Sitta: Sikukejeli vielelezo vya Dk Slaa kuhusu BoT

mizee kama hiii ambayo imeshakuwa kama mibwege kwenye akili zao si iwe inaambiwa ifunge madomo yao??maana kila wakiyafungua mabakuli yao..yanatoa pumba juu ya pumba!!?hawaoni aibuu??

hivi ni kuwa huwa hawashauriani ama kila mtu nafsi yake inamsuta so siku akiamka nafsi imemsuta sana anajikuta tuu karopoka hili mara lile??na bado mafisadi wote mwaka huu watapagawa
 
hivi hawa viongozi hawajui kuomba radhi? yaani kila mmoja anatatufa udhuru wa kuhalalilisha alichofanya...

Kikwete analaumu Benki Kuu
Meghji anamlaumu Balali
Balali anawalaumu "vigogo" kwa kumtumia
Sitta analaumu waandishi wa habari kwa kupotosha
n.k n.k Kuna mtu anaweza kuwajibika kwa vitendo au maneno yake au wote ni wale "viongozi wasiokosea" kwenye "Taifa la wasiokasirika"?
Wooote walaumiane, mie namlaumu nyerere, ndie aliekuwa fisadi wa kwanza, tena ana roho za watu nyingi tuu alizifisadi, kwa kuzilisha kwa simba, chui. kwa kuzigongesha kwa nyoka, kwa kuzilisha mizizi-sumu na maufisadi mengine mengi tu aliyoyafanya. Au hujuwi system ni nini?
 
Mi na shangaa vyombo vya habari wanavo mlea lea Six, huyu kwanini wasimuwekee marudio ya kipindi chake wamuumbue live?? yaani huyu mzee ni kisiki kikubwa sana katika mpambano wa ufisadi TZ, hasa pale anapo tumika kuwabana watetezi wetu bungeni! ananikera sana!
Kweli kabisa tumuombe tido muhando bosi wa tvt yule atuwekeemarudio .yani sitta anadhani tumesahau walivyokuwa wanambeza SLAA tena akishirikiana na akina mzindakaya waliotoa hesabu zinazokaribiana na e&y
 
Kama sikosei katika hii forum kuna ushahidi unaoweza kuthibitisha kwamba fisadi Sitta alitamka bungeni kwamba amevifikisha vielelezo vya ushahidi polisi ili vichunguzwe na hatimaye kumfungulia mashtaka Slaa. Sasa anayakimbia maneno yake mwenyewe! Mwe! kazi ipo mwaka huu.
Kasahau mwana wane kama alishawhi kutamka haya.KWANI haiwezekani wananchi kupiga kura ya kutokuwa na imani na spika mana bungeni wnzake watamkubali kwa wingi wao
 
Nadhani kuwa Sitta ana uwezo wa kuendesha Bunge ila ana kasoro ya kutokujiamini. Hii inatokana na ukweli kuwa post ile aliipata kwa kupewa na watu fulani; kwa hiyo kila anachofanya, hujitahidi kuona kuwa hatawaudhi waliompa post hiyo. Hiyo ndiyo gharama ya kuongozwa na kibaraka hata kama ana uwezo wa kuongoza. Ukibaraka huu ndio uliomfanya atumie mamilioni ya pesa zetu kuchunguza kesi ya Malima na Mengi halafu mwishoni eti "akatumia busara zake" kumaliza kesi ile. Hoja zote zilizoletwa na upinzani pale Bungeni, hakutaka kuzipa uzito ili kulinda umaarufu wa waliompa post ile. Matokeo yake leo hii bunge limekuwa kama kilabu cha pombe za kienyeji kilicho na walevi wengi ambao kila mmoja wao anajiongelea lake bila kujua anaongea nini; kesho yake atakana yote aliyoongea kilabuni pale.

-Leo hii Spika Sitta anakana kukataa hoja ya Slaa.

-Miezi michache iliyopita, Naibu Spika alikana kuwa Zitto hakuadhibiwa kwa madai ya uwongo bali ni kutokana na "lugha aliyotumia"

Spika na naibu wake ni walevi tu hawa.
hawa maspika mi nawashangaa haswa yani leo huyu mama makinda anataka kutuzuga kwa kusingizia kauli alizotumia Zitto.wajue watu huwa tunafuatilia vipindi vyote vya bunge na sasa wasubiri buzwagi mafisafi wakubwa hawa hawana hata huruma na wananchi
 
Sitta nadhani sasa baada ya JK kuchachamaa atakuwa kesha anza kuwa na wasi wasi maana najua magazeti kama mwananchi na Tanzania Daima ,Raia mwema na Said Kubenea watamrudia kusikia kama alikuwa serious na utetezi wake huu . Majira na IPP hawawezi kumchimba .
 
