Ukiunganisha hizo semi za Sitta hapo kwenye red utagundua,Makonda hayupo peke yake,Aliyekuwa Mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba Samwel Sitta amesema kilichomkuta aliyekuwa Mwenyekiti wa tume ya mabadiliko ya Katiba jana ni sawa na kujitakia mwenyewe.
Akihojiwa muda mfupi uliopita na Redio Voice of Tabora kuhusu maoni yake kwa vurugu kubwa iliyoongozwa na Paul Makonda jana, Mzee Sitta amesema kimsingi wananchi walio wengi wanaunga mkono Katiba pendekezwa.
Mzee Sitta amesema Jaji Warioba anapaswa kutulia kwani akiendelea anaweza kuaibishwa kuliko aliyofanyiwa jana pale Ubungo blue pearl.
Mzee Sitta amemtaka Warioba awaachie wananchi Katiba pendekezwa waamue wenyewe kwa njia ya kura.Sitta ameendelea kusema watanzania wa sasa siyo wajinga na wakikuona unawadanganya watakuvamia hapohapo.Amedai uelewa wa wananchi kwa sasa ni mkubwa kuliko wakati mwingine wowote.
Alipoulizwa swali kuhusu Uvumi kwamba yeye ndiye anamfadhili na kumtuma Paul Makonda kupambana na yeyote anayempinga Mzee Sitta amecheka na kusema hatajibu hilo swali.
Una imani na Rais Jakaya Mrisho Kikwete katika mambo yafuatayo?
1: Kuboresha Sekta ya Afya,
2: Kuboresha sekta ya Elimu,
3:Kuboresha Miundombinu,
4: Kusimamia na Kuboresha Utawala bora na Demokrasia,
5: Kutatua tatizo la Ajira kwa vijana,
6: Kusimamia fedha za umma na kuzuia ufujaji wake.
Mimi nilishasema huyu mzee warioba ataendelea kuadhirika Sana. Ile tume ilikuwa Na watu wengi Tu wenye akili Na busara zao wamekaa kimya huyu yeye anajifanya anajua Sana midahalo.ningekuwa Mimi ningekaa kimya ya nini kubishana kila siku kwenye vyombo vya habari hizi kazi angewaachia wanasiasa.
Tunamsubiri nae ajitokeze hadharani, ndio tutajua kati yake na Warioba nani anajitakia mwenyewe.
Tunashkru kama karuhusu na kushabikia vurugu.
Hapa ni kujibu mapigo tu hatuna namna.
Waziri wa Utangamano Afrika Mashariki anaruhusu fujo.......................
Mimi nilishasema huyu mzee warioba ataendelea kuadhirika Sana. Ile tume ilikuwa Na watu wengi Tu wenye akili Na busara zao wamekaa kimya huyu yeye anajifanya anajua Sana midahalo.ningekuwa Mimi ningekaa kimya ya nini kubishana kila siku kwenye vyombo vya habari hizi kazi angewaachia wanasiasa.
Mimi nilishasema huyu mzee warioba ataendelea kuadhirika Sana. Ile tume ilikuwa Na watu wengi Tu wenye akili Na busara zao wamekaa kimya huyu yeye anajifanya anajua Sana midahalo.ningekuwa Mimi ningekaa kimya ya nini kubishana kila siku kwenye vyombo vya habari hizi kazi angewaachia wanasiasa.
Kilichomkuta jana Warioba ni msiba wa kujitakia
Hivi nieleze kuna tofauti gani na wana ccm mbalimbali ambao kila kukicha wanapanda majukwaani na kuwaambia wananchi waikubali katiba iliyopendekweza kwa sababu ni 'nzuri'? Kwani Warioba, au mtu mwingine yeyote yule haruhusiwi kusema kuwa katiba iliyopendekezwa si nzuri?
Jambo ambalo limejitokeza ni kwamba bado katiba iliyopendekezwa haijatolewa kwa wananchi. Badala yake sisi wananchi tunashinikizwa tuikubali hiyo katiba. Ni vyema basi, wakajitokeza watu wenye kuielewa katiba, pamoja na mchakato wake wote, kuelimisha wananchi. Si vyema kuwaburuza wananchi wakubali kitu ambacho hawakielewi vizuri, hasa katiba ambayo itaathiri maisha yao kwa miaka mingi ijayo.
Angalieni njaa zitafanya Sitta awaingilie.
Kweli kabisa mkuu, lakini mzee Warioba aache kabisa, kama anavyowaambia wenzie, kujifichaficha nyuma ya MWALIMU!
Nani kawateua Warioba, na Butiku, kufanya kazi ya 'PRIESTHOOD IN MWALIMU NYERERE'S TEMPLE'? HAWAWEZI KABISA KUONGEA WAO KAMA WAO! KILA KITU MWALIMU MWALIMU MWALIMU!
WATU SASA TUNACHOKA KURUDISHWA NYUMA KIFIKRA NA KUGANDISHWA MIAKA YA SITINI NA SABINI! HEBU TUSONGE MBELE!