sky soldier
JF-Expert Member
- Mar 30, 2020
- 5,408
- 19,033
Nasikitika sana kuona hakuna udhibiti wa bidhaa feki hasa kwenye bidhaa za mwilini, bidhaa halisi na bora zinapotezea sokoni badala yake bidhaa feki zimetawala soko la nchi.
Miaka nenda rudi haya ndio mafuta nayoyapenda kujipakaa mwilini sambamba na sabuni ya kuogea ya Imperial.
Kuingiliwa kwa soko la mafuta haya kulianza kwa kubahatisha kuyakuta original maduka ya mtaani lakini hali ya sasa imekuwa mbaya sana, ni ngumu sana kuyakuta original mtaani.
Mwezi uliopita nilinunua maduka manne tofauti lakini yote nilitupa, yani kuanzia touch yake hadi harufu unaona kabisa ni tofauti.
Nikafikiria wapi naweza pata original nikakumbuka kwamba pharmacy nyingi huwa ni wasambazaji wa haya mafuta, nikaenda kwenye pharmacy kubwa za mjini nikanunua yale madogo kwa elf 3 kasoro, nilipofika nyumbani nikajiridhisha ni yenyewe original kwa kuyanusa sehem yenye hewa safi na kuyapima touch, nikarudi kununua yale makubwa.
Kwa hali ya sasa mitaani napata mashaka sana huenda hata sabuni za kuogea zikawa za mchongo