Sizonje usichanganyikiwe, Mambo bado!!

Sizonje usichanganyikiwe, Mambo bado!!

Sizonje kashakata moto. Hana tofauti na Gari la mkaaa, tripu shamba, tripu gereji .




Nimecheka kwa sauti kubwa!

Hakika JF ni Burudani tosha!


Kumbe magari ya mkaa ndivyo yalivyo?!

Sikujuaga!

Niliwahi kusikia magari ya takakata ya Manispaa mengine yakifika Mlimani hayaingizi gia hivyo inabidi dereva awe na watu 2-3 pale mbele wasaidiane kuishikilia gia ili ikubali isihame hadi wamalize kupanda mlima

Hii ya habari ya gari ya taka nimeisikia leo kwako
 
sizonje,naona wachezaji hawakabi wala kushambulia,mmoja yule kule kalala chali,mwingine yule kipa,hapigi mpira mbele,kakalia kupiga danadana tu,mwingine yule beki anaenda kubadili bukta,aliyonayo imechanika kwa nyuma,bora ulimwambia IGP asimamishe mpira kwanza,hawa ukawa wanashambulia sana,na nina hisi wana njumu za chuma,wachezaji wetu kila wakiwakaba wanaumia
Njumu za China zikiitwaga six meno
 
Sizonje kapiga goti hahahaha mkuu lusumo mungu yu nawe
tapatalk_1601416900707.jpeg
 
Acha Sizonje avune alichopanda ,

Huwezi ligawa Taifa kwa sababu ya tofauti za kiitikadi.

Twende na Mwamba toka kanda ya Kati.
 
Mpendwa Sizonje habari za siku, natumaini u buheri wa afya kibaiolojia japokuwa kiroho u tofauti.

Rafiki yangu Sizonje nakumbuka enzi zile tukijadili mpira ulivyokua hodari kumlaumu kocha!! Kwamba kocha wa timu yetu hawezi, kocha mzembe na anafuga uvundo.

Kadiri tulipokutana kila baada ya sentensi tatu lazima umseme kocha kila siku ikawa hamkani si shwari!

Sizonje utakumbuka kocha alikuvumilia sana japokuwa ulikua huwezi!! Mdomo na maneno mengi yalikubeba kwa mashabiki lakini wachezaji wenzio walikujua!! Ulikua bingwa wa kukariri tarakimu za mchezo bila ujuzi na weledi wa mchezo. Hata kocha alipoonywa sana juu ya kiwango chako kibovu bado alikubeba ingawa ulimsogoa!

Hayawi hayawi yakawa Sizonje!! Kauli zako zikalipa!! Kocha akastaafu na ukocha ukapewa wewe!! Kila mtu ndani ya timu akiduwaa mashabiki waliolewa kauli zako tamu ziso kifani walikubeba hatimaye ukawa kocha.

Awali ulionesha uwezo wa kukonga mashabiki kwa sifa na vitimbi kemkem!! Siku zikasonga mashabiki wakaona timu inarejea nyuma kuliko ilikokuwa kwa kocha mzembe.

Nakujua Sizonje!! Hupendi kukosolewa na wala hupendi kimya cha sifa!! Vigelegele vya mashabiki na vifijo vimekoma!! Mbinu zote za michezo ulizotumia zimebuma!! Timu inarudi nyuma kwa kasi na wachezaji wameshapoteza mori!! Kila ugusapo sasa hapagusiki!! Wachezaji wanaonesha ari machoni pako tu lakini uwanjani wamedorora.

Sizonje usichanganyikiwe, mambo bado ndio kwanza safari inaanza. Ishike ngao na kigao kuyahimili majira.

Kwa leo naishia hapa Sizonje nikija mjini ntakutembelea tule maboga ya enzi zetu.

-----------------------------------------------------------------
UPDATES:
----------------------------------------------- ---------------
Wakuu napenda kuwaarifu kuwa nimepata taarifa nyeti na rasmi kuwa kocha wetu mpendwa Sizonje ameusoma uzi huu na comments zenu zote. Shukrani kwa wote mliotoa ushauri kwa kocha wetu.
Umeongea Kama maalim Nash, nasubiria Diwani part two
 
Back
Top Bottom