Sisi sote ni ndugu, Adui ni CCM!

Sisi sote ni ndugu, Adui ni CCM!

Vp wale waliogoma kukaa guest? Na wao ni ndugu? Siku hizi hamuendi Dubai , bali ni kujilock down guest mkitafuna kodi za Watanzania!
Duh! Hata sijakuelewa mkuu. Kukaa guest ndo kunamfanya mtu awe ndugu mtanzania?

Unafahamu guest niliyojifungia? Nakupa ruhusa uitaje hapa hiyo guest.

Mimi natafuna kodi za wananchi? Umesoma vyema bandiko langu ama umepanikishwa na heading?
 
Natamani watu wote wangeujua ukweli huu.
Muda utaongea. Huwa wanasema baba wa uongo ni shetani. Actually bible inasema hivyo. Hivyo basi kitendo cha wao kuendelea kutawala kwa uongo uongo ni sawa na kumpa shetani nchi aongoze!
 
Mkuu pia suala la rais kuingilia viongozi wa dini na kuwachonganisha na waumini wao kwa kuingiza siasa ni dhahir shahir kwamba ccm wanaligawa Taifa kwa kasi ya hatari kabisa. Hivi ina maana maneno hayo hayo angeweza kuwambia Baba Mtakatifu?🤦🏾‍♂️

Mbona wao viongozi wa dini wanaingilia mambo ya serikari na kuwachonganisha na wananchi wake na huwa mnasema ni haki yao?
 
Mbona wao viongozi wa dini wanaingilia mambo ya serikari na kuwachonganisha na wananchi wake na huwa mnasema ni haki yao?
Tolea mfano walivyoingilia “mambo ya serikari” na kuwachonganisha na wananchi wake.
 
Ipo mbona? Hukuona hizo taarifa?
Sikuiona mkuu.
Ni vigumu sana kwangu kuiamini hii, lakini na wewe hukutaka kunisaidia kwa kunielekeza ninapoweza kuipata hiyo taarifa.
Kama ni kweli ilisemwa hivyo..., aaah, basi tuyaache yalivyo!
 
Sikuiona mkuu.
Ni vigumu sana kwangu kuiamini hii, lakini na wewe hukutaka kunisaidia kwa kunielekeza ninapoweza kuipata hiyo taarifa.
Kama ni kweli ilisemwa hivyo..., aaah, basi tuyaache yalivyo!
Kivipi sikutaka kukusaidia na wakati nimeenda Google nikakuletea link ya JF?

Kuhusu kama ni ukweli ilisemwa hivyo, ni suala la kuipitia hiyo link na kujiridhisha mwenyewe, utizame reliability yake.

All in all, hilo la barakoa si lolote si chochote ukizingatia muktadha.
 
Hapa mwisho umekengeuka.

Lakini nimekusoma hadi mwisho na yafuatayo ndio maoni yangu.

CCM kama chama kusema kweli haipo sasa hivi, kilichopo ni jina la chama na kundi la watu wanaojiita wanachama wa chama hicho kutokana na maslahi binafsi wanayoyapata kwa kuwa katika kundi hilo.

CCM, kama ilivyo sasa nchi yetu Tanzania, ni mateka wa mtu mmoja aliyechaguliwa na wananchi (sijui uhalali wa uchaguzi huo, lakini kiongozi huyo alipewa uhalali huo baada ya yote yaliyofanyika kumkabidhi madaraka.

Baada ya kupewa madaraka kwa hatua zote zilizopaswa kufanyika, huyu mtu akajimilikisha vyombo vyote vya kimadaraka ili vyombo hivyo vitimize matakwa yake, na sio matakwa ya wananchi. Ndio maana nasema kapata mateka, hata sisi raia na CCM iliyomweka hapo ni mateka wake kwa kutumia nguvu za vyombo alivyokabidhiwa ili vimsaidie kutufanyia kazi.

CCM hawana uwezo juu yake, kama sisi wananchi tusivyokuwa na uwezo juu yake kwa wakati huu.

CCM chini ya Kikwete ilikuwa imeoza, lakini bado ilikuwa na muundo wake wa tokea zamami enzi za Mwalimu; kwa hiyo ingeweza kubadilika kama ingempata kiongozi aliyekuwa hataki ubovu aliouvumilia Kikwete.. Lakini aliyechukua akaona autumie ubovu huo kujimilikisha jina la chama. Chama chenyewe hasa hakipo. CCM ni Mwenyekiti wake sasa hivi
Kama huamini, kawaulize Kinana na akina Nnauye, Makamba na wengineo wakitaka kukueleza watakupa ukweli.

Kwa hiyo, hayo yote uliyoyaandika kwenye mada yako hapo juu, ya kufarakanisha na mengineyo, haya yameshamiri zaidi kwa sababu ndio tabia ya mwenye chama.
Hila nyingi zidi ya wapinzani, nieleza, pamoja na kwamba zilikuwepo chini ya Kikwete, lakini hazikufika huku tulikofika sasa hivi chini ya mwenye chama.

Mabeberu wamekuwa marafiki wa wapinzani, kwa hiyo maadui wa waTanzania, hiki ni kibwagizo kinachopendwa sana kutumiwa wakati huu

Ngoja nisikuchoshe sana kwa kumaliza na yafuatayo.

Udhaifu mkubwa unaoonyeshwa na wapinzani wote sasa hivi ni kushindwa kwao kueleza kwa wananchi hii tabia mpya, mbaya kabisa ya kuligawa taifa letu katika makundi mbalimbali.
Wapinzani wameshindwa kabisa kujenga hoja juu ya jambo hili na wakalipeleka kwa wananchi kulieleza ili wananchi walielewe vizuri.
Kazi hii haiwezi kuwa ngumu, kwa sababu huko nyuma umoja wetu ulijulikana duniani na ndiyo iliyokuwa nguvu yetu pamoja na umaskini wetu wa mali.

Hapa wapinzani wanatakiwa wachambue kwa kina kabisa matendo yote, tena yapo mengi mno yaliyofanywa na mwenye chama ambayo yanafanywa kwa maksudi kwa kutugawa waTanzania. ili azidi kututawala kwa raha zake.

Asante sana mkuu, nakubaliana na wewe kwa asilimia 100. Natamani kila mmoja humu JF angesoma hiki ulichochangia kwenye uzi huu!
 
Mkuu unadhani hapo mwisho nimekengeuka? Je ufahamu wa mtanzania hauwi contributed to the ruling class beginning from Independence Day? Kwasababu ndivyo nilivyosema hapo mwishoni unapodai nimekengeuka. Je waweza kuelezea ni kwa vipi nimekengeuka?

Nimeeelewa bandiko lako mara mbili, na hivyo kuwa na maswali mawili respectively.

Moja, je ni kweli upinzani unatumika na mabeberu? And if so, how?

Mbili, inaonekana unamlaumu mwenyekiti peke yake! Tena ukatoa na mifano ya uongozi wa JK ukilinganisha na huu wa kwake kuonyesha huo utofauti. Je ina maana kwamba ccm wako vizuri kasoro mwenyekiti wao?
Kwani shida ipo wapi mkuu 'jmushi1'.
Niliyosema yapo wazi kabisa.

CCM ilishavurugika toka walipochanganyikiwa na kutoka kwenye misingi iliyoiunda, kuwa chama cha kusimamia maslahi ya wananchi na kuanza kuwa ngao ya watu wenye uwezo wa kutumia chama kwa manufaa yao. Ukijua haya yalianzia wapi hutakuwa na shida ya kunielewa nilichoandika.
Lakini katika kuwepo na ubovu wote huo ndani ya chama hicho nyakati hizo. bado palikuwemo ndani ya chama misingi ambayo kama angetokea kiongozi na kutaka kukirekebisha ingewezekana kukirudisha chama katika mwelekeo wake wa mwanzo.
Badala yake, tumeona katika awamu hizi, kukosekana kwa kiongozi wa aina hiyo. Kikwete ndiye kakidhoofisha kabisa na kukiandaa kichukuliwe kirahisi na mtu mmoja anayejua kutumia mabavu na kuhodhi kila kitu. Kanyang'anya hata ule uwezo mdogo uliokuwa umesalia ndani ya chama hicho. Sasa hivi ulivyo mfumo wa chama, hakuna mtu yeyote anayeweza kupaza sauti kwa lolote; kwa sababu wote wamekwishafifishwa.

Hebu nieleze wewe unavyoona. Ni maamuzi gani yanayofanywa ndani ya chama ambayo hayakuasisiwa na kusimamiwa na mwenyekiti. Chama hakina maamzi yoyote, utakilaumu kwa lipi?

Hakuna popote niliposema "upinzani unatumika na mabeberu", mbali ya kuweka msisitizo ambao naona hukuuelewa jinsi propaganda za mwenyekiti zilivyo ili kuwaaminisha wananchi wajinga. Na ndio maana yangu ya kuwashauri wapinzani waweke juhudi kuwaelimisha wananchi kuzitambua hadaa hizi nyepesi nyepesi.

Hilo la "kutokea tupate uhuru" sikubaliani nalo na hata sijui umeliingizaje kwenye mada yako hii.
 
Kivipi sikutaka kukusaidia na wakati nimeenda Google nikakuletea link ya JF?

Kuhusu kama ni ukweli ilisemwa hivyo, ni suala la kuipitia hiyo link na kujiridhisha mwenyewe, utizame reliability yake.

All in all, hilo la barakoa si lolote si chochote ukizingatia muktadha.
Nilikuwa sijaiona hiyo mkuu wangu. Nashukuru kwa uvumilivu na jitihada za kunifahamisha.
 
Ipo mbona? Hukuona hizo taarifa?
Mkuu 'jmushi1', ahsante..., nimeliona hilo bandiko; ingawaje bado ni vigumu kujua uhakika wa taarifa hiyo kama ilivyotolewa kwenye bandiko hilo.

Hawa "wananchi wajinga tokea uhuru"; huu ni ujinga wa kawaida, au kuna kitu kingine cha ziada?

Ni wananchi wa namna gani hawa wasioweza kuelewa maana ya taarifa iliyo wazi kama hiyo iliyomo kwenye bandiko hilo?

Yaani, taarifa ya kwamba ni wanachama pekee wa CCM ndio walio na haki ya kujikinga na hatari ya ugonjwa wa coronavirus?
Hii taarifa imewafikia wananchi na wao wakaikubali na hapo Oktoba wajitokeze kwenda kuwapigia kura viongozi wa CCM hata kama wao wananchi tayari wametengwa kwa kunyimwa hizo barakoa?
Sijui kama unanielewa mkuu, mawazo yangu yanakoelekea.

Hawa wananchi kweli ni wajinga?
Kwa uhakika, mimi sijitambui kuwa ni mjinga, pamoja na kwamba taarifa hiyo ya CCM nilikuwa siijui hadi hapo ulipoileta hapa.
Hivi hatuwezi tukasema wananchi sio wajinga ila hawapati taarifa za kuwawezesha kufanya maamuzi?

Ni nani mwenye wajibu wa kuwafikishia taarifa wananchi?
 
Kwani shida ipo wapi mkuu 'jmushi1'.
Niliyosema yapo wazi kabisa.

