Sitta amweka pabaya JK

Josh Michael

JF-Expert Member
Jun 12, 2009
2,523
77
  • Kauli zake zaivuruga CCM, Kamati ya Mwinyi
na Mwandishi Wetu

lowasa%2Bsita.jpg


MWENENDO na kauli zinazotolewa na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano, Samuel Sitta, zimekivuruga Chama Cha Mapinduzi (CCM) na kuipa kazi ya ziada kamati ya usuluhishi wa mgogoro kati yake na Waziri Mkuu aliyejiuzulu, Edward Lowassa.

Kauli hizo za Sitta zinakwenda sambamba na msimamo wake wa kugoma kumwomba radhi Lowassa, badala yake anataka mbunge huyo wa Monduli ndiyo awaombe radhi Watanzania.

Hivi karibuni, wakati wa hafla ya uzinduzi wa albamu ya kwaya ya Kanisa Katoliki la Mtakatifu Michael, Parokia ya Mtakatifu Xavery, Chang'ombe, Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Sitta alisema ujasiri wake unatokana na nguvu za Mungu.

Alisema nguvu hizo zimekuwa zikimwezesha kutekeleza wajibu wake kwa uhakika bila kuyumbishwa wala kuogopa kitu chochote.

Sitta ambaye siku za hivi karibuni amekuwa akishambuliwa kwamba amewasaliti Watanzania kutokana na kuufunga mjadala wa kashfa ya Richmond, juzi akiwa mjini Songea, alikaririwa akisema alinusurika kuvuliwa uanachama CCM kutokana na ujasiri wake wa kusimamia ukweli.

Kauli hizo zimeonekana kuivuruga zaidi CCM na kamati inayongozwa na Rais Mstaafu Ali Hassan Mwinyi inayorusha karata ya mwisho kuwasuluhisha Sitta na Lowassa.

Wajumbe wengine wa kamati hiyo ambayo imeongezewa muda wa mwezi mmoja kusuluhisha mgogoro huo, ni Makamu Mwenyekiti wa CCM taifa, Pius Msekwa na Mjumbe wa Kamati Kuu (CC) na Halmashauri Kuu (NEC) ya chama hicho, Abdulrahman Kinana.

Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Kapteni John Chiligati, aliiambia Tanzania Daima jana kuwa, CCM imeshangazwa na kauli za Sitta wakati anapaswa kujiandaa kwa usuluhishi.

Chiligati ambaye pia ni Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi, alisema kwa kawaida vikao vya NEC na CC ni vya siri na mjumbe yeyote hapaswi kutoa siri za vikao hivyo.

"Ndugu yangu kweli nimemsikia, inasikitisha sana, lakini sina cha kusema na nakuomba uandike hivi kwamba Chiligati hana cha kusema kuhusu kauli za Sitta," alisema Chiligati.
Alipoulizwa kama Sitta anaweza kuchukuliwa hatua kwa kauli hizo, Chiligati alisisitiza kuwa hawezi kusema chochote kuhusu hilo.

Kwa upande wa Kamati ya Mzee Mwinyi, kauli hizo zimezidi kuwaweka katika wakati mgumu na huenda wakarejesha ripoti katika muda uliopangwa bila kupata suluhu kati ya watu hao.

Akizungumzia kauli za Sitta, Msekwa kama ilivyokuwa kwa Chiligati, alisema hawezi kusema chochote kwani kamati hiyo ni ya CCM na inafanya kazi za CCM na si za CHADEMA.

"Hii kamati ni ya CCM, si ya CHADEMA, ninyi watu wa CHADEMA mnaitakia nini? Hata kama Sitta anatoa kauli tata si kazi yetu, tuacheni jamani, mnaitakia nini CCM?" alilalama Msekwa na kukata simu.

Kwa upande wake, Sitta ambaye pia ni Mbunge wa Urambo Mashariki, aliliambia Tanzania Daima Jumatano kuwa siku zote anasimamia katika ukweli na kuzingatia maadili.

Alisema kauli kwamba alitaka kupokonywa kadi ya CCM kwenye vikao vya NEC mwaka jana na mwaka huu mjini Dodoma ni ya ukweli na kila mtu anajua.

