Siwezi kuishi naye

Siwezi kuishi naye

Mke wangu nimemfumania
mara 2 na marafiki zangu, nilipomuuliza akaanza kunitukana na kunieleza
kwamba nimelala na mama yake mzazi wakati simjui hata kwa sura kwani
wakati tunaoana mwaka 2009 mama yake alishafariki mwaka 2003.

Nifanyeje nimyonge au nijinyonge au nimsamehe au niondoke nikaanze
maisha yangu mapya yeye nimuache?

Naombeni ushauri wenu wana jf.

Bila mwanaume imara ndoa huyumba na hatimae kuteketea, anza kujichunguza kwanza! Naamini wewe km kiongozi wa familia ndio chanzo cha matatizo yote hayo! Njoo huku Himidini mwaga busara zako, nakuaminia sana!
 
Last edited by a moderator:
Mtupilie kuleee! Yanini akupe vidonda vya tumbo mkubwa mwenzio? Hakufai nakwmbia na maradhi haya ohooo! Kosa c kosa kosa kurudia kosa!ye ni nani hata umsamehe mara zote hizo aaagh! Usiwe mpole kihivyo wakati unajiteketeza mwenyewe! Ondoa hiyo !
 
mmh ndoa zina mambo, kuna haja kiapo cha ndoa kifanyiwe marekebisho kwakweli...
pole sana hamna mke hapo,naona malipizi yake yataendelea had kwa ndugu zako as ameanza na marafiki.
 
Advice is what we ask for when we know exactly what we ought to do but we dont wanna do it.
You can quote me
 
achana naye-au hadi akuletee ukimwi ndo uataamua kumwacha-na jiulize kama umebahatika kumfumania mara 2-ni mara ngapi alshagawa mechi bila wewe kujua-SEPA ACHANA NAYE
 
Pia hili sio jukwaa sahihi kwake bro, namshauri apeleke kwenye mahusiano, mapenzi na urafiki huko waweza kusaidiwa yaidi....

nafikiri atakuwa amenisoma ndio maana nikamuuliza mbona hajaweka picha?
 
Back
Top Bottom