CCM ilishavurugika toka walipochanganyikiwa na kutoka kwenye misingi iliyoiunda, kuwa chama cha kusimamia maslahi ya wananchi na kuanza kuwa ngao ya watu wenye uwezo wa kutumia chama kwa manufaa yao. Ukijua haya yalianzia wapi hutakuwa na shida ya kunielewa nilichoandika.
Lakini katika kuwepo na ubovu wote huo ndani ya chama hicho nyakati hizo. bado palikuwemo ndani ya chama misingi ambayo kama angetokea kiongozi na kutaka kukirekebisha ingewezekana kukirudisha chama katika mwelekeo wake wa mwanzo.
Badala yake, tumeona katika awamu hizi, kukosekana kwa kiongozi wa aina hiyo. Kikwete ndiye kakidhoofisha kabisa na kukiandaa kichukuliwe kirahisi na mtu mmoja anayejua kutumia mabavu na kuhodhi kila kitu. Kanyang'anya hata ule uwezo mdogo uliokuwa umesalia ndani ya chama hicho. Sasa hivi ulivyo mfumo wa chama, hakuna mtu yeyote anayeweza kupaza sauti kwa lolote; kwa sababu wote wamekwishafifishwa.

Hebu nieleze wewe unavyoona. Ni maamuzi gani yanayofanywa ndani ya chama ambayo hayakuasisiwa na kusimamiwa na mwenyekiti. Chama hakina maamzi yoyote, utakilaumu kwa lipi?

Hakuna popote niliposema "upinzani unatumika na mabeberu", mbali ya kuweka msisitizo ambao naona hukuuelewa jinsi propaganda za mwenyekiti zilivyo ili kuwaaminisha wananchi wajinga. Na ndio maana yangu ya kuwashauri wapinzani waweke juhudi kuwaelimisha wananchi kuzitambua hadaa hizi nyepesi nyepesi.

Hilo la "kutokea tupate uhuru" sikubaliani nalo na hata sijui umeliingizaje kwenye mada yako hii.
Mkuu labda wewe ndo hukunielewa. Nilimaanisha kwamba tatizo la uelewa wa wananchi, liko attributed to ccm since wao ndo wametawala toka uhuru. Kama ingekuwa the opposite, wangepata sifa zao accordingly.

Kuhusu hilo la wewe “kutokusema” kwamba “upinzani unatumika na mabeberu”, nimekuelewa. Nililizungumzia hilo kwenye thread yangu ambapo niliweka wazi ni kwa jinsi gani ccm ni hatari nyakati za janga hili. Na huko nilizungumzia kuhusu propaganda za ccm ambazo zinazidi kuliangusha taifa zaidi ya kulinufaisha. Tukiwaiga wachina, ni yale yale ya kumuiga Tembo kunya.
 
Mkuu labda wewe ndo hukunielewa. Nilimaanisha kwamba tatizo la uelewa wa wananchi, liko attributed to ccm since wao ndo wametawala toka uhuru. Kama ingekuwa the opposite, wangepata sifa zao accordingly.
Tokea 1995, bado haiwezekani kweli kuwaelimisha watu?
Na huko nilizungumzia kuhusu propaganda za ccm ambazo zinazidi kuliangusha taifa zaidi ya kulinufaisha. Tukiwaiga wachina, ni yale yale ya kumuiga Tembo kunya.
Ni vigumu sana hata kuziita hizi nyepesinyepesi zinazotolewa na mwenyekiti kuziita 'propaganda'.

Propaganda gani hizi hata hazitolewi maelezo yoyote ya kuzibeba ili ziaminike? Huo uwezo hana, na timu aliyonayo hawana uwezo wa kufanya 'propaganda.'

Ni basi tu, bahati mbaya ni kwa wapinzani kutotaka kuyafanyia kazi haya yote yaliyopo ili wananchi wayaone. Tena ninao uhakika watayaelewa vizuri sana.

Tunapowalaumu CCM (mwenyekiti na kundi lake), tusisahau pia kuwalaumu wapinzani kwa kukosa kuzitumia fursa zinazojitokeza.
Lakini najua utaingiza ugumu wa kufanya siasa unaowakabili. Hili tuliache pembeni, kwa sababu sikubaliani nalo kamwe. Kuna udhaifu pia wa aina yake huko ndani ya upinzani. Hii ndio bahati yetu mbaya kama taifa. Wengi ni 'opportunists' wanasubiri embe liwadondokee kichwani.
 
Sitarudia tena kuwaamini wana siasa atakama ni Baba yangu...Rotha siyo wa kutufanyia ivo,hiki kipengele kimefanya nione wanasiasa ote mnataka kupiga hera2 kwa zam then mnasepa nakutuacha kama tulivo hata Rais atoke chadema,cuf,Act nk. Ndo yale yale SIPIGI KURA TENA..

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nimecheka sana,eti adui ni CCM, mkuu si kweli chama pekee kinachoweza kumletea Maendeleo mtanzania kwa sasa na hata miaka mia moja ijayo ni CCM, maana ndiyo chama pekee kisicho na ubinafsi na ni chama cha kila raia

Si CHADEMA au ACT kinauwezo wa kupigania masirahi ya mtanzania,nichukulie mfano CHADEMA kama chama kikuu cha upinzani kinachoelekea kufa,chama hiki kimejawa viwavi,nondo na kila aina ya watu waharibifu,hakina agenda thabiti ya kutatua changamoto za mtanzania zaidi ya kukamia raslimali za nchi na kugawana madaraka

Sasa ukisema adui yetu ni CCM sikweli,maana kwa sasa na hata miaka mia ijayo sijaona chama chenye nia ya kuchukua madaraka na kumletea mwananchi Maendeleo tofauti na ccm ,chadema wao kwa wao hawaaminiani sasa vipi kuhusu mwananchi wa chini kama Mimi nitaiamini vipi CHADEMA?

Kwa taarifa nilizo nazo ambazo hazina shaka ni kuwa mwenyekiti wa CHADEMA na katibu wake John Mnyika kwa sasa hawaelewani ,na juzi mwenyekiti wa chadema alimpigia simu katibu wake ziadi ya Mara tatu hakupokea simu na wala hadi naandika hapa hajamtafuta kujua makusudi ya simu ile toka kwa chairman. Sasa hapa ndo utapata picha kamili,kipi ni chama makini

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hapa mwisho umekengeuka.

Lakini nimekusoma hadi mwisho na yafuatayo ndio maoni yangu.

CCM kama chama kusema kweli haipo sasa hivi, kilichopo ni jina la chama na kundi la watu wanaojiita wanachama wa chama hicho kutokana na maslahi binafsi wanayoyapata kwa kuwa katika kundi hilo.

CCM, kama ilivyo sasa nchi yetu Tanzania, ni mateka wa mtu mmoja aliyechaguliwa na wananchi (sijui uhalali wa uchaguzi huo, lakini kiongozi huyo alipewa uhalali huo baada ya yote yaliyofanyika kumkabidhi madaraka.

Baada ya kupewa madaraka kwa hatua zote zilizopaswa kufanyika, huyu mtu akajimilikisha vyombo vyote vya kimadaraka ili vyombo hivyo vitimize matakwa yake, na sio matakwa ya wananchi. Ndio maana nasema kapata mateka, hata sisi raia na CCM iliyomweka hapo ni mateka wake kwa kutumia nguvu za vyombo alivyokabidhiwa ili vimsaidie kutufanyia kazi.

CCM hawana uwezo juu yake, kama sisi wananchi tusivyokuwa na uwezo juu yake kwa wakati huu.

CCM chini ya Kikwete ilikuwa imeoza, lakini bado ilikuwa na muundo wake wa tokea zamami enzi za Mwalimu; kwa hiyo ingeweza kubadilika kama ingempata kiongozi aliyekuwa hataki ubovu aliouvumilia Kikwete.. Lakini aliyechukua akaona autumie ubovu huo kujimilikisha jina la chama. Chama chenyewe hasa hakipo. CCM ni Mwenyekiti wake sasa hivi
Kama huamini, kawaulize Kinana na akina Nnauye, Makamba na wengineo wakitaka kukueleza watakupa ukweli.

Kwa hiyo, hayo yote uliyoyaandika kwenye mada yako hapo juu, ya kufarakanisha na mengineyo, haya yameshamiri zaidi kwa sababu ndio tabia ya mwenye chama.
Hila nyingi zidi ya wapinzani, nieleza, pamoja na kwamba zilikuwepo chini ya Kikwete, lakini hazikufika huku tulikofika sasa hivi chini ya mwenye chama.

