Source hii ya Rais Magufuli aifukuze haraka...

Nilishangaa juzi aliposema eti serikali yake haijazuia watumishi kupandishwa madaraja ila walikua wanapisha uhakiki kwa miezi Miwili.....Uhakiki wenyewe ulianza mwezi wa Tatu...Hivi Leo miezi miwili bado....Yani huu ni uongo wa kiwango cha bahari ya Atlantic
 
Rais alikuwa haongelei mshahara pekee bali pay package ya baadhi ya watumishi wa serikali.

Prof. Ndulu alichosema ni namna ambavyo hiyo account ilifunguliwa na sio ubaya wa uwepo wa Fixed Account. kwa hiyo hajamkosoa Rais bali alichokisema ndicho Rais alikisema.

Kama Tanzania ingekuwa na waandishi wa habari wazuri, walitakiwa wambane awaeleze maana ya maneno ''namna ambavyo ilifunguliwa'' lakini kwa sababu taaluma imejaa makanjanja basi hawakuweza hata kuuliza

Rais Magufuli hajasema Fixed Account ni mbaya bali zilikuwa zinakuwa abused na baadhi ya wafanyakazi wa mashirika ya umma.

Soma BOT Act 2006 imeeleza kwa kirefu kuhusu Fixed Account kwa taasisi za serikali.
Exactly exactly. Watu wanmapenda kupotosha. Kwani si kweli kuna watu walikuwa walikuwa wanapata package kufuru na wengine hawana?!?!?! Unfortunately kwenye JF kuna watu wa kila level! Na wengine ndio wamelipwa kuichafua hii serekali. Nina hakika baadhi yao walikuwa interest inayopatikana wala hairipotiwi. I am very mcuh sure ni hivyo! Mh. Magufuli endelea tu usikate tamaa!
 
Dah hapa ndipo napo mvulia kofia Hashim Rungwe Spunda alisema " anachofanya jamaa ni kuonyesha tabia zake na sio utendaji "

Oh Jecha apewe tuzo
Mkileta fyokofyoko..
Oh sukari zote nitataifisha na kuwapa wananchi ni wapi aligawa hata kilo moja ?
Oh mshahara wangu ...mbona hiyo salary slip haitoi ?
Oh una roho nzuri sana Kikwete ningekuwa mimi ningewapoteza wote..
Oh mke sijui wa waziri gani trafki blah bla bla

walazwe tu ...
Ni hela za kiwi ......
Fyatueni watoto nitawasomesha wakati waliopo ameshindwa kuwapa mikopo
Oh sijui vilaza wakati mwanae naye pia kilaza tu

Oh sijui magangwala wapewe wananchi na wasukuma wanaitikia ndioooo kumbe yale ni hatari yana sumu kuna namna ya ku handle.

Oh sijaribiwi umekuwa Mungu wewe?

Oh msini drive ... umekuwa combine harvester wapi una accelerator na clutch ?
Bos una millions 7??
 
Akili za kuambiwa changanya na zako, sasa yeye hafikirii kila analoambiwa?? Hivi ras simba bado anafundisha kiingereza maana mimi nipo maporini huku
 
Mimi sijawahi kuiamini hii serikali maana hakuna walichowahi kutwambia ukweli, kila siku wanaruka na kukanyagana tu,cha muhimu kwao ni vinono wanavyokula basi
 
Yawezekana aidha bwana Mafuru au Dr. Magufuli hakufafanua vizuri ni viongozi gani hao na wakiwa kwenye wizara au idara au wakala wa serikali. Hivi mkurugenzi mkuu wa NSSF analipwa mshahara wake kuptia hazina?
 
"Mtu" huyo huyo nido aliyemshauri vibaya Raisi wetu kuwa kuanzia Septemba mwaka huu wahamishe wizara zote na ziwe zimehamia Dododma. Na Raisi wetu aliapiza asiye hamia Dodoma kabla yake hata pata mshahara. Lakini cha kushangaza hakuna hata wizara yeyote iliohamia Dodoma na hakuna waziri yeyote aliekatwa mshahara. Sijui hawa mawaziri wanamwekea mgomo Raisi wetu!

Raisi alikuja na agenda nzuri ya kusafisha jiji mwishoni mwa wiki, lazima "mtu" huyo kamshawishi Raisi wetu kuachana na kusafisha mji, mji wetu bado umetta na taka taka.
Raisi alikuja na ajenda nzuri ya kuboresha mahospitali Tanzania, lakini "mtu" huyu kamshawishi tena Raisi wetu kuachana na hospitali. Eti Muhimbili imeshapata "mahitaji" yote na tuachane na Hospitali ya Temeke, Mwananyamala na hospitali nyingine zote Tanzania.

Huyu mtu anae mfidi raise wetu nashauri ni jipu na atumbuliwe.
 

Attachments

  • 1480621096621.jpg
    1480621096621.jpg
    26.5 KB · Views: 22
Interesting! Kama hadi leo hii tunahitaji kuendelea kuendekeza uswahili wa "rais kadanganywa"; "rais anashauriwa vibaya"; "raisi anaangushwa na watendaji wake" and all sorts of such hogwash! Tangu enzi za JKN hadi leo hii? Halafu tunathubutu kujidai tunatarajia maendeleo ya viwanda tukiwa na viongozi wenye kuhitaji ufafanuzi wa kila aina. Such a bunch of losers we are.
 
...wewe ni mojawapo wa watoa utumbo naowazungumzia....hamuambiliki type yenu....
Type yetu hatuambiliki kwa sababu mnachotuambia hakifanani na hoja zenye uzito. Nyinyi ambao kwa uwezo wa kufikiri mnajiona mnaongea points tu ni wepesi sana kushikiwa akili, sasa sisi hatupendi muendelee kuwa hivyo, na hatuwezi kukaa kimya tu when you allow yourself to be constantly fooled.
 
Back
Top Bottom