Boran Jakutay
Senior Member
- Apr 8, 2023
- 110
- 255
Jeshi la Polisi Mkoa wa Songwe limethibitisha kumkamata Veronica Petro (24) mkazi wa Wilaya na Mkoa wa Songwe akituhumiwa kumuua mtoto wa mume wake, Mageshi Usiga (7) aliyekuwa akimlea.
Kamanda wa polisi mkoani humo, Theopista Malya, amesema mtuhumiwa alitenda kosa hilo baada ya mtoto huyo kupoteza ng’ombe wawili akiwa machungani mwishoni mwa mwezi Februari.
“Mtu anayeitwa Usiga Nabinilo mwenye umri wa miaka 42, aligundua kuuwawa kwa mtoto wake mwenye umri wa miaka 7 aitwaye Mageshi Usiga, na inadaiwa kwamba aliuwawa na mama yake wa kambo.
“Baada ya kufuatilia tuligundua kwamba mama huyu alimtandika mtoto huyu lakini pia alikuwa akimkanyanga maeneo ya kichwani na kifuani, ikapelekea kifo chake.
“Baada ya kuhakikisha mtoto huyo amekufa akaenda kumtupa umbali kama wa mita 352 kutoka nyumbani wanapoishi, lakini polisi walipofika walimchukua mtoto huyo na kumpeleka hospitali kwa uchunguzi kugundua sababu ya kifo chake.
“Lakini sababu iliyopelekea kumpiga mtoto huyo, tarehe 28 mwezi wa pili, huyo mtoto alikuwa machungani na ng’ombe wawili kupotea, ndiyo kilichopelekea mama huyo kumpiga mtoto hadi kumuua.
“Huyo mama kwa sasa yupo magereza kwa ajili ya kesi hiyo inayomkabili ya mauaji,” alisema kamanda Malya.
CHANZO: UFM RADIO
Kamanda wa polisi mkoani humo, Theopista Malya, amesema mtuhumiwa alitenda kosa hilo baada ya mtoto huyo kupoteza ng’ombe wawili akiwa machungani mwishoni mwa mwezi Februari.
“Mtu anayeitwa Usiga Nabinilo mwenye umri wa miaka 42, aligundua kuuwawa kwa mtoto wake mwenye umri wa miaka 7 aitwaye Mageshi Usiga, na inadaiwa kwamba aliuwawa na mama yake wa kambo.
“Baada ya kufuatilia tuligundua kwamba mama huyu alimtandika mtoto huyu lakini pia alikuwa akimkanyanga maeneo ya kichwani na kifuani, ikapelekea kifo chake.
“Baada ya kuhakikisha mtoto huyo amekufa akaenda kumtupa umbali kama wa mita 352 kutoka nyumbani wanapoishi, lakini polisi walipofika walimchukua mtoto huyo na kumpeleka hospitali kwa uchunguzi kugundua sababu ya kifo chake.
“Lakini sababu iliyopelekea kumpiga mtoto huyo, tarehe 28 mwezi wa pili, huyo mtoto alikuwa machungani na ng’ombe wawili kupotea, ndiyo kilichopelekea mama huyo kumpiga mtoto hadi kumuua.
“Huyo mama kwa sasa yupo magereza kwa ajili ya kesi hiyo inayomkabili ya mauaji,” alisema kamanda Malya.
CHANZO: UFM RADIO