"Huo ni ukweli wenyewe, tatizo liko wapi? Maana kila mtu anajua, mimi sioni kama kuna siri hapa, na hili nitaendelea kulisema hata kama wenzangu hawataki," alisema Sitta.

Akizungumzia hoja kwamba kundi lake linaandaa mgombea urais, Sitta alisema katika mzozo wake na Lowassa hapendi kuzungumzia vyeo kwani msimamo wake ni kusimamia maadili.

"Mimi sipendi kuzungumzia vyeo sijui urais au sijui nini, ila nasimamia kwenye maadili na ndiyo maana tunausubiri kwa hamu muswada wa sheria wa kutenganisha siasa na biashara. Haiwezekani mtu umeingia kwenye siasa masikini, unatoka tajiri," alisema.

Sitta alilazimika kuzungumzia suala la urais baada ya kuwapo taarifa kuwa siri ya ugomvi wake na Lowassa ni kinyang'anyiro cha urais mwaka 2015.

Kwa mujibu wa habari hizo, Sitta na Lowassa ambao hadi sasa wameligawa Bunge na chama kwa misimamo yao, kila mmoja anataka rais ajae baada ya Rais Jakaya Kikwete kumaliza muda wake, kama si yeye, atoke kwenye kundi lake.

Kwa hali jinsi ilivyo kuhusu mzozo wa vingunge hao, Kamati ya Mzee Mwinyi ambayo inajipanga kuwakutanisha vigogo hao, inaweza kugonga mwamba kutokana na msimamo wa Sitta na kauli anazozitoa hivi sasa tangu kumalizika kwa kikao cha NEC mjini Dodoma.

Mbali ya kuifanya kazi ya Kamati ya Mwinyi kuwa ngumu, msimamo huo wa Sitta unamweka pabaya Mwenyekiti wa CCM taifa, Rais Jakaya Kikwete kufanya maamuzi magumu.

Tangu kuibuka kwa sakata la mkataba wa kifisadi kati ya Kampuni ya Richmond na TANESCO, uliosainiwa Juni 23, 2006, kisha kusababisha Lowassa kujiuzulu Uwaziri Mkuu na Rais Kikwete kuvunja baraza la mawaziri, CCM na Bunge hata serikali vimejikuta vikiingia katika mgawanyiko mkubwa.

Kundi la Lowassa ambalo linaundwa na watu wenye nguvu ya fedha, limekuwa na ushawishi mkubwa ndani ya CCM na hata bungeni, lakini Spika Sitta akiwa na kundi dogo la watu majasiri wanaojiita wapambanaji wa ufisadi wamesababisha msuguano ndani ya CCM na Bunge ambalo asilimia kubwa ya wabunge ni wa chama hicho tawala.

Mgawanyiko huo ndiyo ulioifanya NEC kuunda Kamati ya Mwinyi kutafuta suluhu. Hata hivyo, kamati hiyo iliyoanza kazi Agosti mwaka jana ilishindwa kumaliza tatizo hilo baada ya Spika kukataa suluhu na Lowassa.

Licha ya Spika kukubali kuizika hoja ya Richmond bungeni, bado msuguano uliendelea ndani ya chama na hivyo mkutano wa NEC uliofanyika hivi karibuni uliamua kuiongezea muda Kamati ya Mwinyi kwa kuitaka ichunguze kiini cha tatizo.
 
Kwa hiyo weupe unaendana na kuwa na pesa? Ama mmoja anafikiri sana kuhusu Watanzania wakati mwingine ni bora liende, hajali chochote?
Mkuu nimeangalia hayo mashati tu! But coming to think about it the contrast is mmoja ana brand ya 'ufisadi' na mwingine ya 'upiganaji'.
 
  • Kauli zake zaivuruga CCM, Kamati ya Mwinyi
na Mwandishi Wetu

lowasa%2Bsita.jpg


MWENENDO na kauli zinazotolewa na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano, Samuel Sitta, zimekivuruga Chama Cha Mapinduzi (CCM) na kuipa kazi ya ziada kamati ya usuluhishi wa mgogoro kati yake na Waziri Mkuu aliyejiuzulu, Edward Lowassa.

