Sisi sote ni ndugu, Adui ni CCM!

jmushi1

Platinum Member
Nov 2, 2007
24,989
22,521
Baada ya kuandika jinsi tabia ya uchakachuaji na uongo ya CCM inavyoendelea kuligharimu taifa. Nimeona pia ccm wakiendeleza siasa zao za migawanyiko(politics of division). Ile mbinu ya mkoloni ya “divide and rule”, wameiadapt kwa umahiri wa hali ya juu kabisa!

Kama ilivyo kwa uongo wao na propaganda, politics of division ni hatari zaidi wakati tunakabiliana na janga hili la corona.

Mbaya zaidi, kwasababu siasa zao ni zile za abracadabra, “now you see it, now you don’t “, ambapo wameachiwa wazitumie nyakati hizi zinazohitaji wataalam kwenye kufanya maamuzi, kutoa taarifa nk. Wao ndo waliotakiwa kuwa msitari wa mbele na wakati wa utoaji wa taarifa, wanakuwa bega kwa bega na viongozi wao, ili kwamba maswali yoyote muhimu yatakayojitokeza, yapatiwe majibu pasina “bureacracy”. Hawa wangetutolea majibu sahihi kabla ya uamuzi wa kupima papai, kondoo, mbuzi na kupima oil.😏

Kuanza kuwabagua wale viongozi walioamuwa kuchukuwa hatua za kujilockdown kwa siku 14 baada ya baadhi ya wabunge wenzao kudhurika, ni siasa hatarishi kwa taifa letu. Siasa zinazoleta chuki na migawanyiko, ni siasa za ccm. Sisi sote ni ndugu tunaotakiwa kuwa pamoja kama Taifa kwenye vita hivi.

Kitendo cha kusema wanaopoteza maisha yao ni kwasababu ya “changamoto ya upumuaji”, imenisikitisha sana, na ikanikumbusha kauli za uongo uongo za ki ccm, mfano “kitu chenye ncha kali”, badala ya kusema risasi, “watu wasiojulikana”, badala ya kusema ni watu wa usalama...watu ambao polisi haiwezi kuthubutu kuwafuatilia. “Maagizo kutoka juu” nk

Kitendo cha katibu Mwenezi Pole pole kudai chadema ni kama covid-19, kinaondoa ule udugu wetu, na kuonyesha tabia ya ccm ya uongo uongo, uzandiki, na kutokuwa serious na Taifa hili. Maana wamedekezwa na kodi zetu toka uhuru. Na kulindwa na dola hivyo kujisahau.

Kitendo cha ccm kusema watatoa barakoa kwa wanachama wao peke yake pia kinaonyesha uwepo wa matabaka kwenye taifa letu yaliyoasisiwa na ccm.

Ni wazi kwamba tukiiweka ccm pembeni kidogo tutapiga hatua, na wao watajipanga watakapokosa na kutambuwa kwamba uongozi ni dhamana na wala siyo fursa. Watajirekebisha, kuleta ushindani wa kweli kwa kujituma na kujifikirisha. Bila ya kuona kana kwamba nchi inatawaliwa na tabaka moja na mawazo ya kiimla.

Hata hili suala la uchunguzi wa vipimo vya corona, lingefanyika kwa siri pasina kutangaza mbinu, kusingeongeza mkanganyiko ambao unaweza kupelekea upuuzwaji ama uzembe kwa wananchi wa kawaida wasio na uelewa mkubwa kutokana na uongozi mbovu wa ccm toka uhuru.

kauli hii ni courtesy of chriss Lukosi
 
Ni wazi kwamba tukiiweka ccm pembeni kidogo tutapiga hatua, na wao watakapokosa na kutambuwa kwamba uongozi ni dhamana na wala siyo fursa.
Mkuu J Mushi, kwanza asante kwa bandiko hili, naunga mkono hoja ya kuiweka CCM pembeni kidogo, tatizo ni uwepo wa uombwe, uiweke pembeni kidogo CCM, hivyo Ikulu yetu tuikabidhi kwa nani?.

Kufuatia kukosekana kwa wa mbadala wa CCM, matokeo yake ni CCM kuendelea kutawala milele!. It's sad but it's the truth, ukweli mchungu!.
P
 
Mkuu J Mushi, kwanza asante kwa bandiko hili, naunga mkono hoja ya kuiweka CCM pembeni kidogo, tatizo ni uwepo wa uombwe, uiweke pembeni kidogo CCM, hivyo Ikulu yetu tuikabidhi kwa nani?.

