yaendelee. Kama ameliona hilo basi kapona. Ila angalizo asije kutuchagulia wabunge wasio na hoja kwenye mjadala.
 
Jana baada ya "UKAWA" kuomba suala la ESCROW lijadiliwe huku wakimuonya kuwa kama kuna nyaraka zinaandaliwa kwa lengo la kumchafua Mh. Spika Makinda kuwa na yeye alipata mgao wa dola millioni moja, nilimuona Makinda anatoa povu huku cheche zikiruka kwa jazba ya ajabu.

Alisema "...kama mimi nimechukua dola mia moja, hizo mnasema sijui dola milioni moja mtanionyesha na MTAKO..., mtanionyesha..."

Inashangaza kuona Makinda kama amekuja KULINDA mafisadi na KAWAPANIA UKAWA vibaya sana. Neno mtako..., lilikuwa na muendelezo wa MTAKOMA!

Kesho Makinda atakuwa na kazi moja tu, KULINDA MAFISADI kwa nguvu zake zote na kutupilia mbali maslahi ya Taifa. Jazba aliyonayo ni ya kuhakikisha Pinda hang'oki. Makinda ameshasema UKAWA WATAKOMA!
 
Naada ya Mnyaa kumwambia kuwa kuna tetesi kuwa naye kavuta USD millioni mama akapaniki na kuanza kutema cheche kuwa mtani... Sijui alikuwa anataka kusema mtanitambua au vipi. Hapo ndio walipo muweza kwani picha imejengeka kuwa akizuia tuu ni kwamba basi naye anahusika na mama wa watu pengine anajijua hajala hata senti ya nini lawama?

Mnyaa alitumia akili sana kumuinclude Makinda maana ile ilimpanikisha halafu ilimuweka dilema makinda.lets wait and see
 
Spika wa Bunge,Anne Makinda amesema kuwa Mjadala wa Ripoti za CAG na TAKUKURU juu ya Escrow hauzuiliki. Spika Makinda alinidokeza kuwa kwa hali iliyopo,mjadala utafanyika na maamuzi kufikiwa. Ameongeza kuwa Ripoti husika zimeshaanza kugawiwa kwa Wabunge kama alivyoahidi jana asubuhi Bungeni.

"Mjadala utafanyika. Kujaribu kuuzuia ni kujitafutia lawama. Sina cha ku-save hapa zaidi ya kuongoza mjadala na kufikia maazimio" alisema Spika Makinda huku akiangua kicheko.

Mambo ni moto. Kaeni mkao wa kula. Kesho msiangalie hata pembeni. Best wishes to Zitto,Parliamentarians and the Cabinet!

Mzee Tupatupa wa Lumumba (Dodoma kwa kazi maalum)

Wahafidhina na mafisadi wamezidiwa na nguvu ya umma katika ujumla wake; Anna amegundua "Hamkani si shwari tena" akijifanya ngagari hasira za wananchi zitahamia kwake; hastahili kusifiwa kama ataendesha mjadala huo to its logical conclusion; huo ndio utashi wa wanachi na hilo ndilo jambo sahihi la kufanya; she is not doing us any favor; that is her rightful duty and cause of action.
 
Ngoja tusubir tuone jinsi Mwenyekiti wa DHADEMA , FREEM MBOWE atakavyojitetea kwa Mwenyekiti wa PAC, ZITTO KABWE

Umeshamwambia Mwenyekiti wako kuwa aanze kuwajibika kabla hajawajibisha?:confused2::sick::sick:
 
"Serikali ilikuwa ni mteja wangu katika kesi kati ya Tanesco na IPTL… nikiwa bungeni siwezi kuongea hadi nipate kibali cha Mwanasheria Mkuu wa Serikali kutokana na maadili ya kazi zetu, lakini uchunguzi ukibainika kwamba nililishwa sumu kwa sababu hiyo nitaweka kando maadili ya kazi." - wakili mkono
 
Amini amini nawaambia kabla jua halijaondoka kasho , baadhi yao watakuwa wameshaondoka.... Tulianza na mungu ! Tunamaliza na allah !
 
Jitihada za MBOWE kuuzuia kupitia MARANDO kwa hiyo zitakuwa zimegonga mwamba

Vipi U-robot wako ni kutokana na kumeza DVD yenye chuki kwa Mbowe??? Huwezi kubadili kidogo ili tuweze kushare views kama watanzania wenye uchungu na nchi yetu?
 
Spika wa Bunge,Anne Makinda amesema kuwa Mjadala wa Ripoti za CAG na TAKUKURU juu ya Escrow hauzuiliki. Spika Makinda alinidokeza kuwa kwa hali iliyopo,mjadala utafanyika na maamuzi kufikiwa. Ameongeza kuwa Ripoti husika zimeshaanza kugawiwa kwa Wabunge kama alivyoahidi jana asubuhi Bungeni.

"Mjadala utafanyika. Kujaribu kuuzuia ni kujitafutia lawama. Sina cha ku-save hapa zaidi ya kuongoza mjadala na kufikia maazimio" alisema Spika Makinda huku akiangua kicheko.

Mambo ni moto. Kaeni mkao wa kula. Kesho msiangalie hata pembeni. Best wishes to Zitto,Parliamentarians and the Cabinet!

Mzee Tupatupa wa Lumumba (Dodoma kwa kazi maalum)

hana cha kupoteza liwalo na liwe a ukizingatia mwakani aingii tena siasani daah .
 
Meaning amejaribu kuzuia akashindwa. Ungekuwa unazuilika, angezuia mjadala usifanyike. Yaani, angepata namna ya kuzuia, angezuia. This implies that mijadala anayoruhusu kufanyika bungeni ni ile ambayo haina madhara kwa watawala au ambayo hukosa namna ya kuzuia. Hatuna speaker. Amejisahau na kuwa sehemu ya serikali.
 
yeye mwenyewe ni mtuhumiwa vp Ndugai ameenda wapi mbona sijamwona bungeni kuanzia jana
 
By thatha:
Ngoja tusubir tuone jinsi Mwenyekiti wa
DHADEMA , FREEM MBOWE atakavyojitetea kwa
Mwenyekiti wa PAC, ZITTO KABWE
Mara ya mwisho kupimwa vipimo vya tezi
dume ilikuwa lini?kweli mkuu inabidi akapime tezi dume huyo.
 
Back
Top Bottom