Mwanahabari Huria
JF-Expert Member
- Jan 29, 2025
- 394
- 258
MASHIRIKA YANAYOCHELEWESHA MIRADI YA PPP SASA KUWEKWA KITIMOTO BUNGENI DODOMA
===
SPIKA ZUNGU amesema kuwa baadhi ya miradi ya PPP imekwama kwa muda mrefu, hali inayosababisha kupungua kwa mapato ya serikali. Amesema kutokana na hilo, amemwagiza Mtendaji Mkuu wa PPP kuwasilisha orodha ya miradi yote ya PPP iliyokwama katika kikao cha pamoja na Kamati ya Bajeti tarehe 25 Juni 2026 kuanzia saa saba mchana mjini Dodoma Bungeni, ambapo wadau wote wanaohusika na miradi hiyo watatakiwa kuhudhuria.
Ameongeza kuwa amemuomba Mhe. Mwanasheria Mkuu (AG) kuchunguza kama sheria za miradi ya PPP bado ni ngumu, na iwapo ni hivyo, watendaji wa PPP wakae pamoja na kuzipitia ili PPP iweze kuchangia maendeleo ya taifa.
Spika Zungu amekumbusha kuwa Bunge lililopitisha Dira ya Taifa kwa kauli moja lilikubaliana kuwa asilimia 70 ya utekelezaji wake utafanywa na sekta binafsi, hivyo sekta binafsi inahitaji mazingira mazuri ya kufanya kazi. Amesisitiza kuwa masilahi ya taifa lazima yawekwe mbele, lakini pia ni muhimu kuwa na sheria ambazo hazitawafanya wawekezaji washindwe na kuondoka.
Soma: David Kafulila: Sasa PPP Tanzania tumefikisha miradi ya TZS 11 TRL na 80% ni ya awamu ya 6
Aidha, amesema kuwa mapato ya ndani ya serikali badala ya kutumika kwenye miradi mikubwa ya maendeleo, yatumike kwa ustawi bora wa wananchi — kama kuwajengea makazi bora, kupandisha mishahara, kuboresha huduma za afya, kutoa elimu bora, na mambo mengine yanayolenga kuwasaidia wananchi.
===
SPIKA ZUNGU amesema kuwa baadhi ya miradi ya PPP imekwama kwa muda mrefu, hali inayosababisha kupungua kwa mapato ya serikali. Amesema kutokana na hilo, amemwagiza Mtendaji Mkuu wa PPP kuwasilisha orodha ya miradi yote ya PPP iliyokwama katika kikao cha pamoja na Kamati ya Bajeti tarehe 25 Juni 2026 kuanzia saa saba mchana mjini Dodoma Bungeni, ambapo wadau wote wanaohusika na miradi hiyo watatakiwa kuhudhuria.
Ameongeza kuwa amemuomba Mhe. Mwanasheria Mkuu (AG) kuchunguza kama sheria za miradi ya PPP bado ni ngumu, na iwapo ni hivyo, watendaji wa PPP wakae pamoja na kuzipitia ili PPP iweze kuchangia maendeleo ya taifa.
Spika Zungu amekumbusha kuwa Bunge lililopitisha Dira ya Taifa kwa kauli moja lilikubaliana kuwa asilimia 70 ya utekelezaji wake utafanywa na sekta binafsi, hivyo sekta binafsi inahitaji mazingira mazuri ya kufanya kazi. Amesisitiza kuwa masilahi ya taifa lazima yawekwe mbele, lakini pia ni muhimu kuwa na sheria ambazo hazitawafanya wawekezaji washindwe na kuondoka.
Soma: David Kafulila: Sasa PPP Tanzania tumefikisha miradi ya TZS 11 TRL na 80% ni ya awamu ya 6
Aidha, amesema kuwa mapato ya ndani ya serikali badala ya kutumika kwenye miradi mikubwa ya maendeleo, yatumike kwa ustawi bora wa wananchi — kama kuwajengea makazi bora, kupandisha mishahara, kuboresha huduma za afya, kutoa elimu bora, na mambo mengine yanayolenga kuwasaidia wananchi.