Solo Thang: Nakupenda ila hujatulia

Solo Thang: Nakupenda ila hujatulia

dah naunga mkono hoja 101% ni bonge la ubunifu aisee dah fumbo mfumbie mjinga nimemkubali solo thang. umenitoa kwenye sehemu ambayo nilianza kuwachambua mamiss mmoja baada ya mwingine sikupata picha duh

Wa kwanza atakuwa Wema 🙂
 
Solothang ni mmoja ya wasanii wenye mashairi makali sana ,nakumbuka wimbo wake wa Homa ya Dunia
 
hii ni mojawapo ya ngoma kali nilizowahi kusikia,traveller mtoto wa mbagala a.k.a msafiri kondo ni kwere.....lugha ya picha iliyotumika km hukutumia kichwa kufikiri unaweza ukadhani anazungumzia mapenzi.
 
Jaman wadau,kama inawezekana naomben mniwekee lyrics zake
 
Baba yake alikuwa mkoloni kipindi huyu Miss
mwali
Mchonga alikata utepe lakini hakuvinjari
Sababu alikua busy kumlinda na geti kali
Kumbe wenzake wanabinjuka, kushtuka akakaa
mbali Demu alikua na heshima kabla haijatangazwa
Rukhsa
Chukua Chako Mapema ukimkonyeza tu
umegusa
Ana kifua kimebetuka sio maziwa ni madini
Kayaacha wazi, watu wanashika hapo ndio anaponiudhi mimi
Watu wanagonga tu Ikulu tena kwa mitindo
huru
Kavu kavu bila kinga hajali vinavyodhuru
Kawa shangingi na amedata hana uwoga wa
kunguru Anapenda sana chapaa haimtoshi kodi na
ushuru
Ana kijungu matata laini kama nyanya masalo
Anatingisha Afrika nzima na mzigo Kilimanjaro
Usimchezee kwa vidani sio pete sio hereni
Anamiliki tanzanite kama ardhi ya Mererani Sura dhahabu inaita kama amezaliwa Geita
Tatizo ndio kicheche kila mwanaume ndio
amepita
Hata Benja hakutoka Kapa huyu demu hajatulia
Kama rushwa ndio kikwapa ananuka na kunukia Kiitikio Miss Tanzania
Nakupenda ila hujatuliaa
Vitendo vyako sitojivunia
Sifa yako kubwa umefulia
Miss Tanzania Ubeti wa Pili Bora angebaki kuwa modo kama Flavian
Matata
Ila demu amejiachia kisa anaendekeza bata
Sitachoka kuwakilisha jinsi anavyoniacha hoi
Juzi juzi kaopolewa na Handsome Boy
Kabla hapo shoga zake wote kashawaona mabwege
Sababu hawana dira na yeye ameshahongwa
ndege
Anafaa kuwa Miss Dunia maandalizi longolongo
Tatizo anakula sana akijamba ni Songosongo
Mara ghafla kanenepa kumbe mimba B.O.T. Kumbe demu aligawa EPA watu wamepiga hafu
jii
Alizugwa na akaunti hewa kuwadi Bwana Bilal
Mara mdomo naye kazimwa bila hata picha ya
kaburi
Kinachomponza huyu shawty utulivu sifuri Ila hakuna anayepinga kwamba huyu demu ni
mzuri
Mixer siasa na biashara demu ameshakuwa
chotara
Mishe za Dar akimaliza Mjengoni anakwenda
lala Kadri miaka inavyokwenda demu anazidi fulia
Kumbe weupe ni mkorogo ona mwili sasa
umefifia
Demu kazidi umalaya wacha mabwana
wamteme
Haogopi kuliwa mtungo kisa anagawa umeme Ubeti wa Tatu Wadaku walishamfuma anakula denda na
Richmond
Dowans akazidi kete akamvisha pete ya
diamond
Binti masikini akanasa bwana mshenga ndio
Lowasa Shemeji hataki hata picha ndio tabia gani sasa
Ndoa ilifungwa kwa vifijo vigogo wakala pizza
Keki nzima wale wao share yetu si ni giza
Sio hayo demu ana mengi ya kuchukiza
Malighafi ashazinadi for sale anajiuza
Mtaani ilivuma rumor demu kawa mama huruma Uchumi umefungwa drip maendeleo ndio kali
homa
Mali asili ndio kitasa kila ufunguo ndio unapita
Toka alipovunja ungo nusu karne imeshapita
Mapenzi kafanya mradi anamegwa na mafisadi
Amani kwa time bomb binti amekumbatia radi Vitendo vyake vibaya vinafanya adharaulike
Tabia Katiba sio Msahafu ndio useme
isibadilike
Mikosi inayomkuta ndio kwanza anatabasamu
Hajali waliomzunguka kama nao binaadamu
Mbagala walimbaka mpaka akamwaga damu Na juzi Gongo la Mboto kaanza kujamba
mabomu
 
Duuu nilijua miss tz gani hasa wema kumbe ni ujumbe tosha. Thax solo thang
 
Jamani mnaweza labda mtaniona niko nyuma kidogo ila leo ndio nimeusikia online huu wimbo wa miss tanzania nahisi umeshakuwa maarufu huko nyumbani. huu wimbo kuna mtu anajua alimuimbia mtu au aliamua kuburudisha tu watu? maana kuna majina ameyataja watu maarufu imeniogopesha kidogo, na kama kuna mtu amekusudiwa ki ukweli amemvua nguo kabisa hadi nguo za ndani ni aibu sana wenye kujua watujuze please solo thang ameshafanya interview na media yoyote kuhusu wimbo huu??

Huu wimbo anaiponda NCHI ya Tanzania namna ilivyo CHAFU
 
  • Thanks
Reactions: UKI
wote wenye vichwa vya kuku huu wimbo utawaumiza vichwa by the way mshkaj nimeupenda mstar wa Keki nzima wale wao share yetu si ni giza
 
Solo Thang sijui kwanini alikuwa anaimba miduara wakati ni MC Mkali
 
kwa hii nchi yetu ninavyoijua, wataufungia tuu huo
 
Jamani mnaweza labda mtaniona niko nyuma kidogo ila leo ndio nimeusikia online huu wimbo wa miss tanzania nahisi umeshakuwa maarufu huko nyumbani. huu wimbo kuna mtu anajua alimuimbia mtu au aliamua kuburudisha tu watu? maana kuna majina ameyataja watu maarufu imeniogopesha kidogo, na kama kuna mtu amekusudiwa ki ukweli amemvua nguo kabisa hadi nguo za ndani ni aibu sana wenye kujua watujuze please solo thang ameshafanya interview na media yoyote kuhusu wimbo huu??

ile ni artistic work..wonderful kaiongelea Tz kama mrembo kw sbb siku zote tuna beutiful country..hatuna handsome country..changamoto kwa ROMA mkatoliki braza anamfundisha jins ya ku deliver Jah msg pon de land..
 
Back
Top Bottom