Soko Ubungo kuiua Kariakoo

Soko Ubungo kuiua Kariakoo

Kwamba wafanyabiashara wa nchi ulizozitaja wao China hawapafahamu??

Wafanyabiashara wa nchi kama zambia, malawi, congo ya lubumbashi na hata zimbabwe wengi pamoja na kuifahamu china hununua bidhaa zao kariakoo kama ilivo wafanyabiashara wa mwanza , kagera ambao hufuata bidhaa zao kampala sio kwamba china hawapafahamu hapana lakini hata mitaji pia inafanya mtu aende sehemu anayomudu, ungesoma vizuri alichoandika usingehoji namna hiyo
 
Serikali ikiua Kariakoo itakuwa kosa kubwa la kihistoria la kiuchumi kuwahi kufanywa Tanzania!
Hapa sio serikali kuiua Kariakoo. Kariakoo ni soko la bidhaa kutoka kokote duniani ingawa asilimia kubwa ya bidhaa ni za China

Hapo Ubungo Mchina anawekeza anaanzisha exhibition trading platform, cros-border E-commerce platform, commodity procurement platform kwa Made in China goods only

Hata huyo mfanyabiashara wa K/koo badala ya kwenda China anaweza kwenda Ubungo akajionea bidhaa anazopenda then akaenda kwa watu wa procure watakaokuwa na ofisi zao hapo hapo akafanya malipo akaagiza mzigo kutoka China. Ubungo itakuwa ni one stop wholesale center

Hakutakuwa na biashara za rejareja Ubungo
 
Kuna bomu litakuja kulipuka mbeleni tuwe wapole tu, muda ni mwalimu. Gap la walionacho na wasionacho ni kubwa sana, hatari sana
Ndio hivyo, viongozi wanawachukulia wabongo wapumbavu. Wanachukua ma mikopo makubwa, wananchi wakilalamika wanaambiwa wahamie Burundi. Maisha magumu wakiambiwa wanaambiwa wenyewe ni wachumi hawakusomea uganga wa kienyeji, kuna siku watu watachoka watakapoona utwana ndani ya nchi yao. Wawalete tu wachina, hao ccm na serikali yao wanadhani wabongo watakua wajinga milele iko siku kitawaka tu. Nchi zilizoendelea hali imekua ngumu pia lakini zinakua zinasaidia watu wa matabaka ya chini . Uvumilivu una mwisho haswa binadamu anapokosa chakula huku wengine wakiwa nacho na wako kwa V8s.
 
Serikali tupo makini na tumefanya upembuzi yakinifu kuhusu ili jambo. Halitaleta madhara yoyote, lengo tunataka zaidi Kariakoo yabakie maduka ya hardware.
 
Si tuna maprof maDr na wabobezi wa uchumi hilo hawalioni?
Bunge letu limejaa ma Dr.
Dr msukuma, Dr Tale, Dr mwigulu, Dr Tulia , na wengine wengi yaani wanazidiwa akili na wachina wafanyabiashara? Siamini . Litakuwa zuri saaana kwa taifa . Acha lije
 
Ukiwa China hizi exhibition trading platform centers ni vitu vya kawaida sana.

Kila jiji la China wanazo ili kuzitangaza bidhaa zao pia zinawasaidia wafanyabiashara wanaoenda China kuona bidhaa mbalimbali zinazotengenezwa China

Sasa hivi Mchina kaamua awafuate wateja hukohuko wanapotoka na kufungua hizi centers za maonyesho ya bidhaa za China ili wafanyabiashara wajionee bidhaa na wafanye kuagiza wakiwa nchi zao bila kwenda China

Mojawapo ni hii itakayofunguliwa Ubungo
 
Wageni walitakiwa kufungua viwanda Tanzania, na sio kufanya Tanzania sehemu ya kuleta mizigo yao.

Ubungo panajengwa soko la jumla la Wachina. Hili soko litakuwa lauza bidhaa za kutoka China kwa bei ya jumla, maana yake watashindana na maduka ya kawaida.

Je, serikali imewafikiria Watanzania na yatayotokea huko mbeleni?

Sent from my M2006C3LG using JamiiForums mobile app
Nadhani wamelegwa zaidi nchi za jirani waje huku kwetu.
 
Ukiwa China hizi exhibition platform centers ni vitu vya kawaida sana.

