Mazee
Senior Member
- Dec 6, 2007
- 128
- 24
Nimejaribu kukaa kimya lakini nafsi yangu inanisuta. Siwezi kuendelea kukaa kimya. My opinion is unpopular, lakini nitasema.
Nitagusa hoja moja baada ya nyingine kama zilivyotolewa na "jumuiya ya madaktari".
Kuongezwa mshahara: Jumuiya imetoa tarakimu zisizo sahihi kuwa mshahara wa daktari ni sh. laki 7. Hii imeandikwa katika ripoti waliyoipeleka kwa waziri mkuu. Hii inadhihirisha kuwa jumuiya hii haiko serious katika hili swala. Lakini tuangalie uhalisia - jumuiya inataka mshahara uongezwe toka hiyo laki 7 (ambayo si sahihi) mpaka miil. 3.5 with immediate effect. Hivi kweli is it reasonable kudai ongezeko la asilimia 500 la mshahara na uongezwe mara moja la sivyo unagoma? Katika historia, swala hili madaktari hawajafanya jitihada za kujadiliana na serikali kidiplomasia. Ulipotokea mgogoro wa interns wa muhimbili kuhamishwa vituo, basi madaktari wakaibuka na kutaka mshahara wa 3.5 mil na kugoma. Mambo hayafanyiki hivi! Tukiwaambia madaktari waonyeshe barua waliyokwishawahi kuiandikia serikalli kuomba mshahara huo, hakuna atakayetoa barua au ushahidi wowote kwa sababu madaktari wameanza na mgomo moja kwa moja. Siungi mkono mgomo wa namna hii.
Madaktari kupewa nyumba: Mara nyingi adui wa daktari huwa daktari mwenzake. Hili swala la nyumba lilishajadiliwa huko nyuma. Nini
kilitokea? Baada ya madaktari wa muhimbili kuthibitishiwwa kuwa wao watalipwa sh laki 4 kila mwezi basi chama cha madaktari ambacho viongozi wake wengi ni madaktari wa muhimbili wakapoteza interest ya kubargain na serikali ili posho hiyo wapate madaktari wa nchi nzima. Chama hicho kilikataa kabisa mara kadhaa kuitisha vikao vya kujadili posho za nyumba huku wakitoa sababu za kuepusha migomo. Sasa hivi inakuja "jumuiya ya madaktari" na kuilazimisha serikali kutoa posho hizo with immediate effect. Siku zote madaktari walikuwa wapi? Je walikuwa wanangoja interns wafukuzwe muhimbili ndio wakumbuke kuwa wanahitaji nyumba? Standing orders za mwaka 1994 zinaeleza kinaga ubaga kuwa daktari anastahili kupewa nyumba, standing orders za mwaka 2009 hazimtaji daktari katika watumishi wanaostahili kupewa nyumba. Maafisa utumishi wote wanatafsiri kuwa standing orders za mwaka 2009 zimemtoa daktari kwenye kundi la watakaopewa nyumba. Ni lini madaktari walienda kujadili hili na wizara ya utumishi? je ni sahihi kuanza na mgomo? Ili madaktari warudishiwe stahili hiyo ni LAZIMA kifungu kwenye standing orders za mwaka 2009 kifanyiwe marekebisho. Je, hilo linaweza kufanyika with immediate effect? Madaktari wamekuwa wavivu kufuatilia mambo yanayowahusu na siwezi kuunga mkono mgomo wa kundi la wavivu wa kubargain na kulobby.
Call allowance: "Jumuiya ya madaktari" inataka call allowance ilipwe kwa half per diem. This is very simple! Kwa nini mnagoma kwenda kazini during working hours? Ni kweli kuwa daktari anastahili kulipwa angalau sh. elfu 40 kwa call lakini solution yake ni rahisi kuliko zote. Madaktari waingie kazini, muda wa kazi ukiisha madaktari warudi nyumbani kama watumishi wengine. Wasikae call mpaka watakapokubaliwa kulipwa kiasi hicho. Kugoma kwenda kazini asubuhi kwa sababu ya malipo madogo ya zamu ya usiku doesn't make sense. lakini again, jitihada gani zimefanyika awali kuhakikisha call inaongezwa? Can doctors provide evidence of their effeorts? HAKUNA.
Mazingira duni ya kazi: Swala la mazingira duni ya kazi ikiwemo wagonjwa kulala chini sio la kulalamikiwa na madaktari. Hili swala waachieni wananchi wenyewe. Daktari unachotakiwa kujua ni capacity ya hospitali yako, beyond that usipokee mgonjwa. Ukishampokea basi unalea ubovu. MV Bukoba, MV spice zilizama kwa sababu ya kubebeshwa mzigo mkubwa kuliko uwezo wake. MV Muhimbili nayo inaingia kwenye hili kundi. Nani alaumiwe? Nahodha lazima awe miongoni mwa watu wa kulaumiwa. Kama madaktarri wataendelea kupekea wagonjwa wengi kuliko idadi ya vitanda it is obvious kuwa wengine watalala chini. hata Ulaya wangekubali kupokea wagonjwa wengi kulikoi uwezo kungekuwa na wagonjwa wanaolala chini. Ila Ulaya swala hilo halipo. Nafasi zikijaa zimejaa, mgonjwa apelekwe wapi, sio swala la daktari. Hata hiyo hospitali unayofanya kazi hujaijenga wewe daktari, ilijengwa kwa sababu mahitaji yalikuwepo. Ukiendelea kupokea wagonjwa wengi kuliko uwezo unaonyesha kuwa mahitaji sio urgent. Wagonjwa wakikosa pa kulazwa ndipo wananchi watashinikiza viongozi wao wawahakikshie facilities za kutosha.
Interns kuhamishiwa hospitali nyingine: Sababu iliyotolewa kuwa hospitali nyingine hazina vifaa inakosa uzito kwa sababu kuna madaktari ambao wapo huko kwenye hizo hospitali nyingine wanafanya intern. Hata hivyo hili swala ni so benign, haliwezi kusababisha mgomo nchi nzima.
Huduma huuzwa na kununuliwa. Bei ya huduma uamuliwa na nguvu za mahitaji na upatikanaji wa huduma. Hakuna daktari aliyelazimishwa kufanya kazi serikali. Kwanini madaktari wanakimbilia kufanya kazi serikalini? Madaktari wawe wakweli na watuambie faida zilizopo serikalini. kwanini madaktari wasitoe notice ya kuacha kazi serikali na kwenda kufanya kazi sehemu bora zaidi. Tanzania kuna soko huria. Kama watu walitumia mamilioni kwenda Loliondo basi hata daktari wanayeamini huduma zake watamfuata popote alipo. Madaktari mnangoja nini kutambua hili?
Mwisho: Mgomo ni risasi ya mwisho. Si sahihi kwa wasomi kutatua changamoto wanazokutana nazo kwa kuanzia na mgomo. Tanzania ni nchi masikini, ili umasikini huo uondoke ni LAZIMA tushirikiane WOTE kuutoa. Ewe daktari, jiulize ni mara ngapi umeingia kazini kwa muda unaostahili na ukafanya kazi mpaka muda wa kazi kuisha? Je, tabia yako ya kila siku kazini inachangia kuondoa umasikini wa nchi yetu? Kila mtu aweke jibu lake moyoni na kujiuliza tena, je mgomo unaoendelea hivi sasa unapaswa kuungwa mkono? Je, kwa siku hizi mlizogoma mshahara mnauchukua wote bila aibu?
Also: Am just curious, nani analipia gharama za kukodi ukumbi wa mikutano wa Starlight Hotel ambao madaktari wamekuwa
wakikutania kwa siku kadhaa?!
Mungu Ibariki Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
TAFADAHLI FUATILIA HIZO HIGHLIGHTED TEXTS STEP WISE
kWA NINI ONGEZEKO LA MSHAHARA KWA AILIMIA 500 SIO SAHIHI? HEBU FAFANUA
JE NI SAHIHI KWA NCHI KAMA ZAMBIA KUMLIPA DAKTARI ZAIDI YA MILIONI NNE KWA MWEZI NCHI INAYOTEGEMEA SHABA,LANDLOCKED COUNTRY E.T.C
RWANDA KUMLIPA DAKTARI MSHAHARA ZAIDI YA MARA TATU YA MSHAHARA WA DAKTARI WA TANZANIA? UNAIJUA MWENYEWE RWANDA ILIVYO SIKUFAFANULII
UNA UHAKIKA KUWA MADAKTARI HAWAJAFANYA JITIHADA ZA AWALI KABLA YA KUCHUKUA HIZI HATUA????
kWA TAARIFA KABLA HATA YA SUALA LA INTERNS MADAKTARI WALIISHAFUATILIA HAYA MASUALA HADI KUFIKISHWA KWA OFISI YA WAZI MKUU NA DOCUMENTS WANAZO NAAMINI WEWE ULIKUWA HUFUATILII HILI SAKATA TANGU AWALI (KASORO SUALA LA MSHAHARA)
LAKINI UNAJUA SWALICHOAMBULIA HUKO NI MATUSI TU YA NGUONI HATA KAMA HUAMINI ILA HUO NDIO UKWELI MATUSI MPAKA UJUMBE ULIOKUWA UNATUMWA ULIPOKUWA UNAWASILISHA TAARIFA MACHOZI YALIKUWA YAKIWALENGA WATU WAZIMA...
STANDING ORDER YA MWAKA 2009 WALA HAIJAKANUSHA KAMA DAKTARI HATAKIWI KUPEWA NYUMBA UMECHEMKA LABDA KWA SBB INAANDIKWA KWA KIZUNGU INAWEZEKANA KABISA UMEPATA SHIDA KUTAFSIRI KWA KISWAHILI KWA HILI NAKUSAMEHE...
UNAKEJELI JUHUDI ZETU KAMA KWELI WEWE HUJAWAHI KUZIONA JUHUDI ZETU BASI U MUST BE BLIND AND SOMEHOW DUMB... MAANA YAKE WAGONJWA WOTE TUNAOWATIBIA SISI WANAKUFA(HAWAPONI)
kUMBE WEWE NI KIAZI MWINGINE HUJAFANYA UTAFITI NGOJA NISHIE HAPA WAGONJWA WANALALA CHINI WEWE UNAONA POA TU SASA MIMI DAKTARI NITAWAONAJE HAO WAGONJWA WAKIWA WAMELALA CHINI NA HILI NI MOJA VIFAA VYA KAZI KWA UJUMLA HAKUNA JARIBU KUTEMBELA HOSPITALI SIKU MOJA HALAFU NDIO UJE UANDIKE HUMU TENA ILA MPAKA SASA NAAMINI WEWE SIO MZIMA MUNGU AKUBARIKI KWANI HATA SISI TUNAAMINI KUWA MUNGU ANATUTUMIA TU KUTENDA MIUJIZA YAKE NAOMBA MUNGU AKUPONYE FROM UR INSANITY