MWK

Ni kweli kabisa huko vijijini hawajui chochote kinachoendelea kuhusu ufisadi Tanzania unaoendelea.........hili nimelithibitisha mwenyewe kwa kuongea na baadhi ya watu huko vijijini na katika mikoa tofauti tofauti.....wengi hawaelewi kabisa.......nafikiri ukiondoa upinzani hata NGOs zinazojihusisha na demokrasia nchini and other pressure groups hawafanyi kazi yao........

nakumbuka hapa JF tulishaliongelea sana suala la kufikisha hizi jumbe kwa wananchi vijijini hata kwa kutumia simu......tuendelee kuelimisha wananchi pale tunapopata nafasi

Usijali Ogah,

Siku zitafika tena si mbali Wananchi watamfanyia kama Wale wa Boko walivyomfanyia Balali (ingawa siungi mkono jambo lile). Watagawana mali zake kama hawana akili nzuri, kwa sasa wanatufanya hatujui mali zao; wako Wanachi wanzaipigia hesabu PDidy keshawahi nyumba ya Masaki na Ubungo.

Kwani Dikteta Mwai Kibaki swahiba yao si alidfhani kuwa Wananchi wa Kenya Vijijini watamuunga mkono katika wizi wa Kura; leo yakoje, imebaki jasho linatoka namna ya kuzima moto huo.
 
Hivi vioja,kila kukicha TZ inaljaa vioja.Huyu, Sitta naye ni fisadi tu japo hajatajwa kwenye tuhuma. Asituletee habari zake,yuko bias sana,asitufanye kama hatukuona bunge live siku ile anatoa hoja hiyo
 
Wooote walaumiane, mie namlaumu nyerere, ndie aliekuwa fisadi wa kwanza, tena ana roho za watu nyingi tuu alizifisadi, kwa kuzilisha kwa simba, chui. kwa kuzigongesha kwa nyoka, kwa kuzilisha mizizi-sumu na maufisadi mengine mengi tu aliyoyafanya. Au hujuwi system ni nini?


Kitu muhimu ni ushahidi tu. BAdo pamoja na madai yote Maisha ya Mtanzania wa daraja la chini yalikuwa ni bora zaidi kuliko Mtz wa leo.

Zaidi ya yote Nyerere ametuachia LEGACY, Jiulize hao waliokuja baada ya Nyerere wametuachia nini? Zaidi sana wanatupeka kwenye vita ya wenyewe kwa wenyewe (God forbid)
 
Kama huyu mzee anasahau anayo yasema tutawezaje kuamini uwezo wake wa kuwa spika na tena haya hajayasema zamani ? Ama kweli mwaka huu Watanzania Mungu kaamua kuwapigania .
 
Unajua hata paka kiumbe mdogo ukimfungia chumbani na kuanza kumpiga hata kama una marungu huwa anshindwa kuvumilia na huwa anakuwa mkubwa kuliko simba na anaweza kukudhuru na silaha yake ndogo ambayo ni kucha na meno.

Sitta alimfungia Dr. slaa bungeni ila ali[pozidiwa aliamua kumshambulia kwa kutumia silaha ndogo ya kucha na meno na hakika kwa sasa anamwona Slaa amekuwa mkubwa kuliko simba hivyo anapata hofu kuwa anaweza kujeruhiwa vibaya na hata kuuwawa na mnyama ambaye hana silaha na pia ni mdogo sana kwa umbo.

Mwaka huu mafisadi wanajikuta wakijiwekea jiwe zito shingoni na hakika wajue kuwa mwaka huu mambo yatakuwa magumu zaidi juu yao na watajikuta wanapata ugonjwa wa m,oyo.

Nasema kuwa Sitta jaribu kuusema ukweli kuwa EL alikuzuia na kukukanya kuwa hoja ya Slaa isioingizwe bungeni baada ya ushauri wa watu wa usalama wa taifa hivyo basi muombe radhi slaa na watanzania wote kwani umewanyima haki yao ya msingi....
 
Asha
Unatumia maneno mazito ambayo viongozi wa CCM hawajawahi kuyaona tangia wakiwa masomoni hadi leo . Samahani ama tumekubali ama Utaifa,haya ni maneno magumu mno na ukaongezea kujiuzuru. Akifanya mmoja lazima Rais akatae maana hate yeye hana maneno hayo wala hakuwahi kuyasikia kabla .
 
Kitu muhimu ni ushahidi tu. BAdo pamoja na madai yote Maisha ya Mtanzania wa daraja la chini yalikuwa ni bora zaidi kuliko Mtz wa leo.

Zaidi ya yote Nyerere ametuachia LEGACY, Jiulize hao waliokuja baada ya Nyerere wametuachia nini? Zaidi sana wanatupeka kwenye vita ya wenyewe kwa wenyewe (God forbid)

Hii ndio legacy?

.... During the 1970s the major expression of interventionism came with the compulsory establishment of "ujamaa" (communal) villages in the rural areas but this policy, which involved high levels of coercion, was later recognized as a social and economic disaster and was abandoned.
 
Back
Top Bottom