Huyu mzee pamoja na unafiki wake, lakini hili la uspika wa makinda kuteuliwa na Rostam liko wazi kabisaa na wala halina ubishi, kwani hata Makinda mwenyewe alishakiri kwamba Rostam alimfuata akamshauri agombee uspika.
Walio muweka makinda ndio walio muweka sita, hapo vipi? concln na yeye aliweka na kutolewa na mafisadi. Sasa basi aliyekuwa rafiki wa mafisadi naye ni fisadi.
Naamini kwa hapa alipofikia siku zake ccm zinahesabika! Jamaa hawatakaa kimya tena, ila tusubiri tuone. CDM tunaanza kujiandaa na uchaguzi maana jamaa lazima wamtose.
Kikwete atajifanya kafanya maamuzi magumu.
Sitta amtuhumu Kubenea kununuliwa na mafisadi.
adai ameitwa kujiunga na vyama vingi vya siasa na kukiri kuwa na mazungumzo.
asema kuna madudu ambayo mwakyembe amefanyiwa na anahisi ni sumu.
adai pia kuwa chama chake (CCM) kimemfanyia mambo mabaya hata kwa kutamkwa
adai kupigwa zengwe kwenye ugombea wa spika kwa kubadilishwa utaratibu ghafla wa kutakiwa mwanamke ndiye agombee
Adai hawezi kususa nafasi yake kwa sababu ya kuisema serikali na atendelea kuisema na itakapofikia hatua ya kuwekewa maneno mdomoni basi atafanya maamuzi mengine na kupiga magoti ili Mungu amuoneshe pa kwenda
aisifu chadema kwa jinsi kinavyojipanga kwenye uchaguzi hasa wa igunga na kuifanya ccm kuingia ICU
Adai ccm inahitajika kufanya marekebisho kabla ya kiama na kuacha uchafu uliojaa ndani yake
Ashangaa vijana kutofanya maandamano kupinga hali yeyote mbaya nchini kwa uzalendo
Aunga mkono maandamano kupinga ufisadi wa DOWANS