Smart Unlimited 4G spidi ikoje?

Smart Unlimited 4G spidi ikoje?

Kang

JF-Expert Member
Joined
Jun 24, 2008
Posts
5,694
Reaction score
2,588
Smile unlimited naona imeniangusha sana mwezi uliopita ile ya 70,000 kuna wakati hata page kufunguka ilikuwa shida.

Nataja nijaribu Smart, ya 70,000 kwa mwezi kuna mtu anaitumia sasa hivi? na ile MiFi yao ningependa kujua spidi unayopata na kama unaweza piga speedtest.net tuone.
 
Yanaweza kuwa yale yale haya makampuni hayatabili jana nime chat na hao jamaa wa Smile maana nilivutiwa na bundle zao wakanambia hizo bundle ni Unlimited kwa speed ulolipia i.e haupimiwi GB/TB za kutumia!
Kuna mtu nchi ya jirani ambako pia kuna Smile alinambia kuwa hizo bundle wanazi misuse nchi kwao unakuta mtu anapewa mpaka 200GB zikiisha imekula kwake!

Router za Smart ni za 4G hivo sina wasi wasi na uwezo wake katika perfomance ila pia Smart ni mtandao pekee ulokua ukitoa Unlimited ya 3G kwa watu waishio nje ya DSM kwa 20,000/= kwa mwezi bila kubaniana speed wala hizo GB kadiri ya mchangiaji mmoja wapo wa jukwaa hili!

Kuna rafiki anaishi Upanga hapo amewai kunitumia speedtest ya smart ilikua inacheza 21Mbps na aki download kwa IDM inapanda hata kufikia 4MB/sec

Mimi mwenyewe nilitumia kipindi cha nyuma kidogo hiyo smart ila speed haikuwa pleasing kwangu kabisa

Pitia Thread hii hapa nilianzisha mimi : Angalie Smart 4G LTE ilivo Slow utafikiri 3G

Kuna mdau alitoa speed test yake kwa kutumia Simu japokuwa which I believe itakua hiyo hiyo kwa router

Kuhusu hizo Bundle za Unlimited labda usubiri kama kuna mtumiaji akupe experience ila vinginevyo waweza kupata picha ya perfomance incase watakua hawabani kitu chochote ila pia ungewapigia wakuhakikishie ili kitu kikienda mlama unawapandia hewani kuwauliza vipi inakuwa kinyume na walivokueleza

Screenshot_2.png
 
Nimenunua Smart Mifi sasa hivi, spidi sio kubwa lakini bora kuliko Smile ilivyokuwa. Nipo ndani ya jengo mjini ofisini inaweza ikawa inapunguza signal ntajaribu sehemu zengine.
Test ya kwanza server za Lodon ya pili server za Bongo.

smartMifi.JPG
 
hivi unamaanisha Smile hata page zilikua hazifunguki hata mwanzo wa Bundle?

If you do not mind kabla ya bundle kuisha mda wake tupe Update kama ni Unlimited through out
 
hivi unamaanisha Smile hata page zilikua hazifunguki hata mwanzo wa Bundle?

If you do not mind kabla ya bundle kuisha mda wake tupe Update kama ni Unlimited through out

Smile ni unlimited downloading, nimetumia miezi miwili ya kwanza kulikuwa hakuna issue nimeshusha zaidi ya 300 GB nadhani.
Mwezi wa tatu ndo matatizo yameeanza yaani connection imekuwa poor sana haikonnect au ikikonect page inashuka nusu nusu picha haziload etc. Hii ilikuwa ni ile ya 70,000 ambayo speed ni up to 2Mbps.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom