Kuna madaktari waliona mshahara wa serikali hautoshi ninatoa live examples.
Dr. Bake: Huyu alikuwa anafanya kazi Tumbi hospital akilipwa sh laki 4 kama specialist wa mifupa. Alikuwa smart enough kuona kuwa hawezi kuishi maisha anayotaka kwa mshahara huo. Aliacha kazi kwa notice ya masaa 24 mwaka 1996. Hivi sasa anamiliki kituo cha afya ya mifupa huko Kibaha. Watu wanasafiri long distance kwenda kumuona. Halalamikii tena mshahara.
Daktari anayelilia serikali imuwezeshe kuishi kama mfalme ni yule ambaye hana uhakika na skills zake. kama una skills watu watakufuata popote. Kama watanzania walitumia mamilioni kwenda Loliondo, hawatashindwa kukufuata wewe utakapokuwa.
Kama madaktari wanaweza kuchangiana mamilioni kwa ajili ya harusi, wanashindwa nini kuchanga kufungua vituo vyao binafsi vya tiba? Madaktari wa kihindi wameonyesha kwamba it is possible: Aga Khan, Regency, TMJ, Hindu Mandal etc. Wake up doctors, kutumia muda mwingi kufikiria jinsi ya kuongezewa mshahara is a wrong approach, tumia muda huo kufikiria jinsi utakavyodevelop private practice. Mkifungua vituo vyenu, serikali itatambua thamani yenu, sasa hivi serikalli inajua mna options chache, prove it wrong...