Kufuatia kukosekana kwa wa mbadala wa CCM, matokeo yake ni CCM kuendelea kutawala milele!. It's sad but it's the truth, ukweli mchungu!.
P
TANU ilikuwaje wakati wa uhuru?
 
Sijawahi juta kuikataa CCM na watu wake.
Mkuu pia suala la rais kuingilia viongozi wa dini na kuwachonganisha na waumini wao kwa kuingiza siasa ni dhahiri shahiri kwamba CCM wanaligawa Taifa kwa kasi ya hatari kabisa. Hivi ina maana maneno hayo hayo angeweza kuwambia Baba Mtakatifu?🤦🏾‍♂️
 
Mkuu pia suala la rais kuingilia viongozi wa dini na kuwachonganisha na waumini wao kwa kuingiza siasa ni dhahir shahir kwamba ccm wanaligawa Taifa kwa kasi ya hatari kabisa. Hivi ina maana maneno hayo hayo angeweza kuwambia Baba Mtakatifu?
Usitulazimishe na sisi tuwaze kama wewe. Thinking capacity yako ndipo ilipoishia ktk uwezo wa kuchanganua mambo. Mimi binafsi niliisikiliza hotuba A to Z, mbona sijapata maana ka yako.!?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Usitulazimishe na sisi tuwaze kama wewe. Thinking capacity yako ndipo ilipoishia ktk uwezo wa kuchanganua mambo. Mimi binafsi niliisikiliza hotuba A to Z, mbona sijapata maana ka yako.!?

Sent using Jamii Forums mobile app
Wewe mwenye uwezo mkubwa wa kuchanganua mambo? Give me a break! What a joke? Uliposikiliza hotuba A to Z umepata maana gani ambayo ni tofauti na yangu? Unaleta ngonjera.
 
Kufuatia kukosekana kwa wa mbadala wa CCM, matokeo yake ni CCM kuendelea kutawala milele!. It's sad but it's the truth, ukweli mchungu!.
P
Your presence in JamiiForums is a necessity. Your passion is inborn and real as you would enjoy inflicting pain on your opponents simply because you are scared they could beat you in a fair contest. With people like you in this forum, the status quo need not worry about JF and so the forum continues to exist and the last thing they would wish for is for you to leave. Keep it up, you are doing just fine.
 
Kitendo cha ccm kusema watatoa barakoa kwa wanachama wao peke yake pia kinaonyesha uwepo wa matabaka kwenye taifa letu yaliyoasisiwa na ccm.
Mkuu 'jmushi1', hii umeitoa wapi mkuu wangu, mbona mimi nilikuwa bado sijaisikia?
Una kielelezo chochote juu yake?

Nilisoma yote uliyoandika huko juu, nilipofika kwenye maneno hayo nikashindwa kuendelea na yaliyobaki chini. Ngoja nikamalizie kusoma ili nitoe mawazo yangu ya jumla kwa mada yako.
 
upuuzwaji ama uzembe kwa wananchi wa kawaida wasio na uelewa mkubwa kutokana na uongozi mbovu wa ccm toka uhuru.
Hapa mwisho umekengeuka.

Lakini nimekusoma hadi mwisho na yafuatayo ndio maoni yangu.

CCM kama chama kusema kweli haipo sasa hivi, kilichopo ni jina la chama na kundi la watu wanaojiita wanachama wa chama hicho kutokana na maslahi binafsi wanayoyapata kwa kuwa katika kundi hilo.

CCM, kama ilivyo sasa nchi yetu Tanzania, ni mateka wa mtu mmoja aliyechaguliwa na wananchi (sijui uhalali wa uchaguzi huo, lakini kiongozi huyo alipewa uhalali huo baada ya yote yaliyofanyika kumkabidhi madaraka.

Baada ya kupewa madaraka kwa hatua zote zilizopaswa kufanyika, huyu mtu akajimilikisha vyombo vyote vya kimadaraka ili vyombo hivyo vitimize matakwa yake, na sio matakwa ya wananchi. Ndio maana nasema kapata mateka, hata sisi raia na CCM iliyomweka hapo ni mateka wake kwa kutumia nguvu za vyombo alivyokabidhiwa ili vimsaidie kutufanyia kazi.

CCM hawana uwezo juu yake, kama sisi wananchi tusivyokuwa na uwezo juu yake kwa wakati huu.