Mabeberu wamekuwa marafiki wa wapinzani, kwa hiyo maadui wa waTanzania, hiki ni kibwagizo kinachopendwa sana kutumiwa wakati huu

Ngoja nisikuchoshe sana kwa kumaliza na yafuatayo.

Udhaifu mkubwa unaoonyeshwa na wapinzani wote sasa hivi ni kushindwa kwao kueleza kwa wananchi hii tabia mpya, mbaya kabisa ya kuligawa taifa letu katika makundi mbalimbali.
Wapinzani wameshindwa kabisa kujenga hoja juu ya jambo hili na wakalipeleka kwa wananchi kulieleza ili wananchi walielewe vizuri.
Kazi hii haiwezi kuwa ngumu, kwa sababu huko nyuma umoja wetu ulijulikana duniani na ndiyo iliyokuwa nguvu yetu pamoja na umaskini wetu wa mali.

Hapa wapinzani wanatakiwa wachambue kwa kina kabisa matendo yote, tena yapo mengi mno yaliyofanywa na mwenye chama ambayo yanafanywa kwa maksudi kwa kutugawa waTanzania. ili azidi kututawala kwa raha zake.
Nimekuelewa mkuu!! Hii CCM mpya ni utata mtupu.
 
Tokea 1995, bado haiwezekani kweli kuwaelimisha watu?

Ni vigumu sana hata kuziita hizi nyepesinyepesi zinazotolewa na mwenyekiti kuziita 'propaganda'.

Propaganda gani hizi hata hazitolewi maelezo yoyote ya kuzibeba ili ziaminike? Huo uwezo hana, na timu aliyonayo hawana uwezo wa kufanya 'propaganda.'

Ni basi tu, bahati mbaya ni kwa wapinzani kutotaka kuyafanyia kazi haya yote yaliyopo ili wananchi wayaone. Tena ninao uhakika watayaelewa vizuri sana.

Tunapowalaumu CCM (mwenyekiti na kundi lake), tusisahau pia kuwalaumu wapinzani kwa kukosa kuzitumia fursa zinazojitokeza.
Lakini najua utaingiza ugumu wa kufanya siasa unaowakabili. Hili tuliache pembeni, kwa sababu sikubaliani nalo kamwe. Kuna udhaifu pia wa aina yake huko ndani ya upinzani. Hii ndio bahati yetu mbaya kama taifa. Wengi ni 'opportunists' wanasubiri embe liwadondokee kichwani.
Umesema vyema mkuu. Ni kweli kuna udhaifu upo ndani ya upinzani, lakini uwepo wao mpaka sasa unaonyesha wazi kabisa kuchoshwa kwa wananchi. Umezungumza vyema kuhusiana na ugumu wa kufanya siasa wanaokabiliana nao.

Kama lengo letu ni kupata siasa zenye ushindani wa kweli, basi lazima tupate kwa kuanzia. Sikubalini na wale wanaosema eti hakuna upinzani. Chama tawala kimekuwa kikitumia nguvu na mabavu kwa kupitia dola. Wameshatumia kila aina ya mbinu chafu. Walishatangaza vifo vya upinzani over and over again!

Mimi ninaamini ccm kuwekwa benchi ni muhimu kama tunataka tuanze kuchukuwa hatua dhabiti za maendeleo ya wananchi na taifa kwa ujumla. Kitendo cha wao kutawala kama a monarch, kimeawaharibu kabisa. Mabavu coupled with politics of division.
 
Sitarudia tena kuwaamini wana siasa atakama ni Baba yangu...Rotha siyo wa kutufanyia ivo,hiki kipengele kimefanya nione wanasiasa ote mnataka kupiga hera2 kwa zam then mnasepa nakutuacha kama tulivo hata Rais atoke chadema,cuf,Act nk. Ndo yale yale SIPIGI KURA TENA..

