Sitta amjibu Sumaye kuhusu mabehewa mabovu

Sitta amjibu Sumaye kuhusu mabehewa mabovu

...pamoja na kutuona malofa na wapumbavu wakumbuke bado tunaweza kufikiri na kupambanua mambo, wakae pembeni Lowassa atosha....
 
Uyu mzee sizani kama bongo yake ipo sawa,ata jana anatete shilika la ndege alijafa,alichosema eti marubani wapo ila ndege tunategemea mpaka december zitakuwa zimefika,ila hawa marubani wanafanya mazezi katika mashilika mengine,anatuletea siasa kipindi hiki,mimi sijamuelewa hebu nisaidieni alikuwa anamaanisha nini hao marubani w@naendesha nini,huyu si ndio amechakachua katiba,alafu mnasema huyu mloho wa madaraka sasa uyu mzee na umli huu na jinsi anavyonekana kuchoka akili kwa nini asipumzike.
 
Kwa hiyo ni kweli upo ufisadi kupitia mabehewa mabovu?naona kama kakiri uwepo wa ufisadi huo.
 
Magufuli ana utangazia umma kuwa ataifumua serekali yake,ataanzisha mahakama maalumu ya kushughulikia mafisadi wakati mafisadi ndio waliokazana kumpigia debe ili aende Ikulu.
 
Huyu Sitta asitufanye wajinga, this time around we are more than serious. CCM out.
 
Edward Lowasa awajibishwe, huyu ndo aliyehusika kwa kutoa maelekezo ya hayo mabehewa kukuu kununuliwa! Fisadi sana! Wala msimpe kura mpuuzeni!
Angalia ulichoandika dakika mbili zilizopita.unajua unachoandika?linganisha na hiki ulichoandika,wewe inaelekea ubongo una shida.kwa taarifa yako TRA ni shirika ambalo lipo chini ya wizara ya mawasiliano na uchukuzi.hivyo yupo waziri mwenye dhamana na suala hilo.usiropoke ovyo.
 
Mwaka huu watajibu yote. Na hili la waliosafirisha magunia 18 ya madawa ya kulevya kwenda South Africa hawajamaliza uchunguzi ili wawafungulie mashtaka hao wahusika?


Mamlaka za RSA zilimwachia huru Agness Masogange na kusema kuwa hazikuwa dawa za kulevya.
 
Mwaka huu mpaka wanye! Sumaye anapiga za chembe!!
 
Jamani hapa cha msingi ni kuitoa ccm madarakani tu hapo Oct 25 maana kila cku ni wizi tu. Tatizo ni ccm
 
Baada ya kufikishwa mahakamani hizo pesa zilizo potea itakuwaje?? Kama wezi wa EPA wameshinda kesi tutegemee nini kwenye hili?? Na muda wote serikali ilikuwa wapi hadi wasemwe majukwaani??
 
Twiga kupanda ndege je?? Hilo limekaaje?? Vituko kila kikicha
 
Uchunguzi huo utakamilika baada ya muda upi? na unafanyaje uchunguzi wakati muhusika bado yuko ofisini? tuache utoto
 
Kuna watu watajitoa kwenye makundi ya kampeni. Magazeti nchi hii yanafanya kazi gani?
 
Wajibu pia kuhusu hili ferry bovu lililotengenezwa 1978 ambalo limeshindwa kwenda Bagamoyo na sasa linaoza pale bandarini. Hili lilisimamiwa na Magufuli
 
Sumaye anashangaza sana na ile heshima kidogo aliyokuwa nayo sasa itapotea!

1) Alichaguliwa Simply kwa uwezo wake mdogo, Mkapa hakutaka, Malechela type au Msuya type ya Prime ministers wenye haiba za Kisiasa na Independent.

2) Analaumu serikali ya Sasa kuwa imeshusha kiwango cha elimu, Wakati ni yeye aliyekuwa mtendaji mkuu wa serikali mwaka 1998 wakati mitihani ya kidato cha nne ikivuja kama njugu, hadi kufikia hatua za Mitihani kubandikwa kwenye mitisimu.

3) Anazungumza Rushwa katika serikali hii, wakati kumbe yeye alipokuwa Waziri mkuu na kiongozi wa shughuli za serikali bungeni, Walitunga Sheria ya TAKRIMA ambayo ni rushwa tupu.

4) Anazungumzia kuhusu Ufisadi, Wakati yeye akiwa Waziri Mkuu tulishuhudia ufisadi mkuu kwenye EPA, Rada, Meremeta, Ndege ya Raisi, Kiwira

5) Anazungumzia kuhusu Haki na Uonevu wakati yeye alipokuwa Waziri mkuu nchi yetu ilizalisha Wakimbizi wa kisiasa, na Mauaji ya Raia watafuta haki huko Zanzibar, ni nani aliyesahau mauaji ya Wazanzibar January ya Mwaka 2001?

Huyu ana Uhalali gani wa kusimama kumnadi mgombea yeyote yule kwa muktadha wa Uadilifu, haki na uwezo?
 
Hao aliowataja wanatilewa kafara, lazima kuna wengine.
 
Hebu Sitta aache kutufanya Watanzania wote majuha. Hivi Mkurugenzi Mtendaji pekee na management team yake (kwenye shirika ambalo ni la umma lenye Waziri mwenye dhamana? pamoja na bodi yake ya Wakurugenzi?) ati ana ubavu wa kuidhinisha ununuzi wa mabehema yenye thamani ya TZ shs. 220 billion bila idhini ya Waziri wake? bodi yake?... Halafu bila ya kupitia na kushindanishwa bodi ya manunuzi?

Common Sitta!..talk to us with your sense!

Wewe ndio hujui kuheshimu professionalism. Nenda ikalale ni wazi hujakomaa kuhoji masuala kwa kijenga hoja katika misingi ya kitaalam na kisheria. UNAKURUPUKA
 
Na kama halikusemwa ..ndo limepita ccm bwana shikwa pabaya sana
 
Back
Top Bottom