Mkuu, Asante kwa video Ulioipost. Kuna mambo ambayo nimeya note nataka kuyazungumzia:
- Sukari kwenye Vitu (coca, maziwa etc)
- Na suala la Junk foods ambalo limezungumziwa na Author wa fast food and mtoto mwisho wa clip.
- Na genetically Modified products.
Sukari Kwenye Vitu - Coca Cola, maziwa etc
Watu wamekuwa wapotoshaji sana katika suala zima la sukari. Nnavojua mimi sukari inatoka kwenye miwa, na hii inatosha kusema kuwa sukari ni natural substance, sio kwamba ni artificial, although ni muwa ambao umekuwa processed mpaka ikapatikana sukari. Sukari huwa inaleta ladha ya utamu.Na sukari ni muhimu kwa mwili wa binaadamu.
Sukari ni Carbohydrate. Unapokunywa mfano soda, ile sukari inabadilishwa na kugeuzwa kuwa energy au inahifadhiwa as fat for later use. Pale unapokaa na njaa mda mrefu sasa hizi fats zinafanya kazi yake. So ikiwa chupa moja ya coca ina sukari sawa na vijiko 30 vya chai, kwanini unywe yote ikiwa kwa siku upate angalau vijiko 9 vya sukari? Over consumption ndio tatizo la watu. Sukari hii iliokuwa processed inakupa sugar rush, craving for more. But as long as you balance it, haiwi tatizo.
Digestion System inafanya kazi yake. Mwili wa binaadamu ni kitu chengine kabisa, unafanya kazi yake vizuri ikiwa kila kitu kitakuwa balanced tu.
Too much of something is Harmful. Hata asali, chukua chupa halafu ibwiye yote apo apo kisha tuletee mrejesho...
Junk Foods/Fast Foods
Hapa ndio nnapowashangaa watu.
Burger ingredients zake ni nini?
Mkate, nyama, na some vegetables. Sasa vipi are we posioned?
Kuna time katika katika ya video kuna notice inazungumzia kuwa ndio maana dua zetu hazijibiwi.
Mkuu, mimi ni muislam. Lakini nikufundishe kitu, Mungu hamhukumu mtu kwa kitu asichokijua. Kwa mfano, sisi kila siku tunanunua nyama buchani tukiamini kuwa ni halali, lakini hatuwezi kuthibitisha sisi wanunuaji kwa sababu hatuchinji wenyewe, tunachinjiwa machinjioni na pia hatuendi uko machinjioni. Kwaio kama unanunua nyama buchani na umeambiwa halal wakati kumbe sio na wewe hujui, basi dhambi atazibeba muuzaji sio wewe mnunuaji. Dhambi za imamu hazibatilishi sala za maamuma. Ikiwa umekwenda supermarket, umekuta nyama imeandikwa halal na nyengine haijaandikwa basi na ukachagua ilokuwa haijaandikwa hapo utakuwa umekosea kweli. Ikiwa dua zako hazijibiwi try to assess yourself again.
Genetically modified food products
Hii ndio kitu pekee naweza kusema kuwa kweli inaweza kuwa sumu. Kama mfato aloutolea mtoto fish tomato, kufikiria tu samaki apo apo ana ladha ya tungule na usamaki basi unaanza kuona kichefu chefu.
Hapa kuna ile mtu ale ajiskie ashibe, lakini nothing to build your body.