Kauli hizo za Sitta zinakwenda sambamba na msimamo wake wa kugoma kumwomba radhi Lowassa, badala yake anataka mbunge huyo wa Monduli ndiyo awaombe radhi Watanzania.

Hivi karibuni, wakati wa hafla ya uzinduzi wa albamu ya kwaya ya Kanisa Katoliki la Mtakatifu Michael, Parokia ya Mtakatifu Xavery, Chang'ombe, Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Sitta alisema ujasiri wake unatokana na nguvu za Mungu.

Alisema nguvu hizo zimekuwa zikimwezesha kutekeleza wajibu wake kwa uhakika bila kuyumbishwa wala kuogopa kitu chochote.

Sitta ambaye siku za hivi karibuni amekuwa akishambuliwa kwamba amewasaliti Watanzania kutokana na kuufunga mjadala wa kashfa ya Richmond, juzi akiwa mjini Songea, alikaririwa akisema alinusurika kuvuliwa uanachama CCM kutokana na ujasiri wake wa kusimamia ukweli.

Kauli hizo zimeonekana kuivuruga zaidi CCM na kamati inayongozwa na Rais Mstaafu Ali Hassan Mwinyi inayorusha karata ya mwisho kuwasuluhisha Sitta na Lowassa.

Wajumbe wengine wa kamati hiyo ambayo imeongezewa muda wa mwezi mmoja kusuluhisha mgogoro huo, ni Makamu Mwenyekiti wa CCM taifa, Pius Msekwa na Mjumbe wa Kamati Kuu (CC) na Halmashauri Kuu (NEC) ya chama hicho, Abdulrahman Kinana.

Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Kapteni John Chiligati, aliiambia Tanzania Daima jana kuwa, CCM imeshangazwa na kauli za Sitta wakati anapaswa kujiandaa kwa usuluhishi.

Chiligati ambaye pia ni Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi, alisema kwa kawaida vikao vya NEC na CC ni vya siri na mjumbe yeyote hapaswi kutoa siri za vikao hivyo.

"Ndugu yangu kweli nimemsikia, inasikitisha sana, lakini sina cha kusema na nakuomba uandike hivi kwamba Chiligati hana cha kusema kuhusu kauli za Sitta," alisema Chiligati.
Alipoulizwa kama Sitta anaweza kuchukuliwa hatua kwa kauli hizo, Chiligati alisisitiza kuwa hawezi kusema chochote kuhusu hilo.

Kwa upande wa Kamati ya Mzee Mwinyi, kauli hizo zimezidi kuwaweka katika wakati mgumu na huenda wakarejesha ripoti katika muda uliopangwa bila kupata suluhu kati ya watu hao.

Akizungumzia kauli za Sitta, Msekwa kama ilivyokuwa kwa Chiligati, alisema hawezi kusema chochote kwani kamati hiyo ni ya CCM na inafanya kazi za CCM na si za CHADEMA.

"Hii kamati ni ya CCM, si ya CHADEMA, ninyi watu wa CHADEMA mnaitakia nini? Hata kama Sitta anatoa kauli tata si kazi yetu, tuacheni jamani, mnaitakia nini CCM?" alilalama Msekwa na kukata simu.

Kwa upande wake, Sitta ambaye pia ni Mbunge wa Urambo Mashariki, aliliambia Tanzania Daima Jumatano kuwa siku zote anasimamia katika ukweli na kuzingatia maadili.

Alisema kauli kwamba alitaka kupokonywa kadi ya CCM kwenye vikao vya NEC mwaka jana na mwaka huu mjini Dodoma ni ya ukweli na kila mtu anajua.

"Huo ni ukweli wenyewe, tatizo liko wapi? Maana kila mtu anajua, mimi sioni kama kuna siri hapa, na hili nitaendelea kulisema hata kama wenzangu hawataki," alisema Sitta.

Akizungumzia hoja kwamba kundi lake linaandaa mgombea urais, Sitta alisema katika mzozo wake na Lowassa hapendi kuzungumzia vyeo kwani msimamo wake ni kusimamia maadili.

