Sitta: Tuna wakati mgumu

Sitta: Tuna wakati mgumu

Pole sana,mzee sita.sasa bac kumbuka ushauri wa mh:Lema kwamba umetupiwa ndoano na mafisadi na wewe bira soni ukaipokea,nasasa imeku kwamia shingoni pekeyako na sasa subili kitoke kindoano (liishe bmk la katiba)ufe vizuri kisiasa tukuzike,maana hutakuwa na cha kutuambia wananchi wako.na ndo hapo mafisadi yalio kutanguliza uaibike itakuwa kicheko na kukuponda pia,"pole sana mzee" sisi wanyonge tunasema mungu atutangulie,na awaumbue wanafiki wote wa aina 6t tuwajuwe mapema uovu wao!!
 
Huyu Mzee ni msanii tu, alikuwa ameishajipigia bajeti ya laki tatu tatu na mkewe hadi October 4 halafu UKAWA wakataka kumpora kitumbua. Huyu mzee viwango vyake viko chini sana mkimpa uraisi kuna hatari tukarudi kupanga foleni ya sukari na sabuni au kuvaa makaniki yale. Amechoka kiakili

Huyu mzee kawa mtu hovyo kabisa hata huo uraisi ni shida tukimpa,ni mroho sana wa hela,hata haibu haoni na ni mbinafsi,hebu ona anataka ile fedha iliyobaki baada ya wana UKAWA kutoka mjengoni eti waitumie,ilihali watu kila siku wanapigia kelele huduma duni za afya,elimu n,k badala ya kusema hii fedha irudishwe serikalini isadie kufanya mambo mengine muhimu yeye anataka wagawane sasa mtu kama huyu tukimpa uraisi si hata skendo kama ya Richmond itakuwa cha mtoto,mzee gani anyekosa busara na anakuwa hana uchungu na fedha ya serikali miaka nenda miaka rudi kafanya siasa ni ajira na ukwasi mkubwa wa fedha lakini wapi baado tu ndio tamaa zinamzidi.Sitta akiwa raisi wa nchi hii nahamia Syria au Iraq nikfie mbali.
 
Mungu ni mwema , maana mie nisiye na chama , kama huyu mzee 6 angesimama kugombea urais ningempa kura yangu kabla ya BMK.ila kwasasa nashukuru nimemjua vizuri ata udiwani hafai.
 
Huyu Mzee ni msanii tu, alikuwa ameishajipigia bajeti ya laki tatu tatu na mkewe hadi October 4 halafu UKAWA wakataka kumpora kitumbua. Huyu mzee viwango vyake viko chini sana mkimpa uraisi kuna hatari tukarudi kupanga foleni ya sukari na sabuni au kuvaa makaniki yale. Amechoka kiakili

Huyu akiwa Rais nahamia Congo hakyamungu!! ptuuuuuu!!
 
Tatizo kubwa la sisi wabongo ni uvivu wa kusoma between the lines, yaani sentensi hata hazifiki kumi kuzisoma kwa utulivu na kuzielewa ni sheeedah je kitabu? No wonder wazungu wanatutania kwamba kwa mswahili ficha fedha kwenye vitabu utazikuta!! Namnukuu mleta mada...''Hayo ameyaongea wakati akiwa na kikao na kamati ya uongozi pamoja na ile iliyoandaa rasimu ya tatu ya katiba....'' wapi amekuambia ameyaongelea bungeni?

Mkuu umenichekesha sana du!
Jibu hli ni zur sana
 
Mzee huyu kwanza analaana za watu wa Urambo,hapa nilipo sasa nimelala gesti moja ipo kama mita 100 hivi kutoka nyumbani kwa sita,yeye mwenyewe ndo ana nyumba dizain kama ilitakiwa ijengwe ghorofa ila hakupanda,Urambo watu wanakunywa maji ya kisima,na nikasikia kuwa kuna internal conflicts kati yake na mkewe,wanagombea nani agombee ubunge!tehteh;mzee wetu tunakuheshimu sana,rudi kwenu Urambo,japo mgawane marupurupu ya BMK
 
Mnaishi kwa ndoto.
Na ndoto zenu hazina athari kwa 6,ccm wala watanzania. Uzuri ni kwamba, mnatunga uongo kisha mnajidanganya then mnauamini uongo huohuo.
We keep on keeping on. Tunawatungia katiba
mkuu umeacha wizi wa simu?
 
Kwa mara ya kwanza hapa Dodoma, Samwel Sitta kiongozi wa bunge maalum la katiba amekiri kwamba wana wakati mgumu.

Hayo ameyaongea wakati akiwa na kikao na kamati ya uongozi pamoja na ile iliyoandaa rasimu ya tatu ya katiba, nimethibitisha.

"Kwa kweli muda unavyozidi kwenda na kila jambo tunalofanya tunakumbana na upinzani mkali kinyume kabisa na matarajio yetu" alisema Sitta.

Sitta pia katika kikao hicho amesema kuwa anajiuliza sana ni kwa nini upepo unawabadilikia hivyo na anaonekana kukata tamaa kama rais Kikwete ataridhia rasimu ipigiwe kura mapema.

