Soda ni Sumu; Je, TFDA wanafanya nini?

Soda ni Sumu; Je, TFDA wanafanya nini?

Kuna vitu vingine mtu unajiongeza mwenyewe. Siku hizi karibia kila kitu ni sumu na inaleta effect baadae. Assume tuchukulie sirias kila kitu.

Mfano mimi nina mwaka sasa toka nimeacha kunywa soda aina yoyote ile. Ila sasa napiga kitimoto kama sina akili. Yale mafuta yake vip.? Huyu kaacha sigara lakini pombe anakunywa.

Ndio maisha yetu haya.
Hahahahahahahahh
 
Nilikuwa nasikiliza BBC, kule Mexico Coca-Cola inatumika kwa kiwango kikubwa sana kuanzia watoto hadi wakubwa yaani mtu akisikia kiu ni soda tu, sasa kuna mlipuko mkubwa wa vitambi na uzito uliopitiliza, ambapo huchangia idadi kubwa ya watu kuwa na magonjwa ya pressure na kisukari
 
soda ni sumu inayoua taratibu sawa
kwani nani anataka kufa haraka ?

wanaotaka kufa haraka watakunywa sumu ya panya ila sisi ambao hatutaki kufa haraka tutakunywa soda
ww jamaa weka mbali na watoto!!!
 
Ama punguza kabisa unywaji,
Sijaskia mgonjwa akishauriwa kunywa soda kwa tatizo lake ila nimeskia akishauriwa kiacha kabisa soda,
Soda ni hatari kwa afya zaidi hata ya pombe
Mgonjwa sukar ikishuka kama hakuna ulazima wa drip huwa anashauriwa kupata at least kinywaji cha soda, inasaidia
 
Habari zenu ndugu zangu

Niende moja kwa moja kwenye dukuduku langu... ni kuhusu kinywaji cha (aina ya) soda ambacho wataalamu wengi wa afya (kama sio wote) wamekifafanua sana kwamba ni hatari kwa afya na ni sumu inayoua polepole.

Sasa cha ajabu ni kwamba hapa kwetu (nchini) kinywaji hiki kimekuwa kikitumiwa (kuuzwa na kunywewa) bila hata ya tahadhari wala miongozo yoyote.

Cha ajabu zaidi na kushangaza kama sio kusikitisha ni pale ambapo Mkuu wa kitengo kinachohusika na maswala hayo (ya vyakula na madawa) yaani TFDA alipoulizwa kuhusu jambo hilo na akatoa majibu mepesi na hoja tepetepe kabisa.
>>>alijibu soda sio kinywaji hatari kwakuwa kinatumiwa na watu wengi duniani.

Wananchi huwa tunapokea maelekezo kwa wataalam kutoka mamlaka husika Sasa je kwa hali hii tutategemea tuna mamlaka imara ya kutulinda wananchi kweli dhidi ya afya zetu?, mana hiyo ni soda tu je na vingine (ambavyo huenda tunatumia na wao wapo kimya)

Nimeshindwa kuweka link hapo lakini nimesoma kwenye Muungwana anayeweza anisaidie tafadhali
Wewe utakuwa m7to
 
Hakuna ntu inayonganganizwa kunya soda.ndo maana mimi nakunya juisi ya kutengeneza mm yenyewe sinyi soda kwa sabab ako na sumu na.vile vile kwa tank ya kuchanganyia.makemikal ili soda apatikane hata mende panya au mjusi akitumbukia huwa hawatoi anayeyuyikia humohumo ndo maana waweza.kuta.soda mingine na ladha kama chai
 
Kuna mambo mengine sio mpaka serikali ase, wewe mwananchi wa kawaida unatakiwa kujielimisha na kuchukua hatua
Sawa ila kujielimisha si kunataka muelimishaji, au utaoteshwa kama manabii.
Halafu kuna watu ambao hawaamini kitu mpaka mamlaka husika za serikali zitoe tamko; vipi sasa pale mamlaka zinapokuwa na matamko yenye udhaifu au kutokuwa na matamko kabisa?
Mfano mdogo tu zile neti za msaada kutoka Marekani wataalam walipima wakagundua zina madhara kwa afya lakini wakawa wakisema wanapuuzwa kwakuwa watu wanataka tamko litoke kwa mamlaka husika za serikali
 
Kila kitu kwa dunia ya sasa kiko contaminated na sumu kuanzia hewa tunayovuta ,maji tunayijunywa,vyakula tunavyokula sijui usalama wetu uko wapi.
Hata hizi simu zetu za kupangusa ni sumu.baada ya miaka 18 sizani kama kuna mwana jf atakua salama na macho yake
 
Nimeshindwa kuweka link hapo lakini nimesoma kwenye Muungwana anayeweza anisaidie tafadhali


Anayeweza akusaidie link ya nini, TFDA wakisema soda sio sumu au wataalam wanaoonyesha kwamba soda ni sumu?

Katika masuala ya uthibitisho na migongano ya hoja yule anaesema kitu chanya ndio anadaiwa proof. Ukisema soda ni sumu wewe ndio thibitisha. Mimi nikisema Mungu hayupo siwezi kudaiwa uthibitisho kwa sababu hayupo, nitam prove vipi?

Sasa wewe tueleze umesikia wapi kwamba soda ni sumu, na ni sumu gani, na inafanyaje kazi mwilini, biochemically.
 
Sometimes tuache lalamika ovyo tufanye kazi!... sasa unaifungulia soda thread ipigwe marufuku je sigara na pombe hujaona madhara yake ya haraka zaidi!?..Kila kitu kina madhara hata maji ELIMU ELIMU!!..
 
wakuu msipuuzie,ukishapatwa na kisukari ndio mtamkumbuka huyu mtoa mada...
Mada zingine ni pumba sasa anataka TFDA watoe tamko kuzuia utengenezaji wa soda?.. Kuna vitu vingine ni kujiongeza tu kama msomi.
Hilo tamko la TFDA likitoka soda ni sumu bado mtu wa porini atakuona unampigia kelele asipate tam tam!! thats y wanabaki toa ushauri usinywe nyingi tu!.
 
Mkuu naomba maana ya sumu ikiambatana na mifano ya kipi ni sumu na kipi sio sumu

Based na hiyo maana utakayoitoa,naomba utuletee utafiti unaoonesha kuwa soda ni sumu
Neno sumu ni dhana pana kuelezea hapa sitaweza na kuhusu tafiti juu ya soda kuwa sumu sijafanya utafiti wa kitaalam huo unaoutaka kwakuwa mimi sio mtaalam lakini zipo tafiti nyingi ila nimeshindwa kuweka link hapa
 
Back
Top Bottom