Sitosahau siku ambayo tulifika Mbeya saa saba mchana. Njia nzima nilitubu dhambi zangu

Chizi Maarifa

JF-Expert Member
Jul 29, 2013
10,471
23,744
Miaka ya 90. Sikumbuki vizuri ilikuwa Bus gani kati ya Matema au Safina. Tulitoka Dar saa 12 asubuhi kwa mara ya kwanza naelekea Mbeya.

Tulitoka na hilo Bus tukavuka mataa tukaitafuta Kimara Mbezi tukakamata barabara sasa ya Mkoani huko mbele. Hapo ndo nilianza kuona milango ya mbinguni ikifunguka na kufunga.

Sikuwahi kuona Dereva anapiga mti/mpini kama yule jamaa.Gari ilikuwa inakimbia sijapata kuona duniani. Abiria tulikuwa tunaogopa hata kukohoa au kupiga chafya kwa wasiwasi kuwa unaweza mtingisha dereva ukasababisha ajali.

Dereva alikuwa anapiga mkono/mpini balaaa njia nzima nikawa nasali nikitubu dhambi zangu zote na kuomba msamaha maana sikuwa na hakika kama tungefika salama. Nilikumbuka mapambio mbalimbali na nyimbo za kuelezea Ukuu wa Mungu.

Yeye dereva alikuwa kimya akihesabu tu gear zake kama vile anasoma Rozari au Tasbihi na wakati mwingine akibadilishana maneno mawili matatu na konda.

Alipiga mpini kiroho mbaya/ile kinyama sana. Saa saba na robo anaanza kupangua gia kaingia town tupo Mbeya.Aisee siwezi sahau safari ile nilikuwa naona mbingu zinafunguka na kufunga. Nawakumbuka ndugu na jamaa zangu huku machozi ya kitoka ila tulifika.

Ghafla tuliona gari ya Polisi imetuunganishia mitaa fulani hivi kumechangamka.Dereva hakusimama akaendelea kupiga mpini mpaka tumefika stand ....

Tulikuja shtuka tumefika stand watu wamejaaa hawaamini.Nadhani jamaa aliweka historia haikuwahi kutokea hapo nyuma. Tumefika stand bus imesimama akazipangua gia mpaka zero akaiacha gari inanguruma yeye kaegamia usukani. Baada ya dakika kadhaa Polisi wakafika. Wakamfuata dereva mbele wakamwambia ashuke wakamtia pingu. Wakaondoka naye.

Nakumbuka mimi nilifika nyumbani kwa wenyeji wangu wanatenga meza wale chakula cha mchana.lile bus ilikuwa lielekee Kyela alienda nalo dereva mwingine yule jamaa walimweka ndani.

Najiuliza yule dereva aliendelea na upigaji ule wa mpini? Na je kwa sasa yupo wapi?
 
Mzee spidi kama hizo zilinikuta kwenye magari ya IT. Nilishuka njiani kwenye kijiji nikamwambia dereva wewe endelea tu. Na spidi hizo ndio mawazo yananijia naangalia kama kuna bolt, bati karibu na kichwa nawaza hivi impact ikitokea nikapiga kichwa hapa si balaa. Anyway Mungu anatulinda sana.
 
Sio Matema Beach wala Safina iliyoingia Mbeya SAA saba, ni Scania 113 TZH 710 ikiendeshwa na Giriki na kondakta wake alikuwa Ally Bonge.
Nilikuwa ndani ya hiyo gari kuanzia inaanza safari Mnazi Mmoja hadi Mbeya. Na Mimi nilikuwa ni mdau Mkubwa sana wa mabasi enzi hizo Ofisi yangu ukiwa jirani na Ofisi ya mabasi ya Embakassy.
Dar moro mlitumia muda gani....?