"Mimi sipendi kuzungumzia vyeo sijui urais au sijui nini, ila nasimamia kwenye maadili na ndiyo maana tunausubiri kwa hamu muswada wa sheria wa kutenganisha siasa na biashara. Haiwezekani mtu umeingia kwenye siasa masikini, unatoka tajiri," alisema.

Sitta alilazimika kuzungumzia suala la urais baada ya kuwapo taarifa kuwa siri ya ugomvi wake na Lowassa ni kinyang'anyiro cha urais mwaka 2015.

Kwa mujibu wa habari hizo, Sitta na Lowassa ambao hadi sasa wameligawa Bunge na chama kwa misimamo yao, kila mmoja anataka rais ajae baada ya Rais Jakaya Kikwete kumaliza muda wake, kama si yeye, atoke kwenye kundi lake.

Kwa hali jinsi ilivyo kuhusu mzozo wa vingunge hao, Kamati ya Mzee Mwinyi ambayo inajipanga kuwakutanisha vigogo hao, inaweza kugonga mwamba kutokana na msimamo wa Sitta na kauli anazozitoa hivi sasa tangu kumalizika kwa kikao cha NEC mjini Dodoma.

Mbali ya kuifanya kazi ya Kamati ya Mwinyi kuwa ngumu, msimamo huo wa Sitta unamweka pabaya Mwenyekiti wa CCM taifa, Rais Jakaya Kikwete kufanya maamuzi magumu.

Tangu kuibuka kwa sakata la mkataba wa kifisadi kati ya Kampuni ya Richmond na TANESCO, uliosainiwa Juni 23, 2006, kisha kusababisha Lowassa kujiuzulu Uwaziri Mkuu na Rais Kikwete kuvunja baraza la mawaziri, CCM na Bunge hata serikali vimejikuta vikiingia katika mgawanyiko mkubwa.

Kundi la Lowassa ambalo linaundwa na watu wenye nguvu ya fedha, limekuwa na ushawishi mkubwa ndani ya CCM na hata bungeni, lakini Spika Sitta akiwa na kundi dogo la watu majasiri wanaojiita wapambanaji wa ufisadi wamesababisha msuguano ndani ya CCM na Bunge ambalo asilimia kubwa ya wabunge ni wa chama hicho tawala.

Mgawanyiko huo ndiyo ulioifanya NEC kuunda Kamati ya Mwinyi kutafuta suluhu. Hata hivyo, kamati hiyo iliyoanza kazi Agosti mwaka jana ilishindwa kumaliza tatizo hilo baada ya Spika kukataa suluhu na Lowassa.

Licha ya Spika kukubali kuizika hoja ya Richmond bungeni, bado msuguano uliendelea ndani ya chama na hivyo mkutano wa NEC uliofanyika hivi karibuni uliamua kuiongezea muda Kamati ya Mwinyi kwa kuitaka ichunguze kiini cha tatizo.

Chiligati Chiligati ambaye pia ni Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi, anasema kwa kawaida vikao vya NEC na CC ni vya siri na mjumbe yeyote hapaswi kutoa siri za vikao hivyo, Hivi anadhani watanzani tumesahau yeye Chiligati na Makamba walivyokuwa wanatoa habari za vikao vya CCM kwenye vyombo vya habari kuwa Sitta alikosea bungeni?

Hiyo siri inakuja pale anaposema Sitta. CCM iliwachukulia hatua Makamba na Chiligati?
 
Kweli siasa za Tanzani ni ajabu ajabu sana na za kukatisha tamaa sana
 
Aluta continua.....Mzee Sitta...tuanakuunga mkono....hata CCJ tutakuuonga mkono kama watakuletea za kuletwa. Chama Cha Mapinduzi....kilishapindua wananchi, huna haja ya kukingaángánia
 
Aluta continua.....Mzee Sitta...tuanakuunga mkono....hata CCJ tutakuuonga mkono kama watakuletea za kuletwa. Chama Cha Mapinduzi....kilishapindua wananchi, huna haja ya kukingaángánia
Hakuna kitu kipya hapa ila ni usanii wa kisiasa tu maana walifanya hvyo na wanaendelea kufanya hivyo
 
