Kwani hayo makaratasi yana tofauti gani na yale makaratasi mengine yanayoitwa Fedha?
Mitazamo (Perception) ya watu usipoinyumbulisha utayumbishwa mpaka uchanganyikiwe. Kwani dhahabu zaidi ya kuwa pambo ina kazi gani nyingine hadi ipewe thamani inayopewa?
Mifumo ikishawekwa una mambo mawili tu ya kufanya. Ama uiheshimu au uibomoe uweke ya kwako itakayoendana na matamanio yako.
Hata hivyo jamaa anahimiza jambo la muhimu sana, Kuwa Ajira ni jambo gumu sana kupata Tanzania , hivyo hata kama umesoma (Kwa miaka 17-20) rudi mtaani katafute jambo la kufanya kama vile hujawahi kusoma.
Swali la kujiuliza. Kama watu wanasoma halafu wanarudi kufanya kazi za wasiosoma ,Kwa nini walisoma kwa miaka yote hiyo?
Hivi kuwa winga ama kuuza mahindi kunahitaji mpaka mtu afike chuo kikuu? Huyu jamaa hasemi wajibu wa Serikali kuhakikisha kuna mazingira mazuri ya wanaosoma kuajiriwa/kujiajiri ili kusudi la kusoma liwe halisi.