CCM chini ya Kikwete ilikuwa imeoza, lakini bado ilikuwa na muundo wake wa tokea zamami enzi za Mwalimu; kwa hiyo ingeweza kubadilika kama ingempata kiongozi aliyekuwa hataki ubovu aliouvumilia Kikwete.. Lakini aliyechukua akaona autumie ubovu huo kujimilikisha jina la chama. Chama chenyewe hasa hakipo. CCM ni Mwenyekiti wake sasa hivi
Kama huamini, kawaulize Kinana na akina Nnauye, Makamba na wengineo wakitaka kukueleza watakupa ukweli.

Kwa hiyo, hayo yote uliyoyaandika kwenye mada yako hapo juu, ya kufarakanisha na mengineyo, haya yameshamiri zaidi kwa sababu ndio tabia ya mwenye chama.
Hila nyingi zidi ya wapinzani, nieleza, pamoja na kwamba zilikuwepo chini ya Kikwete, lakini hazikufika huku tulikofika sasa hivi chini ya mwenye chama.

Mabeberu wamekuwa marafiki wa wapinzani, kwa hiyo maadui wa waTanzania, hiki ni kibwagizo kinachopendwa sana kutumiwa wakati huu

Ngoja nisikuchoshe sana kwa kumaliza na yafuatayo.

Udhaifu mkubwa unaoonyeshwa na wapinzani wote sasa hivi ni kushindwa kwao kueleza kwa wananchi hii tabia mpya, mbaya kabisa ya kuligawa taifa letu katika makundi mbalimbali.
Wapinzani wameshindwa kabisa kujenga hoja juu ya jambo hili na wakalipeleka kwa wananchi kulieleza ili wananchi walielewe vizuri.
Kazi hii haiwezi kuwa ngumu, kwa sababu huko nyuma umoja wetu ulijulikana duniani na ndiyo iliyokuwa nguvu yetu pamoja na umaskini wetu wa mali.

Hapa wapinzani wanatakiwa wachambue kwa kina kabisa matendo yote, tena yapo mengi mno yaliyofanywa na mwenye chama ambayo yanafanywa kwa maksudi kwa kutugawa waTanzania. ili azidi kututawala kwa raha zake.
 
Kufuatia kukosekana kwa wa mbadala wa CCM, matokeo yake ni CCM kuendelea kutawala milele!. It's sad but it's the truth, ukweli mchungu!.
P
Huo mbadala unatakiwa uweje ndipo ujue kuna mbadala?

Yaani CCM haiwezi kabisa ikawa mbaya kabisa kuliko mbadala wowote ule?

Imebidi niulize haya maswali pamoja na kujua kuwa hayana maana yoyote kwako!
 
Mkuu 'jmushi1', hii umeitoa wapi mkuu wangu, mbona mimi nilikuwa bado sijaisikia?
Una kielelezo chochote juu yake?

Nilisoma yote uliyoandika huko juu, nilipofika kwenye maneno hayo nikashindwa kuendelea na yaliyobaki chini. Ngoja nikamalizie kusoma ili nitoe mawazo yangu ya jumla kwa mada yako.
Ipo mbona? Hukuona hizo taarifa?
 
Mkuu unadhani hapo mwisho nimekengeuka? Je ufahamu wa mtanzania hauwi contributed to the ruling class beginning from Independence Day? Kwasababu ndivyo nilivyosema hapo mwishoni unapodai nimekengeuka. Je waweza kuelezea ni kwa vipi nimekengeuka?

Nimeeelewa bandiko lako mara mbili, na hivyo kuwa na maswali mawili respectively.

Moja, je ni kweli upinzani unatumika na mabeberu? And if so, how?

Mbili, inaonekana unamlaumu mwenyekiti peke yake! Tena ukatoa na mifano ya uongozi wa JK ukilinganisha na huu wa kwake kuonyesha huo utofauti. Je ina maana kwamba ccm wako vizuri kasoro mwenyekiti wao?
 
Huo mbadala unatakiwa uweje ndipo ujue kuna mbadala?

Yaani CCM haiwezi kabisa ikawa mbaya kabisa kuliko mbadala wowote ule?

Imebidi niulize haya maswali pamoja na kujua kuwa hayana maana yoyote kwako!
Ni sawa na kusema “jambazi hana mbadala”🤦🏾‍♂️
 
Vipi wale waliogoma kukaa guest? Na wao ni ndugu? Siku hizi hamuendi Dubai , bali ni kujilock down guest mkitafuna kodi za Watanzania!
 
Back
Top Bottom