kingunge wa jf
JF-Expert Member
- Dec 24, 2013
- 466
- 467
Basi ilikuwa trh 24 siku 1 kabla Christmas kama kawaida maza na mshua wakaniambia twende mjini kununua nguo. Basi nikajiandaa fasta huku akili yangu ikijua lazima kile kiatu ninunue.
Basi tukazunguka duka la kwanza la pili mpk karibia maduka yote. Si unajua tena pale wilaya kipindi kile ni sawa tu na kijijini.
Shauku yangu kubwa ili Christmas itimie lazima nivae *MOKA* ndo kiatu kilichokuwa kwenye chati. Hili pia lilichangiwa na kuona mtoto wa tajiri mmoja pale kijijini kanunuliwa MOKA huku mzee na ndo vile alikuwa hataki mtu akatize mbele kizembekizembe. Lakini km kawaida yetu wasukuma sare sare ndo maisha yetu ya kila siku.
Tukaendelea na kusaka viatu vile, Mara paaap! Tukaingia duka la Mangi mmoja hivi. Jamani Tuwaache wachaga wawe tu mbele kwa sabb wameanza kufight kitambo, kujilinganisha na hawa watu ni sawa na kulinganisha Tanzania na Marekani. Kama Tanzania ingekuwa na wachaga wote basi tungekuwa sawa na Angalau South Africa kabisa
Tulipoingia tukaona MOKA nyeusi nzuri ngozi ngozi kweli! Sio za siku hizi mara pale ngozi huku carpet mchanganyiko km rangi ya Mkwele aliyejichubua.
Nikajaribishia ile MOKA lakn ilikuwa kubwa. Wakagoma kununua lkn mie nkalazimisha huku nikilia.
Basi mshua akasema tuendelee kutafta ili wanitoe pale dukani. Tulitafta kila sehemu lkn hatukupata wakaniambia ninunue viatu vingine... nikagoma. Duuuh maza akavimba! Akataka anishushie kipigo pale pale. Lkn mzee kamzuia.
Kumbuka tumefika mjini saa 3 mpk saa 10 sasa tunatafta kiatu changu. Basi ikabidi wamenitema. Wakaanza kufanya yao. Badae maza akasema 'atavaa vya zamani'. Hapo ndio mambo yote yaliharibika. Heeee! Nilijawa na hasira nkalia kwa nguvu badae wakanibembeleza nkanyamaza.
Badae nikaona mzee anachukua pikipiki tukapanda kurudi home aisee nilianza kulia njia nzima hakuna aliyenijali. Nafika home nashuka kwny pikipiki nalia tu.
Mzee alipo park pikipiki yake, maza alipoingia ndani kurudi. Baada ya Dakika 3 sikujua nilifikaje kwa jirani huku nikiwa na manundu kila sehemu afu kesho Christmas.
Basi usiku wakanifata kumbe mzee alikrudia ile MOKA kwa Mangi.
Wakaniambia nijaribishe nikavaa suti yangu na ile MOKA huku MOKA inanizidi mbali sn.
Basi kesho yake kwenda kanisani huku usoni manundu na domo limevimbaa, dada zangu na majirani wananicheka, huku MOKA kubwa nashindwa kutembea. Daaah! Basi Christmas ile ilikuwa tabu sana kwangu.
Watu walinijua kwa kupiga viwalo pale kijijini lkn siku ile pamoja na kuwa vitu vilikuwa bei kubwa lkn kiatu over size na manundu juu. Safari hii Nilikula sikukuu ile nikiwa mnyonge na mwenye kutengwa na jamii.
Je, ipi ilikuwa sikukuu mbaya kwako au nzr?
Basi tukazunguka duka la kwanza la pili mpk karibia maduka yote. Si unajua tena pale wilaya kipindi kile ni sawa tu na kijijini.
Shauku yangu kubwa ili Christmas itimie lazima nivae *MOKA* ndo kiatu kilichokuwa kwenye chati. Hili pia lilichangiwa na kuona mtoto wa tajiri mmoja pale kijijini kanunuliwa MOKA huku mzee na ndo vile alikuwa hataki mtu akatize mbele kizembekizembe. Lakini km kawaida yetu wasukuma sare sare ndo maisha yetu ya kila siku.
Tukaendelea na kusaka viatu vile, Mara paaap! Tukaingia duka la Mangi mmoja hivi. Jamani Tuwaache wachaga wawe tu mbele kwa sabb wameanza kufight kitambo, kujilinganisha na hawa watu ni sawa na kulinganisha Tanzania na Marekani. Kama Tanzania ingekuwa na wachaga wote basi tungekuwa sawa na Angalau South Africa kabisa
Tulipoingia tukaona MOKA nyeusi nzuri ngozi ngozi kweli! Sio za siku hizi mara pale ngozi huku carpet mchanganyiko km rangi ya Mkwele aliyejichubua.
Nikajaribishia ile MOKA lakn ilikuwa kubwa. Wakagoma kununua lkn mie nkalazimisha huku nikilia.
Basi mshua akasema tuendelee kutafta ili wanitoe pale dukani. Tulitafta kila sehemu lkn hatukupata wakaniambia ninunue viatu vingine... nikagoma. Duuuh maza akavimba! Akataka anishushie kipigo pale pale. Lkn mzee kamzuia.
Kumbuka tumefika mjini saa 3 mpk saa 10 sasa tunatafta kiatu changu. Basi ikabidi wamenitema. Wakaanza kufanya yao. Badae maza akasema 'atavaa vya zamani'. Hapo ndio mambo yote yaliharibika. Heeee! Nilijawa na hasira nkalia kwa nguvu badae wakanibembeleza nkanyamaza.
Badae nikaona mzee anachukua pikipiki tukapanda kurudi home aisee nilianza kulia njia nzima hakuna aliyenijali. Nafika home nashuka kwny pikipiki nalia tu.
Mzee alipo park pikipiki yake, maza alipoingia ndani kurudi. Baada ya Dakika 3 sikujua nilifikaje kwa jirani huku nikiwa na manundu kila sehemu afu kesho Christmas.
Basi usiku wakanifata kumbe mzee alikrudia ile MOKA kwa Mangi.
Wakaniambia nijaribishe nikavaa suti yangu na ile MOKA huku MOKA inanizidi mbali sn.
Basi kesho yake kwenda kanisani huku usoni manundu na domo limevimbaa, dada zangu na majirani wananicheka, huku MOKA kubwa nashindwa kutembea. Daaah! Basi Christmas ile ilikuwa tabu sana kwangu.
Watu walinijua kwa kupiga viwalo pale kijijini lkn siku ile pamoja na kuwa vitu vilikuwa bei kubwa lkn kiatu over size na manundu juu. Safari hii Nilikula sikukuu ile nikiwa mnyonge na mwenye kutengwa na jamii.
Je, ipi ilikuwa sikukuu mbaya kwako au nzr?