ChoiceVariable
JF-Expert Member
- May 23, 2017
- 43,044
- 49,727
Mambo ya wivu wa kimapenzi.
Wanawake ogopa sana kutolewa na wanaume wanaojifanya wanawapenda sana au Wana wivu sama mtakuwa mnakatwa vichwa.
Olewa na watu sampuli ya Mimi hata nikikuta Watoto sio wangu na move on maisha yaendelee na Leo hao hao na Wala sijihangaishi kuwakagua.
R.I.P mama na mtoto uliolewa na jitu punguani.
=====
JESHI la Polisi Mkoa wa Songwe linamshikilia mwanamume mkazi wa Kijiji cha Kaloleni, wilayani Songwe (jina linahifadhiwa kwa sababu za kiuchunguzi) kwa tuhuma za mauaji ya Editha Msokwa (38) na mtoto wake mchanga wa miezi sita, Esther Emanuel.
Chanzo cha mauaji hayo kinadaiwa ni wivu wa mapenzi baada ya mtuhumiwa huyo kumtuhumu mkewe huyo kuzaa mtoto nje ya ndoa.
Mtuhumiwa huyo ambaye kwa sasa amelazwa katika Hospitali ya Mwambani, wilayani Songwe baada ya kujeruhiwa na wananchi, anadaiwa kumvizia mkewe akiwa amelala usiku na mtoto wake huyo wa miezi sita na kuwanyonga kabla ya kuuburuta mwili wa mkewe huyo na kwenda kuuficha katika kibanda nje ya nyumba yao.
Akithibitisha kushikiliwa kwa mtuhumiwa huyo, Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Songwe, Rashid Ngonyani, alisema jana kuwa kuwa mtuhumiwa huyo alikamatwa Septemba 24 mwaka huu.
Alisema mtuhumiwa alikamatwa baada ya kuokolewa na viongozi wa kijiji chini ya Mwenyekiti Laiton Waya kutoka katika kundi la wananchi wenye hasira kali waliomkamata baada ya kufanya tukio hilo la mauaji ya kinyama na kuanza kumshushia kipigo.
“Mtuhumiwa huyo kwa sasa amelazwa katika Hospitali ya Mwambani akiwa chini ya ulinzi, na uchunguzi wa awali wa Jeshi la Polisi unaonesha mtuhumiwa kabla ya kutekeleza mauaji hayo walikuwa na mgogoro na mkewe kwa kumtuhumu kuzaa nje ya ndoa,” alisema Kaimu Kamanda Ngonyani.
Alisema kuwa jeshi hilo linaendelea na uchunguzi na pindi utakapokamilika, mtuhumiwa atafikishwa mahakamani.
Wanawake ogopa sana kutolewa na wanaume wanaojifanya wanawapenda sana au Wana wivu sama mtakuwa mnakatwa vichwa.
Olewa na watu sampuli ya Mimi hata nikikuta Watoto sio wangu na move on maisha yaendelee na Leo hao hao na Wala sijihangaishi kuwakagua.
R.I.P mama na mtoto uliolewa na jitu punguani.
=====
JESHI la Polisi Mkoa wa Songwe linamshikilia mwanamume mkazi wa Kijiji cha Kaloleni, wilayani Songwe (jina linahifadhiwa kwa sababu za kiuchunguzi) kwa tuhuma za mauaji ya Editha Msokwa (38) na mtoto wake mchanga wa miezi sita, Esther Emanuel.
Chanzo cha mauaji hayo kinadaiwa ni wivu wa mapenzi baada ya mtuhumiwa huyo kumtuhumu mkewe huyo kuzaa mtoto nje ya ndoa.
Mtuhumiwa huyo ambaye kwa sasa amelazwa katika Hospitali ya Mwambani, wilayani Songwe baada ya kujeruhiwa na wananchi, anadaiwa kumvizia mkewe akiwa amelala usiku na mtoto wake huyo wa miezi sita na kuwanyonga kabla ya kuuburuta mwili wa mkewe huyo na kwenda kuuficha katika kibanda nje ya nyumba yao.
Akithibitisha kushikiliwa kwa mtuhumiwa huyo, Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Songwe, Rashid Ngonyani, alisema jana kuwa kuwa mtuhumiwa huyo alikamatwa Septemba 24 mwaka huu.
Alisema mtuhumiwa alikamatwa baada ya kuokolewa na viongozi wa kijiji chini ya Mwenyekiti Laiton Waya kutoka katika kundi la wananchi wenye hasira kali waliomkamata baada ya kufanya tukio hilo la mauaji ya kinyama na kuanza kumshushia kipigo.
“Mtuhumiwa huyo kwa sasa amelazwa katika Hospitali ya Mwambani akiwa chini ya ulinzi, na uchunguzi wa awali wa Jeshi la Polisi unaonesha mtuhumiwa kabla ya kutekeleza mauaji hayo walikuwa na mgogoro na mkewe kwa kumtuhumu kuzaa nje ya ndoa,” alisema Kaimu Kamanda Ngonyani.
Alisema kuwa jeshi hilo linaendelea na uchunguzi na pindi utakapokamilika, mtuhumiwa atafikishwa mahakamani.