Na iyovi mlipasua zile kona na speed ipi mdau..?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Miaka ya 90. Sikumbuki vizuri ilikuwa Bus gani kati ya Matema au Safina. Tulitoka ubungo saa 12 asubuhi kwa mara ya kwanza naelekea Mbeya.
Tulitoka na hilo Bus tukavuka mataa tukaitafuta kimara mbezi tukakamata barabara sasa ya Mkoani huko mbele.
Sikuwahi kuona Dereva anapiga mti kama yule jamaa.gari ilikuwa inakimbia sijapata kuona duniani. Abiria tulikuwa tunaogopa hata kukohoa au kupiga chafya kwa waswas kuwa unaweza mtingisha dereva ukasababisha ajali.
Dereva alikuwa anapiga mkono balaaa....njia nzima nikawa nasali nikitubu dhambi zangu zote na kuomba msamaha maana sikuwa na hakika kama tungefika salama. Yeye dereva alikuwa kimya akihesabu tu gear na wakati mwingine akibadilishana maneno mawili matatu na konda.
Alipiga mpini kiroho mbaya saa saba na robo tupo Mbeya.... Ghafla tuliona gari ya Polisi imetuunganishia mitaa flani hivi kumechangamka.dereva hakusimama.akaendelea kupiga mpini mpaka tumefika stand ....
Tulikuja shtuka tumefika stand watu wamejaaa hawaamini....nadhani jamaa aliweka historia haikuwahi kutokea hapo nyuma. Tumefika stand bus imesimama...baada ya dakika kadhaa Polisi wakafika. Wakamfuata dereva mbele hakuwa ameshuka.wakamwambia ashuke wakamtia pingu.
Nakumbuka mimi nlifika nyumbani kwa wenyeji wangu wanatenga meza wale chakula cha mchana.lile bus ilikuwa lielekee Kyela alienda nalo dereva mwingine yule jamaa walimweka ndani.
Najiuliza yule dereva aliendelea na upigaji ule wa mpini? Na je kwa sasa yupo wapi kwa sasa?
Hii umesinuliwa hukuwemo kwenye gari, hamna Tawaqal iliyokuwa ikienda Kyela, Tawaqal walikuwa wana basi za kuishia Mbeya na nyingine Tunduma
 
Sio Matema Beach wala Safina iliyoingia Mbeya SAA saba, ni Scania 113 TZH 710 ikiendeshwa na Giriki na kondakta wake alikuwa Ally Bonge.
Nilikuwa ndani ya hiyo gari kuanzia inaanza safari Mnazi Mmoja hadi Mbeya. Na Mimi nilikuwa ni mdau Mkubwa sana wa mabasi enzi hizo Ofisi yangu ukiwa jirani na Ofisi ya mabasi ya Embakassy.
shkamoo ankal buji! Si Kwa kumbukumbu hizi! Yaelekea darasani ulikua kipanga wa kukariri!
 
Sio Matema Beach wala Safina iliyoingia Mbeya SAA saba, ni Scania 113 TZH 710 ikiendeshwa na Giriki na kondakta wake alikuwa Ally Bonge.
Nilikuwa ndani ya hiyo gari kuanzia inaanza safari Mnazi Mmoja hadi Mbeya. Na Mimi nilikuwa ni mdau Mkubwa sana wa mabasi enzi hizo Ofisi yangu ukiwa jirani na Ofisi ya mabasi ya Embakassy.
90 ulikuwa muajiriwa 😀
 
Dar moro mlitumia muda gani....?
Na iyovi mlipasua zile kona na speed ipi mdau..?
Sent using Jamii Forums mobile app
Tena enzi hizo ile barabara ilikuwa ni nyembamba.
Ile njia ilikuwa na madereva vichaa sana, mwingine ni Henry Mwamtobe au Henule.
Giriki Siku hizi anaendesha magari ya mafuta, ila henule sijui yuko wapi? Mara ya mwisho nilipanda gari yake akiendesha basi za kampuni ya Zainabs, Volve V8 engine
 
Sio Matema Beach wala Safina iliyoingia Mbeya SAA saba, ni Scania 113 TZH 710 ikiendeshwa na Giriki na kondakta wake alikuwa Ally Bonge.
Nilikuwa ndani ya hiyo gari kuanzia inaanza safari Mnazi Mmoja hadi Mbeya. Na Mimi nilikuwa ni mdau Mkubwa sana wa mabasi enzi hizo Ofisi yangu ukiwa jirani na Ofisi ya mabasi ya Embakassy.
Kwahiyo ni kweli hilo bus lilifika Mbeya hii hii yenye milima ya kitonga + kona kona za morogoro SAA 7???, akii nilidhani mleta Uzi anatupa chai. Au ilikua helicopter huwenda mmesahau ,si bus

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Miaka ya 90. Sikumbuki vizuri ilikuwa Bus gani kati ya Matema au Safina. Tulitoka ubungo saa 12 asubuhi kwa mara ya kwanza naelekea Mbeya.

Tulitoka na hilo Bus tukavuka mataa tukaitafuta kimara mbezi tukakamata barabara sasa ya Mkoani huko mbele.

Sikuwahi kuona Dereva anapiga mti kama yule jamaa.gari ilikuwa inakimbia sijapata kuona duniani. Abiria tulikuwa tunaogopa hata kukohoa au kupiga chafya kwa waswas kuwa unaweza mtingisha dereva ukasababisha ajali.

Dereva alikuwa anapiga mkono balaaa....njia nzima nikawa nasali nikitubu dhambi zangu zote na kuomba msamaha maana sikuwa na hakika kama tungefika salama. Yeye dereva alikuwa kimya akihesabu tu gear na wakati mwingine akibadilishana maneno mawili matatu na konda.

Alipiga mpini kiroho mbaya saa saba na robo tupo Mbeya.... Ghafla tuliona gari ya Polisi imetuunganishia mitaa flani hivi kumechangamka.dereva hakusimama.akaendelea kupiga mpini mpaka tumefika stand ....

Tulikuja shtuka tumefika stand watu wamejaaa hawaamini....nadhani jamaa aliweka historia haikuwahi kutokea hapo nyuma. Tumefika stand bus imesimama...baada ya dakika kadhaa Polisi wakafika. Wakamfuata dereva mbele hakuwa ameshuka.wakamwambia ashuke wakamtia pingu.

Nakumbuka mimi nlifika nyumbani kwa wenyeji wangu wanatenga meza wale chakula cha mchana.lile bus ilikuwa lielekee Kyela alienda nalo dereva mwingine yule jamaa walimweka ndani.

Najiuliza yule dereva aliendelea na upigaji ule wa mpini? Na je kwa sasa yupo wapi kwa sasa?
Hyo ilkua hatariii mkubwaa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwahiyo ni kweli hilo bus lilifika Mbeya hii hii yenye milima ya kitonga + kona kona za morogoro SAA 7???, akii nilidhani mleta Uzi anatupa chai. Au ilikua helicopter huwenda mmesahau ,si bus
Sent using Jamii Forums mobile app
Ni kweli.
Mabasi ya kawaida mbeya yalikuwa yanafika SAA Tisa na SAA kumi, Embakassy ilikuwa inafika SAA 12 na nauli yake ilikuwa kati ya buku saba na elfu tano. Watu walikuwa hawalipendi linachelewa sana
 
kweli tutasubiri sana nchi yetu,kwani kutoka Dar hadi Mbeya ni km ngapi?sio 800km ?sasa hizi ni swala la ajabu bus kuondoka Dar saa 6am na kuwasili Mbeya saa 13:30?,inabidi mtoa hoja one day nikupe lift kutoka Windhoek (Namibia) hadi katima mulilo(mpakani na Zambia)ni kama 1400km na tunatambaa kwa masaa 12tu,na sio speed tu bali barabara imetengenezwa kwa viwango na inaangaliwa ili isiharibike,sasa sisi tunajenga barabara safi kuanzia pale nje kidogo ya mbeya hadi few kabla ya iringa na inaiwekea matuta!!wapi uliona matuta ndani ya Freeways???;wakati nchi ina heshima na adabu ilikuwa bus ya kampuni ya taifa ya KAMATA ikiingia pale Songea wananchi wanashangilia hasa inapokuwa bado ipo bombambili kabla ya kupanda kile kilima kwa mkuu wa mkoa(kumbuka ni CD kipindi hicho na tope za lukumburu zimepakaza bus Zima),tuanze kuishi kama wenzetu Dar to Iringa ni kama 500km huu ni mwendo wa 6hrs pamoja na mapumziko!!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom