sijui nini
JF-Expert Member
- Sep 29, 2010
- 2,553
- 1,285
MGOMBEA urais kwa tiketi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dk. Willibrod Slaa, amewataka Watanzania kupuuza ujumbe mfupi wa maneno (sms) unaosambazwa kupitia simu mikononi kuwa ni ujanja wa Chama cha Mapinduzi (CCM), baada ya kuona kimekabwa koo kila kona. Akihutubia mamia ya wananchi katika mkutano wake wa kampeni uliofanyika katika kijiji cha Kalinzi, Dk. Slaa alisema CCM imekabwa koo kila idara hivyo imelazimika kutuma ujumbe kuwahadaa Watanzania ili waamini uongo unaosambazwa.
Nimesikia wanasambaza ujumbe kwenye simu za mikononi wanasema mimi ni mropokaji nawaambia Watanzania wenzagu, wapuuzeni CCM hii ni dalili tosha kwamba tumewakamata kila kona wanahaha kujinasua hizi ni porojo za CCM; zinaonyesha wazi sasa wameanza kutapatapa kama mtu anayetaka kufa, imeonyesha sasa ni kama inapumulia mashine, alisema Dk. Slaa.
Alisema kutokana na hali hiyo, CCM imekuwa bingwa wa kumzushia mambo mbalimbali ambayo hayana ukweli wowote mbele ya jamii.
Akizungumzia suala la yeye kuambiwa anataka kwenda Ikulu kwa njia ya kumwaga damu, Dk. Slaa alisema amekuwa mbunge wa jimbo la Karatu kwa kipindi cha miaka 15 bila kumwaga damu ni kitu ambacho hakiwezekani hata siku moja.
Nimekuwa mbunge wa Karatu kwa kipindi cha miaka 15, sikumwaga damu sasa hiyo damu itatoka wapi? Kwa vile tumefanikiwa kuwabana wanahangaika kujinasua, alisema Dk. Slaa.
Alisema pamoja na yeye kuitwa mropokaji, anakubali kwa vile uropokaji huo umezaa matunda kipindi chote alichokuwa bungeni.
Wananiita mropokaji, mimi nasema sawa nimeropoka na matunda yangu yameonekana, niliwataja watu kama Basil Mramba, Gray Mgonja na Daniel Yona mbona wamefikishwa mahakamani? Kama nisingefanya hivi wangeendelea kutafuna fedha za walipa kodi wa nchi hii .nawaambieni jamani hata wakati ule nilimtaja Rais Jakaya Kikwete mbona hawajanikamata kama ulikuwa uongo? alihoji Dk. Slaa na kushangiliwa na maelfu ya wananchi.
Nimesikia wanasambaza ujumbe kwenye simu za mikononi wanasema mimi ni mropokaji nawaambia Watanzania wenzagu, wapuuzeni CCM hii ni dalili tosha kwamba tumewakamata kila kona wanahaha kujinasua hizi ni porojo za CCM; zinaonyesha wazi sasa wameanza kutapatapa kama mtu anayetaka kufa, imeonyesha sasa ni kama inapumulia mashine, alisema Dk. Slaa.
Alisema kutokana na hali hiyo, CCM imekuwa bingwa wa kumzushia mambo mbalimbali ambayo hayana ukweli wowote mbele ya jamii.
Akizungumzia suala la yeye kuambiwa anataka kwenda Ikulu kwa njia ya kumwaga damu, Dk. Slaa alisema amekuwa mbunge wa jimbo la Karatu kwa kipindi cha miaka 15 bila kumwaga damu ni kitu ambacho hakiwezekani hata siku moja.
Nimekuwa mbunge wa Karatu kwa kipindi cha miaka 15, sikumwaga damu sasa hiyo damu itatoka wapi? Kwa vile tumefanikiwa kuwabana wanahangaika kujinasua, alisema Dk. Slaa.
Alisema pamoja na yeye kuitwa mropokaji, anakubali kwa vile uropokaji huo umezaa matunda kipindi chote alichokuwa bungeni.
Wananiita mropokaji, mimi nasema sawa nimeropoka na matunda yangu yameonekana, niliwataja watu kama Basil Mramba, Gray Mgonja na Daniel Yona mbona wamefikishwa mahakamani? Kama nisingefanya hivi wangeendelea kutafuna fedha za walipa kodi wa nchi hii .nawaambieni jamani hata wakati ule nilimtaja Rais Jakaya Kikwete mbona hawajanikamata kama ulikuwa uongo? alihoji Dk. Slaa na kushangiliwa na maelfu ya wananchi.