Hansen, fanya utafiti kwanza kuhusu miundo na uendashaji wa serikali za majimbo.nimekuelewa kuwa una kero kubwa kuhusu ukanda fulani kuwa tajiri zaidi kirasilimali na kwamba kipato kitokanacho na rasilimali hizo kitaishia kuendeleza ukanda huo.Lakini,kama moja ya provisions za katiba itatamka kwamba (kwa mfano) asilimia 50 ya pato la jimbo itakwenda federal govt,na iliyobaki state/provincial govt,shida iko wapi?pato litakalo kwenda federal govt litakuwa linaelekezwa kwenye majimbo yanayohitaji support kujiendeleza,kama jimbo lako kwa mfano!kwa karne zote za serikali ya jamhuri mbona kanda flani bado ziko nyuma?mbona serikali za majimbo katika Marekani zimeendelea sana kwa mfumo wa state govt kama tunaohitaji?Penda usipende,hakuna mtawala yeyote mtakaeletewa ambae sio mzaliwa wa ukanda wenu ambae atakuwa na uchungu wa rasilimali zenu,matumizi yake na maendeleo mnayoyataka kama mtawala mzawa wa jimbo lenu na aliyepewa dhamana na wanajimbo lenu na hivyo kuwajibika kwenu.Lakini la msingi sana ni kwamba mtakuwa na fursa ya pekee ya kumchagua governor wa jimbo lenu kwa sifa mnazozitaka wenyewe.kwa mfano uzawa wake,vision yake kwa jimbo LAKE, mikakati yake kwa jimbo LAKE, na mengineyo mengi kwa jimbo LAKE.Lakini pia,huyu kiongozi atakuwa accountable kwa wanajimbo waliomchagua!na siyo kwa mtu fulani mmoja.Faida za kuwa na serikali za majimbo ni nyingi sana!Kama taifa,tume-centralize sana power & authority.na ndiyo maana mfumo huu unachelewesha maamuzi muhimu na ya haraka katika kanda.rasilimali za taifa letu zinapotea kwa sababu ya wanaotakiwa kuzilinda kutokuwa na uchungu nazo kwa sababu ama siyo wazawa na au wanawajibika kwa mtu fulani na sio wanajimbo au kanda!msipotoshwe na kuchoshwa na propaganda za chama kilichotufikisha kwenye umaskini tulionao.abject poverty.FIKIRIA,CHUKUA HATUA!