Sent using Jamii Forums mobile app
Doing nothing is not a solution. Sijui kama una uwezo wa kuisoma signature yangu. Walioko kwenye desktop mode ndo wanaiona, inasema hivi...

“One of the penalties for refusing to participate in politics is that you end up being governed by your inferiors”-Plato

Kwa kifupi, ina maana kwamba ukisusa, utakuja kutawaliwa na mtu ambaye kiuhalisia, alitakiwa kuwa houseboy wako! Je utaishi kwa furaha?
 
Mkuu 'jmushi1', ahsante..., nimeliona hilo bandiko; ingawaje bado ni vigumu kujua uhakika wa taarifa hiyo kama ilivyotolewa kwenye bandiko hilo.

Hawa "wananchi wajinga tokea uhuru"; huu ni ujinga wa kawaida, au kuna kitu kingine cha ziada?

Ni wananchi wa namna gani hawa wasioweza kuelewa maana ya taarifa iliyo wazi kama hiyo iliyomo kwenye bandiko hilo?

Yaani, taarifa ya kwamba ni wanachama pekee wa CCM ndio walio na haki ya kujikinga na hatari ya ugonjwa wa coronavirus?
Hii taarifa imewafikia wananchi na wao wakaikubali na hapo Oktoba wajitokeze kwenda kuwapigia kura viongozi wa CCM hata kama wao wananchi tayari wametengwa kwa kunyimwa hizo barakoa?
Sijui kama unanielewa mkuu, mawazo yangu yanakoelekea.

Hawa wananchi kweli ni wajinga?
Kwa uhakika, mimi sijitambui kuwa ni mjinga, pamoja na kwamba taarifa hiyo ya CCM nilikuwa siijui hadi hapo ulipoileta hapa.
Hivi hatuwezi tukasema wananchi sio wajinga ila hawapati taarifa za kuwawezesha kufanya maamuzi?

Ni nani mwenye wajibu wa kuwafikishia taarifa wananchi?
Ngoja nikuangazie zaidi kidogo, usijikite kwenye semantics...

Kuna mtu niliongea naye, akasema “Kwanza mimi nilikuwa sili mapapai, kwahiyo nina nafuu zaidi”, nikamwambia mapapai yatakusaidia kupata vitamin C ambayo ni muhimu kwenye kupambana na magonjwa kama covid. Mipapai imekatiwa chini nk. Ikapelekea Makonda kutoa taarifa.

Kwamba ni “wanachama wa ccm pekee ndiyo wanaotakiwa kujilinda”, haina mwelekeo wowote wa kile ninachokimaanisha.
 
Kwamba ni “wanachama wa ccm pekee ndiyo wanaotakiwa kujilinda”, haina mwelekeo wowote wa kile ninachokimaanisha
Tutazungushana bure..., ni kipi nisichokielewa unachomaanisha, mbona nilikuelewa toka mwanzo! Ila hapa wewe ndie hukuelewa nilichoandika, na sio mara ya kwanza hili kujitokeza kwenye mada hii.
Lakini haya tuyaache, kwa sababu sioni tofauti kubwa kati ya unayoandika na ninayoandika mimi.
Sasa anagalia hili hapa chini; la mipapai.

Hii nayo kweli unaweza ukaiita ni 'propaganda'?
Mbona tunataka kuwageuza waTanzania waonekane kuwa kama mahuha jameni?

Haya basi tuseme ni 'propaganda' ya kuwalaza akili waTanzania wasioelewa kitu. Wapinzani wanashindwa kuwaondoa ujinga hawa mazuzu, kwa vipi? Hili ndilo swali la msingi.
Kuna mtu niliongea naye, akasema “Kwanza mimi nilikuwa sili mapapai, kwahiyo nina nafuu zaidi”, nikamwambia mapapai yatakusaidia kupata vitamin C ambayo ni muhimu kwenye kupambana na magonjwa kama covid. Mipapai imekatiwa chini nk. Ikapelekea Makonda kutoa taarifa.
 
Back
Top Bottom