Soko la ajira kwa waliosoma nje

Soko la ajira kwa waliosoma nje

Joined
Mar 24, 2014
Posts
34
Reaction score
23
Habari wanajamii,

Mimi nimesoma shahada yangu nje ya nchi. Wakati nipo nasoma, watu wengi walikuwa wananiambia "aaah we ukija ajira fasta, vyeti vya mbele vinauza". Nimerudi hamna cha mauzo wala nini.

Kwa mnaosoma nje, usiweke high expections kuhusu ajira mkirudi Bongo, tena afadhal waliosoma huku wanajua pa kuanzia, ajira Bongo ni ngumu,,unless unajulikana. Kila la kheri kwa tunaotafuta kazi na wasomi wa nje masomo mema.

Nawasilisha.
 
The same to me.. Hadi nimeamua kujikita kwene biashara zangu
 
Jaribu kuelewa nilichoandika,,sio ugomvi ni ushaur tu nilikuwa natoa kwa wanaosoma nje. Kusoma nje kusoma ndan kote ni kusoma,usikurupuke kucomment boss

inategemea na huko nje umesomea chuo gan,kuna baadhi ya vyuo vya india na malaysia ambavyo havina ubora kivile,so hata waajiri wengi huwa wanavipotezea
 
inategemea na huko nje umesomea chuo gan,kuna baadhi ya vyuo vya india na malaysia ambavyo havina ubora kivile,so hata waajiri wengi huwa wanavipotezea

Sijasoma india wala nchi yoyote ya asia,thanx tho,nimejua hilo ss na waliopo malaysia n india watakuwa wamejua wajipangaje
 
Sahv ngoma droo,nna rafiki yangu kasoma russia na mwingine kasoma india,wote tupo nao mtaani mmoja ameamua kufungua banda la kuprint tshirt kariakoo,mwingine ana mpango wa kuolewa,yan mjomba sahivi ni techinical know who na sio technical know how,kama huna memo hata uwe umesoma mbinguni utaishia kusaga lami,hii ndo Tanzania ila nakupongeza pia kwa kuwapa watu ushauri manake wapo bado wenye kasumba kwamba wakisoma nje ajira mteremko
 
kuna vyou huko nje bora ni bora ungeabakiaga veta tuu....ila waliosoma Havard, St Georgia, aaaaaaaaaah wanapeta mbna na hv lugha imechangamka, sasa wale mliosoma Help college malaysia mkija muanze na veta kidg...:A S embarassed:
 
Unaweza ukasoma nje lakini chuo chako ni design ya sekomu au vile vya uchochoroni kariakoo. Kusoma nje sio kigezo cha kupata kazi.
 
Umesomea nini? Unatafuta kazi gani?

Sio unaenda kutuchukulia degree ya "American Civil War History" huko na kuongezea masters ya "Art History in the Antebellum South" halafu unataka kuwa Senior Geologist Barrick Gold just because "umesoma nje".

Kabla ya kurudi ulitakiwa kujua soko la ajira likoje. Na kujipanga accordingly.
 
Pole sana kijana atleast umesafisha macho finance mbele wakat bongo watu nyomi na hizo coz cha msingi coz za maana ndo ajira sio kisa mbele
 
Umesomea nini? Unatafuta kazi gani?

Sio unaenda kutuchukulia degree ya "American Civil War History" huko na kuongezea masters ya "Art History in the Antebellum South" halafu unataka kuwa Senior Geologist Barrick Gold just because "umesoma nje".

Kabla ya kurudi ulitakiwa kujua soko la ajira likoje. Na kujipanga accordingly.

Hahahaaa umenifurahisha Kiranga,American civl war history af unataka kazi barrick. Ni kwel kuna umuhim wa kuangalia unachosoma,bado ndugu zetu wanaenda nje hata wengine weng humu wanataman kwenda nje..mi nasisitiza tu usijiwekee expecttions kubwa,na unaenda kusoma wap nin ni muhim,,
 
Inabidi tufikiri upya kuhusu ajira na kusoma kwetu, wengi wanahitimu shahada, stashahada,vyeti na kazi zinazoanzishwa ni chache sana.
Tuanzishe kazi kama twaweza

Dogo aliyeuza Whatsapp kwa Facebook kwa dola bilioni (bilioni, si milioni, dola za Marekani, si shilingi) 19, alikuja Marekani kama immigrant na familia yake kutoka Ukraine.

Baba yake akafariki akabaki na mama, kahangaika high school, kahangaika college hata hakumaliza kaona inampotezea muda.

Akaamua kununua vitabu kujifunza computer programming mwenyewe.

Kawa mzuri, akaajiriwa Yahoo. Akajenga network, kafanya kazi na watu, akaona kuajiriwa uduanzi.

Akatafuta a challenging project.

Akaona kila network ya simu inazingua watu kwa kuwachaji kutuma text message, platforms zenyewe mbovu haziko web friendly, halafu kila mtu anakufungia kwenye ecosystem yake ukituma nje anazidisha charge.

Akasema nitaondoa ujinga huu na kubadilisha jinsi dunia nzima inavyotuma text, nitaongeza multimedia friendliness na kufanya a more web like platform. Bila kuchaji watu hela.

Kweli, akanzisha Wahatsapp na wenzake.

Hana degree wala nini.

Imemtoa, juzi tunaambiwa Facebook inainunua Whatsapp kwa dola bilioni 19, halafu Mark Zuckerberg mhuni yule anakwambia "that is cheap".

Sie tumebaki too conventional, hata kufikiri in an unorthodox way tabu. Mtu anafukuza degree, aajiriwe, ajenge nyumba na kununua gari.

Well maybe that's your thing. Lakini ukiambiwa ajira hamna usishangae.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom