Tonny Kapola Gas Station
JF-Expert Member
- Aug 14, 2025
- 361
- 944
1. "Oktoba 29 tulitumia nguvu kubwa Kwa sababu ya Vurugu, mlitaka tutumie nguvu ndogo ili iwaje"
2. "Waliohamasisha maandamano Oktoba 29 ni Kwa sababu ya shida za maisha, na walifanya hivyo ili Watanzania wanunue bando wawaangalie ili walipwe"
3. "Kuna watu tunawaambia waje mezani kwenye Maridhiano Ila wao wanajifanya kutaka kutupangia kwamba Hadi tufanye kitu Fulani ndio waje, Niwaambie tu Serikali yangu haitapangiwa Wala kuamrishwa na Watu , Serikali ya wanafunzi na waalimu ndio itakayopangiwa na siyo Serikali yangu"
4. "Wapinzani walihamasisha maandamano Kwa sababu waliishiwa Pawa"
5. "Mnalalamika Vijana wenu wameuliwa, kwanini hamkuwazuia wasiende?"
6. "Vurugu za Oktoba 29 zililenga kuiangusha Dola, walishindwa"
7. "Nasikia Kuna lingine wamepanga kukifanya December 9 , Niwaambie tu na Hilo halitafanikiwa hata kidogo"
8. "Mimi ndio Rais wa Tanzania na Serikali ninayoiongoza inafanya Kazi, uwe unaitambua au huitambui Ila Ndiyo Serikali na Mimi ndiyo Rais.