Sitta ajitosa mgogoro wa Umeya Arusha

Sitta ajitosa mgogoro wa Umeya Arusha

Lini?Kama ni Leo kumbuka ni Jumapili na Pale Kanisani kuna section ya Tutakiane Amani,Umeshawahi ona wanaotakiana amani?Nakuhakikishia ilikuwa ni sehemu ya Ibada Japo yaweza kuwa Imefanyika Nyumbani,Kumbuka askofu au Padre anaweza fanya Ibada popote.Hamna amani na MAGAMBA wewe,Mpaka waondoke Magogoni ndio tutajua Amani imepatikana!!!😛oa

Hilo nalo neno
 
Mbele ya Askofu mkuu Josephat Leburu, Mbunge wa Afrika mashariki Mh. Samweli Sitta .Mbunge Lema ashikana mikono na mkuu wa mkoa wa Arusha na Meya wa Arusha. Lema akihaidi hadharani hana chuki na mtu yeyote binafsi ila hata choka kupigania haki kama haki haita tendeka katika jamii. Amemwomba Mbunge huyo wa Afrika Mashariki kumaliza mgogoro huo mapema. Wadau toeni mchango wenu katika hili.
Hapo kwenye nyekundu jamaa kangea point!
 
Huyu jamaa amefanya miradi mingi sana ya kanisa hilo. Lakini ni kama waumini hawakumbuki. Wanachokumbuka ni kwamba yeye ni sababu ya mauaji ya ndugu zao na wale waliopata majeraha na vilema. Ndio maana hawakumshangilia.

Anyway, baba Askofu amezungumza neno angalau wakapeana mikono! Ila damu zilizomwagika ni jinamizi litakalomwandama kwa muda mrefu sana!
 
Amebana ameachia. Ccm ni chama dume.
 
anachong'ang'ania ni kipi? Si aachie ngazi tu?
 
title na ulivyoviandika havishabihiani kabisa
Hata hivyo bado tunaombea sana amani ipatikane Arusha Kama alivyosema mkuu tatizo hata yeye halijui maana aliagiza wakae walimalize lakini kuna wachache kwa masilahi yao hawataki

Wa upande gani magamba cdm?
 
hicho kichwa cha habari sijakielewa...! Kushikana mikono haimaanishi ndiyo mmepatana. Ikulu watu hawakuishia kushikana mikono tu...watu walichekeana kama ngedere na kuna wakati Mkulu mwenyewe alikuwa anatoa huduma za juice kama beki tatu....je walipatana?

nilikuwa nimenuna siku nzima lakini post yako imenivunja mbavu.
 
Hapo Lema yuko sawa, kwani ujumbe wake unasisitiza kuwa amani ya kweli ni tunda la haki. Hivyo haki ndio itakayosababisha amani katika jamii. Hata neno la Mungu katika biblia linasisitiza kuwa 'hapana amani kwao watendao maovu'.
.
 
N series nashukuru kwa kufafanua!!Umenisoma kabisa !!
Wananchi wameshamkataa,angetoka tu!!Yeye sio chaguo la Mungu!!!
 
Exegate kidogo hichi kifungu cha mandiko. Tunashindwa kuelewa kwamba ni nani hasa alifunga hapa duniani ni wana wa Arusha au ni serekali ya CCM. Iliyomteua diwani huyo kuwa meya wakitumia kivuli cha uchaguzi geresha, a.k.a usanii wa kishamba.
:juggle:Acha kung'ang'ania lugha za watu wakati hujui hata unaandika nini. Tunashindwa kuelewa kwamba hilo neno (highlighted) kwanza ni lugha gani na pili linahusiana vipi na maelezo mengine yanayofuata. Tumia kiswahili, lugha yetu ya taifa ni nzuri tu.
 
:juggle:Acha kung'ang'ania lugha za watu wakati hujui hata unaandika nini. Tunashindwa kuelewa kwamba hilo neno (highlighted) kwanza ni lugha gani na pili linahusiana vipi na maelezo mengine yanayofuata. Tumia kiswahili, lugha yetu ya taifa ni nzuri tu.
Tumemuelewa, ni typo tu hiyo.
Sio lazima utumie kiswahili kwa kila neno, usiharibu topics za watu hapa!......
Hlo tu.:mimba:
 
:juggle:Acha kung'ang'ania lugha za watu wakati hujui hata unaandika nini. Tunashindwa kuelewa kwamba hilo neno (highlighted) kwanza ni lugha gani na pili linahusiana vipi na maelezo mengine yanayofuata. Tumia kiswahili, lugha yetu ya taifa ni nzuri tu.

Hizo lugha unazoziita ni lugha za watu, kwani wewe ulikuwa unataka lugha za nyani. Ujinga mzigo!!! Usicho kijua waachie wenye kuijua!!!
 
Mimi nilikuwepo na habari ilikuwa kama ifuatavyo , Mb Arusha mjini ( Lema) alipewa mic na Mh Sitta asalimie wananchi na kuchangia harambee hiyo na Bwana Lema , alimtambua Meya feki kama Diwani wa Olorieni na siyo meya huku akisisitiza kuwa yeye hana ugomvi binafsi na Meya isipokuwa mfumo uliompata meya unamfanya meya huyo kuwa katili wa haki za binadamu na utu .

Nukuu Lema " Mh Baba Askofu na mgeni rasmi mimi kama mbunge nitakuwa mtu waq ajabu kama nitashindwa kusimamia haki mbele ya madhabau hii ya Mungu na hivyo ukweli unabaki kuwa Arusha mjini hakuna Meya na mimi mbunge simtambui meya ila natambua uwepo wa Diwani wa Kata ya Olorieni bwana Gaudensi Lyimo.

Naomba ileweke kuwa mimi sina ugomvi binafsi na Bwana Gaudensi na hata akitaka kunywa chai kwangu namkaribisha sana isipokuwa nimuombe tena Mh Sitta kama mzee wetu kwenye siasa muda mrefu awaambie wakubwa wengine hasa waziri mkuu kwamba tatizo hili si afya kwa Arusha lakini hata hivyo hatutarudi nyuma kupigania haki iliyoporwa katika uchaguzi wa umeya na kama kuna mtu anakerwa na mgogoro wowote unaotafuta hakli basi yeye aendelee kukerwa na sisi kwetu ni baraka kwani haki tutaitafuta by the ballot or the bullet.

Bwana Gaudensi alivyotaka kumjibu Lema ndipo waumini wote wakaanza kumzomea Bwana Lyimo, na Mh Sitta akahaidi kusaidia mchakato wa mazungumzo yalioanzishwa na Bwana Pinda na Mbowe kufikia tamati kabla ya 2012.
 
Back
Top Bottom