Kila jiji la China wanazo ili kuzitangaza bidhaa zao pia zinawasaidia wafanyabiashara wanaoenda China kuona bidhaa mbalimbali zinazotengenezwa China

Sasa hivi Mchina kaamua awafuate wateja hukohuko wanapotoka na kufungua hizi centers za maonyesho ya bidhaa za China ili wafanyabiashara wajionee bidhaa na wafanye kuagiza wakiwa nchi zao bila kwenda China

Mojawapo ni hii itakayofunguliwa Ubungo
Safi sana sisi tuakikishe wafanya biashara wa nje na majirani zetu wanakuja kwa wingi hapo ilitukusane kodi za kutosha.
 
Hii nchi uko inakokwenda inatengeneza vita vya wenyewe kwa wenyewe maana gap la walionacho na wasio nacho linazidi kuongezeka kwa kasi sana.

Mwendazake alijaribu kulipunguza lakini huyu Hangaya kaja na yake. Anyway time will tell.
ANGALIZO: Mimi sio mmoja wa wasio nacho, ni wa walionacho, ila ninawaza tu kwa kuangalia jicho la tatu.
Hizi Stori za Vijiweni mkuu, mwendazake Aliongeza Income inequalities, MO hakuwa Billionea, ila ndani ya miaka 5 ya huyo jamaa utajiri ukafika hadi 1.5B usd.

GSM walikuwa Tajiri wa kawaida ila ndani ya Awamu Yake tumeona biashara zake zilivyokua.

Bakhresa utajiri wake nao umekua Sana bado kidogo na yeye Ajiunge Billionaires Club.

Rostam tuliona alivyopewa Tenda kibao, etc.

Wakati hao matajiri wakizidi kuwa matajiri masikini nao wakizidi kuwa masikini, hakukuwa na Ajira, walio na Ajira wakapunguzwa etc.

Kupunguza gape baina ya matajiri na masikini ni kuhakikisha pato la masikini linaongezeka na njia kubwa ya kuongeza pato la masikini ni kuongeza Minimum wage, toka 2016 tuna minimum wage Ile Ile Hali ya kuwa maisha gharama Zina panda, unasemaje ni kupunguza Gape baina ya Matajiri na Masikini?
 
Safi sana sisi tuakikishe wafanya biashara wa nje na majirani zetu wanakuja kwa wingi hapo ilitukusane kodi za kutosha.
Naona Mchina ameona bandari ya Dar au akija kula shavu ile ya Bagamoyo ni potential ni lango la kusafirisha bidhaa zao kwenda Congo, Rwanda, Burundi, Zambia, Malawi, Uganda

Hawa ni wazee wa fursa na uwekezaji wa kimkakati
 
Hapa sio serikali kuiua Kariakoo. Kariakoo ni soko la bidhaa kutoka kokote duniani ingawa asilimia kubwa ya bidhaa ni za China

Hapo Ubungo Mchina anawekeza anaanzisha exhibition trading platform, cros-border E-commerce platform, commodity procurement platform kwa Made in China goods only

Hata huyo mfanyabiashara wa K/koo badala ya kwenda China anaweza kwenda Ubungo akajionea bidhaa anazopenda then akaenda kwa watu wa procure watakaokuwa na ofisi zao hapo hapo akafanya malipo akaagiza mzigo kutoka China. Ubungo itakuwa ni one stop wholesale center

Hakutakuwa na biashara za rejareja Ubungo
Asante Mzee wa Kupambanua mambo!
 
Wageni walitakiwa kufungua viwanda Tanzania, na sio kufanya Tanzania sehemu ya kuleta mizigo yao.

Ubungo panajengwa soko la jumla la Wachina. Hili soko litakuwa lauza bidhaa za kutoka China kwa bei ya jumla, maana yake watashindana na maduka ya kawaida.

Je, serikali imewafikiria Watanzania na yatayotokea huko mbeleni?

Sent from my M2006C3LG using JamiiForums mobile app
Kajifunze kichina uwe makalimani hapo sokoni
 
Kule kenya wameshakiamsha, serikali itathmini athari za uvamizi wa wachina kwenye biashara za wananchi.
 
Wangejenga viwanda ningewaona wa maana sana .kuliko wazalishe bidhaa kwao
 
Back
Top Bottom