VPN USED2020OCTOBER28
JF-Expert Member
- Oct 27, 2011
- 1,505
- 676
Pole sana jamaaa
Nawe kuwa makini pia ...!!
Ni kweli mkuu imani za kishirikina zilikuwa ziko juu sana kanda ya ziwa mf. Hai n mama yangu baba ake alikuwa n mwalimu ukerewe miaka ya 1988 alipoenda msibani toka mwanza walionywa wasile chakula toka nje ya nyumbani kwao,kwani kwa taratibu za huko msiba ukitokea majirani huja na chakula toka makwao kikiwa kimepikwa,pia cha kushangaza wakati wako msibani walipata taarifa na kushuhudia karatasi ikiwa imebandikwa kwenye mti ikionesha tarehe,siku na mwaka na saa ya kufa kwa babu ikiwa imeandikwa na wengine pia waliokuwa wanafuata yaani kuna daftari kabisa la kujua fulani anakufa siku Fulani,tare he, saa na mwaka..yaan wamegeuka kama wao ndio israeli,hali kama hiyo ilitokea mwanza kata ya Kirumba ,mtaa wa kabuhoro barabara ya kwenda ibanda ,ambapo majina yalikuwa yanabandikwa kwenye nguzo za umeme watu waliokuwa wanatakiwa kufa na kweli wanakufa hasa vijana,ndipo vijana walipogoma kuchimba makaburi kwa kusema' kama wanatuua sisi wakachimbe wao makaburi' ilikuwa sokomoko balaa mpaka diwani akaangilia miaka hyo ya 2005-2010,diwani alikuwa anaitwa Richard Rukambula,ndipo mambo yakatulia na hao wachawi au wapaisha tiara, wakapunguza
Mkuu uchawi tena wa kutisha kanda ya ziwa
Nakubaliana na wewe
Nambie dada yangu ...!!
Haya mambo hata sumbawanga yapo,Kigoma yapo hata Tanga pia na mikoa mingine
Hii dhana ya kudhani mahali fulani ni kiboko ni dhana ya hovyo kwasababu siku hizi ukiwa na hela tu unaweza kuununua uchawi unaoutaka!
nimesoma nusu, ntarudi kuimalizia baadae....
Wewe nawe ni mmoja wa wale vilaza?