Sitta kwa mara ya kwanza tangu aanze mchakato huu wa katiba amesikika akisema kuwa ana wasiwasi huenda akageukwa siku za usoni na mahasimu wake kisiasa ndani ya CCM kwa lengo la kulipa kisasi ingawa hakugusia ni kisasi cha aina gani.

Ni ukweli usiopingika kuwa Samwel Sitta amejikuta akipoteza kabisa mvuto aliokuwa nao kisiasa baada ya kulingoza bunge la katiba na kujikuta akikosolewa na kutupiwa shutuma nzito waziwazi kama msaliti mkubwa wa wananchi kwa sasa.
Watu wengi wanashindwa kuelewa ni kwa nini Sitta anakuwa mzito kuelewa hali ya kisiasa nchini.

Rais JK ni mjanja na ameliona hilo siku nyingi sana baada ya kupima upepo, na amejiweka mahali pazuri kisiasa kwa ingalau kukutana na TCD ya mzee Cheyo.

Kwa hali ilivyo hata wana CCM kwa sasa wana wasi wasi mkubwa wa yanayoendelea katika BMK kwani maoni ya wananchi yatawarudi tu, muda ukifika.
 
Mkuu masopakyindi MACCM hawaikutaka katiba mpya tangu mwanzo. Walishakubaliana watafanya lolote lile kuhakikisha katiba mpya haipatikani au kama itapatikana basi itakuwa ni ile waitakayo wao ya kuendelea kung'ang'ania madaraka milele. Huyo Kikwete naye hajajiweka pazuri popote baada ya hotuba yake kwa kiasi kikubwa kuchangia kutoelewana kwenye hilo Bunge la Posho, pia baada ya UKAWA kuondoka alikuwa nafasi kama Rais kuizuia aibu iliyokuwa ikiendelea ndani ya hilo Bunge na kuokoa mabilioni ya pesa za walipa kodi lakini hakufanya hivyo kwa kisingizio cha kutokuwa na mamlaka ya kulivunja/kulisimamisha na hivyo kupoteza mabilioni ya pesa ambazo zingeweza kutumika kwa mambo mengine muhimu. Kwa maoni yangu hakuna tofauti ya Kikwete na Sitta kwenye hili sakata la Bunge haramu la Posho.

Watu wengi wanashindwa kuelewa ni kwa nini Sitta anakuwa mzito kuelewa hali ya kisiasa nchini.

Rais JK ni mjanja na ameliona hilo siku nyingi sana baada ya kupima upepo, na amejiweka mahali pazuri kisiasa kwa ingalau kukutana na TCD ya mzee Cheyo.

Kwa hali ilivyo hata wana CCM kwa sasa wana wasi wasi mkubwa wa yanayoendelea katika BMK kwani maoni ya wananchi yatawarudi tu, muda ukifika.
 
Wazo la kusimamisha mchakato wa katiba ndiyo wazo mwafaka. Nia njema ya mchakato unaoendelea haionekani. Kundi kubwa la wananchi hawakubaliani nao. Hata kama ccm watumia nguvu nyingi kuwashawishi wananchi wa mijini na vijini waikubali bado uhalali wake hauonekani. Mimi nashauri katiba inayopendekezwa iwekwe kapuni na baada ya uchaguzi tuanze upya. Tuanzie pale ukawa walipotoka bungeni. Ni heri tutumie gharama kubwa kupata katiba yenye maridhiano kuliko kukwepa gharama na tupate katiba itakayotuvunjia amani.
 
Mwanzo wa hili Bunge LEMA alimuambia SITA kuwa sasa hivi umepatikana na upo ktk mtego mkubwa sana, ukifanikiwa itakuwa faida kwako lakini ukishindwa ndio mwisho wako umefika. sita akawa mpoleeee siku ile nadhani leo atakuwa anaikumbuka ile kauli ya LEMA. Mwisho wake umefika.
 
ni kweli mkuu kila MTU anayemzungumzia sita lazima aseme kauli hii

"NIlikuwa namkubali sitta lakini kwa hili amesusha hadhi yake"
 
Mna kumbuka kale ka wimbo shuleni wakati wa mchaka mchaka kaliko kua kanahamasisha uzalendo? tulikua tukiimba hivi,, Idd Amin akifa akifa mimi siwezi kulia kulia nitamtupa Kagera Kagera awe chakulaaaa cha mamba cha mamba. Nimeipenda sana hiyo stori na SITTA akishindwa kwenye mission yake hiyo mimi siwezi kulia bali nitafurahu sana na kuchekelea maana baadae lazima awe chakula cha wapinzani wake kisiasa(mamba) kwisha habari yake na atakula jeuri yake na huo unaweza kuwa ndio mwisho wake kisiasa.
 
Mnaishi kwa ndoto.
Na ndoto zenu hazina athari kwa 6,ccm wala watanzania. Uzuri ni kwamba, mnatunga uongo kisha mnajidanganya then mnauamini uongo huohuo.
We keep on keeping on. Tunawatungia katiba

pumbf senu. Kuleni poso mtatukuta uraiani
 
Back
Top Bottom