Mh. Sitta ninakuunga mkono kwa maamuzi yako ukweli lazima usemwe kwa rangi yake! hata kama usinge sema sasa ipo siku tungejua ukweli halisi " No matter how deep they bury the truth, it will always manage to surface"

Napenda kuchagiza ushujaa huu wa Sitta kwa maneno haya ya Solomon Mahlangu mpigania uhuru wa SA alisema na nakuu" Tell my people that I love them, and they must continue the struggle. My blood will nourish the tree that will bear the fruits of freedom" mwisho wa kunukuu. Mh Sitta we love you and your blood will nourish the tree that will bear the fruits of democracy!
 
"Huo ni ukweli wenyewe, tatizo liko wapi? Maana kila mtu anajua, mimi sioni kama kuna siri hapa, na hili nitaendelea kulisema hata kama wenzangu hawataki," alisema Sitta.


"Mimi sipendi kuzungumzia vyeo sijui urais au sijui nini, ila nasimamia kwenye maadili na ndiyo maana tunausubiri kwa hamu muswada wa sheria wa kutenganisha siasa na biashara. Haiwezekani mtu umeingia kwenye siasa masikini, unatoka tajiri," alisema.

Yes hapo nakubali kabisa - mtu anaingia kwenye siasa kunganga njaa au kutafuta utajiri hiyo si maadili kabisa.

Kuhusu wewe sita kukunyanganya kadi tuliipata - ila ni safi umeisema hadharani na wao wamesikia.

Swali Je utaweza kupigana ukiwa ndani ya chama chako? huoni kwamba hawa jamaa watakumaliza mapema tu - ukizingatika hii kauli imewakata maini kabisa hasa katibu wako mwenezi chiligati.

Mwisho bado watanzania tuna imani na wewe ingawa hatuna imani kabisa na chama chako mweshimiwa.
 
Elnino usijali uwezo wa Sitta kuendesha mapambano akiwa ndani ya CCM, unajua kidonda ni bora ukivunike kwa kitambaa cheupe ili kiweze kuonekana ili usaidiwe kipone, kuliko kukifunika kwa kitenge watu wasikione! Tunamuhitaji sana watu kama Sitta ndani ya CCM ili waweze kutusidia kuona mabaya ya CCM yanayoficha kwa kivuli cha CC na NEC
 
Sasa mbona alikuwa anayumbishwa kama vile gorori vile maana kila wakati akijitahidi ila anashindwa kufanya kitu
 
Josh mimi bado nina imani kubwa sana na Sitta na kundi lake, kumbuka hata boti inapokuwa safarini siku zote hupigwa na mawimbi makubwa hata abiria kuingia hofu kama itafika ufukweni salama lakini mwisho wa siku boti hutia nanga.

Usitishwe na misukosuko aliyopata Sitta, kinyango ulichochonga mwenyewe hakiwewezi kukutisha! CCM hawawezi kustamili kuona Sitta na kundi lake wanondoka ndani ya chama na hiyo ni Turufu kwa watanzania!
 
ngoja ninunue pop koni nikae sawa maana ya kusikia ..mwaka huu kuna mengi ya kusikia
 
Hapa sioni single mpya hizi ni zile zile zilipendwa. Tunataka tusikie yale ambayo hatujayasikia!!!!! Hasira za mkisi tijara ya mvuvi!!!
 
-Mimi naona kitu kimoja,kamata ya mzee mwinyi pia ni dhaifu hasa pale ambapo kuna mjumbe kama Msekwa ambae ana bifu na sitta

Pia msekwa yuko upande wa mafisadi

Hii kamati haitweza kufanya kazi

Naona pia sitta anataka kuwakasirisha CCM ili ahalalishe kufukuzwa na kwenda huko CCJ ,anataka kutoka na turufu ya upambanaji dhidi ya ufisadi.

Sasa najiuliza ujasiri wake huu mbona hakuonyesha wakati wa hitimisho la RICHMOND?

Anatakiwa atuombe radhi watanzania yeye pamoja na akina Mwakyembe!
 
Back
Top Bottom