KVM hata mitumba huko inakotoka inashonwa, lakini inashonwa kwenye viwanda bora mashine za kisasa na ubora wa vitambaa vinavyotumika unakuwa wa hali ya juu sana. Tanzania tulikuwa na kiwanda cha kushona Jeans kilikuwa kinaitwa Ubungo Garments kilikuwa kinauza nguo zake mpaka Marekani, sasa hivi kimegeuzwa kuwa Ofisi za wanaharakati wa kupigania haki za kijinsia!
Vile vimashine vinavyoitwa Butterfly ambavyo vimeenea kwa washonaji wetu Bongo vinatia kinyaa kabisa. Hizo mashine tunazoita za kisasa kama Juki n.k. hazina bei za ajabu hata kidogo. Tanzania imejaa vitu vingi sana vya gharama kuliko hata hizo cherehani za bei ya juu.
Kile kiwanda cha Ubungo Garments kama nakumbuka vyema kilikuwa ni SU. Kilikuwa kinachukua hata vijana waliokuwa wanamaliza JKT. Walikuwa na tenda ya kupeleka nguo Marekani - Jeans na Makaptula. Lakini kama zilivyo SU zote kikajifia kwa vile walikuwa wanashindwa kulinda Standards.
Jiulize kiwanda cha maturubai Morogor kimeishia wapi? Kile kiwanda kilipewa mpaka tenda ya ku-supply maturubai kwenye jeshi la Marekani. Wakafilisika bila sababu ya maana.
Nimebahatika kutemblea Bangkok mara kadhaa. Hizo nguo tunazokwenda kununua kule Thailand hazishonwi na viwanda vikubwa bali na viduka vidogo vidogo kama vile vilivyopo Mwenge. Hapa nazungumzia masoko kama Indra Market pale Bangkok. Wao wameweza sisi tunashindwa nini?
Kwa maoni yangu narudia tena ni bora kabisa kupiga marufuku uuingizaji wa mitumba Tanzania. Na tukipandisha kidogo kodi ya nguo zilizoshonwa watu wataweza kuanza kushona nguo kwa ushindani. Watu binafsi siyo mashirika.
Ni aibu kuona mpaka leo hii tuanaagiza nje mashati ya watoto wa shule. Kweli yanatushinda kushona? Mbona zamani zile tulikuwa na kiwanda cha Gossage kule Tanga amabcho kilikuwa kinavuma Afrika Mashariki nzima?