Slaa amgomea JK

Slaa amgomea JK

nasri, wewe huijui tanzania vizuri! Hivi ni sehemu gani hamna raslimali kama unavyosema? Kanda ya kati kuna dhahabu, uranium, chuma e.t.c. Kusini kuna mafuta, gesi, dhahabu, n.k. Kaskazini hivyohivyo nchi yetu hamna kanda maskini kama unavyofikilia maskini ni mawazo yetu tuu

ukosawa, tatizo letu hatyupendi kufikiri. Hakuna sehemu masikini tz. Uvivu ktk kufikiri na kutenda juu ya raslimali zetu bahari,maziwa, mito,ardhi yenye rutuba namenginer mengi vinatosha kutoaumasikini.jambo jingine muhimu ni uadilifu kwa tulio wapa mamlaka.
 
"Now or Never".
Kutokana na mapitio ya maoni yafauti taliyotangulia, ninachokiona hapa ni kuwa bado CCM wameganda katika sera za Chama kushika Hatamu bila ya kujali kuwa kuanzia 1992 CCM haina mamlaka ya Tanzania yote.

Kama watu kadhaa humu wanavyokuwa wanadhihaki lakini ndio ukweli, CCM ni janga la Taifa.

Ndugu zangu, hii ni fursa ya mwisho kwetu kama Watanzania na wala sio kama wanasisiemu, kuhakikisha tunaandika yetu inayotokana na maoni ya wengi. Vyenginevyo, hiyo kejeli inayosemwa kuwa CCM ni janga kwa taifa itakuja kuwa kweli pale tutakapowaachia kufanya watakavyo. TusipotahadhCCari patakuja kuchimika hapa. Miaka 50 ya kuburuzwa inatosha.

MTU HAWEZI KUKUPANDIA MGONGONI IKIWA HUKUINAMA - Tusiwaruhusu zaidi CCM kutupandia migongoni.

Hatamu hakuna tena, mjadala unarudi kwa wananchi, ieleweke hii ni katiba mpya. Hakuna mwenye haki ya kuhodhi mjadala, hata wabunge wa CCM wamekiona cha moto. Na bado, inawezekana ukarudi bungeni kwa marekebisho. Mwisho tunataka maoni ya wenye nchi (Umma) yaheshimiwe. Kwa upande mwingine tujitahidi kusoma historia iliyojificha, itatusaidia.
 
Hatamu hakuna tena, mjadala unarudi kwa wananchi, ieleweke hii ni katiba mpya. Hakuna mwenye haki ya kuhodhi mjadala, hata wabunge wa CCM wamekiona cha moto. Na bado, inawezekana ukarudi bungeni kwa marekebisho. Mwisho tunataka maoni ya wenye nchi (Umma) yaheshimiwe. Kwa upande mwingine tujitahidi kusoma historia iliyojificha, itatusaidia.
Heshima Mkuu!
Ninakubaliana na wewe na wengine wengi juu ya kile "Tunachokita", lakini kwa bahati mbaya, kilichopo ni kile "Tulichopewa". Naomba upitie thread ya Mwanakijiji ambapo inaonesha kuwa Watanzania tumepitishwa katika uchochoro usio na pa kutokea. Bado naamini kuwa tunaweza kubadilisha hili, sio kwa kushiriki japo kwa wingi katika kutoa maoni kwani maoni yetu yanaweza kuwekwa upande na kutumikia matakwa ya CCM, bali kuupinga mchakato huu hivi sasa katika Mahakama ya Katiba kabla haijafikia hiyo hatua ya katiba kupitishwa.
 
Heshima Mkuu!
Ninakubaliana na wewe na wengine wengi juu ya kile "Tunachokita", lakini kwa bahati mbaya, kilichopo ni kile "Tulichopewa". Naomba upitie thread ya Mwanakijiji ambapo inaonesha kuwa Watanzania tumepitishwa katika uchochoro usio na pa kutokea. Bado naamini kuwa tunaweza kubadilisha hili, sio kwa kushiriki japo kwa wingi katika kutoa maoni kwani maoni yetu yanaweza kuwekwa upande na kutumikia matakwa ya CCM, bali kuupinga mchakato huu hivi sasa katika Mahakama ya Katiba kabla haijafikia hiyo hatua ya katiba kupitishwa.

Ni sisi sote kuhamasisha watanzania umuhimu wa zoezi hili. Kila mahala tutakapokuko kuamsha mazungumzo kuhusu umuhimu wa kujiandaa kutoa maoni katika hii tume. Kwa sasa tusubiri kidogo ili tuone mwenendo wa tume kabla ya kwenda mahakamani. Kwa sababu tunajadili katiba ya muungano na si ya tanganyika, wamejiweka wenyewe katika mtego.
 
Hansen, fanya utafiti kwanza kuhusu miundo na uendashaji wa serikali za majimbo.nimekuelewa kuwa una kero kubwa kuhusu ukanda fulani kuwa tajiri zaidi kirasilimali na kwamba kipato kitokanacho na rasilimali hizo kitaishia kuendeleza ukanda huo.Lakini,kama moja ya provisions za katiba itatamka kwamba (kwa mfano) asilimia 50 ya pato la jimbo itakwenda federal govt,na iliyobaki state/provincial govt,shida iko wapi?pato litakalo kwenda federal govt litakuwa linaelekezwa kwenye majimbo yanayohitaji support kujiendeleza,kama jimbo lako kwa mfano!kwa karne zote za serikali ya jamhuri mbona kanda flani bado ziko nyuma?mbona serikali za majimbo katika Marekani zimeendelea sana kwa mfumo wa state govt kama tunaohitaji?Penda usipende,hakuna mtawala yeyote mtakaeletewa ambae sio mzaliwa wa ukanda wenu ambae atakuwa na uchungu wa rasilimali zenu,matumizi yake na maendeleo mnayoyataka kama mtawala mzawa wa jimbo lenu na aliyepewa dhamana na wanajimbo lenu na hivyo kuwajibika kwenu.Lakini la msingi sana ni kwamba mtakuwa na fursa ya pekee ya kumchagua governor wa jimbo lenu kwa sifa mnazozitaka wenyewe.kwa mfano uzawa wake,vision yake kwa jimbo LAKE, mikakati yake kwa jimbo LAKE, na mengineyo mengi kwa jimbo LAKE.Lakini pia,huyu kiongozi atakuwa accountable kwa wanajimbo waliomchagua!na siyo kwa mtu fulani mmoja.Faida za kuwa na serikali za majimbo ni nyingi sana!Kama taifa,tume-centralize sana power & authority.na ndiyo maana mfumo huu unachelewesha maamuzi muhimu na ya haraka katika kanda.rasilimali za taifa letu zinapotea kwa sababu ya wanaotakiwa kuzilinda kutokuwa na uchungu nazo kwa sababu ama siyo wazawa na au wanawajibika kwa mtu fulani na sio wanajimbo au kanda!msipotoshwe na kuchoshwa na propaganda za chama kilichotufikisha kwenye umaskini tulionao.abject poverty.FIKIRIA,CHUKUA HATUA!

Pia utawala wa kimajimbo unasaidia kupata Rais mzuri wa nchi kama wanavyofanya wamarekani,ambapo wanaowania Urais wamekuwa masenetor ktk majimbo yao hivyo sheria ikitengenezwa hivy tutakuwa na reference nzuri ktk kuleta maendeleo ktk majimbo yao.

Pia serikali za majimbo zinasaidia kuepuka iwapo kiongozi aliopo madarakani si mtendaji mzuri au msimamizi mzuri wa shughuli za serikali au fedha hivyo udhaifu huo unakuwa hauenei nchi nzima.

Pia kuna masuala ya kushughulia masuala ya matatizo ya kijamii,serikali za majimbo inatatua harka zaidi kuliko ilivyo kama uendeshaji unaoendelea hivi sasa
 
Wapi? Mbona unaishia njiani?
Kwani NIGERIA HAWANA SERIKALI ZA MAJIMBO? Mbona hayo majimbo yanataka kujitenga? Mbona Jos ambako kuna mafuta wanataka uhuru?
Au unamaanisha CONGO? Au Kenya? Au Angola? Ambako Cabinda hainufaiki na mfuta yake?
Mkuu ukizungumzia majimbo, usifananishe United States na hizi nchi zetu za Africa, wenzetu wameanzisha hayo majimbo from scratch, na majimbo yalipotaka kujitenga ilibidi wauane sana!
Ni rahisi sana kusema HAYA MAMBO HAYAWEZI KUTOKDEA TANZANIA

Hizi akili huwa tunazipata wapi ngd zanguni..Mbona tunakuwa wagumu wa kufikir.
Leo hii viwanda vinatengeneza ndege ila haziachi kuzitengeneza kwa kuwa kuna nyingine zinaanguka na kuuwa watu..Suala la kutengeneza na kuanguka ni vitu viwili tofauti ila vinavyoshabiana kiamtukio na linalobaki kuwa ni changamoto kwa kila kimoja.
Tukibaki kusema tukifanya hivi mbona kule yanatokea hivi huo utakuwa ni ufinyu wa AKILI tena si kidogo.....

Ndg Kobelo nadhani unaufaham udhaifu wa mfumo tuliona sisi na ubora wa mfumo wa majimbo......

Leo hii Kenya katiba yao ni wa mfumo wa majimbo,tutazidi kutanguliwa na Wakenya kwa kila jambo kwa kuwa na vichwa vingi vibovu serikalini vinavyofikiri kidogo kama samaki kama anavyopinga KOBELLO
 
I said the same thing but in a different way.

Huwezi kusema unataka kupata katiba mpya ya jamuhuri ya muungano wa Tanzania bila kuuzungumzia muungano.

Hiyo siyo katiba ya wananchi.

Hapo mtanisamehe.
 
Mi hata sioni hiyo faida ya kuungana, kama kweli tuna jeshi kwanini kaeneo kama Zanzibar katuzingue? Si tujitenge nao tu halafu kila upande uchukue 50 zake? Maana hakuna kwenye Muungano anayefaidika, kila upande unalalamika tu... Hii ni sawa na wanandoa ambao hawaelewani wala hawana mahusiano ya kindoa lakini bado wameng'ang'ana kukaa nyumba moja. Si ajabu ipo siku mmoja atamchoma hata kisu mwenziwe! Sababu zinazotolewa kuhalalisha Muungano ni za kihuni, eti tuna-undugu wa damu, eti tumechanganyikana, n.k. Hivi huo undugu wa damu upo kati ya Tanganyika na Zanzibar tu? Hivi hakuna Wamasai wa Tz na Kenya? Hakuna Wajaluo Mara na Kenya? Hakuna Wamakonde Mtwara na Msumbiji? Hivi Tz imepakana na nchi ngapi, huko watu wetu hawajaoa na kuolewa? Sasa wote hao si ndugu zetu wa damu? Mbona hatuongelei kuungana na nchi zote zilizotuzunguka kama kweli tunaamini ktk Muungano? Sasa nakubaliana na yule Meya wa Dsm aliyesema baadhi yetu tunafikiri kwa kutumia makalio!
Bado tuna wasomi na wengine wakijiita Wataalamu wa Katiba! Shit! Sasa kama wapo hao na huku tangu Muungano uasisiwe kumekuwa na kero chungu nzima, huku fedha za walipa kodi zikiteketea kwa UFISADI wa kuzitatua kero hizo, na wengine wakijidai kuwa kuna mambo mengi yameongezwa ambayo hayakuwa ya Muungano, mbona Wanasheria wetu wasidai hazi hizo kupitia Mahakama za Kikatiba au hata za Kimataifa kuliko kuendelea kulaumu tu humu? Hivi ni nani aliyeziona hizo nakala za HATI NA MKATABA WA MUUNGANO? Watz wangapi walishaziona? Sasa iweje kutupotezea muda na rasilimali kujadili NADHARIA ambayo nina uhakika hata hao Wazanzibari wenyewe wanaisikia tu midomoni mwa watu? Si Mwanasheria wao Mkuu ndiye aliyesema hakuwahi kuziona hizo HATI? Sasa Mpemba wa kawaida anayevua samaki mwambao wa bahari ndiye anayelalamika utafikiri alikuwepo au alikuwa Mgeni rasmi wakati wa utiaji saini wa Mikataba hiyo feki?
THIS IS AMAZING. Hebu Mungu Atujalie ili ktk nafasi hii finyu tusipoteze muda kujadili upuuzi kama huu wakati Mtz wa kawaida hana uhakika wa hata mlo wa siku halafu Mwanasiasa aliyeshiba kwa fedha za EPA akimtaka ajadili Muungano!! Hivi ni kipi kilianza, KUKU (kwa maana ya Mtanzania) ama YAI (kwa maana ya Muungano wa watu wawili waliovalia suti huku wakipulizwa na upepo wa Magogoni?)
 
Kuvunjika kwa muungano kutasababishwa na kutukuuzungumzia katika hili zoezi. Ubishi mwingine wa kishabiki hausaidii. Kwanza ikumbukwe muungano haukuwa na referendum bali ulikuwa wa viongozi wa juu. Huu ni wakati muafaka kuurekebisha.

Kumbukeni
Makamu wa Pili wa Rais na Waziri Mkuu wa Tanzania, John Malecela na Katibu Mkuu wa CCM, Harace Kolimba wakajiondoa bila ya wao kutaka ili kuinusuru nchi.
Katika pendekezo la kugeuza mfumo wa Muungano wa Serikali mbili na kuundwa kwa mfumo wa Shirikisho la Serikali Tatu, CCM kwa wakati huo ilikataa mfumo huo kwa hoja dhaifu sana.
Hata hivyo, Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania lilipitisha azimio la kuundwa kwa Serikali ya Tanganyika ndani ya Jamhuri ya Muungano baada ya kundi la wabunge 55 kutoka majimbo ya Tanzania Bara kuwasilisha hoja binafsi Bungeni na kukubaliwa.
Kimsingi Bunge lilipitisha kwa kauli moja, Agosti 1993 Azimio la kutaka Serikali ya Tanzania kupelekwa muswada wa sheria kubadili Katiba ya Jamhuri ya Muungano ili kuwa na Serikali ya Tanganyika ndani ya Muungano.
 
Katiba yoyote duniani huwa na misingi mikuu. Katika nchi ya
kidemokrasia msingi mkuu wa Katiba ni ule unaoweka mamlaka
yote mikononi mwa wananchi. Misingi mingine ni:-
(a) Katiba ni lazima iwezeshe wananchi kuridhiana kitaifa
(b) Ushiriki wa wananchi ni lazima uwe wa kutosheleza ili
kuwezesha umiliki wa wananchi wa Katiba husika
(c) Katiba huwa ni ya kipekee kutokana na historia ya nchi husika
(d) Katiba yeyote hairuhusu ubaguzi wa aina yeyote miongoni
mwa raia wake
(e) Katiba lazima itoe maono ya mbele ya taifa husika
(f) Katiba ni sheria mama katika nchi ambapo hakuna sheria
inayotungwa itaruhusiwa kukinzana nayo.

Soma zaidi hapa:
http://www.policyforum-tz.org/files/MwongozowaKatibakwaRaia.pdf
 
Tume inaanza kazi lini, maana tuna mengi sana ya kuchangia. Jf ina nafasi gani katika hili.
 

KATIBU Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dk. Willibrod Slaa, ameeleza kushtushwa na kauli ya Rais Jakaya Kikwete inayolenga kuzuia wananchi kujadili kuhusu Muungano wakati wa mchakato wa marekebisho ya Katiba.
Dk. Slaa aliye katika ziara ya kichama kukagua uhai wa chama hicho ikiwa ni pamoja na kukijenga, alitoa dukuduku lake hilo jana wakati akihutubia mkutano mkubwa wa hadhara uliofanyika katika viwanja vya Shycom, mjini Shinyanga.
Katibu mkuu huyo wa CHADEMA alitoa kauli hiyo ikiwa ni siku moja tu tangu Rais Kikwete alipowaapisha wajumbe 30 wa Tume ya kukusanya maoni ya Katiba mpya inayoongozwa na mwanasheria na mwanasiasa anayeheshimika, Jaji Joseph Warioba.
Wakati akizindua tume hiyo juzi, pamoja na mambo mengine, Rais Kikwete alisema tume hiyo katika kazi yake haitahusika katika kuhoji kuhusu kuwapo ama kutokuwapo kwa muungano.
Kwa upande wake Dk. Slaa aliwataka Watanzania kuachana na maneno ya watawala na kutobweteka baada ya kuundwa kwa tume hiyo ya Jaji Warioba.
“Jamani Watanzania wenzangu wa Shinyanga, naomba tuzungumze kidogo hili la Katiba mpya, kwanza nawaomba msibweteke eti kwa sababu tume imeundwa, kuundwa tume hakuleti katiba mpya na bora. Pia tunataka Kikwete ajue kuwa Watanzania hawatengenezi katiba ya Kikwete wala ya CCM. Wanataka Katiba mpya na bora ya kwao.
“Nami namuomba ni bora akajitahidi kujiepusha na matamko ya ajabu, maana anaendelea kutupatia ajenda. Anasema suala la muungano lisijadiliwe wakati wa mchakato wa utoaji maoni. Hapa anataka kutuma ujumbe gani…” alisema Dk. Slaa na kushangiliwa.
Akiuchambua muungano, Dk. Slaa alisema ni haki ya Watanzania kwa maana ya wale wa Zanzibar na wa Bara kujadili muungano wanaoutaka kwani kufanya hivyo hakuna nia ya kuuvunja.
“Sisi CHADEMA tunasimamia nini? Tunataka Watanzania wajadili wanataka muungano wa aina gani, tunataka Zanzibar ipate haki zake kama ilivyokuwa mwaka 1964.
“Hapa hoja si muungano uwepo ama usiwepo, hoja ni aina gani ya muungano wa kisiasa Watanzania wanautaka. Tunaamini kuwa hakuna mwanasiasa mwenye akili timamu anaweza kuhubiri kuvunja muungano.
“Mwanasiasa anayezungumzia kuvunja muungano huyo ni mwendawazimu, maana muungano wa kweli wa Watanzania uko kwenye damu zao. Lakini katika suala la kiutawala wananchi waachwe waamue wanataka aina gani, hii ndiyo hoja hapa,” alisema Dk. Slaa.
Akifafanua, Dk. Slaa alisema wanazo taarifa kwamba tayari CCM kupitia katika Halmashauri Kuu yao ya Taifa wameshafikia hatua ya kuwatumia makada wao, wakiwamo viongozi wa kiserikali kama wakuu wa mikoa na wilaya katika kuhakikisha yale ambayo chama hicho tawala kinayataka, yanaingizwa katika Katiba mpya.
“Napenda kumwambia haya huku akijua kuwa, mkononi kwangu au ofisini kwetu tayari tunao uamuzi wa Halmashauri Kuu ya chama chao, ambayo imewaagiza viongozi ambao ni makada wao, kuhakikisha masuala ambayo chama hicho kinataka yanaingia katika Katiba mpya, hii ni hatari,” alisema Dk. Slaa.
Akifafanua, alisema chama hicho kitaendelea kuwa mstari wa mbele kuwaongoza Watanzania waandike Katiba mpya inayozingatia haki za msingi kama vile masuala ya ardhi, huku pia akisisitiza kuwa suala la mamlaka ya rais linapaswa kuangaliwa upya na kurekebisha.
Aliongeza kuwa, moja ya mwarobaini wa kuachana na wateule wengi wa rais ni kuwa na serikali za majimbo ambako viongozi wake sharti wachaguliwe na watu badala ya sasa wananchi kutawaliwa na mkuu wa mkoa au wilaya wasiyemjua.


[TD="bgcolor: #FFFFFF"]
Slaa amgomea JK
• Amtaka aache Watanzania waunde Katiba yao

na Mwandishi wetu, Shinyanga


[/TD]
[TD="width: 140, bgcolor: #FFFFFF"]
amka2.gif

[/TD]
"Muungano ni kama koti joto likizidi unalivua" Ni kawaida kwa binadamu wenye akili timamu kila linapotokea tatizo la kutokuelewana katika jamii au baina ya watu wawili njia pekee ya kuleta maelewano baina yao ni kukaa chini na kulizungumza tatizo lao kwa maana ya kutaka kulipatia ufumbuzi na shuluhisho la kudumu ili katika siku za baadae lisitokee tena. Kwetu sisi tuna tatizo Wazanzibari wanasema kwa uwazi kabisa kuwa kuna kasoro katika muungano wetu japo Watanganyika tuliowengi hatusemi kwa nguvu kama wenzetu wa Zanzibar lakini kasoro zipo na tunaziona.Kwa kulitambua hilo ndio maana hata serikali ya JMT imeunda idara maalum chini ya ofisi ya makamu wa rais ili kushughulikia kero za muungano. Sasa kama tunatambua kuwa zipo kero kwani zisijadiliwe na wananchi ambao ndio wenye muungano?
 
"Muungano ni kama koti joto likizidi unalivua" Ni kawaida kwa binadamu wenye akili timamu kila linapotokea tatizo la kutokuelewana katika jamii au baina ya watu wawili njia pekee ya kuleta maelewano baina yao ni kukaa chini na kulizungumza tatizo lao kwa maana ya kutaka kulipatia ufumbuzi na shuluhisho la kudumu ili katika siku za baadae lisitokee tena. Kwetu sisi tuna tatizo Wazanzibari wanasema kwa uwazi kabisa kuwa kuna kasoro katika muungano wetu japo Watanganyika tuliowengi hatusemi kwa nguvu kama wenzetu wa Zanzibar lakini kasoro zipo na tunaziona.Kwa kulitambua hilo ndio maana hata serikali ya JMT imeunda idara maalum chini ya ofisi ya makamu wa rais ili kushughulikia kero za muungano. Sasa kama tunatambua kuwa zipo kero kwani zisijadiliwe na wananchi ambao ndio wenye muungano?

Serikali ya Jamhuri ya Muungano haiwezi kushughulikia matatizo ya muungano kwa niaba ya watanganyika. Sasa ni wakati wa kushughulikia matatizo ya muungano, bila kufumba macho. Sina maana ya kuvunja muungano. Ni kama mtu ukiwa katika ndoa, halafu kukatokea hitilafu, basi pande zote mbili zinawajibika kutafuta suluhu. Kungekuwa na serikali tatu mengi yasingetokea.
 
Mwisho wa malalamiko ni kuwa na Serikali tatu,

Wananchi waamasishwe kuwepo kwa serikali ya tatu

a. Serikali ndogo ya Muungano yenye makao makuu Dar es Salaam

b. Serikali ya Tanganyika yenye makao makuu yake Dodoma

c. Serikali ya watu wa zanzibar yenye makao makuu unguja (kama sasa)
 
Mwisho wa malalamiko ni kuwa na Serikali tatu,

Wananchi waamasishwe kuwepo kwa serikali ya tatu

a. Serikali ndogo ya Muungano yenye makao makuu Dar es Salaam

b. Serikali ya Tanganyika yenye makao makuu yake Dodoma

c. Serikali ya watu wa zanzibar yenye makao makuu unguja (kama sasa)

Tena hii itatoa mwanya wa nchi nyingine kuingia katika muungano. Huu wa sasa ni kizungumkuti.
 
Back
Top Bottom