Sitathubutu kuoa wala kupata mtoto

Sitathubutu kuoa wala kupata mtoto

Habarini,

Mimi ni mtu mzima na nina Akili timamu nimefikia maamuzi ya kutokuja kuoa wala kuwa na moto maisha yangu yote! Sio kwamba sina uwezo wa kuoa lahasha nina uwezo wa kuoa hata wanawake wa 5 na kupata watoto chungu nzima lakini nimekaa nimetafakari sana nimeamua kufikia mamuzi hayo.

Baada ya kuteseka sana na mapenzi ya umri wetu, baada ya kushuhuduia ujinga na usaliti wanao fanya akina dada wa miaka hii, mateso ya kwenye ndoa wanayo yapata watu na adha zingine chungu nzima mimi nimefikia hatua kutotaka kuoa wala kupata mtoto

Nina kazi yangu nzuri tu ambayo naweza kumudu kulea familia hata ya watu 10 lakini kamwe sitokaa kudhubutu kuoa na kuwa na mtoto na sitaki utani katika hili! Nimesh ichosha sana akili yangu katika mapenzi na nimeshuhudia mengi sana katika mapenzi sasa bahati mbaya yote niliyokuwa nayashuhudia ni ya usaliti na mateso katika ndoa na hii inatoka na akili walizonazo dada zetu.

Hivyo sina mda wa kukaa kuchambua kupata huyu anafaa huyu hafai huo mda sina nitahakikisha nafanya kila niwezalo kwa kutumia uwezo wangu wote niwe na maisha mazuri miaka yote! Jasho langu watafaidi wadogo zangu na wazazi wangu, nitapigania kufa na kupona katika kusaka pesa! Katika kumshukuru Mungu kwa pale alipo nifikisha nita adapte mtoto mmoja yatima nitamsomesha na kuishi naye miaka yote tena shule nzuri nitampeleka! Nyumba yangu itakuwa na mfanyakazi mmoja na mtoto mmoja na mimi basi.

Dada yoyote hatadhubutu kuja kwangu kwa namna yoyote ile na wala asijipendekeze kuja kwangu labda awe hana uwezo wa kuzaa ambao hospitalini wamethibitisha ili asije kunikeletea vimimba vya uwongo na ukweli.

Sitaki stress siku hata nikiwa sina hata mia nitaishi kwa amani hakuna wakunisumbua kuliko kuwa na mke sa nne usiku kakuomba hela unamwambia sina mnalala wote sa kumi na mbili asubuhi anakuomba tena hela hivi usiku anadhani alilala peke ake? Mimi nilikuwa kutafuta pesa? Mwisho wa siku mnaishia kugombana na kununiana hiyo mimi hapana sitaki kabisa.

Mwisho haya ni maamuzi binafsi nimeamua kushare nanyi.
Kaka nimependa maamuz yako kama ulivyoeleza,,,naamin ktk maamuz ya mtu,,,,,
 
Kuoa haihusian na uwezo wa kulisha familia kumi.... Unaweza usioe na ukawa na uwezo wa kulisha mapera watu mia tano... Ni suala la kuwepo na miti ya mipera tuuu.
 
Usijifunze kwa walioshindwa maana hata hapo ulipo wapo walioshindwa kufika.
Ichi kineno chako kimenifanya nikitafakari lkn nimeshindwa kuelewa,ni kineno kidogo sana lkn ukisoma kwa makini utagundua ni neno lenye maana kubwa saaaaaana na hakuna mtu wakuweza kufikiri akapata muongozo wake leo ama kesho,,
 
Ichi kineno chako kimenifanya nikitafakari lkn nimeshindwa kuelewa,ni kineno kidogo sana lkn ukisoma kwa makini utagundua ni neno lenye maana kubwa saaaaaana na hakuna mtu wakuweza kufikiri akapata muongozo wake leo ama kesho,,
Kwa namna ulivyoeleza unaonekana umeelewa kwa sehemu
 
Kwa hiyo unataka tukubembeleze uoe? Kwanza nani alikuambia kuna uhusiano wowote kati ya kuoa na kupata watoto?
 
Habarini,

Mimi ni mtu mzima na nina Akili timamu nimefikia maamuzi ya kutokuja kuoa wala kuwa na moto maisha yangu yote! Sio kwamba sina uwezo wa kuoa lahasha nina uwezo wa kuoa hata wanawake wa 5 na kupata watoto chungu nzima lakini nimekaa nimetafakari sana nimeamua kufikia mamuzi hayo.

Baada ya kuteseka sana na mapenzi ya umri wetu, baada ya kushuhuduia ujinga na usaliti wanao fanya akina dada wa miaka hii, mateso ya kwenye ndoa wanayo yapata watu na adha zingine chungu nzima mimi nimefikia hatua kutotaka kuoa wala kupata mtoto

Nina kazi yangu nzuri tu ambayo naweza kumudu kulea familia hata ya watu 10 lakini kamwe sitokaa kudhubutu kuoa na kuwa na mtoto na sitaki utani katika hili! Nimesh ichosha sana akili yangu katika mapenzi na nimeshuhudia mengi sana katika mapenzi sasa bahati mbaya yote niliyokuwa nayashuhudia ni ya usaliti na mateso katika ndoa na hii inatoka na akili walizonazo dada zetu.

Hivyo sina mda wa kukaa kuchambua kupata huyu anafaa huyu hafai huo mda sina nitahakikisha nafanya kila niwezalo kwa kutumia uwezo wangu wote niwe na maisha mazuri miaka yote! Jasho langu watafaidi wadogo zangu na wazazi wangu, nitapigania kufa na kupona katika kusaka pesa! Katika kumshukuru Mungu kwa pale alipo nifikisha nita adapte mtoto mmoja yatima nitamsomesha na kuishi naye miaka yote tena shule nzuri nitampeleka! Nyumba yangu itakuwa na mfanyakazi mmoja na mtoto mmoja na mimi basi.

Dada yoyote hatadhubutu kuja kwangu kwa namna yoyote ile na wala asijipendekeze kuja kwangu labda awe hana uwezo wa kuzaa ambao hospitalini wamethibitisha ili asije kunikeletea vimimba vya uwongo na ukweli.

Sitaki stress siku hata nikiwa sina hata mia nitaishi kwa amani hakuna wakunisumbua kuliko kuwa na mke sa nne usiku kakuomba hela unamwambia sina mnalala wote sa kumi na mbili asubuhi anakuomba tena hela hivi usiku anadhani alilala peke ake? Mimi nilikuwa kutafuta pesa? Mwisho wa siku mnaishia kugombana na kununiana hiyo mimi hapana sitaki kabisa.

Mwisho haya ni maamuzi binafsi nimeamua kushare nanyi.
Pole sana kwa yaliyokukuta....! Lakini tafadhali uwaombe wazazi wako msamaha kwa kuwakosoa kuwa walifanya vibaya kuoana na kukuzaaa wewe...!
Again take note that;
  1. It is better to expect "the good" and getting "the very good" than expecting "the most excellent", and getting "the excellent". So, never look for the most perfect partner, because you will end up crying in your lifetime....!
  2. The most complex animal in the world is the human being....! So, Never trust a human being, even yourself because only LORD deserves to be trusted...! And only fools may trust a human being....!
  3. Whenever you find right to change your mind, come back and tell us so and why, as you did now.....!
 
eti mfanyakazi wa ndani na mtoto....kama sio kutuzuga nini.....unataka umle mzigo mfayakazi wa ndani af unadai hutaoa....
 
Huyu jamaa yuko radhi akasomeshe na kulea mtoto wa kuasili/ adapt kuliko kuhonga (au kuombwa hela na) mwanamke wake na akazaliwa watoto wake. Si bure ana jambo.
 
Hongera sana mkuu, Kila mara nasema kuwa hakuna umuhimu wowote wa kuoa zaidi ya kupata stresses.

Ila jitahidi upate mtoto na mwanamke yeyote tu halafu umlee mtoto na mama yake bila mkataba wowote wa kindoa.

Hongera sana.
 
Kwa experience yangu Na misukosuko niliwai kupitia kuna vitu viwili nimejifunza.

Kuna wife type na Girl friend type.
Hawa ni viumbe wawili tofauti sana kwenye hii Dunia.
Wanawake ni viumbe ambavyo wameumbwa Na tamaa iwe ya kimwili au ki Hali.
Kitu ambacho nimejifunza ni mpaka mwanamke atake mwenyewe kubadili status ndio atabidi Ila sio wewe umbadilishe kutoka Girl Friend kuwa Wife.

Wife material Waziri ni wale ambao walisha experience marriage halafu for some reason wakatoka Na itakuwa better zaidi kama akiwa Na mtoto au hata wawili, age kuanzia 25 kwenda mbele hadi 35. Kwani Ile haina makombo.

Hapo utaenjoy ndugu. Ila wasichana wa mjini watakuuwa.
 
Yalishawahi kunikuta maisha kama yako,pesa ndiyo iliyokuwa inanipa kiburi cha kuongea kama unavyoandika,nilikuwa na mlinzi,madereva wawili,mpishi aliyekuwa ananipikia,tena nilimtoa hotelini baada ya kupendezewa na chakula nilichokuwa nakula pale,mwisho wa siku niliishiwa kila kitu,nikaanza kujificha rafiki zangu wasinione,wafanyakazi walinishitaki,maana nilishindwa kuwalipa mishahara,wanawake wale wa zamani niliokuwa nawakataa nikawa nawakimbia,mwisho wa siku nilikuja kusaidiwa na mwanamke ambaye,alinipa chakula,nikawa nalala kwake,yaani nikiwa sina hata kitu,analipa kodi,ananunua chakula,ananinunulia mpaka nguo.Basi ikabidi nimuowe,maisha yangu yameludi upya kwa kushilikiana na yeye leo nina watoto wawili nawapenda sana kuliko kitu chochote kile,nina mali nyingi tu,zaidi ya zile nilizopoteza,
Pole ngoja mimi nisioe lakini nijipange kutofikia wewe ulipo fikia wewe uliendekeza starehe lakini mimi sijasema sitaoa ili nifanye starehee! Hapana nitaishi maisha ya kawaida na kushiriki kila sehemu nayo takiwa kushirikii
 
Huna lolote mbegu zako zimebunguliwa na dumuzi
Najua mtasema hivyo na wala haya maneno hayata nitisha hadi kufikia kupata mtoto msimamo utabaki pale pale lakini ukweli mimi naujua kwani najua nyumbani mwanamke nitakaye pata naye mtoto watataka nioe
 
Back
Top Bottom