Soko Ubungo kuiua Kariakoo

Soko Ubungo kuiua Kariakoo

Hiyo si sawa maana wataua kabisa viwanda vya ndani.

Wao walipaswa waje kujenga viwanda ili wananchi wapate ajira, na sio kuleta ready made items

Sent from my M2006C3LG using JamiiForums mobile app
Mchina anachotaka ni repatriation of foreign earned profits back to their firm's home country China
 
Hii nchi uko inakokwenda inatengeneza vita vya wenyewe kwa wenyewe maana gap la walionacho na wasio nacho linazidi kuongezeka kwa kasi sana.

Mwendazake alijaribu kulipunguza lakini huyu Hangaya kaja na yake. Anyway time will tell.
alipunguza gap kwa kushusha walio juu badala ya kutupandisha tulio chini
 
Kwamba wafanyabiashara wa nchi ulizozitaja wao China hawapafahamu??
Kwamba wafanyabishara wote wa nchi jirani wanaenda China, India, Dubai na kwingineko kuagiza bidhaa?
Ninao ushahidi wafanyabishara kutoka nchi jirani kuchukua bidhaa Kariakoo. Na sio hivyo tu, wanaoagiza nje ya nchi wanatumia makampuni ya kibongo kina Silent Ocean, Tosh, GNM, Mapembelo na wengine.
Wachina wana shipping lines zao kubwa duniani ambazo husaidia makampuni yao ya usafirishaji, hapa nchini nimeona makampuni yao ya clearing & forwarding na logistics yanaongezeka. Hapo Mchina aende COSCO Shipping afunge mamia ya makontena aje ashindane na kina Silent Ocean wanaovizia meli za transit sijui za Wamisri mara South Africa?

Tukiendelea hivi hata maandazi watatuuzia. Hao sio wa kuendekeza, huwezi kuwa na nchi uchumi wake umeshikwa na wageni. Tuna Waarabu na Wahindi wamepanga zao NHC wanaendesha viwanda sometimes bila kufuata taratibu, leo tunakaribisha Wachina. Ukitaka kujua hawa ni nguo ya kuazima pata changamoto za kiuchumi na kiusalama uone Mhindi gani atabaki bongo wakati ana offshore account Canada. Vita ya Uganda Wahindi na Waarabu wangapi walishiriki?

Huu sio ubaguzi wala na nchi serious zina sera zake sekta mbalimbali. Marekani sio wajinga kuzuia baadhi ya services za Huawei na ZTE za China au Kaspersky ya Urusi. Wala China sio wajinga kuzuia baadhi ya services za Marekani, wala India sio wajinga kuzingatia 'Make in India' policy.
 
alipunguza gap kwa kushusha walio juu badala ya kutupandisha tulio chini
Ni kweli, lakini kuwapandisha walio chini inahitaji muda mrefu kidogo. angekaa miaka mingine mitano angewapandisha walio chini pia, ndio maana alikuja na vision ya viwanda ili kutengeneza ajira kwa vijana.
 
Serikali na Wananchi na wafanyabiashara wote wanaona fahali kununua bidhaa na huduma nje-hapo hapo bado unaambiwa zitatengenezwa ajira na vipato vya watu vitaboreshwa.

Labda Viongozi wetu wanajua vizuri kuliko sisi,but hii ni zaidi ya pwagu na pwaguzi
 
Ni kweli, lakini kuwapandisha walio chini inahitaji muda mrefu kidogo. angekaa miaka mingine mitano angewapandisha walio chini pia, ndio maana alikuja na vision ya viwanda ili kutengeneza ajira kwa vijana.
Ukipata nafasi ya Rais wa Nchi unahitaji mwaka mmoja tu wa kufanya mabadiliko.Tengeneza mifumo ya kiutawala na iwekee sheria hiyo mifumo isitenguliwe kirahisi-huwezo kuongoza kwa kutumia utashi wako tu ukafanikiwa siku usipokuwepo kila kitu kitalala tena.
 
Wageni walitakiwa kufungua viwanda Tanzania, na sio kufanya Tanzania sehemu ya kuleta mizigo yao.

Ubungo panajengwa soko la jumla la Wachina. Hili soko litakuwa lauza bidhaa za kutoka China kwa bei ya jumla, maana yake watashindana na maduka ya kawaida.

Je, serikali imewafikiria Watanzania na yatayotokea huko mbeleni?

Sent from my M2006C3LG using JamiiForums mobile app
Acha waje ili akili zisogee bila hivyo tuta endelea kuwa wajinga hivi hivi.

Tumeachiwa nchi tuzi endeleze tumeshindwa unategemea nini sasa kutoka kwetu ?
 
Mchina aende COSCO Shipping afunge mamia ya makontena aje ashindane na kina Silent Ocean wanaovizia meli za transit sijui za Wamisri mara South Africa?
Kama naziona vile Chinese Int'l shipping companies COSCO, CIMC, HANJIN, YANG MING zikila mashavu wakiifanya Ubungo soko kuu la bidhaa za China

Na sijajua suala la bandari ya Bagamoyo limefikia wapi kati ya Tz na huyu Mchina?

Hawa watu wapo kimkakati sana aisee.

Na wakifanikiwa kula mkataba wa kujenga ile bandari hizo container shipping firms zao ndio zitatamba pale
 
Hii nchi uko inakokwenda inatengeneza vita vya wenyewe kwa wenyewe maana gap la walionacho na wasio nacho linazidi kuongezeka kwa kasi sana.

Mwendazake alijaribu kulipunguza lakini huyu Hangaya kaja na yake. Anyway time will tell.
ANGALIZO: Mimi sio mmoja wa wasio nacho, ni wa walionacho, ila ninawaza tu kwa kuangalia jicho la tatu.
Kuna bomu litakuja kulipuka mbeleni tuwe wapole tu, muda ni mwalimu. Gap la walionacho na wasionacho ni kubwa sana, hatari sana
 
Jamaa wanatuletea Kama Ile CHINA SQUARE ya Nairobi.
Raia wa kawaida wanaletewa bidha za China ambazo tunauziwa kariakoo kwa Bei ya juu wao watauzia wanunuaji kwa Bei ya chini. Hi ni habari mbaya kwa wafanyabuashara wa kariakoo na ni habari njema kwa consumers.
 
Wageni walitakiwa kufungua viwanda Tanzania, na sio kufanya Tanzania sehemu ya kuleta mizigo yao.

Ubungo panajengwa soko la jumla la Wachina. Hili soko litakuwa lauza bidhaa za kutoka China kwa bei ya jumla, maana yake watashindana na maduka ya kawaida.

Je, serikali imewafikiria Watanzania na yatayotokea huko mbeleni?

Sent from my M2006C3LG using JamiiForums mobile app
Inawezekana vyote vikafanyika kwa pamoja, kuna uwekezaji wa viwanda 200 eneo la kwala Pwani...wawekezaji ni hao hao wachina.

Watu hawawezi kusubiri mjenge viwanda mahitaji hayanasubira...

Na watz tunatabia ya kulalamika kila kitu,Sio watu wamaamuzi,hii tabia chafu ya kutafuta visingizio ndio maana tuko hapa tulipo

Sent from my SM-A035F using JamiiForums mobile app
 
Wageni walitakiwa kufungua viwanda Tanzania, na sio kufanya Tanzania sehemu ya kuleta mizigo yao.

Ubungo panajengwa soko la jumla la Wachina. Hili soko litakuwa lauza bidhaa za kutoka China kwa bei ya jumla, maana yake watashindana na maduka ya kawaida.

Je, serikali imewafikiria Watanzania na yatayotokea huko mbeleni?

Sent from my M2006C3LG using JamiiForums mobile app
Serikali iko mikononi mwa mafisadi tutegemee maumivu zaidi
 
Inawezekana vyote vikafanyika kwa pamoja, kuna uwekezaji wa viwanda 200 eneo la kwala Pwani...wawekezaji ni hao hao wachina.

Watu hawawezi kusubiri mjenge viwanda mahitaji hayanasubira...

Na watz tunatabia ya kulalamika kila kitu,Sio watu wamaamuzi,hii tabia chafu ya kutafuta visingizio ndio maana tuko hapa tulipo

Sent from my SM-A035F using JamiiForums mobile app
Ni viwanda vya consumer goods au capital goods?

Tunahitaji viwanda vya capital goods hizo consumer goods hata wasipowekeza sio mbaya sana
 
Wageni walitakiwa kufungua viwanda Tanzania, na sio kufanya Tanzania sehemu ya kuleta mizigo yao.

Ubungo panajengwa soko la jumla la Wachina. Hili soko litakuwa lauza bidhaa za kutoka China kwa bei ya jumla, maana yake watashindana na maduka ya kawaida.

Je, serikali imewafikiria Watanzania na yatayotokea huko mbeleni?

Sent from my M2006C3LG using JamiiForums mobile app
Serikali ikiua Kariakoo itakuwa kosa kubwa la kihistoria la kiuchumi kuwahi kufanywa Tanzania!
 
Back
Top Bottom